< یوحنا 7 >

و بعد از آن عیسی در جلیل می‌گشت زیرانمی خواست در یهودیه راه رود چونکه یهودیان قصد قتل او می‌داشتند. ۱ 1
Na baada ya mambo haya Yesu alisafiri hivi katika Galilaya, kwa sababu hakupenda kwenda Uyahudi kwa sababu wayahudi walikuwa wakifanya mipango ya kumwua.
و عید یهود که عید خیمه‌ها باشد نزدیک بود. ۲ 2
Sasa sikukuu ya Wayahudi, sikukuu ya Vibanda, ilikuwa karibu.
پس برادرانش بدو گفتند: «از اینجا روانه شده، به یهودیه برو تاشاگردانت نیز آن اعمالی را که تو می‌کنی ببینند، ۳ 3
Ndipo ndugu zake walipomwambia, “Ondoka mahali hapa uende Uyahudi, ili kwamba wanafunzi wako vile vile wayaone matendo ufanyayo.
زیرا هر‌که می‌خواهد آشکار شود در پنهانی کارنمی کند. پس اگر این کارها را می‌کنی خود را به جهان بنما.» ۴ 4
Hakuna afanyaye lolote kwa siri iwapo yeye mwenyewe anataka kujulikana wazi. Iwapo unafanya mambo haya, jionyeshe mwenyewe kwa ulimwengu.”
زیرا که برادرانش نیز به او ایمان نیاورده بودند. ۵ 5
Hata ndugu zake pia hawakumwamini.
آنگاه عیسی بدیشان گفت: «وقت من هنوز نرسیده، اما وقت شما همیشه حاضراست. ۶ 6
Ndipo Yesu alipowaambia, “Wakati wangu haujafika bado, lakini wakati wenu kila mara uko tayari.
جهان نمی تواند شما را دشمن دارد ولیکن مرا دشمن می‌دارد زیرا که من بر آن شهادت می‌دهم که اعمالش بد است. ۷ 7
Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi, bali unanichukia mimi kwa sababu ninaushuhudia kuwa matendo yake ni maovu.
شما برای این عیدبروید. من حال به این عید نمی آیم زیرا که وقت من هنوز تمام نشده است.» ۸ 8
Pandeni kwenda katika sikukuu; mimi siendi katika sikukuu hii kwa sababu muda wangu haujakamilika bado.”
چون این را بدیشان گفت، در جلیل توقف نمود. ۹ 9
Baada ya kusema mambo hayo kwao, alibaki Galilaya.
لیکن چون برادرانش برای عید رفته بودند، او نیز آمد، نه آشکار بلکه در خفا. ۱۰ 10
Hata hivyo, ndugu zake walipokuwa wamekwenda katika sikukuu, ndipo naye alienda, siyo kwa wazi bali kwa siri.
اما یهودیان در عید او را جستجو نموده، می‌گفتند که او کجااست. ۱۱ 11
Wayahudi walikuwa wakimtafuta katika sikukuu na kusema, “Yuko wapi?”
و در میان مردم درباره او همهمه بسیاربود. بعضی می‌گفتند که مردی نیکو است ودیگران می‌گفتند نی بلکه گمراه‌کننده قوم است. ۱۲ 12
Kulikuwa na majadiliano mengi miongoni mwa makutano juu yake. Wengine walisema, “Ni mtu mwema.” Wengine walisema, “Hapana, huwapotosha makutano.”
و لیکن بسبب ترس از یهود، هیچ‌کس درباره اوظاهر حرف نمی زد. ۱۳ 13
Hata hivyo hakuna aliyezungumza wazi juu yake kwa kuwaogopa Wayahudi.
و چون نصف عید گذشته بود، عیسی به هیکل آمده، تعلیم می‌داد. ۱۴ 14
Wakati sikukuu ilipofika katikati, Yesu alipanda kwenda Hekaluni na kuanza kufundisha.
