< عزرا 10 >

پس چون عزرا دعا و اعتراف می‌نمود وگریه‌کنان پیش خانه خدا رو به زمین نهاده بود، گروه بسیار عظیمی از مردان و زنان واطفال اسرائیل نزد وی جمع شدند، زیرا قوم زارزار می‌گریستند. ۱ 1
Wakati Ezra alipokuwa anaomba na kuungama, huku akilia na kujitupa chini mbele ya nyumba ya Mungu, umati mkubwa wa Waisraeli, wanaume, wanawake na watoto walikusanyika kumzunguka. Nao pia wakalia sana.
و شکنیا ابن یحئیل که ازبنی عیلام بود جواب داد و به عزرا گفت: «ما به خدای خویش خیانت ورزیده، زنان غریب ازقومهای زمین گرفته‌ایم، لیکن الان امیدی برای اسرائیل در این باب باقی است. ۲ 2
Kisha Shekania mwana wa Yehieli, mmoja wa wazao wa Elamu, akamwambia Ezra, “Tumekosa uaminifu kwa Mungu wetu kwa kuoa wanawake wa kigeni kutoka mataifa yanayotuzunguka. Lakini pamoja na hili, bado liko tumaini kwa ajili ya Israeli.
پس حال باخدای خویش عهد ببندیم که آن زنان و اولادایشان را برحسب مشورت آقایم و آنانی که از امرخدای ما می‌ترسند دور کنیم و موافق شریعت عمل نماییم. ۳ 3
Sasa na tufanye agano mbele za Mungu wetu kuwafukuza hawa wanawake wote pamoja na watoto wao, kulingana na maonyo ya bwana wangu pamoja na wale ambao wanaogopa amri za Mungu wetu. Hili na lifanyike sawasawa na hii Sheria.
برخیز زیرا که این کار تو است و مابا تو می‌باشیم. پس قوی‌دل باش و به‌کار بپرداز.» ۴ 4
Inuka, suala hili lipo mikononi mwako. Sisi tutaungana nawe, uwe na ujasiri ukatende hili.”
آنگاه عزرا برخاسته، روسای کهنه و لاویان و تمامی اسرائیل را قسم داد که برحسب این سخن عمل نمایند، پس قسم خوردند. ۵ 5
Basi Ezra akainuka na kuwaapisha makuhani viongozi, Walawi na Israeli yote kufanya lile lililokuwa limependekezwa. Nao wakaapa.
و عزرا ازپیش روی خانه خدا برخاسته، به حجره یهوحانان بن الیاشیب رفت و نان نخورده و آب ننوشیده، به آنجا رفت، زیرا که به‌سبب تقصیراسیران ماتم گرفته بود. ۶ 6
Ndipo Ezra akaondoka hapo mbele ya nyumba ya Mungu akaenda kwenye chumba cha Yehohanani mwana wa Eliashibu. Wakati alipokuwa hapo, hakula chakula wala hakunywa maji, kwa sababu aliendelea kuomboleza kuhusu kukosa uaminifu kwa watu wa uhamishoni.
و به همه اسیران در یهوداو اورشلیم ندا دردادند که به اورشلیم جمع شوند. ۷ 7
Ndipo lilipotolewa tangazo Yuda yote na Yerusalemu kwa watu wote waliokuwa uhamishoni kukusanyika Yerusalemu.
و هر کسی‌که تا روز سوم، برحسب مشورت سروران و مشایخ حاضر نشود، اموال او ضبطگردد و خودش از جماعت اسیران جدا شود. ۸ 8
Yeyote ambaye hangejitokeza kwa muda wa siku tatu angepoteza mali yake yote, kulingana na uamuzi wa maafisa na wazee, naye mtu huyo angefukuzwa kutoka kusanyiko la watu waliokuwa uhamishoni.
پس در روز سوم که روز بیستم ماه نهم بود، همه مردان یهودا و بنیامین در اورشلیم جمع شدند وتمامی قوم در سعه خانه خدا نشستند. و به‌سبب این امر و به‌سبب باران، سخت می‌لرزیدند. ۹ 9
Katika muda wa siku tatu, watu wote wa Yuda na Benyamini wakawa wamekusanyika huko Yerusalemu. Kwenye siku ya ishirini ya mwezi wa tisa, watu wote walikuwa wameketi ndani ya uwanja mbele ya nyumba ya Mungu, wakiwa na majonzi mno kwa tukio hilo na kwa sababu ya mvua kubwa.
