< دوم پادشاهان 17 >
در سال دوازدهم سلطنت آحاز، پادشاه یهودا، هوشع (پسر ایلا) پادشاه اسرائیل شد و نه سال در سامره سلطنت نمود. | 1 |
Katika mwaka wa kumi na mbili wa utawala wa Ahazi mfalme wa Yuda, Hoshea mwana wa Ela akawa mfalme wa Israeli katika Samaria, akatawala kwa miaka tisa.
او نسبت به خداوند گناه ورزید، اما نه به اندازهٔ پادشاهانی که قبل از او در اسرائیل سلطنت میکردند. | 2 |
Akafanya maovu machoni pa Bwana, lakini si kama wafalme wengine wa Israeli waliomtangulia.
در زمان او شلمناسر، پادشاه آشور به اسرائیل لشکر کشید؛ هوشع تسلیم شلمناسر شد و از آن به بعد هر سال به او باج و خراج میپرداخت. | 3 |
Mfalme Shalmanesa wa Ashuru akainuka dhidi ya Mfalme Hoshea, ambaye hapo mbeleni alikuwa mtumwa wake na kumlipa ushuru.
اما یک سال از پرداخت باج و خراج سر باز زد و قاصدانی به مصر فرستاد تا از «سو» پادشاه آنجا کمک بخواهد. وقتی شلمناسر از این توطئه باخبر شد هوشع را به زنجیر کشیده، به زندان انداخت. | 4 |
Lakini mfalme wa Ashuru akagundua kuwa Hoshea alikuwa msaliti, kwa kuwa alikuwa ametuma wajumbe kwa So mfalme wa Misri, naye hakuendelea kulipa ushuru kwa mfalme wa Ashuru tena kama alivyokuwa anafanya kila mwaka. Kwa hiyo Shalmanesa akamkamata na kumtia gerezani.
سپس، شلمناسر سراسر سرزمین اسرائیل را اشغال نمود و سامره پایتخت اسرائیل را به مدت سه سال محاصره کرد. | 5 |
Mfalme wa Ashuru akaishambulia nchi yote, akapigana dhidi ya Samaria na kuizunguka kwa majeshi miaka mitatu.
سرانجام در نهمین سال سلطنت هوشع، شلمناسر شهر سامره را گرفت و مردم اسرائیل را اسیر نمود و به آشور برد. او بعضی از اسرا را در شهر حلح، برخی دیگر را در شهر جوزان که کنار رود خابور است، و بقیه را در شهرهای سرزمین ماد سکونت داد. | 6 |
Katika mwaka wa tisa wa Hoshea, mfalme wa Ashuru akaiteka Samaria na kuwahamishia Waisraeli huko Ashuru. Akawaweka huko Hala, na Gozani karibu na Mto Habori, na katika miji ya Wamedi.
این بلا از این جهت بر قوم اسرائیل نازل شد که نسبت به خداوند، خدای خود که ایشان را از بندگی در مصر نجات داده بود، گناه کرده بودند. آنها بتها را میپرستیدند | 7 |
Yote haya yalitokea kwa sababu Waisraeli walikuwa wametenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wao, ambaye alikuwa amewapandisha kutoka Misri akiwatoa chini ya utawala wa nguvu wa Farao mfalme wa Misri. Waliabudu miungu mingine
و از رسوم قومهایی که خداوند آنها را از سرزمین کنعان بیرون رانده بود، پیروی میکردند و از کارهای پادشاهان اسرائیل سرمشق میگرفتند. | 8 |
na kufuata desturi za mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele yao, pamoja na desturi ambazo wafalme wa Israeli walizileta.
بنیاسرائیل مخفیانه نسبت به خداوند گناه ورزیده بودند. آنها در هر گوشه و کنار اسرائیل بتخانهای ساخته بودند. | 9 |
Waisraeli wakafanya vitu kwa siri dhidi ya Bwana Mungu wao, ambavyo havikuwa sawa. Kuanzia kwenye mnara wa ulinzi hadi kwenye mji wenye maboma walijijengea wenyewe mahali pa juu pa kuabudia miungu katika miji yao yote.
روی هر تپهای و زیر هر درخت سبزی مجسمه و بت گذاشته بودند | 10 |
Wakaweka mawe ya kuabudiwa na nguzo za Ashera juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila mti uliotanda.
