< حزقیال 10 >

پس نگریستم و اینک بر فلکی که بالای سر کروبیان بود چیزی مثل سنگ یاقوت کبود و مثل نمایش شبیه تخت بر زبر آنهاظاهر شد. ۱ 1
Nikatazama, nikaona juu ya ile nafasi iliyokuwa juu ya vichwa vya wale makerubi kulikuwa na kitu mfano wa kiti cha enzi cha yakuti samawi.
و آن مرد را که به کتان ملبس بودخطاب کرده گفت: «در میان چرخها در زیرکروبیان برو و دستهای خود را از اخگرهای آتشی که در میان کروبیان است پر کن و بر شهربپاش.» و او در نظر من داخل شد. ۲ 2
Bwana akamwambia mtu yule aliyekuwa amevaa nguo ya kitani, “Ingia katikati ya yale Magurudumu yaliyo chini ya makerubi. Ukaijaze mikono yako makaa ya mawe ya moto kutoka katikati ya makerubi na uyatawanye juu ya mji.” Nilipokuwa nikiangalia, akaingia ndani.
و چون آن مردداخل شد، کروبیان بطرف راست خانه ایستاده بودند و ابر، صحن اندرونی را پر کرد. ۳ 3
Basi wale makerubi walikuwa wamesimama upande wa kusini wa Hekalu wakati yule mtu alipoingia ndani, wingu likaujaza ule ukumbi wa ndani.
و جلال خداوند از روی کروبیان به آستانه خانه برآمد وخانه از ابر پر شد و صحن از فروغ جلال خداوندمملو گشت. ۴ 4
Kisha utukufu wa Bwana ukainuka kutoka juu ya wale makerubi ukaenda kwenye kizingiti cha Hekalu. Wingu likajaza Hekalu, nao ukumbi ukajawa na mngʼao wa utukufu wa Bwana.
و صدای بالهای کروبیان تا به صحن بیرونی مثل آواز خدای قادر مطلق حینی که تکلم می کند، مسموع شد. ۵ 5
Sauti ya mabawa ya wale makerubi ingeweza kusikika mpaka kwenye ukumbi wa nje, kama sauti ya Mungu Mwenyezi wakati anapoongea.
و چون آن مرد را که ملبس به کتان بود امرفرموده، گفت که «آتش را از میان چرخها از میان کروبیان بردار.» آنگاه داخل شده، نزد چرخهاایستاد. ۶ 6
Bwana alipomwamuru yule mtu aliyevaa nguo za kitani akisema, “Chukua moto toka katikati ya magurudumu, kutoka katikati ya makerubi,” yule mtu aliingia ndani akasimama pembeni mwa gurudumu.
و یکی از کروبیان دست خود را از میان کروبیان به آتشی که در میان کروبیان بود درازکرده، آن را برداشت و به‌دست آن مردی که به کتان، ملبس بود نهاد و او آن را گرفته، بیرون رفت. ۷ 7
Ndipo mmoja wa wale makerubi akanyoosha mkono wake kwenye moto uliokuwa katikati yao. Akachukua baadhi ya moto na kuutia mikononi mwa yule mtu aliyevaa mavazi ya kitani, naye akaupokea akatoka nje.
و در کروبیان شبیه صورت دست انسان زیربالهای ایشان ظاهر شد. ۸ 8
(Chini ya mabawa ya makerubi paliweza kuonekana kitu kilichofanana na mikono ya mwanadamu.)
و نگریستم و اینک چهار چرخ به پهلوی کروبیان یعنی یک چرخ به پهلوی یک کروبی وچرخ دیگر به پهلوی کروبی دیگر ظاهر شد. ونمایش چرخها مثل صورت سنگ زبرجد بود. ۹ 9
Nikatazama, nikaona magurudumu manne kando ya makerubi, moja kando ya kila kerubi. Magurudumu hayo yalimetameta kama kito cha zabarajadi.
و اما نمایش ایشان چنین بود. آن چهار را یک شباهت بود که گویا چرخ در میان چرخ باشد. ۱۰ 10
Kule kuonekana kwake, yote manne yalifanana kila gurudumu lilikuwa kama linazunguka ndani ya lingine.
وچون آنها می‌رفت بر چهار جانب خود می‌رفت وحینی که می‌رفت به هیچ سو میل نمی کرد، بلکه به‌جایی که سر به آن متوجه می‌شد از عقب آن می‌رفت. و چون می‌رفت به هیچ سو میل نمی کرد. ۱۱ 11
Yalipozunguka, yalikwenda kokote katika pande nne walikoelekea wale makerubi. Magurudumu hayakugeuka wakati makerubi yalipokwenda. Makerubi walikwenda upande wowote kichwa kilikoelekea pasipo kugeuka walipokuwa wakienda.
