< اول تواریخ 15 >

داوود برای خود چند کاخ سلطنتی در شهرش ساخت و یک خیمهٔ تازه هم برای صندوق عهد خدا درست کرد. 1
Baada ya Daudi kujijengea nyumba zake katika Mji wa Daudi, akatengeneza sehemu kwa ajili ya Sanduku la Mungu, kisha akasimamisha hema kwa ajili yake.
آنگاه چنین دستور داد: «کسی غیر از لاویان نباید صندوق عهد را بردارد، چون خداوند ایشان را برای همین منظور انتخاب کرده است. آنها خدمتگزاران همیشگی او هستند.» 2
Kisha Daudi akasema, “Hakuna mtu yeyote anayeruhusiwa kulibeba Sanduku la Mungu isipokuwa Walawi peke yao, kwa sababu Bwana aliwachagua kulibeba Sanduku la Bwana na kuhudumu mbele zake milele.”
پس داوود تمام قوم اسرائیل را به شهر اورشلیم احضار نمود تا در مراسم انتقال صندوق عهد به خیمهٔ جدید شرکت کنند. 3
Daudi akawakusanya Israeli wote huko Yerusalemu ili kulipandisha Sanduku la Bwana na kulileta hadi kwenye sehemu aliyokuwa ametengeneza kwa ajili yake.
این است تعداد کاهنان نسل هارون و لاویانی که در اورشلیم حاضر شدند: ‏ ۱۲۰ نفر از طایفهٔ قهات به سرپرستی اوری‌ئیل؛ ‏ ۲۲۰ نفر از طایفهٔ مراری به سرپرستی عسایا؛ ‏ ۱۳۰ نفر از طایفهٔ جرشوم به سرپرستی یوئیل؛ ‏ ۲۰۰ نفر از خاندان الیصافان به سرپرستی شمعیا؛ ‏ ۸۰ نفر از خاندان حبرون به سرپرستی ایلی‌ئیل؛ ‏ ۱۱۲ نفر از خاندان عزی‌ئیل به سرپرستی عمیناداب. 4
Kisha Daudi akawakusanya pamoja wazao wa Aroni na Walawi:
5
Kutoka wazao wa Kohathi, Urieli kiongozi na ndugu zake 120,
6
Kutoka wazao wa Merari, Asaya kiongozi na ndugu zake 220.
7
Kutoka wazao wa Gershoni, Yoeli kiongozi na ndugu zake 130.
8
Kutoka wazao wa Elisafani, Shemaya kiongozi na ndugu zake 200.
9
Kutoka wazao wa Hebroni, Elieli kiongozi na ndugu zake 80.
10
Kutoka wazao wa Uzieli, Aminadabu kiongozi na ndugu zake 112.
سپس داوود صادوق و اَبیّاتار کاهنان اعظم و اوری‌ئیل، عسایا، یوئیل، شمعیا، ایلی‌ئیل و عمیناداب رهبران لاویان را به حضور خواست 11
Kisha Daudi akawaita makuhani Sadoki na Abiathari, pamoja na Walawi Urieli, Asaya, Yoeli, Shemaya, Elieli na Aminadabu.
و به ایشان گفت: «شما سران طایفه‌های لاویان هستید؛ پس خود را با سایر برادران تقدیس کنید تا صندوق عهد خداوند، خدای اسرائیل را به خیمه‌ای که برایش آماده کرده‌ام بیاورید. 12
Akawaambia, “Ninyi ndio viongozi wa jamaa za Walawi. Ninyi pamoja na Walawi wenzenu inawapasa mjitakase na kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli hadi mahali ambapo nimetengeneza kwa ajili yake.
دفعهٔ پیش به سبب اینکه شما لاویان آن را حمل نکردید و این برخلاف دستور خدا بود خداوند ما را تنبیه کرد.» 13
Ilikuwa ni kwa sababu hii, ninyi Walawi, hamkulipandisha Sanduku la Bwana mara ya kwanza, hata ikasababisha Bwana Mungu wetu kuwaka hasira dhidi yetu. Hatukumuuliza jinsi ya kufanya ili tupate kulileta jinsi alivyoagiza.”
پس کاهنان و لاویان خود را تقدیس کردند تا صندوق عهد خداوند، خدای اسرائیل را به محل جدید بیاورند. 14
Kwa hiyo makuhani pamoja na Walawi wakajitakasa ili kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli.
آنگاه لاویان، همان‌طور که خداوند به موسی فرموده بود، چوبهای حامل صندوق عهد را روی دوش خود گذاشتند و آن را حمل نمودند. 15
Nao Walawi wakalichukua Sanduku la Mungu mabegani mwao wakitumia mipiko, kama vile Mose alivyoamuru sawasawa na neno la Bwana.
داوود به رهبران لاویان دستور داد که از میان لاویان دستهٔ موسیقی تشکیل دهند تا عود و بربط و سنج بنوازند و با صدای بلند و شاد سرود بخوانند. 16
Daudi akawaambia viongozi wa Walawi kuwaweka ndugu zao waimbaji ili waimbe nyimbo za shangwe, wakiwa na vyombo vya uimbaji: zeze, vinubi na matoazi.