آنگاه عزرای کاهن برخاسته، به ایشان گفت: «شما خیانت ورزیده و زنان غریب گرفته، جرم اسرائیل را افزوده‌اید. ۱۰ 10
Ndipo Kuhani Ezra aliposimama akawaambia, “Mmekosa uaminifu, mmeoa wanawake wa kigeni, mkaongezea hatia ya Israeli.
پس الان یهوه خدای پدران خود را تمجید نمایید و به اراده او عمل کنید و خویشتن را از قومهای زمین و از زنان غریب جدا سازید.» ۱۱ 11
Sasa tubuni kwa Bwana, Mungu wa baba zenu mkafanye mapenzi yake. Jitengeni na mataifa wanaowazunguka na wake zenu wa kigeni.”
تمامی جماعت به آواز بلند جواب دادند وگفتند: «چنانکه به ما گفته‌ای همچنان عمل خواهیم نمود. ۱۲ 12
Kusanyiko lote likajibu kwa sauti kubwa: “Uko sawa kabisa! Ni lazima tufanye kama unavyosema.
اما خلق بسیارند و وقت باران است و طاقت نداریم که بیرون بایستیم و این امرکار یک یا دو روز نیست، زیرا که در این باب گناه عظیمی کرده‌ایم. ۱۳ 13
Lakini hapa pana watu wengi na ni wakati wa mvua, hivyo hatuwezi kusimama nje. Hata hivyo, shauri hili haliwezi kumalizika kwa siku moja au mbili, kwa sababu tumefanya dhambi kubwa katika jambo hili.
پس سروران ما برای تمامی جماعت تعیین بشوند و جمیع کسانی که درشهرهای ما زنان غریب گرفته‌اند، در وقت های معین بیایند و مشایخ و داوران هر شهر همراه ایشان بیایند، تا حدت خشم خدای ما درباره این امر از ما رفع گردد.» ۱۴ 14
Maafisa wetu na wafanye kwa niaba ya kusanyiko lote. Kisha kila mmoja katika miji yetu ambaye ameoa mwanamke wa kigeni aje kwa wakati uliopangwa, akiwa pamoja na wazee na waamuzi wa kila mji, hadi hasira kali ya Mungu wetu katika shauri hili itakapoondolewa kwetu.”
لهذا یوناتان بن عسائیل و یحزیا ابن تقوه براین امر معین شدند و مشلام و شبتائی لاوی، ایشان را اعانت نمودند. ۱۵ 15
Yonathani mwana wa Asaheli na Yazeya mwana wa Tikwa peke yao, wakiungwa mkono na Meshulamu na Shabethai Mlawi, ndio waliopinga jambo hili.
و اسیران چنین کردندو عزرای کاهن و بعضی از روسای آبا، برحسب خاندانهای آبای خود منتخب شدند و نامهای همه ایشان ثبت گردید. پس در روز اول ماه دهم، برای تفتیش این امر نشستند. ۱۶ 16
Basi watu wa uhamishoni wakafanya kama ilivyokuwa imependekezwa. Kuhani Ezra akachagua wanaume waliokuwa viongozi wa jamaa, mmoja kutoka kila mgawanyo wa jamaa, nao wote wakachaguliwa kwa majina. Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kumi waliketi kuchunguza mashauri hayo.
و تا روز اول ماه اول، کار همه مردانی را که زنان غریب گرفته بودند، به اتمام رسانیدند. ۱۷ 17
Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza wakawa wamemaliza kushughulikia wanaume wote waliokuwa wameoa wanawake wa kigeni.
و بعضی از پسران کاهنان پیدا شدند که زنان غریب گرفته بودند. ازبنی یشوع بن یوصاداق و برادرانش معسیا و الیعزرو یاریب و جدلیا. ۱۸ 18
Miongoni mwa wazao wa makuhani, wafuatao walikuwa wameoa wanawake wa kigeni: Kutoka wazao wa Yeshua mwana wa Yosadaki na ndugu zake: Maaseya, Eliezeri, Yaribu na Gedalia.
و ایشان دست دادند که زنان خود را بیرون نمایند و قوچی به جهت قربانی جرم خود گذرانیدند. ۱۹ 19
(Wote walitoa nadhiri kwa kuandika kwa mikono yao kuwafukuza wake zao, kwa hatia yao, kila mmoja akatoa kondoo dume kutoka kundini mwake kama sadaka ya hatia.)
و از بنی امیر، حنانی و زبدیا. ۲۰ 20
Kutoka wazao wa Imeri: Hanani na Zebadia.
و ازبنی حاریم، معسیا و ایلیا و شمعیا و یحیئیل وعزیا. ۲۱ 21
Kutoka wazao wa Harimu: Maaseya, Eliya, Shemaya, Yehieli na Uzia.
