< لاویان 16 >
و خداوند موسی را بعد از مردن دو پسرهارون، وقتی که نزد خداوند آمدند ومردند خطاب کرده، گفت: | ۱ 1 |
Bwana akasema na Mose baada ya kifo cha wale wana wawili wa Aroni waliokufa walipokaribia mbele za Bwana.
«پس خداوند به موسی گفت: برادر خود هارون را بگو که به قدس درون حجاب پیش کرسی رحمت که بر تابوت است همه وقت داخل نشود، مبادا بمیرد، زیرا که در ابر بر کرسی رحمت ظاهر خواهم شد. | ۲ 2 |
Bwana akamwambia Mose: “Mwambie ndugu yako Aroni asije wakati wowote atakavyo yeye ndani ya Patakatifu pa Patakatifu, nyuma ya pazia pale mbele ya kiti cha rehema kile kilichoko juu ya Sanduku la Agano, la sivyo atakufa, kwa sababu huwa ninatokea ndani ya wingu juu ya kile kiti cha rehema.
و بااین چیزها هارون داخل قدس بشود، با گوسالهای برای قربانی گناه، و قوچی برای قربانی سوختنی. | ۳ 3 |
“Hivi ndivyo Aroni atakavyoingia katika mahali patakatifu: atachukua fahali mchanga kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa.
و پیراهن کتان مقدس را بپوشد، و زیر جامه کتان بر بدنش باشد، و به کمربند کتان بسته شود، و به عمامه کتان معمم باشد. اینها رخت مقدس است. پس بدن خود را به آب غسل داده، آنها را بپوشد. | ۴ 4 |
Atavaa koti takatifu la kitani, pamoja na nguo za ndani za kitani; atafunga mshipi wa kitani kiunoni, na kuvaa kilemba cha kitani. Haya ni mavazi matakatifu, kwa hiyo ni lazima aoge kwa maji kabla ya kuyavaa mavazi hayo.
و از جماعت بنیاسرائیل دو بز نرینه برای قربانی گناه، و یک قوچ برای قربانی سوختنی بگیرد. | ۵ 5 |
Atachukua mbuzi dume wawili kutoka kwa jumuiya ya Israeli kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa.
و هارون گوساله قربانی گناه را که برای خود اوست بگذراند، و برای خود و اهل خانه خود کفاره نماید. | ۶ 6 |
“Aroni atamtoa huyo fahali kwa ajili ya sadaka yake ya dhambi ili afanye upatanisho kwa ajili yake mwenyewe na nyumba yake.
و دو بز را بگیرد و آنها را به حضور خداوند به در خیمه اجتماع حاضر سازد. | ۷ 7 |
Kisha atawachukua wale mbuzi dume wawili na kuwaleta mbele za Bwana kwenye ingilio la Hema la Kukutania.
و هارون بر آن دو بز قرعه اندازد، یک قرعه برای خداوند و یک قرعه برای عزازیل. | ۸ 8 |
Aroni atapiga kura kwa ajili ya hao mbuzi wawili, mmoja kwa ajili ya Bwana na mwingine kwa ajili ya kubebeshwa dhambi.
و هارون بزی را که قرعه برای خداوند بر آن برآمد نزدیک بیاورد، و بجهت قربانی گناه بگذراند. | ۹ 9 |
Aroni atamleta yule mbuzi ambaye kura ya Bwana imemwangukia na kumtoa dhabihu kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
و بزی که قرعه برای عزازیل بر آن برآمد به حضور خداوندزنده حاضر شود، و بر آن کفاره نماید و آن را برای عزازیل به صحرا بفرستد. | ۱۰ 10 |
Lakini mbuzi aliyechaguliwa kwa kura kuwa wa kubebeshwa dhambi atatolewa akiwa hai mbele za Bwana, atumike kwa kufanya upatanisho kwa kumwacha aende jangwani akiwa amebebeshwa dhambi.
«و هارون گاو قربانی گناه را که برای خوداوست نزدیک بیاورد، و برای خود و اهل خانه خود کفاره نماید، و گاو قربانی گناه را که برای خود اوست ذبح کند. | ۱۱ 11 |
“Aroni atamleta yule fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi yake mwenyewe, ili kufanya upatanisho kwa ajili yake na nyumba yake, naye atamchinja huyo fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi yake mwenyewe.
و مجمری پر از زغال آتش از روی مذبح که به حضور خداوند است ودو مشت پر از بخور معطر کوبیده شده برداشته، به اندرون حجاب بیاورد. | ۱۲ 12 |
Atachukua chetezo kilichojaa makaa yanayowaka kutoka madhabahuni mbele za Bwana, na konzi mbili za uvumba laini uliosagwa vizuri wenye harufu, na kuvipeleka nyuma ya pazia.
