< خروج 39 >

و از لاجورد و ارغوان و قرمز رختهای بافته شده ساختند، برای خدمت کردن در قدس، و رختهای مقدس برای هارون ساختند، چنانکه خداوند به موسی‌امر نموده بود. ۱ 1
Na kutokana na ule uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili wakafanya mavazi yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika mahali patakatifu. Basi wakafanya yale mavazi matakatifu yaliyokuwa kwa ajili ya Aruni, kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
و ایفود را از طلا و لاجورد و ارغوان و قرمزو کتان نازک تابیده شده، ساخت. ۲ 2
Basi akaifanya ile naivera ya dhahabu, uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa.
و تنگه های نازک از طلا ساختند و تارها کشیدند تا آنها را درمیان لاجورد و ارغوان و قرمز و کتان نازک به صنعت نساج ماهر ببافند. ۳ 3
Kisha wakafua mabamba ya dhahabu yawe mabamba membamba, naye akakata nyuzi za kufuma pamoja na ule uzi wa bluu na ile sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kile kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kile kitani bora, kama kazi ya mjenzi.
و کتفهای پیوسته شده برایش ساختند، که بر دو کنار پیوسته شد. ۴ 4
Wakaifanyia vipande vya begani vilivyounganishwa. Iliunganishwa kwenye miisho yake miwili.
و زنار بسته شده‌ای که بر آن بود از همان پارچه واز همان صنعت بود، از طلا و لاجورد و ارغوان وقرمز و کتان نازک تابیده شده، چنانکه خداوند به موسی‌امر فرموده بود. ۵ 5
Nao mshipi, uliokuwa juu yake ili kuifunga, ulikuwa wa kitambaa kilekile kulingana na ufundi wake, wa dhahabu, uzi wa bluu, na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa, kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
و سنگهای جزع مرصع در دو طوق طلا، و منقوش به نقش خاتم، موافق نامهای بنی‌اسرائیل درست کردند. ۶ 6
Kisha wakafanya mawe ya shohamu yaliyopangwa kwenye mapambo ya dhahabu, yaliyochongwa kwa michoro ya muhuri kulingana na majina ya wana wa Israeli.
آنها را بر کتفهای ایفود نصب کرد، تا سنگهای یادگاری برای بنی‌اسرائیل باشد، چنانکه خداوند به موسی‌امر فرموده بود. ۷ 7
Bezaleli akayaweka kwenye vile vipande vya begani vya naivera yawe mawe ya ukumbusho kwa ajili ya wana wa Israeli, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.
و سینه بند را موافق کار ایفود از صنعت نساج ماهر ساخت، از طلا و لاجورد و ارغوان وقرمز و کتان نازک تابیده شده. ۸ 8
Kisha akafanya kile kifuko cha kifuani kwa ufundi wa mjenzi, kama ule ufundi wa naivera, kutokana na dhahabu, uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa.
و آن مربع بود وسینه بند را دولا ساختند طولش یک وجب وعرضش یک وجب دولا. ۹ 9
Kilikuwa mraba kilipokunjwa. Walikifanya kile kifuko cha kifuani, kinapokunjwa, shubiri moja urefu wake na shubiri moja upana wake.
و در آن چهار رسته سنگ نصب کردند، رسته‌ای از عقیق سرخ ویاقوت زرد و زمرد. این بود رسته اول. ۱۰ 10
Kisha wakakijaza kwa mistari minne ya mawe. Mstari wa zabarijadi, topazi na zumaridi ulikuwa mstari wa kwanza.
و رسته دوم از بهرمان و یاقوت کبود و عقیق سفید. ۱۱ 11
Nao mstari wa pili ulikuwa feruzi, yakuti na yaspi.
ورسته سوم از عین الهر و یشم و جمست. ۱۲ 12
Nao mstari wa tatu ulikuwa jiwe la leshemi, akiki na amethisti.
ورسته چهارم از زبرجد و جزع و یشب در ترصیعه خود که به دیوارهای طلا احاطه شده بود. ۱۳ 13
Nao mstari wa nne ulikuwa krisolito na shohamu na yashefi. Yaliwekwa katika mapambo ya dhahabu katika mahali pake.
وسنگها موافق نامهای بنی‌اسرائیل دوازده بود، مطابق اسامی ایشان، مثل نقش خاتم، هر یکی به اسم خود برای دوازده سبط. ۱۴ 14
Na mawe hayo yalikuwa kulingana na majina ya wana wa Israeli. Yalikuwa kumi na mawili kulingana na majina yao, kwa michongo ya muhuri, kila moja kulingana na jina lake kwa ajili ya yale makabila kumi na mawili.
