< اعداد 1 >
و در روز اول ماه دوم از سال دوم از بیرون آمدن ایشان از زمین مصر، خداوند دربیابان سینا در خیمه اجتماع موسی را خطاب کرده، گفت: | ۱ 1 |
Bwana alisema na Mose katika Jangwa la Sinai, katika Hema la Kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Akamwambia,
«حساب تمامی جماعت بنیاسرائیل را برحسب قبایل و خاندان آبای ایشان، به شماره اسم های همه ذکوران موافق سرهای ایشان بگیرید. | ۲ 2 |
“Hesabu watu wa jumuiya yote ya Waisraeli kwa kufuata koo zao na jamaa zao, ukiorodhesha kila mwanaume kwa jina lake, mmoja mmoja.
از بیست ساله و زیاده، هرکه از اسرائیل به جنگ بیرون میرود، تو وهارون ایشان را برحسب افواج ایشان بشمارید. | ۳ 3 |
Wewe na Aroni mtawahesabu kwa migawanyo yao wanaume wote katika Israeli wenye miaka ishirini na kuendelea ambao wanaweza kutumika katika jeshi.
و همراه شما یک نفر از هر سبط باشد که هر یک رئیس خاندان آبایش باشد. | ۴ 4 |
Mwanaume mmoja kutoka kila kabila, kila aliye kiongozi wa jamaa yake, atawasaidia.
و اسم های کسانی که با شما باید بایستند، این است: از روبین، الیصوربن شدیئور. | ۵ 5 |
Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia: “kutoka Reubeni, ni Elisuri mwana wa Shedeuri;
و از شمعون، شلومیئیل بن صوریشدای. | ۶ 6 |
kutoka Simeoni, ni Shelumieli mwana wa Surishadai;
و از یهودا، نحشون بن عمیناداب. | ۷ 7 |
kutoka Yuda, ni Nashoni mwana wa Aminadabu;
و از یساکار، نتنائیل بن صوغر. | ۸ 8 |
kutoka Isakari, ni Nethaneli mwana wa Suari;
و از زبولون، الیاب بن حیلون. | ۹ 9 |
kutoka Zabuloni, ni Eliabu mwana wa Heloni;
و از بنی یوسف: از افرایم، الیشمع بن عمیهود. و از منسی، جملیئیل بن فدهصور. | ۱۰ 10 |
kutoka wana wa Yosefu: kutoka Efraimu, ni Elishama mwana wa Amihudi; kutoka Manase, ni Gamalieli mwana wa Pedasuri;
از بنیامین، ابیدان بن جدعونی. | ۱۱ 11 |
kutoka Benyamini, ni Abidani mwana wa Gideoni;
و از دان، اخیعزر بن عمیشدای. | ۱۲ 12 |
kutoka Dani, ni Ahiezeri mwana wa Amishadai;
و از اشیر، فجعیئیل بن عکران. | ۱۳ 13 |
kutoka Asheri, ni Pagieli mwana wa Okrani;
و از جاد، الیاساف بن دعوئیل. | ۱۴ 14 |
kutoka Gadi, ni Eliasafu mwana wa Deueli;
و از نفتالی، اخیرع بن عینان.» | ۱۵ 15 |
kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”
اینانند دعوتشدگان جماعت و سروران اسباط آبای ایشان، و روسای هزاره های اسرائیل. | ۱۶ 16 |
Hawa walikuwa wanaume walioteuliwa kutoka jumuiya, viongozi wa makabila ya baba zao. Walikuwa wakuu wa koo za Israeli.
و موسی و هارون این کسان را که به نام، معین شدند، گرفتند. | ۱۷ 17 |
Mose na Aroni wakawachukua wanaume hao waliokuwa wamepewa majina yao,
و در روز اول ماه دوم، تمامی جماعت را جمع کرده، نسب نامه های ایشان را برحسب قبایل و خاندان آبای ایشان، به شماره اسمها از بیست ساله و بالاتر موافق سرهای ایشان خواندند. | ۱۸ 18 |
wakaita jumuiya yote pamoja katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Watu wakaonyesha nasaba zao kwa koo zao na jamaa zao, nao wanaume waliokuwa na miaka ishirini au zaidi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja,
چنانکه خداوندموسی را امر فرموده بود، ایشان را در بیابان سینابشمرد. | ۱۹ 19 |
kama Bwana alivyomwagiza Mose. Hivyo aliwahesabu katika Jangwa la Sinai:
و اما انساب بنی روبین نخست زاده اسرائیل، برحسب قبایل و خاندان آبای ایشان، موافق نامها و سرهای ایشان این بود: هر ذکور ازبیست ساله و بالاتر، جمیع کسانی که برای جنگ بیرون میرفتند. | ۲۰ 20 |
Kutoka wazao wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
شمرده شدگان ایشان از سبطروبین، چهل و شش هزار و پانصد نفر بودند. | ۲۱ 21 |
Idadi kutoka kabila la Reubeni ilikuwa watu 46,500.
