< مزامیر 78 >
قصیده آساف ای قوم من شریعت مرا بشنوید! گوشهای خود را به سخنان دهانم فراگیرید! | ۱ 1 |
Utenzi wa Asafu. Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
دهان خود را به مثل باز خواهم کرد به چیزهایی که از بنای عالم مخفی بود تنطق خواهم نمود. | ۲ 2 |
Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo, nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:
که آنها را شنیده و دانستهایم و پدران مابرای ما بیان کردهاند. | ۳ 3 |
yale ambayo tuliyasikia na kuyajua, yale ambayo baba zetu walituambia.
از فرزندان ایشان آنها راپنهان نخواهیم کرد. تسبیحات خداوند را برای نسل آینده بیان میکنیم و قوت او و اعمال عجیبی را که او کرده است. | ۴ 4 |
Hatutayaficha kwa watoto wao; tutakiambia kizazi kijacho matendo yastahiliyo sifa ya Bwana, uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.
زیرا که شهادتی دریعقوب برپا داشت و شریعتی در اسرائیل قرار دادو پدران ما را امر فرمود که آنها را به فرزندان خودتعلیم دهند؛ | ۵ 5 |
Aliagiza amri kwa Yakobo na akaweka sheria katika Israeli, ambazo aliwaamuru baba zetu wawafundishe watoto wao,
تا نسل آینده آنها را بدانند وفرزندانی که میبایست مولود شوند تا ایشان برخیزند و آنها را به فرزندان خود بیان نمایند؛ | ۶ 6 |
ili kizazi kijacho kizijue, pamoja na watoto ambao watazaliwa, nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.
و ایشان به خدا توکل نمایند و اعمال خدا رافراموش نکنند بلکه احکام او را نگاه دارند. | ۷ 7 |
Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu, nao wasingesahau matendo yake, bali wangalizishika amri zake.
ومثل پدران خود نسلی گردن کش و فتنه انگیزنشوند، نسلی که دل خود را راست نساختند وروح ایشان بسوی خدا امین نبود. | ۸ 8 |
Ili wasifanane na baba zao, waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi, ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake, ambao roho zao hazikumwamini.
بنی افرایم که مسلح و کمان کش بودند، درروز جنگ رو برتافتند. | ۹ 9 |
Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde, walikimbia siku ya vita.
عهد خدا را نگاه نداشتند و از سلوک به شریعت او ابا نمودند، | ۱۰ 10 |
Hawakulishika agano la Mungu na walikataa kuishi kwa sheria yake.
واعمال و عجایب او را فراموش کردند که آنها رابدیشان ظاهر کرده بود، | ۱۱ 11 |
Walisahau aliyokuwa ameyatenda, maajabu aliyokuwa amewaonyesha.
و در نظر پدران ایشان اعمال عجیب کرده بود، در زمین مصر و در دیارصوعن. | ۱۲ 12 |
Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
دریا را منشق ساخته، ایشان را عبورداد و آبها را مثل توده برپا نمود. | ۱۳ 13 |
Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
و ایشان را درروز به ابر راهنمایی کرد و تمامی شب به نورآتش. | ۱۴ 14 |
Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
در صحرا صخرهها را بشکافت و ایشان را گویا از لجه های عظیم نوشانید. | ۱۵ 15 |
Alipasua miamba jangwani na akawapa maji tele kama bahari,
پس سیلها رااز صخره بیرون آورد و آب را مثل نهرها جاری ساخت. | ۱۶ 16 |
alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.
و بار دیگر بر او گناه ورزیدند و برحضرت اعلی در صحرا فتنه انگیختند، | ۱۷ 17 |
Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
و دردلهای خود خدا را امتحان کردند، چونکه برای شهوات خود غذا خواستند. | ۱۸ 18 |
Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.
و برضد خداتکلم کرده، گفتند: «آیا خدا میتواند در صحراسفرهای حاضر کند؟ | ۱۹ 19 |
Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
اینک صخره را زد و آبهاروان شد و وادیها جاری گشت. آیا میتواند نان رانیز بدهد. و گوشت را برای قوم خود حاضرسازد؟» | ۲۰ 20 |
Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
پس خدا این را شنیده، غضبناک شد و آتش در یعقوب افروخته گشت و خشم بر اسرائیل مشتعل گردید. | ۲۱ 21 |
Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
زیرا به خدا ایمان نیاوردند و به نجات او اعتماد ننمودند. | ۲۲ 22 |
kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
پس ابرها را از بالاامر فرمود و درهای آسمان را گشود | ۲۳ 23 |
Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
و من را برایشان بارانید تا بخورند و غله آسمان را بدیشان بخشید. | ۲۴ 24 |
akawanyeshea mana ili watu wale; aliwapa nafaka ya mbinguni.
