< خروج 40 >
و خداوند موسی را خطاب کرده، گفت: | ۱ 1 |
Kisha Bwana akamwambia Mose:
«در غره ماه اول مسکن خیمه اجتماع را برپا نما. | ۲ 2 |
“Simika Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza.
و تابوت شهادت را در آن بگذار. وحجاب را پیش تابوت پهن کن. | ۳ 3 |
Weka Sanduku la Ushuhuda ndani yake na ulifunike kwa pazia. Ingiza meza na kupanga vitu vyake juu yake.
و خوان رادرآورده، چیزهایی را که میباید، بر آن ترتیب نما. و چراغدان را درآور و چراغهایش را آراسته کن. | ۴ 4 |
Kisha ingiza kinara cha taa na uweke taa zake juu yake.
و مذبح زرین را برای بخور پیش تابوت شهادت بگذار، و پرده دروازه را بر مسکن بیاویز. | ۵ 5 |
Weka madhabahu ya dhahabu ya kufukizia uvumba mbele ya Sanduku la Ushuhuda kisha uweke pazia kwenye lango la Maskani ya Mungu.
و مذبح قربانی سوختنی را پیش دروازه مسکن خیمه اجتماع بگذار. | ۶ 6 |
“Weka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa mbele ya lango la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania;
و حوض را در میان خیمه اجتماع و مذبح بگذار، و آب در آن بریز. | ۷ 7 |
weka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, na uweke maji ndani yake.
و صحن را گرداگرد برپا کن. و پرده دروازه صحن رابیاویز. | ۸ 8 |
Fanyiza ua kuzunguka maskani na uweke pazia penye ingilio la ua.
و روغن مسح را گرفته، مسکن را با آنچه در آن است مسح کن، و آن را با همه اسبابش تقدیس نما تا مقدس شود. | ۹ 9 |
“Chukua mafuta ya upako, ipake Maskani ya Mungu pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake; iweke wakfu pamoja na vitu vyote vilivyomo ndani mwake, nayo itakuwa takatifu.
و مذبح قربانی سوختنی را با همه اسبابش مسح کرده، مذبح راتقدیس نما. و مذبح، قدس اقداس خواهد بود. | ۱۰ 10 |
Kisha yapake mafuta hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka pamoja na vifaa vyake vyote; weka wakfu madhabahu nayo yatakuwa takatifu sana.
و حوض را با پایهاش مسح نموده، تقدیس کن. | ۱۱ 11 |
Paka sinia mafuta pamoja na kishikilio chake na uviweke wakfu.
و هارون و پسرانش را نزد دروازه خیمه اجتماع آورده، ایشان را به آب غسل ده. | ۱۲ 12 |
“Mlete Aroni na wanawe kwenye ingilio la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
وهارون را به رخت مقدس بپوشان، و او را مسح کرده، تقدیس نما، تا برای من کهانت کند. | ۱۳ 13 |
Kisha mvike Aroni yale mavazi matakatifu, umtie mafuta na kumweka wakfu ili apate kunitumikia katikati ya ukuhani.
وپسرانش را نزدیک آورده، ایشان را به پیراهنهابپوشان. | ۱۴ 14 |
Walete wanawe na uwavike makoti.
و ایشان را مسح کن، چنانکه پدرایشان را مسح کردی تا برای من کهانت نماید. ومسح ایشان هر آینه برای کهانت ابدی در نسلهای ایشان خواهد بود.» | ۱۵ 15 |
Kisha watie mafuta kama ulivyomtia baba yao, ili nao pia wanitumikie katika kazi ya ukuhani. Kutiwa mafuta kwao kutakuwa kwa ajili ya ukuhani utakaoendelea kwa vizazi vyote vijavyo.”
پس موسی موافق آنچه خداوند او را امر فرموده بود کرد، و همچنین به عمل آورد. | ۱۶ 16 |
Mose akafanya kila kitu sawa kama vile Bwana alivyomwagiza.
و واقع شد در غره ماه اول از سال دوم که مسکن برپا شد، | ۱۷ 17 |
Kwa hiyo Maskani ya Mungu ilisimikwa katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, katika mwaka wa pili.
و موسی مسکن را برپا نمود، وپایه هایش را بنهاد و تخته هایش را قایم کرد، وپشت بندهایش را گذاشت، و ستونهایش را برپانمود، | ۱۸ 18 |
Mose alipoweka wakfu Maskani ya Mungu, aliweka vitako mahali pake, akasimamisha mihimili, akatia mataruma na kusimamisha nguzo.
و خیمه را بالای مسکن کشید، و پوشش خیمه را بر زبر آن گسترانید، چنانکه خداوند به موسیامر نموده بود. | ۱۹ 19 |
Kisha akalitandaza hema juu ya Maskani ya Mungu na kuifunika hema, kama Bwana alivyomwagiza.
و شهادت را گرفته، آن رادر تابوت نهاد، و عصاها را بر تابوت گذارد، وکرسی رحمت را بالای تابوت گذاشت. | ۲۰ 20 |
Akachukua ule Ushuhuda na kuuweka ndani ya Sanduku la Agano, akaweka ile mipiko ya kubebea hilo Sanduku na kuweka kiti cha rehema juu yake.