و انساب بنی شمعون برحسب قبایل وخاندان آبای ایشان، کسانی که از ایشان شمرده شدند، موافق شماره اسمها و سرهای ایشان این بود: هر ذکور از بیست ساله و بالاتر، هرکه برای جنگ بیرون میرفت. | ۲۲ 22 |
Kutoka wazao wa Simeoni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi walihesabiwa na kuorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
شمرده شدگان ایشان ازسبط شمعون، پنجاه و نه هزار و سیصد نفر بودند. | ۲۳ 23 |
Idadi kutoka kabila la Simeoni walikuwa watu 59,300.
و انساب بنی جاد برحسب قبایل و خاندان آبای ایشان، موافق شماره اسمها، از بیست ساله وبالاتر، هرکه برای جنگ بیرون میرفت. | ۲۴ 24 |
Kutoka wazao wa Gadi: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
شمرده شدگان ایشان از سبط جاد، چهل و پنج هزار و ششصد و پنجاه نفر بودند. | ۲۵ 25 |
Idadi kutoka kabila la Gadi walikuwa watu 45,650.
و انساب بنی یهودا برحسب قبایل وخاندان آبای ایشان، موافق شماره اسمها ازبیست ساله و بالاتر، هرکه برای جنگ بیرون میرفت. | ۲۶ 26 |
Kutoka wazao wa Yuda: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
شمرده شدگان ایشان از سبط یهودا، هفتاد و چهار هزار و شش صد نفر بودند. | ۲۷ 27 |
Idadi kutoka kabila la Yuda walikuwa watu 74,600.
و انساب بنی یساکار برحسب قبایل وخاندان آبای ایشان، موافق شماره اسمها ازبیست ساله و بالاتر، هرکه برای جنگ بیرون میرفت. | ۲۸ 28 |
Kutoka wazao wa Isakari: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
شمرده شدگان ایشان از سبط یساکار، پنجاه و چهار هزار و چهارصد نفر بودند. | ۲۹ 29 |
Idadi kutoka kabila la Isakari walikuwa watu 54,400.
و انساب بنی زبولون برحسب قبایل وخاندان آبای ایشان، موافق شماره اسمها ازبیست ساله و بالاتر، هرکه برای جنگ بیرون میرفت. | ۳۰ 30 |
Kutoka wazao wa Zabuloni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
شمرده شدگان ایشان از سبط زبولون پنجاه و هفت هزار و چهارصد نفر بودند. | ۳۱ 31 |
Idadi kutoka kabila la Zabuloni walikuwa watu 57,400.
و انساب بنی یوسف از بنی افرایم برحسب قبایل و خاندان آبای ایشان، موافق شماره اسم هااز بیست ساله و بالاتر، هرکه برای جنگ بیرون میرفت. | ۳۲ 32 |
Kutoka wana wa Yosefu: Kutoka wazao wa Efraimu: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
شمرده شدگان ایشان از سبط افرایم، چهل هزار و پانصد نفر بودند. | ۳۳ 33 |
Idadi kutoka kabila la Efraimu walikuwa watu 40,500.
و انساب بنی منسی برحسب قبایل وخاندان آبای ایشان، موافق شماره اسمها، ازبیست ساله و بالاتر، هرکه برای جنگ بیرون میرفت. | ۳۴ 34 |
Kutoka wazao wa Manase: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
شمرده شدگان ایشان از سبط منسی، سی و دو هزار و دویست نفر بودند. | ۳۵ 35 |
Idadi kutoka kabila la Manase walikuwa watu 32,200.
و انساب بنی بنیامین برحسب قبایل وخاندان آبای ایشان، موافق شماره اسمها، ازبیست ساله بالاتر، هرکه برای جنگ بیرون میرفت. | ۳۶ 36 |
Kutoka wazao wa Benyamini: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
شمرده شدگان ایشان از سبط بنیامین، سی و پنج هزار و چهارصد نفر بودند. | ۳۷ 37 |
Idadi kutoka kabila la Benyamini walikuwa watu 35,400.
و انساب بنی دان برحسب قبایل و خاندان آبای ایشان، موافق شماره اسمها از بیست ساله وبالاتر، هرکه برای جنگ میرفت. | ۳۸ 38 |
Kutoka wazao wa Dani: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
شمرده شدگان ایشان از سبط دان، شصت و دو هزار و هفتصد نفر بودند. | ۳۹ 39 |
Idadi kutoka kabila la Dani walikuwa watu 62,700.