و تمامی بدن و پشتها و دستها وبالهای ایشان و چرخها یعنی چرخهایی که آن چهار داشتند از هر طرف پر از چشمها بود. ۱۲ 12
Miili yao yote, pamoja na migongo yao, mikono na mabawa yao yote yalikuwa yamejaa macho kabisa kama yalivyokuwa yale magurudumu yao manne.
وبه سمع من به آن چرخها ندا در‌دادند که «ای چرخها!» ۱۳ 13
Nikasikia magurudumu yakiitwa, “Magurudumu ya kisulisuli.”
و هر یک را چهار رو بود. روی اول روی کروبی بود و روی دوم روی انسان و سوم روی شیر و چهارم روی عقاب. ۱۴ 14
Kila mmoja wa wale makerubi alikuwa na nyuso nne: Uso mmoja ulikuwa kama vile wa kerubi, uso wa pili ulikuwa wa mwanadamu, uso wa tatu ulikuwa wa simba na uso wa nne ulikuwa wa tai.
پس کروبیان صعود کردند. این همان حیوان است که نزد نهر خابور دیده بودم. ۱۵ 15
Kisha makerubi wakapaa juu. Hawa ndio wale viumbe walio hai niliowaona kando ya Mto Kebari.
و چون کروبیان می‌رفتند، چرخها به پهلوی ایشان می‌رفت و چون کروبیان بالهای خود را برافراشته، از زمین صعود می‌کردند، چرخها نیز از پهلوی ایشان برنمی گشت. ۱۶ 16
Wakati makerubi walipokwenda, magurudumu yaliyoko kando yao yalikwenda na wakati makerubi walipotanda mabawa yao wapate kupaa juu kutoka ardhi, magurudumu yale hayakuondoka pembeni mwao.
چون ایشان می‌ایستادندآنها می‌ایستاد و چون ایشان صعود می‌نمودند، آنها با ایشان صعود می‌نمود، زیرا که روح حیوان در آنها بود. ۱۷ 17
Makerubi yaliposimama kimya, nayo pia yalitulia kimya, nao makerubi yalipoinuka juu, magurudumu nayo yaliinuka juu pamoja nao, kwa sababu roho ya vile viumbe hai ilikuwa ndani yake.
و جلال خداوند از بالای آستانه خانه بیرون آمد و بر زبر کروبیان قرار گرفت. ۱۸ 18
Kisha utukufu wa Bwana ukaondoka pale kwenye kizingiti cha Hekalu na kusimama juu ya wale makerubi.
وچون کروبیان بیرون رفتند بالهای خود رابرافراشته، به نظر من از زمین صعود نمودند. وچرخها پیش روی ایشان بود و نزد دهنه دروازه شرقی خانه خداوند ایستادند. و جلال خدای اسرائیل از طرف بالا بر ایشان قرار گرفت. ۱۹ 19
Nilipokuwa nikitazama, makerubi yakatanda mabawa yao na kuinuka kutoka ardhini, nao walipokuwa wakienda, yale magurudumu yakaenda pamoja nao. Wakasimama kwenye ingilio la lango la mashariki la nyumba ya Bwana, nao utukufu wa Mungu wa Israeli ukawa juu yao.
این همان حیوان است که زیر خدای اسرائیل نزد نهرخابور دیده بودم، پس فهمیدم که اینان کروبیانند. ۲۰ 20
Hawa walikuwa ndio viumbe hai niliokuwa nimewaona chini ya Mungu wa Israeli kando ya Mto Kebari, nami nikatambua ya kuwa hao walikuwa makerubi.
هر یک را چهار روی و هر یک را چهار بال بودو زیر بالهای ایشان شبیه دستهای انسان بود. ۲۱ 21
Kila mmoja alikuwa na nyuso nne, mabawa manne, chini ya mabawa yao kulikuwa na kile kilichoonekana kama mikono ya mwanadamu.
واما شبیه رویهای ایشان چنین بود. همان رویها بودکه نزد نهر خابور دیده بودم. هم نمایش ایشان وهم خود ایشان (چنان بودند) و هر یک به راه مستقیم می‌رفت. ۲۲ 22
Nyuso zao zilifanana kama zile nilizokuwa nimeziona kando ya Mto Kebari. Kila mmoja alikwenda mbele moja kwa moja.

< حزقیال 10 >