وتابوت را به مسکن درآورد، و حجاب ستر راآویخته، آن را پیش تابوت شهادت کشید. چنانکه خداوند به موسیامر فرموده بود. | ۲۱ 21 |
Kisha Mose akalileta Sanduku ndani ya Maskani ya Mungu, akatundika pazia ili kulifunika Sanduku la Ushuhuda, kama Bwana alivyomwagiza.
و خوان را در خیمه اجتماع به طرف شمالی مسکن، بیرون حجاب نهاد. | ۲۲ 22 |
Mose akaweka meza ndani ya Hema la Kukutania, upande wa kaskazini ya Maskani ya Mungu nje ya pazia
و نان را به حضور خداوند بر آن ترتیب داد، چنانکه خداوند به موسیامر فرموده بود. | ۲۳ 23 |
na kupanga mikate juu yake mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
و چراغدان را در خیمه اجتماع، مقابل خوان به طرف جنوبی مسکن نهاد. | ۲۴ 24 |
Akaweka kinara cha taa ndani ya Hema la Kukutania mkabala na meza upande wa kusini mwa Maskani ya Mungu
و چراغها رابه حضور خداوند گذاشت، چنانکه خداوند به موسیامر فرموده بود. | ۲۵ 25 |
na kuziweka taa mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
و مذبح زرین را درخیمه اجتماع، پیش حجاب نهاد. | ۲۶ 26 |
Mose akaweka madhabahu ya dhahabu ndani ya Hema la Kukutania mbele ya pazia
و بخورمعطر بر آن سوزانید، چنانکه خداوند به موسیامر فرموده بود. | ۲۷ 27 |
na kufukiza uvumba wenye harufu nzuri, kama Bwana alivyomwagiza.
و پرده دروازه مسکن راآویخت. | ۲۸ 28 |
Kisha akaweka pazia kwenye ingilio la Maskani ya Mungu.
و مذبح قربانی سوختنی را پیش دروازه مسکن خیمه اجتماع وضع کرد، و قربانی سوختنی و هدیه را بر آن گذرانید، چنانکه خداوند به موسیامر فرموده بود. | ۲۹ 29 |
Mose akaweka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa karibu na ingilio la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, na kutoa juu yake sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka kama Bwana alivyomwagiza.
و حوض رادر میان خیمه اجتماع و مذبح وضع کرده، آب برای شستن در آن بریخت. | ۳۰ 30 |
Akaweka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, akaweka maji ndani yake kwa ajili ya kunawia,
و موسی و هارون وپسرانش دست و پای خود را در آن شستند. | ۳۱ 31 |
Naye Mose, Aroni na wanawe wakayatumia kwa kunawia mikono na miguu yao.
وقتی که به خیمه اجتماع داخل شدند ونزد مذبح آمدند شست و شو کردند، چنانکه خداوند به موسیامر فرموده بود. | ۳۲ 32 |
Wakanawa kila walipoingia katika Hema la Kukutania au walipoikaribia madhabahu kama Bwana alivyomwagiza Mose.
و صحن راگرداگرد مسکن و مذبح برپا نمود، و پرده دروازه صحن را آویخت. پس موسی کار را به انجام رسانید. | ۳۳ 33 |
Kisha Mose akafanya ua kuizunguka Maskani ya Mungu na madhabahu, pia akaweka pazia kwenye ingilio la huo ua. Hivyo Mose akaikamilisha kazi.
آنگاه ابر، خیمه اجتماع را پوشانید و جلال خداوند مسکن را پر ساخت. | ۳۴ 34 |
Ndipo wingu likafunika Hema la Kukutania, na utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
و موسی نتوانست به خیمه اجتماع داخل شود، زیراکه ابربر آن ساکن بود، و جلال خداوند مسکن را پرساخته بود. | ۳۵ 35 |
Mose hakuweza kuingia ndani ya Hema la Kukutania kwa sababu wingu lilikuwa limetua juu ya Hema, nao utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
و چون ابر از بالای مسکن برمی خاست، بنیاسرائیل در همه مراحل خودکوچ میکردند. | ۳۶ 36 |
Katika safari yote ya Waisraeli, kila wakati wingu lilipoinuka kutoka juu ya Maskani ya Mungu, wangeondoka;
و هرگاه ابر برنمی خاست، تاروز برخاستن آن، نمی کوچیدند. | ۳۷ 37 |
lakini kama wingu halikuinuka, hawakuondoka, mpaka siku lilipoinuka.
زیرا که در روز، ابر خداوند بر مسکن و در شب، آتش بر آن میبود، در نظر تمامی خاندان اسرائیل، در همه منازل ایشان. | ۳۸ 38 |
Kwa hiyo wingu la Bwana lilikuwa juu ya maskani mchana, na moto ulikuwa katika hilo wingu wakati wa usiku, machoni pa nyumba yote ya Israeli siku zote za safari zao.