و انساب بنی اشیر برحسب قبایل و خاندان آبای ایشان، موافق شماره اسمها از بیست ساله وبالاتر، هرکه برای جنگ بیرون میرفت. | ۴۰ 40 |
Kutoka wazao wa Asheri: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
شمرده شدگان ایشان از سبط اشیر، چهل ویک هزار و پانصد نفر بودند. | ۴۱ 41 |
Idadi kutoka kabila la Asheri walikuwa watu 41,500.
و انساب بنی نفتالی برحسب قبایل وخاندان آبای ایشان، موافق شماره اسمها ازبیست ساله و بالاتر، هرکه برای جنگ بیرون میرفت. | ۴۲ 42 |
Kutoka wazao wa Naftali: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
شمرده شدگان ایشان از سبط نفتالی، پنجاه و سه هزار و پانصد نفر بودند. | ۴۳ 43 |
Idadi kutoka kabila la Naftali walikuwa watu 53,400.
اینانند شمرده شدگانی که موسی و هارون با دوازده نفر از سروران اسرائیل، که یک نفر برای هر خاندان آبای ایشان بود، شمردند. | ۴۴ 44 |
Hawa walikuwa wanaume waliohesabiwa na Mose, Aroni na viongozi kumi na wawili wa Israeli, kila mmoja akiwakilisha jamaa yake.
و تمامی شمرده شدگان بنیاسرائیل برحسب خاندان آبای ایشان، از بیست ساله و بالاتر، هر کس از اسرائیل که برای جنگ بیرون میرفت. | ۴۵ 45 |
Wanaume wote Waisraeli waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi la Israeli walihesabiwa kufuatana na jamaa zao.
همه شمرده شدگان، ششصد و سه هزار و پانصد وپنجاه نفر بودند. | ۴۶ 46 |
Jumla ya hesabu yao ilikuwa watu 603,550.
اما لاویان برحسب سبط آبای ایشان در میان آنها شمرده نشدند. | ۴۷ 47 |
Hata hivyo, jamaa ya kabila la Lawi hawakuhesabiwa pamoja na wengine.
زیرا خداوند موسی را خطاب کرده، گفت: | ۴۸ 48 |
Bwana alikuwa amemwambia Mose:
«اما سبط لاوی را مشمار و حساب ایشان را درمیان بنیاسرائیل مگیر. | ۴۹ 49 |
“Kamwe usihesabu kabila la Lawi wala kuwaweka pamoja katika hesabu ya Waisraeli wengine.
لیکن لاویان را برمسکن شهادت و تمامی اسبابش و بر هرچه علاقه به آن دارد بگمار، و ایشان مسکن و تمامی اسبابش را بردارند، و ایشان آن را خدمت نمایندو به اطراف مسکن خیمه زنند. | ۵۰ 50 |
Badala yake, waweke Walawi kuwa viongozi wa Maskani ya Ushuhuda, juu ya samani zake na kila kitu kilichomo ndani yake. Wao watabeba Maskani na samani zake zote; wataitunza na kupiga kambi kuizunguka.
و چون مسکن روانه شود لاویان آن را پایین بیاورند، و چون مسکن افراشته شود لاویان آن را برپا نمایند، وغریبی که نزدیک آن آید، کشته شود. | ۵۱ 51 |
Wakati wowote Maskani inapohamishwa, Walawi wataifungua, na wakati wowote maskani inapotakiwa kusimamishwa, Walawi watafanya kazi hiyo. Mtu yeyote mwingine ambaye atasogea karibu nayo atauawa.
و بنیاسرائیل هر کس در محله خود و هر کس نزدعلم خویش برحسب افواج خود، خیمه زنند. | ۵۲ 52 |
Waisraeli watapiga mahema yao kwa makundi makundi, kila mwanaume katika kambi yake mwenyewe chini ya bendera yake.
و لاویان به اطراف مسکن شهادت خیمه زنند، مبادا غضب بر جماعت بنیاسرائیل بشود، ولاویان شعائر مسکن شهادت را نگاه دارند.» | ۵۳ 53 |
Hata hivyo, Walawi watapiga mahema yao kuzunguka Maskani ya Ushuhuda ili ghadhabu isiipate jumuiya ya Waisraeli. Walawi watawajibika kwa utunzaji wa Maskani ya Ushuhuda.”
پس بنیاسرائیل چنین کردند، و برحسب آنچه خداوند موسی را امر فرموده بود، به عمل آوردند. | ۵۴ 54 |
Waisraeli walifanya yote haya sawasawa kama Bwana alivyomwamuru Mose.