و بخور را بر آتش به حضور خداوند بنهد تا ابر بخور کرسی رحمت راکه بر تابوت شهادت است بپوشاند، مبادا بمیرد. | ۱۳ 13 |
Ataweka uvumba juu ya moto mbele za Bwana, na moshi wa uvumba utafunika kile kiti cha rehema kilicho juu ya Ushuhuda, ili asife.
و از خون گاو گرفته، بر کرسی رحمت به انگشت خود به طرف مشرق بپاشد، و قدری ازخون را پیش روی کرسی رحمت هفت مرتبه بپاشد. | ۱۴ 14 |
Atachukua sehemu ya damu ya fahali, na kwa kidole chake atanyunyiza sehemu ya mbele ya kiti cha rehema; kisha atanyunyiza sehemu ya hiyo damu kwa kidole chake mara saba mbele ya kiti cha rehema.
پس بز قربانی گناه را که برای قوم است ذبح نماید، و خونش را به اندرون حجاب بیاورد، وبا خونش چنانکه با خون گاو عمل کرده بودعمل کند، و آن را بر کرسی رحمت و پیش روی کرسی رحمت بپاشد. | ۱۵ 15 |
“Kisha atamchinja mbuzi wa sadaka ya dhambi kwa ajili ya watu, na kuichukua damu yake nyuma ya pazia, na aifanyie kama alivyofanya kwa damu ya fahali: Atanyunyiza juu ya kiti cha rehema na mbele yake.
و برای قدس کفاره نماید بهسبب نجاسات بنیاسرائیل، و بهسبب تقصیرهای ایشان با تمامی گناهان ایشان، و برای خیمه اجتماع که با ایشان در میان نجاسات ایشان ساکن است، همچنین بکند. | ۱۶ 16 |
Kwa njia hii atafanya upatanisho kwa ajili ya Patakatifu pa Patakatifu kwa sababu ya unajisi na uasi wa Waisraeli, kwa dhambi zao zozote. Atafanya hivyo kwa ajili ya Hema la Kukutania, ambalo liko miongoni mwao katikati ya unajisi wao.
و هیچکس درخیمه اجتماع نباشد، و از وقتی که برای کردن کفاره داخل قدس بشود تا وقتی که بیرون آید، پس برای خود و برای اهل خانه خود و برای تمامی جماعت اسرائیل کفاره خواهد کرد. | ۱۷ 17 |
Mtu yeyote haruhusiwi kuwa ndani ya Hema la Kukutania, kuanzia wakati Aroni anapoingia kufanya upatanisho katika Patakatifu pa Patakatifu, hadi atakapotoka nje, baada ya kujifanyia upatanisho yeye mwenyewe na nyumba yake, pamoja na jumuiya yote ya Israeli.
پس نزد مذبح که به حضور خداوند است بیرون آید، و برای آن کفاره نماید، و از خون گاو و ازخون بز گرفته، آن را بر شاخه های مذبح بهر طرف بپاشد. | ۱۸ 18 |
“Kisha atatoka aje kwenye madhabahu yaliyo mbele za Bwana na kufanya upatanisho kwa ajili yake. Atachukua sehemu ya damu ya fahali na sehemu ya damu ya mbuzi, na kuiweka kwenye pembe za madhabahu.
و قدری از خون را به انگشت خود هفت مرتبه بر آن بپاشد و آن را تطهیر کند، و آن رااز نجاسات بنیاسرائیل تقدیس نماید. | ۱۹ 19 |
Atanyunyiza baadhi ya hiyo damu juu ya madhabahu kwa kidole chake mara saba, ili kuitakasa na kuiweka wakfu kutokana na unajisi wa Waisraeli.
«و چون از کفاره نمودن برای قدس و برای خیمه اجتماع و برای مذبح فارغ شود، آنگاه بززنده را نزدیک بیاورد. | ۲۰ 20 |
“Aroni atakapokuwa amemaliza kufanya upatanisho kwa ajili ya Patakatifu pa Patakatifu, Hema la Kukutania na madhabahu, atamleta mbele yule mbuzi aliye hai.
و هارون دو دست خودرا بر سر بز زنده بنهد، و همه خطایای بنیاسرائیل و همه تقصیرهای ایشان را با همه گناهان ایشان اعتراف نماید، و آنها را بر سر بز بگذارد و آن را بهدست شخص حاضر به صحرا بفرستد. | ۲۱ 21 |
Aroni ataweka mikono yake miwili juu ya kichwa cha mbuzi aliye hai na kuungama juu yake uovu wote na uasi wa Waisraeli, yaani dhambi zao zote, ili kuziweka juu ya kichwa cha huyo mbuzi. Atamwachia huyo mbuzi akimbilie jangwani kwa uangalizi wa mtu aliyepewa wajibu huo.
و بزهمه گناهان ایشان را به زمین ویران بر خودخواهد برد. پس بز را به صحرا رها کند. | ۲۲ 22 |
Yule mbuzi atachukua juu yake dhambi zao zote mpaka mahali pasipo na watu; naye yule mtu atamwachia akimbilie jangwani.