و یهودیان تعجب نموده، گفتند: «این شخص هرگز تعلیم نیافته، چگونه کتب را می‌داند؟» ۱۵ 15
Wayahudi walikuwa wakishangaa na kusema, “Kwa jinsi gani mtu huyu anajua mambo mengi? Hajasoma kamwe.”
عیسی در جواب ایشان گفت: «تعلیم من از من نیست، بلکه ازفرستنده من. ۱۶ 16
Yesu akawajibu na kuwaambia, “Mafundisho yangu siyo yangu, bali ni yake yeye aliyenituma.
اگر کسی بخواهد اراده او را به عمل آرد، درباره تعلیم خواهد دانست که از خدااست یا آنکه من از خود سخن می‌رانم. ۱۷ 17
Iwapo yeyote atapenda kufanya mapenzi yake yeye, atajua kuhusu mafundisho haya, kama yanatoka kwa Mungu, au kama ninazungumza kutoka kwangu mwenyewe.
هر‌که ازخود سخن گوید، جلال خود را طالب بود و اماهر‌که طالب جلال فرستنده خود باشد، او صادق است و در او ناراستی نیست. ۱۸ 18
Kila anayezungumza yatokayo kwake mwenywe hutafuta utukufu wake, bali kila atafutaye utukufu wake yeye aliyemtuma, mtu huyo ni wa kweli, na ndani yake hakuna kutotenda haki.
آیا موسی تورات را به شما نداده است؟ و حال آنکه کسی از شما نیست که به تورات عمل کند. از برای چه می‌خواهید مرا به قتل رسانید؟» ۱۹ 19
Musa hakuwapa nyinyi sheria? Lakini hakuna hata mmoja kati yenu atendaye sheria. Kwa nini mnataka kuniua?
آنگاه همه درجواب گفتند: «تو دیو داری. که اراده دارد تو رابکشد؟» ۲۰ 20
Makutano wakajibu, “Una pepo. Nani anataka kukuua?”
عیسی در جواب ایشان گفت: «یک عمل نمودم وهمه شما از آن متعجب شدید. ۲۱ 21
Yesu akajibu na akawaambia, “Nimetenda kazi moja, nanyi nyote mmeshangazwa kwa sababu yake.
موسی ختنه را به شما داد نه آنکه از موسی باشد بلکه از اجداد و در روز سبت مردم را ختنه می‌کنید. ۲۲ 22
Musa aliwapa tohara (siyo kwamba inatoka kwa Musa, bali ile inatoka kwa mababa), na katika Sabato mnamtahili mtu.
پس اگر کسی در روز سبت مختون شود تا شریعت موسی شکسته نشود، چرا بر من خشم می‌آورید از آن سبب که در روز سبت شخصی را شفای کامل دادم؟ ۲۳ 23
Iwapo mtu atapokea tohara katika siku ya Sabato ili kwamba sheria ya Musa isivunjwe, kwa nini mnanikasirikia mimi kwa sababu nimemfanya mtu kuwa mzima kabisa katika Sabato?
بحسب ظاهرداوری مکنید بلکه به راستی داوری نمایید.» ۲۴ 24
Msihukumu kulingana na mwonekano, bali hukumuni kwa haki.
پس بعضی از اهل اورشلیم گفتند: «آیا این آن نیست که قصد قتل او دارند؟ ۲۵ 25
Baadhi yao kutoka Yerusalemu wakasema, “Siye huyu wanayemtafuta kumwua?
و اینک آشکارا حرف می‌زند و بدو هیچ نمی گویند. آیاروسا یقین می‌دانند که او در حقیقت مسیح است؟ ۲۶ 26
Na tazama, anaongea wazi wazi, na hawasemi chochote juu yake. Haiwezi ikawa kwamba viongozi wanajua kweli kuwa huyu ni Kristo, inaweza kuwa?
لیکن این شخص را می‌دانیم از کجا است، امامسیح چون آید هیچ‌کس نمی شناسد که از کجااست.» ۲۷ 27
Tunajua huyu mtu anatokea wapi. Kristo atakapokuja, hata hivyo, hakuna atakayejua wapi anakotoka.”