و بر سینه بندزنجیرهای تابیده شده، مثل کار طنابها از طلای خالص ساختند. ۱۵ 15
Nao wakafanya juu ya kile kifuko cha kifuani minyororo yenye mashada, msokoto wa kamba, wa dhahabu safi.
و دو طوق زرین و دو حلقه زرین ساختند و دو حلقه را بر دو سر سینه بندگذاشتند. ۱۶ 16
Kisha wakafanya mapambo mawili ya dhahabu na pete mbili za dhahabu na kuziweka hizo pete mbili kwenye ile miisho miwili ya kile kifuko cha kifuani.
و آن دو زنجیر تابیده شده زرین رادر دو حلقه‌ای که بر سرهای سینه بند بود، گذاشتند. ۱۷ 17
Baada ya hilo wakapitisha zile kamba mbili za dhahabu kwenye zile pete mbili zilizo kwenye miisho ya kile kifuko cha kifuani.
و دو سر دیگر آن دو زنجیر را بر دوطوق گذاشتند، و آنها را بر دو کتف ایفود در‌پیش نصب کردند. ۱۸ 18
Nao wakapitisha ile miisho miwili ya zile kamba mbili kwenye yale mapambo mawili. Halafu wakaiweka juu ya vile vipande vya begani vya naivera, mbele yake.
و دو حلقه زرین ساختند، آنها رابر دو سر سینه بند گذاشتند، بر کناری که بر طرف اندرونی‌ایفود بود. ۱۹ 19
Kisha wakafanya pete mbili za dhahabu na kuziweka kwenye ile miisho miwili ya kile kifuko cha kifuani kwenye upindo wake ulio upande unaoelekea ile efodi upande wa ndani.
و دو حلقه زرین دیگرساختند، و آنها را بر دو کتف ایفود، به طرف پایین، از جانب پیش، مقابل پیوستگیش بالای زنار ایفود گذاشتند. ۲۰ 20
Halafu wakafanya pete mbili za dhahabu na kuziweka juu ya vile vipande viwili vya begani vya efodi upande wake wa chini, sehemu yake ya mbele, karibu na mahali pake pa kuungania, juu ya ule mshipi wa naivera.
و سینه بند را به حلقه هایش با حلقه های ایفود به نوار لاجوردی بستند، تا بالای زنار ایفود باشد. و سینه بند از ایفود جدا نشود، چنانکه خداوند به موسی‌امرفرموده بود. ۲۱ 21
Mwishowe wakakifunga kile kifuko cha kifuani kwa pete zake kwenye zile pete za efodi kwa uzi wa bluu, ili kipate kuwa juu ya mshipi wa efodi na kile kifuko cha kifuani kisiondoke juu ya efodi, kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
و ردای ایفود را از صنعت نساج، تمام لاجوردی ساخت. ۲۲ 22
Bezaleli akafanya lile koti la naivera, lote la uzi wa zambarau, kazi ya mshonaji.
و دهنه‌ای در وسط ردابود، مثل دهنه زره با حاشیه‌ای گرداگرد دهنه تادریده نشود. ۲۳ 23
Na sehemu wazi ya hilo koti ilikuwa katikati yake, kama sehemu wazi ya vazi la chuma. Sehemu hiyo iliyo wazi ilikuwa na ukingo kuizunguka pande zote ili isiraruke.
و بر دامن ردا، انارها از لاجورد وارغوان و قرمز و کتان تابیده شده ساختند. ۲۴ 24
Halafu wakafanya kwenye upindo wa hilo koti makomamanga ya uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili, vilivyosokotwa pamoja.
وزنگوله‌ها از طلای خالص ساختند. و زنگوله‌ها رادر میان انارها بر دامن ردا گذاشتند، گرداگردش درمیان انارها. ۲۵ 25
Wakafanya kengele za dhahabu safi na kuziweka kengele hizo katikati ya makomamanga kwenye upindo wa lile koti kuzunguka pande zote, katikati ya makomamanga;
و زنگوله‌ای و اناری، و زنگوله‌ای واناری گرداگرد دامن ردا برای خدمت کردن، چنانکه خداوند به موسی‌امر فرموده بود. ۲۶ 26
kengele na komamanga, kengele na komamanga kwenye upindo wa hilo koti kuzunguka pande zote, kwa ajili ya kuhudumu, kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
وپیراهنها را برای هارون و پسرانش از کتان نازک ازصنعت نساج ساختند. ۲۷ 27
Kisha wakafanya zile kamba za kitani bora, kwa ajili ya Haruni na wanawe.