وهارون به خیمه اجتماع داخل شود، و رخت کتان را که در وقت داخل شدن به قدس پوشیده بودبیرون کرده، آنها را در آنجا بگذارد. | ۲۳ 23 |
“Kisha Aroni ataenda ndani ya Hema la Kukutania na kuvua yale mavazi ya kitani aliyoyavaa kabla ya kuingia katika Patakatifu pa Patakatifu, naye atayaacha pale.
و بدن خود را در جای مقدس به آب غسل دهد، ورخت خود را پوشیده، بیرون آید، و قربانی سوختنی خود و قربانی سوختنی قوم را بگذراند، و برای خود و برای قوم کفاره نماید. | ۲۴ 24 |
Ataoga kwa maji katika mahali patakatifu na kuvaa mavazi yake ya kawaida. Kisha atatoka na kutoa dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa kwa ajili yake na sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya watu, ili kufanya upatanisho kwa ajili yake mwenyewe, na kwa ajili ya watu.
و پیه قربانی گناه را بر مذبح بسوزاند. | ۲۵ 25 |
Pia atachoma mafuta ya mnyama wa sadaka ya dhambi juu ya madhabahu.
و آنکه بز رابرای عزازیل رها کرد رخت خود را بشوید و بدن خود را به آب غسل دهد، و بعد از آن به لشکرگاه داخل شود. | ۲۶ 26 |
“Yule mtu anayemwachia yule mbuzi wa kubebeshwa dhambi ni lazima afue nguo zake na kuoga kwa maji; baadaye anaweza kuingia kambini.
و گاو قربانی گناه و بز قربانی گناه را که خون آنها به قدس برای کردن کفاره آورده شد، بیرون لشکرگاه برده شود، و پوست و گوشت و سرگین آنها را به آتش بسوزانند. | ۲۷ 27 |
Yule fahali na mbuzi waliotolewa kwa ajili ya sadaka za dhambi, ambao damu yao ilikuwa imeletwa Patakatifu pa Patakatifu kwa ajili ya kufanya upatanisho, ni lazima watolewe nje ya kambi. Ngozi zao, nyama, na matumbo pamoja na mavi vitateketezwa kwa moto.
و آنکه آنهارا سوزانید رخت خود را بشوید و بدن خود را به آب غسل دهد، و بعد از آن به لشکرگاه داخل شود. | ۲۸ 28 |
Mtu atakayevichoma ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji; baadaye ataweza kuingia kambini.
«و این برای شما فریضه دائمی باشد، که درروز دهم از ماه هفتم جانهای خود را ذلیل سازید، و هیچ کار مکنید، خواه متوطن خواه غریبی که درمیان شما ماوا گزیده باشد. | ۲۹ 29 |
“Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yenu: Katika siku ya kumi ya mwezi wa saba ni lazima mfunge, wala msifanye kazi yoyote, iwe mzawa au mgeni anayeishi miongoni mwenu,
زیرا که در آن روزکفاره برای تطهیر شما کرده خواهد شد، و ازجمیع گناهان خود به حضور خداوند طاهرخواهید شد. | ۳۰ 30 |
kwa sababu siku hii upatanisho utafanyika kwa ajili yenu ili kuwatakasa. Kisha mtakuwa safi mbele za Bwana kutokana na dhambi zenu zote.
این سبت آرامی برای شماست، پس جانهای خود را ذلیل سازید. این است فریضه دائمی. | ۳۱ 31 |
Ni Sabato ya mapumziko, na lazima mfunge; ni agizo la kudumu.
و کاهنی که مسح شده، و تخصیص شده باشد، تا در جای پدر خود کهانت نمایدکفاره را بنماید. و رختهای کتان یعنی رختهای مقدس را بپوشد. | ۳۲ 32 |
Kuhani ambaye ametiwa mafuta na kuwekwa wakfu ili kuingia mahali pa baba yake kama kuhani mkuu atafanya upatanisho. Atavaa mavazi matakatifu ya kitani,
و برای قدس مقدس کفاره نماید، و برای خیمه اجتماع و مذبح کفاره نماید، و برای کهنه و تمامی جماعت قوم کفاره نماید. | ۳۳ 33 |
na kufanya upatanisho kwa ajili ya Patakatifu pa Patakatifu, Hema la Kukutania na madhabahu, na pia kwa ajili ya makuhani, pamoja na jumuiya yote ya watu.
و این برای شما فریضه دائمی خواهد بود تابرای بنیاسرائیل از تمامی گناهان ایشان یک مرتبه هر سال کفاره شود.» پس چنانکه خداوندموسی را امر فرمود، همچنان بعمل آورد. | ۳۴ 34 |
“Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yenu: Upatanisho utafanywa mara moja tu kwa mwaka kwa ajili ya dhambi zote za Waisraeli.” Ndivyo ilivyofanyika, kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.