< دوم تواریخ 7 >

وقتی دعای سلیمان به پایان رسید، از آسمان آتشی فرود آمد و قربانیها را سوزانید و حضور پرجلال خداوند عبادتگاه را پر کرد، به طوری که کاهنان نتوانستند داخل خانهٔ خداوند شوند! 1
Baada ya Solomoni kumaliza kuomba, moto ukashuka kutoka mbinguni na kuteketeza sadaka ya kuteketezwa na dhabihu, nao utukufu wa Bwana ukalijaza Hekalu.
2
Makuhani hawakuweza kuingia ndani ya Hekalu la Bwana kwa sababu utukufu wa Bwana ulilijaza.
بنی‌اسرائیل چون این منظره را دیدند بر خاک افتاده، خداوند را به سبب نیکویی و محبت بی‌پایانش سجده و ستایش کردند. 3
Waisraeli wote walipoona moto ukishuka na utukufu wa Bwana ukiwa juu ya Hekalu, wakapiga magoti sakafuni wakasujudu nyuso zao mpaka chini, nao wakamwabudu na kumshukuru Bwana wakisema, “Yeye ni mwema; upendo wake unadumu milele.”
آنگاه پادشاه و همۀ قوم قربانیها به خداوند تقدیم کردند. 4
Ndipo mfalme na watu wote wakatoa dhabihu mbele za Bwana Mungu.
سلیمان پادشاه بیست و دو هزار گاو و صد و بیست هزار گوسفند قربانی کرد. به این ترتیب، پادشاه و همۀ قوم خانۀ خدا را تبرک نمودند. 5
Naye Mfalme Solomoni akatoa dhabihu ya ngʼombe 22,000 pamoja na kondoo na mbuzi 120,000. Hivyo ndivyo mfalme na watu wote walivyoweka wakfu Hekalu la Mungu.
کاهنان سر خدمت بودند و لاویان سرود شکرگزاری می‌خواندند و می‌گفتند: «محبت او بی‌پایان است.» آنها از آلات موسیقی‌ای استفاده می‌کردند که داوود پادشاه ساخته بود و در زمان او برای ستایش خداوند به کار می‌رفت. سپس وقتی کاهنان شیپورها را نواختند، تمام جماعت بر پا ایستادند. 6
Makuhani wakasimama kwenye nafasi zao, vivyo hivyo Walawi wakiwa na vyombo vya uimbaji vya Bwana ambavyo Mfalme Daudi alikuwa ametengeneza kwa ajili ya kumsifu Bwana, navyo vilitumika wakati aliposhukuru, akisema, “Upendo wake wadumu milele.” Mkabala na Walawi, makuhani walipiga tarumbeta zao, nao Waisraeli wote walikuwa wamesimama.
سلیمان آن روز، وسط حیاط خانهٔ خداوند را برای قربانی کردن تقدیس کرد، زیرا مذبح مفرغین گنجایش آن همه قربانیهای سوختنی و هدایای آردی و چربی قربانیهای سلامتی را نداشت. 7
Solomoni akaweka wakfu sehemu ya katikati ya ua uliokuwa mbele ya Hekalu la Bwana na hapo akatoa sadaka za kuteketezwa na mafuta ya sadaka za amani, kwa sababu madhabahu ya shaba aliyokuwa ametengeneza haikutosha kuweka sadaka hizo zote za kuteketezwa, sadaka za nafaka na za mafuta.
سلیمان و تمام مردم اسرائیل، عید خیمه‌ها را تا هفت روز جشن گرفتند. عدهٔ زیادی از گذرگاه حمات تا سرحد مصر آمده بودند تا در این جشن شرکت کنند. 8
Hivyo Solomoni akaiadhimisha sikukuu wakati ule kwa muda wa siku saba, na Israeli wote pamoja naye. Walikuwa kusanyiko kubwa sana, watu kutoka Lebo-Hamathi hadi Kijito cha Misri.
آنها هفت روز برای تبرک مذبح و هفت روز دیگر برای عید خیمه‌ها صرف کردند و در روز آخر، جشن دیگری بر پا داشتند. 9
Katika siku ya nane walifanya kusanyiko, kwa kuwa walikuwa wanaadhimisha kuwekwa wakfu kwa madhabahu kwa muda wa siku saba na sikukuu kwa muda wa siku nyingine saba zaidi.
روز بعد یعنی بیست و سوم ماه هفتم، سلیمان مردم را روانهٔ خانه‌هایشان کرد. آنها برای تمام برکاتی که خداوند به داوود و سلیمان و قوم خود اسرائیل عطا کرده بود، خوشحال بودند. 10
Katika siku ya ishirini na tatu ya mwezi wa saba Solomoni akawaaga watu waende nyumbani mwao, wakishangilia na kufurahi mioyoni mwao, kwa wema mwingi Bwana Mungu aliomtendea Daudi na Solomoni na kwa ajili ya watu wake Israeli.