و از بنی فشحور، الیوعینای و معسیا واسمعیل و نتنئیل و یوزاباد و العاسه. ۲۲ 22
Kutoka wazao wa Pashuri: Elioenai, Maaseya, Ishmaeli, Nethaneli, Yozabadi na Elasa.
و ازلاویان، یوزاباد و شمعی و قلایا که قلیطا باشد. وفتحیا و یهودا و الیعزر. ۲۳ 23
Miongoni mwa Walawi: Yozabadi, Shimei, Kelaya (ndiye Kelita), Pethahia, Yuda na Eliezeri.
و از مغنیان، الیاشیب واز دربانان، شلوم و طالم و اوری. ۲۴ 24
Kutoka waimbaji: Eliashibu. Kutoka mabawabu: Shalumu, Telemu na Uri.
و اما ازاسرائیلیان: از بنی فرعوش، رمیا و یزیا و ملکیا ومیامین و العازار و ملکیا و بنایا. ۲۵ 25
Miongoni mwa Waisraeli wengine: Kutoka wazao wa Paroshi: Ramia, Izia, Malkiya, Miyamini, Eleazari, Malkiya na Benaya.
و از بنی عیلام، متنیا و زکریا و یحیئیل و عبدی و یریموت و ایلیا. ۲۶ 26
Kutoka wazao wa Elamu: Matania, Zekaria, Yehieli, Abdi, Yeremothi na Eliya.
و از بنی زتو، الیوعینای و الیاشیب و متنیا ویریموت و زاباد و عزیزا. ۲۷ 27
Kutoka wazao wa Zatu: Elioenai, Eliashibu, Matania, Yeremothi, Zabadi na Aziza.
و از بنی بابای، یهوحانان و حننیا و زبای و عتلای. ۲۸ 28
Kutoka uzao wa Bebai: Yehohanani, Hanania, Zabai na Athlai.
و ازبنی بانی، مشلام و ملوک و عدایا و یاشوب و شال و راموت. ۲۹ 29
Kutoka wazao wa Bani: Meshulamu, Maluki, Adaya, Yashubu, Sheali na Yeremothi.
و از بنی فحت، موآب عدنا و کلال وبنایا و معسیا و متنیا و بصلئیل و بنوی و منسی. ۳۰ 30
Kutoka wazao wa Pahath-Moabu: Adna, Kelali, Benaya, Maaseya, Matania, Bezaleli, Binui na Manase.
و از بنی حاریم، الیعزر و اشیا و ملکیا و شمعیا وشمعون. ۳۱ 31
Kutoka wazao wa Harimu: Eliezeri, Ishiya, Malkiya, Shemaya, Shimeoni,
و بنیامین و ملوک و شمریا. ۳۲ 32
Benyamini, Maluki, na Shemaria.
ازبنی حاشوم، متنای و متاته و زاباد و الیفلط ویریمای و منسی و شمعی. ۳۳ 33
Kutoka wazao wa Hashumu: Matenai, Matata, Zabadi, Elifeleti, Yeremai, Manase na Shimei.
از بنی بانی، معدای و عمرام و اوئیل. ۳۴ 34
Kutoka wazao wa Bani: Maadai, Amramu, Ueli,
و بنایا و بیدیا وکلوهی. ۳۵ 35
Benaya, Bedeya, Keluhi,
و ونیا و مریموت و الیاشیب. ۳۶ 36
Vania, Meremothi, Eliashibu,
ومتنیا و متنای و یعسو. ۳۷ 37
Matania, Matenai na Yaasu.
و بانی و بنوی و شمعی. ۳۸ 38
Kutoka wazao wa Binui: Shimei,
و شلمیا و ناتان و عدایا. ۳۹ 39
Shelemia, Nathani, Adaya,
ومکندبای و شاشای و شارای. ۴۰ 40
Maknadebai, Shashai, Sharai,
و عزرئیل وشلمیا و شمریا. ۴۱ 41
Azareli, Shelemia, Shemaria,
و شلوم و امریا و یوسف. ۴۲ 42
Shalumu, Amaria na Yosefu.
از بنی نبو، یعیئیل و متتیا و زاباد و زبینا و یدوو یوئیل و بنایا. ۴۳ 43
Kutoka wazao wa Nebo: Yeieli, Matithia, Zabadi, Zebina, Yadai, Yoeli na Benaya.
جمیع اینها زنان غریب گرفته بودند و بعضی از ایشان زنانی داشتند که از آنهاپسران تولید نموده بودند. ۴۴ 44
Hawa wote walikuwa wameoa wanawake wa kigeni, na baadhi yao walikuwa wamezaa nao watoto.

< عزرا 10 >