و برای بتهای قومهایی که خداوند ایشان را بیرون رانده و سرزمینشان را به قوم اسرائیل داده بود، بخور میسوزاندند. آنها با اعمال زشت خود خشم خداوند را برانگیختند | 11 |
Wakafukiza uvumba kila mahali palipoinuka, kama yalivyofanya yale mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele yao. Wakafanya mambo maovu ambayo yalimghadhibisha Bwana.
و از کلام خداوند که به آنها دستور داده بود که بتها را نپرستند، اطاعت نکردند. | 12 |
Wakaabudu sanamu, ingawa Bwana alikuwa amesema, “Msifanye mambo haya.”
خداوند پیامبران را یکی پس از دیگری فرستاد تا به اسرائیل و یهودا بگویند: «از راههای بد خود برگردید و دستورهای خداوند را که انبیا به اجداد شما دادهاند، اطاعت کنید.» | 13 |
Bwana akawaonya Israeli na Yuda kupitia kwa manabii na waonaji wake wote: “Acheni njia zenu mbaya. Shikeni amri na maagizo yangu, kufuatana na sheria yangu yote niliyowaagiza baba zenu kuitii ambayo niliileta kwenu kupitia kwa watumishi wangu manabii.”
ولی آنها نه فقط اطاعت نمیکردند بلکه مانند اجدادشان که به خداوند، خدای خود ایمان نداشتند، یاغی بودند. | 14 |
Lakini hawakusikiliza, walikuwa na shingo ngumu kama baba zao, ambao hawakumtegemea Bwana Mungu wao.
آنها از دستورهای خدا سرپیچی کردند، عهد او را که با اجدادشان بسته بود، شکستند و به هشدارهای او توجه ننمودند و برخلاف اوامر خداوند، از روی حماقت، بتهای اقوام همسایه را عبادت کردند. | 15 |
Walizikataa amri zake, na agano alilokuwa amelifanya na baba zao, na maonyo aliyokuwa amewapa. Wakafuata sanamu zisizofaa, nao wenyewe wakawa hawafai. Wakayaiga mataifa yaliyowazunguka, ingawa Bwana alikuwa amewaonya akiwaambia, “Msifanye kama wanavyofanya,” nao wakafanya mambo ambayo Bwana alikuwa amewakataza wasifanye.
آنها از تمام دستورهای خداوند، خدای خود سرپیچی نمودند و دو بت گوساله شکل از طلا و بتهای شرمآور دیگر ساختند. بت بعل را پرستش کردند و در مقابل آفتاب و ماه و ستارگان سجده نمودند. | 16 |
Wakayaacha maagizo yote ya Bwana Mungu wao na kujitengenezea sanamu mbili, walizozisubu katika sura ya ndama na nguzo ya Ashera. Wakasujudia mianga yote ya angani, na wakamtumikia Baali.
بر آتش بتکدهها، دختران و پسران خود را قربانی کردند. از فالگیران راهنمایی خواستند، جادوگری کردند و خود را به گناه فروختند. از این رو خداوند بسیار خشمگین شد و آنها را از حضور خود دور انداخت؛ فقط قبیلهٔ یهودا باقی ماند. | 17 |
Wakawatoa kafara wana wao na mabinti zao katika moto. Wakafanya uaguzi na uchawi, nao wakajiuza wenyewe katika kutenda uovu machoni pa Bwana, wakamghadhibisha.
Basi Bwana akawakasirikia sana Israeli na kuwaondoa kwenye uwepo wake. Ni kabila la Yuda tu lililobaki;
اما یهودا نیز دستورهای خداوند، خدای خود را اطاعت نکرد و به همان راههای بدی رفت که اسرائیل رفته بود. | 19 |
na hata hivyo nao Yuda hawakuzishika amri za Bwana Mungu wao. Wakafuata desturi ambazo Israeli walikuwa wamezianzisha.
پس خداوند از تمام بنیاسرائیل دل کند و آنها را به دست دشمن سپرد تا نابود شوند و به سزای اعمال خود برسند. | 20 |
Kwa hiyo Bwana aliwakataa watu wote wa Israeli; akawatesa na kuwaachia katika mikono ya wateka nyara hadi alipowaondoa kutoka kwenye uwepo wake.