پس از آنکه سلیمان بنای خانهٔ خداوند و کاخ سلطنتی خود را تمام کرد و تمام طرحهایی را که برای آنها داشت تکمیل نمود، 11
Solomoni alipomaliza kujenga Hekalu la Bwana na jumba la kifalme, naye akiwa amefanikiwa kutenda yale yote aliyokuwa nayo moyoni mwake kufanya katika Hekalu la Bwana na katika jumba lake mwenyewe la kifalme,
یک شب، خداوند بر او ظاهر شد و فرمود: «من دعای تو را مستجاب کرده و این خانه را انتخاب نموده‌ام تا مردم در آنجا برای من قربانی کنند. 12
Bwana akamtokea Solomoni usiku na kumwambia: “Nimesikia maombi yako nami nimechagua mahali hapa kwa ajili yangu mwenyewe kuwa Hekalu kwa ajili ya dhabihu.
هرگاه آسمان را ببندم تا باران نبارد، یا امر کنم که ملخ تمام محصولات زمین را بخورد، و بلا بر قوم خود نازل کنم، 13
“Wakati nitakapofunga mbingu ili isiwepo mvua, au nikiamuru nzige kula mazao ya nchi au nikituma tauni miongoni mwa watu wangu,
اگر قوم من که به اسم من خوانده می‌شوند فروتن شده، دعا کنند و مرا بطلبند و از راههای بد خویش بازگشت نمایند، آنگاه ایشان را از آسمان اجابت نموده، گناهانشان را می‌بخشم و سلامتی را به سرزمین آنها باز می‌گردانم. 14
kama watu wangu, wanaoitwa kwa Jina langu, watajinyenyekesha na kuomba na kuutafuta uso wangu na kuacha njia zao mbaya, basi nitasikia toka mbinguni na kuwasamehe dhambi yao na nitaiponya nchi yao.
از این پس، چشمانم بر این خانه خواهد بود و گوشهایم دعاهایی را که در آنجا کرده می‌شود خواهد شنید، 15
Sasa macho yangu yatafumbuka na masikio yangu yatasikiliza kwa makini maombi yaombwayo mahali hapa.
زیرا این خانه را برگزیده‌ام و آن را تقدیس کرده‌ام تا نام من تا به ابد بر آن باشد. چشم و دل من همیشه بر این خانه خواهد بود. 16
Kwa maana sasa nimechagua na kutakasa Hekalu hili ili kwamba Jina langu lipate kuwa huko milele. Macho yangu na moyo wangu utakuwepo huko daima.
«اگر تو مثل پدرت داوود مرا پیروی کنی و اوامر و احکام مرا نگه داری، 17
“Kwa habari yako wewe, kama ukienenda mbele zangu kama Daudi baba yako alivyoenenda na kufanya yote nikuamuruyo, nawe ukizishika amri zangu na sheria zangu,
آنگاه همان‌طور که به پدرت داوود قول داده‌ام همیشه یک نفر از نسل او بر اسرائیل سلطنت خواهد کرد. 18
Nitakiimarisha kiti chako cha enzi kama nilivyoagana na Daudi baba yako niliposema, ‘Hutakosa kamwe mtu wa kutawala juu ya Israeli.’
«ولی اگر شما از دستورهایی که به شما داده‌ام سرپیچی کنید و از من روی بگردانید و به بت‌پرستی بگرایید، 19
“Lakini kama ukigeuka na kuyaacha maagizo na amri nilizowapa na kwenda kuitumikia miungu mingine na kuiabudu,
آنگاه بنی‌اسرائیل را از این سرزمین که به آنان بخشیده‌ام، بیرون می‌رانم و حتی این خانه را که به نام خود تقدیس نموده‌ام ترک خواهم گفت، به طوری که اسرائیل رسوا شده، زبانزد قومهای دیگر خواهد شد. 20
ndipo nitakapoingʼoa Israeli kutoka nchi yangu niliyowapa, nami nitalikataa Hekalu hili nililolitakasa kwa ajili ya Jina langu. Nitalifanya kitu cha kudharauliwa na kitu cha kudhihakiwa miongoni mwa watu wote.
این خانه که چنین شهرتی دارد با خاک یکسان خواهد گردید، به طوری که هر کس از کنارش بگذرد حیران شده، خواهد پرسید:”چرا خداوند با این سرزمین و این خانه چنین کرده است؟“ 21
Ingawa Hekalu hili linavutia sana sasa, wote watakaolipita watashangaa na kusema, ‘Kwa nini Bwana amefanya kitu kama hiki katika nchi hii na kwa Hekalu hili?’
در جواب خواهند گفت:”چون بنی‌اسرائیل خداوند، خدای اجدادشان را که آنها را از مصر بیرون آورده بود ترک گفته، بت‌پرست شدند، به همین علّت خدا این بلا را بر سر آنها آورده است.“» 22
Watu watajibu, ‘Ni kwa sababu wamemwacha Bwana, Mungu wa baba zao, aliyewatoa Misri, nao wamekumbatia miungu mingine, wakaiabudu na kuitumikia, ndiyo sababu ameyaleta maafa haya yote juu yao.’”

< دوم تواریخ 7 >