و عیسی چون در هیکل تعلیم می‌داد، ندا کرده، گفت: «مرا می‌شناسید و نیز می‌دانید ازکجا هستم و از خود نیامده‌ام بلکه فرستنده من حق است که شما او را نمی شناسید. ۲۸ 28
Yesu alikuwa akipaza sauti yake hekaluni, akifundisha na kusema, “Ninyi nyote mnanijua mimi na mnajua nitokako. Sikuja kwa nafsi yangu, bali yeye aliyenituma ni wa kweli, na hamumjui yeye.
اما من اورا می‌شناسم زیرا که از او هستم و او مرا فرستاده است.» ۲۹ 29
Ninamjua yeye kwa sababu nimetoka kwake na alinituma.”
آنگاه خواستند او را گرفتار کنند ولیکن کسی بر او دست نینداخت زیرا که ساعت او هنوزنرسیده بود. ۳۰ 30
Walikuwa wanajaribu kumkamata, lakini hakuna hata mmoja aliyeinua mkono wake juu yake kwa sababu saa yake ilikuwa bado haijafika.
آنگاه بسیاری از آن گروه بدوایمان آوردند و گفتند: «آیا چون مسیح آید، معجزات بیشتر از اینها که این شخص می‌نماید، خواهد نمود؟» ۳۱ 31
Hata hivyo, wengi katika makutano walimwamini. Walisema, “Kristo atakapokuja, atafanya ishara nyingi kuliko alizofanya mtu huyu?”
چون فریسیان شنیدند که خلق درباره اواین همهمه می‌کنند، فریسیان و روسای کهنه خادمان فرستادند تا او را بگیرند. ۳۲ 32
Mafarisayo waliwasikia makutano wakinong'onezana mambo haya kuhusu Yesu, na wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakatuma maafisa ili kumkamata.
آنگاه عیسی گفت: «اندک زمانی دیگر با شما هستم، بعد نزدفرستنده خود می‌روم. ۳۳ 33
Ndipo Yesu aliposema, “Bado kuna muda kitambo niko pamoja nanyi, na baadaye nitakwenda kwake yeye aliyenituma.
و مرا طلب خواهید کردو نخواهید یافت و آنجایی که من هستم شمانمی توانید آمد.» ۳۴ 34
Mtanitafuta wala hamtaniona; kule niendako, hamtaweza kuja.”
پس یهودیان با یکدیگرگفتند: «او کجا می‌خواهد برود که ما او رانمی یابیم؟ آیا اراده دارد به سوی پراکندگان یونانیان رود و یونانیان را تعلیم دهد؟ ۳۵ 35
Kwa hiyo Wayahudi wakasemezana wao kwa wao, “Mtu huyu atakwenda wapi kwamba tusiweze kumuona? Ataenda kwa Waliotawanyika kati ya Wayunani na kuwafundisha Wayunani?
این چه کلامی است که گفت مرا طلب خواهید کرد ونخواهید یافت و جایی که من هستم شمانمی توانید آمد؟» ۳۶ 36
Ni neno gani hili alilolisema, 'Mtanitafuta wala hamtaniona; kule niendako hamtamweza kuja'?”
و در روز آخر که روز بزرگ عید بود، عیسی ایستاده، ندا کرد و گفت: «هر‌که تشنه باشدنزد من آید و بنوشد. ۳۷ 37
Sasa katika siku ya mwisho, siku kubwa ya sikukuu, Yesu alisimama akapaza sauti, akisema, “Ikiwa yeyote ana kiu, na aje kwangu anywe.
کسی‌که به من ایمان آورد، چنانکه کتاب می‌گوید، از بطن او نهرهای آب زنده جاری خواهد شد.» ۳۸ 38
Yeye aniaminiye mimi, kama maandiko yalivyosema, kutoka ndani yake itatiririka mito ya maji ya uzima.”