مردمان، نان زورآوران را خوردند وآذوقهای برای ایشان فرستاد تا سیر شوند. | ۲۵ 25 |
Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
بادشرقی را در آسمان وزانید و به قوت خود، بادجنوبی را آورد، | ۲۶ 26 |
Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
و گوشت را برای ایشان مثل غبار بارانید و مرغان بالدار را مثل ریگ دریا. | ۲۷ 27 |
Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, ndege warukao kama mchanga wa pwani.
وآن را در میان اردوی ایشان فرود آورد، گرداگردمسکن های ایشان. | ۲۸ 28 |
Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
پس خوردند و نیکو سیرشدند و موافق شهوات ایشان بدیشان داد. | ۲۹ 29 |
Walikula na kusaza, kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
ایشان از شهوت خود دست نکشیدند. و غذاهنوز در دهان ایشان بود | ۳۰ 30 |
Kabla hawajamaliza kula walichokitamani, hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,
که غضب خدا برایشان افروخته شده؛ تنومندان ایشان را بکشت وجوانان اسرائیل را هلاک ساخت. | ۳۱ 31 |
hasira ya Mungu ikawaka juu yao, akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao, akiwaangusha vijana wa Israeli.
با وجود این همه، باز گناه ورزیدند و به اعمال عجیب او ایمان نیاوردند. | ۳۲ 32 |
Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi, licha ya maajabu yake, hawakuamini.
بنابراین، روزهای ایشان را در بطالت تمام کرد و سالهای ایشان را درترس. | ۳۳ 33 |
Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili na miaka yao katika vitisho.
هنگامی که ایشان را کشت اورا طلبیدند و بازگشت کرده، درباره خدا تفحص نمودند، | ۳۴ 34 |
Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta, walimgeukia tena kwa shauku.
و به یاد آوردند که خدا صخره ایشان، و خدای تعالی ولی ایشان است. | ۳۵ 35 |
Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao, kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao.
اما به دهان خود او را تملق نمودند و به زبان خویش به اودروغ گفتند. | ۳۶ 36 |
Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, wakisema uongo kwa ndimi zao,
زیرا که دل ایشان با او راست نبودو به عهد وی موتمن نبودند. | ۳۷ 37 |
mioyo yao haikuwa thabiti kwake, wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
اما او به حسب رحمانیتش گناه ایشان راعفو نموده، ایشان را هلاک نساخت بلکه بارهاغضب خود را برگردانیده، تمامی خشم خویش را برنینگیخت. | ۳۸ 38 |
Hata hivyo alikuwa na huruma, alisamehe maovu yao na hakuwaangamiza. Mara kwa mara alizuia hasira yake, wala hakuchochea ghadhabu yake yote.
و به یاد آورد که ایشان بشرند، بادی که میرود و بر نمی گردد. | ۳۹ 39 |
Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu, upepo upitao ambao haurudi.
چند مرتبه درصحرا بدو فتنه انگیختند و او را در بادیه رنجانیدند. | ۴۰ 40 |
Mara ngapi walimwasi jangwani na kumhuzunisha nyikani!
و برگشته، خدا را امتحان کردند وقدوس اسرائیل را اهانت نمودند، | ۴۱ 41 |
Walimjaribu Mungu mara kwa mara, wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
و قوت او رابهخاطر نداشتند، روزی که ایشان را از دشمن رهانیده بود. | ۴۲ 42 |
Hawakukumbuka uwezo wake, siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,
که چگونه آیات خود را در مصرظاهر ساخت و معجزات خود را در دیار صوعن. | ۴۳ 43 |
siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri, maajabu yake huko Soani.
و نهرهای ایشان را به خون مبدل نمود ورودهای ایشان را تا نتوانستند نوشید. | ۴۴ 44 |
Aligeuza mito yao kuwa damu, hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.
انواع پشهها در میان ایشان فرستاد که ایشان را گزیدند وغوکهایی که ایشان را تباه نمودند؛ | ۴۵ 45 |
Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala, na vyura wakawaharibu.
و محصول ایشان را به کرم صد پا سپرد و عمل ایشان را به ملخ داد. | ۴۶ 46 |
Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao, mazao yao kwa nzige.
تاکستان ایشان را به تگرگ خراب کردو درختان جمیز ایشان را به تگرگهای درشت. | ۴۷ 47 |
Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.
بهایم ایشان را به تگرگ سپرد و مواشی ایشان را به شعله های برق. | ۴۸ 48 |
Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe, akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.