رهبران، این افراد را تعیین کردند تا سنجهای مفرغین بنوازند: هیمان (پسر یوئیل)، آساف (پسر برکیا) و ایتان (پسر قوشیا) از طایفهٔ مراری. برای کمک به ایشان این افراد نیز تعیین شدند تا با نواختن عود ایشان را همراهی کنند: زکریا، بین، یعزی‌ئیل، شمیراموت، یحی‌ئیل، عونی، الی‌آب، بنایا و معسیا. برای نواختن بربط نیز اشخاص زیر انتخاب شدند: مَتّیتیا، الیفلیا، مقنیا، عزریا و همچنین عوبید ادوم و یعی‌ئیل که هر دو از نگهبانان خیمه بودند. 17
Basi Walawi wakawaweka Hemani mwana wa Yoeli; kutoka miongoni mwa ndugu zake, Asafu mwana wa Berekia; kutoka miongoni mwa ndugu zao Wamerari, Ethani mwana wa Kushaiya;
18
hawa ndio waliochaguliwa kuwa wasaidizi wao: Zekaria, Yaazieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Benaya, Maaseya, Matithia, Elifelehu, Mikneya, pamoja na mabawabu Obed-Edomu na Yehieli.
19
Waimbaji Hemani, Asafu na Ethani walichaguliwa kupiga matoazi ya shaba;
20
Zekaria, Azieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Maaseya na Benaya walikuwa wapiga zeze kufuatana na sauti ya alamothi,
21
na Matithia, Elifelehu, Mikneya, Obed-Edomu, Yehieli na Azazia walikuwa wapiga vinubi, wakiongozwa kwa kufuata sauti ya sheminithi.
رهبر سرایندگان کننیا رئیس لاویان بود که به خاطر مهارتش انتخاب شد. 22
Kenania kiongozi wa Walawi alikuwa msimamizi wa uimbaji; huu ndio uliokuwa wajibu wake kwa sababu alikuwa stadi katika hilo.
برکیا و القانه محافظ صندوق عهد بودند. 23
Berekia na Elikana walikuwa mabawabu kwa ajili ya Sanduku.
شبنیا، یوشافاط، نتن‌ئیل، عماسای، زکریا، بنایا و الیعزر که همه کاهن بودند، پیشاپیش صندوق عهد شیپور می‌نواختند. عوبید ادوم و یحیی از صندوق عهد مواظبت می‌کردند. 24
Shebania, Yoshafati, Nethaneli, Amasai, Zekaria, Benaya na Eliezeri, makuhani, walikuwa wapiga tarumbeta mbele ya Sanduku la Mungu. Obed-Edomu na Yehiya waliwekwa pia kuwa mabawabu wa Sanduku.
آنگاه داوود و بزرگان اسرائیل و سرداران سپاه با شادی فراوان به خانهٔ عوبید ادوم رفتند تا صندوق عهد را به اورشلیم بیاورند. 25
Basi Daudi pamoja na wazee wa Israeli na majemadari wa vikosi vya elfu wakaenda ili kulipandisha Sanduku la Agano la Bwana kutoka nyumba ya Obed-Edomu kwa shangwe.
آنها هفت گاو و هفت قوچ قربانی کردند، زیرا خدا لاویان را کمک کرد تا صندوق عهد را بتوانند حمل کنند. 26
Kwa sababu Mungu alikuwa amewasaidia Walawi waliokuwa wanalichukua Sanduku la Agano la Bwana, mafahali saba na kondoo dume saba walitolewa dhabihu.
داوود و لاویانی که صندوق عهد را حمل می‌کردند، سرایندگان و کننیا رهبر سرایندگان، همه لباسهایی از کتان لطیف پوشیده بودند. داوود نیز لباس مخصوص کاهنان را بر تن کرده بود. 27
Basi Daudi alikuwa amevaa joho la kitani safi, kama walivyokuwa wamevaa Walawi wote waliokuwa wanalichukua lile Sanduku, waimbaji nao walivaa vivyo hivyo, pamoja na Kenania aliyekuwa anaongoza nyimbo za waimbaji. Daudi alivaa pia kisibau cha kitani safi.
به این ترتیب بنی‌اسرائیل با هلهله و شادی و صدای سرنا و شیپور، سنج و عود و بربط، صندوق عهد را به اورشلیم آوردند. 28
Hivyo Israeli wote wakalipandisha Sanduku la Agano la Bwana kwa shangwe, wakipiga pembe za kondoo dume, tarumbeta, matoazi, wakipiga zeze na vinubi.
هنگامی که صندوق عهد خداوند وارد اورشلیم شد، میکال زن داوود که دختر شائول پادشاه بود، از پنجره نگاه می‌کرد. وقتی داوود را دید که با شادی می‌رقصد در دل خود او را تحقیر کرد. 29
Sanduku la Agano la Bwana lilipokuwa linaingia katika Mji wa Daudi, Mikali binti Sauli akachungulia dirishani. Naye alipomwona Mfalme Daudi akicheza na kusherehekea, akamdharau moyoni mwake.

< اول تواریخ 15 >