< اول تواریخ 7 >
پسران یساکار: تولاع، فوه، یاشوب، شمرون. | 1 |
Wana wa Isakari walikuwa: Tola, Pua, Yashubu na Shimroni; wote ni wanne.
پسران تولاع که هر یک از آنها رئیس یک طایفه بود: عزی، رفایا، یریئیل، یحمای، یبسام و سموئیل. در زمان داوود پادشاه، تعداد کل مردان جنگی این طایفهها ۲۲٬۶۰۰ نفر بود. | 2 |
Wana wa Tola walikuwa: Uzi, Refaya, Yerieli, Yahmai, Ibsamu na Shemueli waliokuwa viongozi wa jamaa zao. Wakati wa utawala wa Mfalme Daudi, wazao wa Tola walioorodheshwa kama wapiganaji katika ukoo wao walikuwa watu 22,600.
یزرحیا پسر عزی بود. یزرحیا و چهار پسرش به نامهای میکائیل، عوبدیا، یوئیل و یشیا، هر یک رئیس طایفهای بودند. | 3 |
Mwana wa Uzi alikuwa: Izrahia. Wana wa Izrahia walikuwa: Mikaeli, Obadia, Yoeli na Ishia. Wote hawa watano walikuwa wakuu wao.
آنها زنان و پسران زیادی داشتند به طوری که توانستند ۳۶٬۰۰۰ مرد برای خدمت سربازی بفرستند. | 4 |
Kulingana na ukoo wa jamaa zao, walikuwa na watu hodari wa vita wapatao 36,000, kwa sababu walikuwa na wanawake na watoto wengi.
تعداد کل مردانی که از قبیلهٔ یساکار برای خدمت سربازی آمادگی داشتند ۸۷٬۰۰۰ جنگجوی زبده بود که نام تمام آنها در نسب نامه نوشته شد. | 5 |
Jamaa ya watu waliokuwa wapiganaji hodari kutoka koo zote za Isakari, kama ilivyoorodheshwa katika ukoo wao, jumla yao walikuwa 87,000.
پسران بنیامین اینها بودند: بالع، باکر و یدیئیل. | 6 |
Wana watatu wa Benyamini walikuwa: Bela, Bekeri na Yediaeli.
پسران بالع: اصبون، عزی، عزیئیل، یریموت، عیری. این پنج نفر رئیس طایفه بودند. تعداد سربازان این طوایف به ۲۲٬۰۳۴ نفر میرسید که نام آنها در نسب نامه نوشته شد. | 7 |
Wana wa Bela walikuwa: Esboni, Uzi, Uzieli, Yeremothi na Iri; walikuwa viongozi wa jamaa zao; wote ni watano. Watu wapiganaji walioorodheshwa katika ukoo wao walikuwa 22,034.
پسران باکر: زمیره، یوعاش، الیعازار، الیوعینای، عمری، یریموت، ابیا، عناتوت و علمت. | 8 |
Wana wa Bekeri walikuwa: Zemira, Yoashi, Eliezeri, Elioenai, Omri, Yeremothi, Abiya, Anathothi na Alemethi. Hawa wote walikuwa wana wa Bekeri.
تعداد سربازان این طایفه به ۲۰٬۲۰۰ نفر میرسید که نام آنها همراه نام رؤسای طوایف در نسب نامه ثبت شد. | 9 |
Orodha ya ukoo wao iliyoandikwa viongozi wa jamaa zao walikuwa wapiganaji 20,200.
بلهان پسر یدیعئیل بود. پسران بلهان اینها بودند: یعیش، بنیامین، ایهود، کنعنه، زیتان، ترشیش و اخیشاحر. | 10 |
Mwana wa Yediaeli alikuwa: Bilhani. Wana wa Bilhani walikuwa: Yeushi, Benyamini, Ehudi, Kenaana, Zethani, Tarshishi na Ahishahari.
اینها رؤسای طوایف یدیعئیل بودند که ۱۷٬۲۰۰ مرد جنگی داشتند. | 11 |
Hawa wana wote wa Yediaeli walikuwa viongozi wa jamaa zao. Kulikuwako wanaume wapiganaji 17,200 waliokuwa tayari kwenda vitani.