اما این را گفت درباره روح که هر‌که به او ایمان آرد او را خواهدیافت زیرا که روح‌القدس هنوز عطا نشده بود، چونکه عیسی تا به حال جلال نیافته بود. ۳۹ 39
Lakini aliyasema haya kuhusu Roho, ambaye wao wamwaminio watampokea; Roho alikuwa bado hajatolewa kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa bado.
آنگاه بسیاری از آن گروه، چون این کلام راشنیدند، گفتند: «در حقیقت این شخص همان نبی است.» ۴۰ 40
Baadhi ya makutano, waliposikia maneno haya, walisema, “Kweli huyu ni nabii.”
و بعضی گفتند: «او مسیح است.» وبعضی گفتند: «مگر مسیح از جلیل خواهد آمد؟ ۴۱ 41
Wengine walisema, “Huyu ni Kristo.” Lakini wengine walisema, “nini, Kristo aweza kutoka Galilaya?
آیا کتاب نگفته است که از نسل داود و ازبیت لحم، دهی که داود در آن بود، مسیح ظاهر خواهد شد؟» ۴۲ 42
Maandiko hayajasema kuwa Kristo atatokea katika ukoo wa Daudi na kutoka Bethlehemu, kijiji ambacho Daudi alikuwa?
پس درباره او در میان مردم اختلاف افتاد. ۴۳ 43
Hivyo, pale ukainuka mgawanyiko katikati ya makutano kwa ajili yake.
و بعضی از ایشان خواستند او رابگیرند و لکن هیچ‌کس بر او دست نینداخت. ۴۴ 44
Wengine kati yao wangelimkamata, lakini hakuna aliyenyoosha mikono yake juu yake.
پس خادمان نزد روسای کهنه و فریسیان آمدند. آنها بدیشان گفتند: «برای چه او رانیاوردید؟» ۴۵ 45
Ndipo wale maofisa wakarudi kwa wakuu wa makuhani na Mafarisayo, nao wakawaambia, “Kwa nini hamjamleta?”
خادمان در جواب گفتند: «هرگزکسی مثل این شخص سخن نگفته است!» ۴۶ 46
Maofisa wakajibu, “Hakuna mtu aliyewahi kuzungumza kama huyu kabla.”
آنگاه فریسیان در جواب ایشان گفتند: «آیاشما نیز گمراه شده‌اید؟ ۴۷ 47
Ndipo Mafarisayo walipowajibu, “Na nyinyi pia mmepotoshwa?
مگر کسی از سرداران یا از فریسیان به او ایمان آورده است؟ ۴۸ 48
Kuna yeyote kati ya watawala anayemwamini, au yeyote wa Mafarisayo?
ولیکن این گروه که شریعت را نمی دانند، ملعون می‌باشند.» ۴۹ 49
Bali hawa makutano wasiojua sheria - wamelaaniwa.”
نیقودیموس، آنکه در شب نزد اوآمده و یکی از ایشان بود بدیشان گفت: ۵۰ 50
Nikodemo akawaambia (yeye aliyemwendea Yesu zamani, akiwa mmoja wa Mafarisayo),
«آیاشریعت ما بر کسی فتوی می‌دهد، جز آنکه اول سخن او را بشنوند و کار او را دریافت کنند؟» ۵۱ 51
“Je sheria yetu inamhukumu mtu isipokuwa amesikilizwa kwanza na kujua anachokifanya?”
ایشان در جواب وی گفتند: «مگر تو نیزجلیلی هستی؟ تفحص کن و ببین زیرا که هیچ نبی از جلیل برنخاسته است.» پس هر یک به خانه خود رفتند. ۵۲ 52
Walijibu na kumwambia, “Na wewe pia unatokea Galilaya? Tafuta na uone kwamba hakuna nabii aliyetokea Galilaya.”
۵۳ 53
(Zingatia: Baadhi ya maneno ya Yohana 7: 53 - 8: 11 hayamo katika nakala bora za kale). Kisha kila mtu alienda nyumbani kwake.

< یوحنا 7 >