وقتی خداوند اسرائیل را از خاندان داوود جدا کرد، مردم اسرائیل یربعام (پسر نباط) را به پادشاهی خود انتخاب کردند. یربعام هم اسرائیل را از پیروی خداوند منحرف کرده، آنها را به گناه بزرگی کشاند. | 21 |
Alipokwisha kuwatenga Israeli mbali na nyumba ya Daudi, wakamfanya Yeroboamu mwana wa Nebati kuwa mfalme wao. Yeroboamu akawashawishi Israeli waache kumfuata Bwana na akawasababisha kutenda dhambi kuu.
اسرائیل از گناهانی که یربعام ایشان را بدان آلوده کرده بود، دست برنداشتند، | 22 |
Nao Israeli wakadumu katika dhambi zote za Yeroboamu mwana wa Nebati, nao hawakuziacha
تا اینکه خداوند همانطور که بهوسیلۀ تمام انبیا خبر داده بود، آنها را از حضور خود دور انداخت. بنابراین مردم اسرائیل به سرزمین آشور تبعید شدند و تا به امروز در آنجا به سر میبرند. | 23 |
hadi Bwana alipowaondoa kutoka kwenye uwepo wake, kama vile alivyokuwa ameonya kupitia watumishi wake wote manabii. Hivyo watu wa Israeli wakaondolewa kutoka nchi yao kwenda uhamishoni Ashuru, nao wako huko mpaka sasa.
پادشاه آشور مردمی از بابِل، کوت، عوا، حمات، سفروایم آورد و آنها را به جای تبعیدیهای اسرائیلی در شهرهای اسرائیل سکونت داد و آنها سامره و سایر شهرهای اسرائیل را اشغال کردند. | 24 |
Mfalme wa Ashuru akawaleta watu kutoka Babeli, Kutha, Ava, Hamathi na Sefarvaimu na kuwaweka katika miji ya Samaria badala ya Waisraeli. Wakaimiliki Samaria na kuishi katika miji yake.
ولی این مردم در ابتدای ورود به سرزمین اسرائیل، خداوند را عبادت نمیکردند؛ پس خداوند شیرهایی به میان آنها فرستاد که بعضی از ایشان را دریدند. | 25 |
Wakati walianza kuishi humo, hawakumwabudu Bwana, kwa hiyo akatuma simba miongoni mwao, wakawaua baadhi ya watu.
به پادشاه آشور خبر رسید که چون ساکنان جدیدِ سرزمین اسرائیل با قوانین خدای آن سرزمین آشنا نیستند، او شیرهایی را به میان آنها فرستاده است تا بدین وسیله آنها را نابود کند. | 26 |
Habari ikapelekwa kwa mfalme wa Ashuru, kusema: “Watu uliowahamisha na kuwaweka katika miji ya Samaria hawajui kile Mungu wa nchi hiyo anachokitaka. Ametuma simba miongoni mwao, ambao wanawaua, kwa sababu watu hawajui anachokitaka.”
پادشاه چنین دستور داد: «یکی از کاهنان تبعیدی سامره به اسرائیل بازگردد و قوانین خدای آن سرزمین را به مردمان تازه وارد آنجا یاد دهد.» | 27 |
Ndipo mfalme wa Ashuru akaamuru hivi: “Mtwae mmoja wa makuhani uliowachukua mateka kutoka Samaria ili arudi kuishi humo na awafundishe watu kile ambacho Mungu wa nchi anataka.”
پس یکی از کاهنان اسرائیلی که از سامره تبعید شده بود به بیتئیل بازگشت و به مردم آنجا یاد داد چگونه خداوند را عبادت کنند. | 28 |
Basi mmoja wa makuhani ambaye alikuwa amepelekwa uhamishoni kutoka Samaria akaja kuishi Betheli na kuwafundisha jinsi ya kumwabudu Bwana.
ولی هر یک از این طوایف بیگانه به پرستش بت خود ادامه دادند. آنها بتهای خود را در معابد بالای تپهها که اسرائیلیها ساخته بودند و در نزدیکی شهرهایشان بود، گذاشتند. | 29 |
Hata hivyo, kila kikundi cha taifa lililoletwa Samaria kilitengeneza miungu yao wenyewe katika miji kadhaa mahali walipoishi, nao wakaiweka mahali pa ibada za miungu ambapo watu wa Samaria walikuwa wametengeneza katika mahali pa juu.