شوفیها و حوفیها از نسل عیر بودند و حوشیها از نسل احیر. | 12 |
Washupimu na Wahupimu walikuwa wazao wa Iri. Wahushimu walikuwa wazao wa Aheri.
پسران نفتالی: یحصیئیل، جونی، یصر و شلوم. (اینها نوههای بلهه، کنیز یعقوب بودند.) | 13 |
Wana wa Naftali walikuwa: Yahzieli, Guni, Yeseri na Shalumu; hao walikuwa wazao wa Bilha.
پسران منسی که از کنیز او که ارامی بود، به دنیا آمدند، اسرئیل و ماخیر (پدر جلعاد) بودند. | 14 |
Wana wa Manase walikuwa: Asirieli alikuwa mzao wake kutokana na suria wake wa Kiaramu. Huyu suria akamzaa Makiri baba wa Gileadi.
ماخیر از میان شوفیها و حوفیها برای خود زن گرفت. او خواهری به نام معکه داشت. صلفحاد یکی دیگر از فرزندان منسی بود که فقط چند دختر داشت. | 15 |
Makiri akatwaa mke kutoka miongoni mwa Wahupimu na Washupimu. Jina la dada yake aliitwa Maaka. Mwana wa pili wa Makiri aliitwa Selofehadi, ambaye alikuwa na wasichana tu.
زن ماخیر که او هم معکه نام داشت پسری زایید و نام او را فارش گذاشتند. اسم برادرش شارش بود و پسرانش اولام و راقم نام داشتند. | 16 |
Maaka mkewe Makiri akamzaa mwana aliyemwita Pereshi. Jina la nduguye lilikuwa Shereshi. Wana wa Pereshi walikuwa Ulamu na Rakemu.
بدان پسر اولام بود. اینها پسران جلعاد، نوههای ماخیر و نبیرههای منسی بودند. | 17 |
Mwana wa Ulamu alikuwa: Bedani. Hawa ndio waliokuwa wana wa Gileadi mwana wa Makiri, mwana wa Manase.
همولکه (خواهر جلعاد) سه پسر به دنیا آورد به نامهای: ایشهود، ابیعزر و محله. | 18 |
Dada yake aliyeitwa Hamolekethi aliwazaa Ish-Hodi, Abiezeri na Mahla.
اخیان، شکیم، لقحی، انیعام پسران شمیداع بودند. | 19 |
Wana wa Shemida walikuwa: Ahiani, Shekemu, Liki na Aniamu.
نسل افرایم به ترتیب عبارت بودند از: شوتالح، بارد، تحت، العادا، تحت، زاباد، شوتالح، عازر و العاد. العاد و عازر قصد داشتند گلههای جتیها را که در آن سرزمین ساکن بودند غارت کنند، ولی به دست روستاییهای آنجا کشته شدند. | 20 |
Wana wa Efraimu walikuwa: Shuthela, ambaye alimzaa Beredi, Beredi akamzaa Tahathi, Tahathi akazaa Eleada, Eleada akamzaa Tahathi,
Tahathi akamzaa Zabadi, na Zabadi akamzaa Shuthela. Ezeri na Eleadi waliuawa na wenyeji wa Gathi walipokuwa wamekwenda huko kuwanyangʼanya mifugo yao.
پدرشان افرایم مدت زیادی برای آنها ماتم گرفت و اقوامش به دلداری او آمدند. | 22 |
Baba yao Efraimu akawaombolezea kwa siku nyingi, na jamaa zake wakaja kumfariji.
پس از آن، زن افرایم حامله شده پسری زایید و به یاد آن مصیبت نام او را بریعه (یعنی «فاجعه») گذاشتند. | 23 |
Kisha akakutana kimwili na mke wake tena, naye akachukua mimba, akamzalia mwana. Akamwita Beria, kwa sababu ya misiba iliyoipata nyumba yake.
نام دختر افرایم، شیره بود. شیره، بیتحورون پایین و بالا و اوزین شیره را بنا کرد. | 24 |
Beria alikuwa na binti jina lake Sheera. Huyu ndiye aliijenga miji ya Beth-Horoni ya Juu na Beth-Horoni ya Chini, pamoja na Uzen-Sheera.