و آتش خشم خود را برایشان فرستاد، غضب و غیظ و ضیق را، به فرستادن فرشتگان شریر. | ۴۹ 49 |
Aliwafungulia hasira yake kali, ghadhabu yake, hasira na uadui, na kundi la malaika wa kuharibu.
و راهی برای غضب خود مهیا ساخته، جان ایشان را از موت نگاه نداشت، بلکه جان ایشان را به وبا تسلیم نمود. | ۵۰ 50 |
Aliitengenezea njia hasira yake, hakuwaepusha na kifo, bali aliwaachia tauni.
و همه نخست زادگان مصر را کشت، اوایل قوت ایشان را در خیمه های حام. | ۵۱ 51 |
Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.
و قوم خود را مثل گوسفندان کوچانید وایشان را در صحرا مثل گله راهنمایی نمود. | ۵۲ 52 |
Lakini aliwatoa watu wake kama kundi, akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani.
وایشان را در امنیت رهبری کرد تا نترسند و دریادشمنان ایشان را پوشانید. | ۵۳ 53 |
Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa, bali bahari iliwameza adui zao.
و ایشان را به حدودمقدس خود آورد، بدین کوهی که بهدست راست خود تحصیل کرده بود. | ۵۴ 54 |
Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu, hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa.
و امتها را از حضورایشان راند و میراث را برای ایشان به ریسمان تقسیم کرد و اسباط اسرائیل را در خیمه های ایشان ساکن گردانید. | ۵۵ 55 |
Aliyafukuza mataifa mbele yao, na kuwagawia nchi zao kama urithi, aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.
لیکن خدای تعالی را امتحان کرده، بدو فتنه انگیختند و شهادات او را نگاه نداشتند. | ۵۶ 56 |
Lakini wao walimjaribu Mungu, na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana, wala hawakuzishika sheria zake.
وبرگشته، مثل پدران خود خیانت ورزیدند و مثل کمان خطا کننده منحرف شدند. | ۵۷ 57 |
Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu, wakawa wasioweza kutegemewa kama upinde wenye kasoro.
و به مقامهای بلند خود خشم او را به هیجان آوردند و به بتهای خویش غیرت او را جنبش دادند. | ۵۸ 58 |
Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.
چون خدااین را بشنید غضبناک گردید و اسرائیل را به شدت مکروه داشت. | ۵۹ 59 |
Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.
پس مسکن شیلو را ترک نمود، آن خیمهای را که در میان آدمیان برپاساخته بود، | ۶۰ 60 |
Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
و (تابوت ) قوت خود را به اسیری داد و جمال خویش را بهدست دشمن سپرد، | ۶۱ 61 |
Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
وقوم خود را به شمشیر تسلیم نمود و با میراث خود غضبناک گردید. | ۶۲ 62 |
Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
جوانان ایشان را آتش سوزانید و برای دوشیزگان ایشان سرود نکاح نشد. | ۶۳ 63 |
Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
کاهنان ایشان به دم شمشیر افتادند وبیوه های ایشان نوحه گری ننمودند. | ۶۴ 64 |
makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
آنگاه خداوند مثل کسیکه خوابیده بودبیدار شد، مثل جباری که از شراب میخروشد، | ۶۵ 65 |
Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini, kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.
و دشمنان خود را به عقب زد و ایشان را عارابدی گردانید. | ۶۶ 66 |
Aliwapiga na kuwashinda adui zake, akawatia katika aibu ya milele.
و خیمه یوسف را رد نموده، سبط افرایم را برنگزید. | ۶۷ 67 |
Ndipo alipozikataa hema za Yosefu, hakulichagua kabila la Efraimu,
لیکن سبط یهودا رابرگزید و این کوه صهیون را که دوست میداشت. | ۶۸ 68 |
lakini alilichagua kabila la Yuda, Mlima Sayuni, ambao aliupenda.
و قدس خود را مثل کوههای بلند بنا کرد، مثل جهان که آن را تا ابدالاباد بنیاد نهاد. | ۶۹ 69 |
Alijenga patakatifu pake kama vilele, kama dunia ambayo aliimarisha milele.
و بنده خود داود را برگزید و او را از آغلهای گوسفندان گرفت. | ۷۰ 70 |
Akamchagua Daudi mtumishi wake na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.
از عقب میشهای شیرده او را آورد تاقوم او یعقوب و میراث او اسرائیل را رعایت کند. | ۷۱ 71 |
Kutoka kuchunga kondoo alimleta kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo, wa Israeli urithi wake.
پس ایشان را به حسب کمال دل خود رعایت نمود و ایشان را به مهارت دستهای خویش هدایت کرد. | ۷۲ 72 |
Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo, kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.