مردمی که از بابِل بودند، بُت سُکّوتبِنوت را عبادت میکردند. آنانی که از کوت بودند، بت نرجل را و اهالی حمات، بت اشیما را میپرستیدند. | 30 |
Watu kutoka Babeli wakamtengeneza Sukoth-Benothi kuwa mungu wao, watu kutoka Kutha wakamtengeneza Nergali, na watu kutoka Hamathi wakamtengeneza Ashima;
پرستندگان بتهای نبحز و ترتاک کسانی بودند که از عوا و سفروایم آمده بودند که حتی فرزندان خود را بر بالای مذبحها برای بتهای ادرملک و عنملک میسوزاندند. | 31 |
Waavi wakatengeneza Nibhazi na Tartaki, nao Wasefarvi wakachoma watoto wao kama kafara kwa Adrameleki na Anameleki, miungu ya Sefarvaimu.
این مردم در ضمن، خداوند را هم عبادت میکردند و از میان خود کاهنانی را انتخاب کردند تا روی مذبحهای بالای تپهها برای خداوند قربانی کنند. | 32 |
Walimwabudu Bwana, lakini pia waliteua aina zote za watu wao ili kuwawakilisha kama makuhani katika mahali pa kuabudia miungu kwenye mahali pa juu pa ibada.
به این ترتیب هم خداوند را میپرستیدند و هم طبق آداب و رسوم کشور خودشان بتهای خود را پرستش میکردند. | 33 |
Walimwabudu Bwana, lakini pia waliitumikia miungu yao kulingana na desturi za mataifa walikotoka.
آنها تا به امروز هم به جای اینکه خداوند را عبادت نمایند و مطیع احکام و دستورهایی باشند که او به فرزندان یعقوب (که خداوند بعد اسمش را اسرائیل گذاشت) داد، مطابق آداب و رسوم گذشتهٔ خود رفتار میکنند. | 34 |
Mpaka leo wanashikilia desturi zao za zamani. Hawamwabudu Bwana wala kuzishika hukumu na maagizo, sheria na amri ambazo Bwana aliwapa uzao wa Yakobo, ambaye alimwita Israeli.
خداوند با قوم اسرائیل عهد بسته، به آنها دستور داده بود که بتهای اقوام خدانشناس را عبادت نکنند، آنها را سجده و پرستش ننمایند و به آنها قربانی تقدیم نکنند، | 35 |
Wakati Bwana alipofanya Agano na Waisraeli, aliwaamuru akisema: “Msiiabudu miungu mingine yoyote wala kuisujudia, wala kuitumikia wala kuitolea dhabihu.
بلکه فقط خداوند را عبادت کنند و او را سجده نمایند و به او قربانی تقدیم کنند، زیرا او بود که با معجزات و قدرت شگفتانگیز، آنها را از مصر بیرون آورد. | 36 |
Bali imewapasa kumwabudu Bwana aliyewapandisha kutoka Misri kwa uwezo wake mkuu na kwa mkono wake ulionyooshwa. Kwake yeye mtasujudu na kwake yeye mtatoa dhabihu.
پس آنها میبایست همواره تمام احکام و دستورهای خداوند را اطاعت کنند و هرگز بت نپرستند. | 37 |
Imewapasa daima kuwa waangalifu kutunza hukumu na maagizo, sheria na amri alizowaandikia. Msiabudu miungu mingine.
زیرا خداوند فرموده بود: «عهدی را که با شما بستم هرگز فراموش نکنید و بتها را نپرستید. | 38 |
Msisahau agano nililofanya nanyi, wala msiabudu miungu mingine.
فقط یهوه خدای خود را عبادت کنید و من شما را از چنگ دشمنانتان نجات خواهم داد.» | 39 |
Bali, mtamwabudu Bwana Mungu wenu, kwani yeye ndiye atakayewakomboa kutoka mikononi mwa adui zenu wote.”
ولی این قومها توجهی به این احکام ننمودند و به پرستش بت ادامه دادند. آنها خداوند را عبادت میکردند و در ضمن از بتپرستی دست نکشیدند و فرزندان آنها نیز تا به امروز به همان شکل عمل میکنند. | 40 |
Hata hivyo hawakusikiliza, lakini waliendelea na desturi zao za awali.
Hata wakati watu hawa walipokuwa wanamwabudu Bwana, walikuwa bado wakitumikia sanamu zao. Mpaka leo watoto wao na watoto wa watoto wao wanaendelea kufanya kama baba zao walivyofanya.