افرایم پسر دیگری داشت به نام رافح که نسل او عبارت بودند از: راشف، تالح، تاحن، | 25 |
Beria akamzaa pia Refa, naye Refa akamzaa Reshefu, Reshefu akamzaa Tela, Tela akamzaa Tahani,
لعدان، عمیهود، الیشمع، | 26 |
Tahani akamzaa Ladani, Ladani akamzaa Amihudi, Amihudi akamzaa Elishama,
Elishama akamzaa Nuni, Nuni akamzaa Yoshua.
ناحیهای که آنها در آن زندگی میکردند شامل بیتئیل و روستاهای اطرافش بود که از طرف شرق تا نعران و از سمت غرب تا جازر و روستاهای حوالی آن امتداد مییافت. شهرهای دیگر این ناحیه شکیم و ایه با دهکدههای اطراف آنها بودند. | 28 |
Nchi zao na makazi yao yalijumuisha Betheli na vijiji vilivyouzunguka, Naarani ilikuwa upande wa mashariki, Gezeri pamoja na vijiji vyake upande wa magharibi, pia Shekemu na vijiji vyake hadi kufikia Aya na vijiji vyake.
قبیلهٔ منسی که از نسل یوسف پسر یعقوب بودند، شهرهای زیر و نواحی اطراف آنها را در اختیار داشتند: بیتشان، تعناک، مجدو و دُر. | 29 |
Katika mipaka ya Manase walikuwepo Beth-Shani, Taanaki, Megido na Dori pamoja na vijiji vyake. Wana wa Yosefu mwana wa Israeli waliishi katika miji hii.
پسران اشیر عبارت بودند از: یمنه، یشوه، یشوی و بریعه. اشیر دختری به نام سارح نیز داشت. | 30 |
Wana wa Asheri walikuwa: Imna, Ishva, Ishvi na Beria. Dada yao alikuwa Sera.
پسران بریعه عبارت بودند از: حابر و ملکیئیل (پدر برزاوت). | 31 |
Wana wa Beria walikuwa: Heberi na Malkieli, aliyekuwa baba yake Birzaithi.
پسران حابر عبارت بودند از: یفلیط، شومیر و حوتام. حابر دختری به نام شوعا نیز داشت. | 32 |
Heberi akawazaa Yafleti, Shomeri na Hothamu, na Shua dada yao.
پسران یفلیط عبارت بودند از: فاسک، بمهال و عشوت. | 33 |
Wana wa Yafleti walikuwa: Pasaki, Bimhali na Ashvathi. Hawa walikuwa wana wa Yafleti.
پسران شومیر برادر یفلیط اینها بودند: روهجه، یحبه و ارام. | 34 |
Wana wa Shemeri walikuwa: Ahi, Roga, Yehuba na Aramu.
پسران برادر او هیلام عبارت بودند از: صوفح، یمناع، شالش و عامال. | 35 |
Wana wa Helemu ndugu yake walikuwa: Sofa, Imna, Sheleshi na Amali.
پسران صوفح عبارت بودند از: سوح، حرنفر، شوعال، بیری، یمره، | 36 |
Wana wa Sofa walikuwa: Sua, Harneferi, Shuali, Beri, Imra,
باصر، هود، شما، شلشه، یتران و بئیرا. | 37 |
Bezeri, Hodu, Shama, Shilsha, Ithrani na Beera.
پسران یتر عبارت بودند از: یفنه، فسفا و آرا. | 38 |
Wana wa Yetheri walikuwa: Yefune, Pispa na Ara.
پسران علا عبارت بودند از: آرح، حنیئیل و رصیا. | 39 |
Wana wa Ula walikuwa: Ara, Hanieli na Risia.
همهٔ فرزندان اشیر که سران طایفهها بودند، جنگاورانی کارآزموده و رهبرانی برجسته محسوب میشدند. تعداد مردان جنگی این طایفه که در نسب نامه ثبت گردید ۲۶٬۰۰۰ نفر بود. | 40 |
Hawa wote ndio waliokuwa wazao wa Asheri, viongozi wa jamaa zao, watu bora, mashujaa walio hodari na viongozi maarufu. Idadi ya watu waliokuwa tayari kwa vita, kama ilivyoorodheshwa katika ukoo wao, walikuwa 26,000.