و عمامه را از کتان نازک و دستارهای زیبا را از کتان نازک، و زیرجامهای کتانی را از کتان نازک تابیده شده. ۲۸ 28
Na kile kilemba cha kitani bora na yale mavalio ya kichwani ya mapambo ya kitani bora na zile suruali za kitani bora kilichosokotwa,
و کمربند رااز کتان نازک تابیده شده، و لاجورد و ارغوان وقرمز از صنعت طراز، چنانکه خداوند به موسی‌امر فرموده بود. ۲۹ 29
na ule ukumbuu wa kitani bora kilichosokotwa na uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili, kazi ya mfumaji, kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
و تنگه افسر مقدس را ازطلای خالص ساختند، و بر آن کتابتی مثل نقش خاتم مرقوم داشتند: قدوسیت برای یهوه. ۳۰ 30
Mwishowe wakafanya lile bamba linalong’aa, ishara takatifu ya wakfu, kutokana na dhahabu safi na kuandika juu yake maandishi kwa mchongo wa muhuri: “Utakatifu kwa Yahweh.”
و برآن نواری لاجوردی بستند تا آن را بالای عمامه ببندند، چنانکه خداوند به موسی‌امر فرموده بود. ۳۱ 31
Kisha wakalitia uzi wa bluu ili waliweke juu ya kile kilemba upande wa juu. Kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
پس همه کار مسکن خیمه اجتماع تمام شد، و بنی‌اسرائیل ساختند. موافق آنچه خداوندبه موسی‌امر فرموده بود، عمل نمودند. ۳۲ 32
Basi kazi ya ile maskani ya hema la mkutano ikafikia mwisho wake. Kwa maana wana wa Israeli waliendelea kufanya kulingana na yote ambayo Yahweh alikuwa amemwamuru Musa.
ومسکن خیمه را نزد موسی آوردند، با همه اسبابش و تکمه‌ها و تخته‌ها و پشت بندها وستونها و پایه هایش. ۳۳ 33
Nao wakaileta maskani kwa Musa, lile hema pamoja na vyombo vyake vyote, kulabu zake, viunzi vyake vya mbao, miti yake na nguzo zake na vikalio vyake,
و پوشش از پوست قوچ سرخ شده و پوشش از پوست خز و حجاب ستر. ۳۴ 34
na kifuniko chake cha ngozi za kondoo-dume zilizotiwa rangi nyekundu na kifuniko chake cha ngozi za sili na pazia la kisitiri,
و تابوت شهادت و عصاهایش و کرسی رحمت. ۳۵ 35
na sanduku la ushuhuda na miti yake na kifuniko.
و خوان و همه اسبابش و نان تقدمه. ۳۶ 36
Wakaleta meza, vyombo vyake vyote, na ule mkate wa wonyesho,
و چراغدان طاهر و چراغهایش، چراغهای آراسته شده و همه اسبابش، و روغن برای روشنایی. ۳۷ 37
kile kinara cha taa cha dhahabu safi, taa zake, ule mstari wa taa, na vyombo vyake vyote na yale mafuta ya kuangazia taa,
و مذبح زرین و روغن مسح و بخورمعطر و پرده برای دروازه خیمه. ۳۸ 38
na madhabahu ya dhahabu na yale mafuta yanayotumiwa kutia mafuta na ule uvumba uliotiwa manukato na kile kisitiri kwa ajili ya mwingilio wa hema,
و مذبح برنجین و شبکه برنجین آن، و عصاهایش و همه اسبابش و حوض و پایه‌اش. ۳۹ 39
ile madhabahu ya shaba na kile kiunzi chake cha shaba, miti yake na vyombo vyake vyote, ile beseni na kinara chake,
و پرده های صحن و ستونها و پایه هایش و پرده دروازه صحن، وطنابهایش و میخهایش و همه اسباب خدمت مسکن برای خیمه اجتماع. ۴۰ 40
Wakaleta mapazia ya ua, nguzo zake na vikalio vyake na kile kisitiri kwa ajili ya lango la ua, kamba zake za hema na misumari yake ya hema na vyombo vyote kwa ajili ya utumishi wa maskani, kwa ajili ya hema ya kukutania.
و رختهای بافته شده برای خدمت قدس، و رخت مقدس برای هارون کاهن، و رختها برای پسرانش تا کهانت نمایند. ۴۱ 41
Wakaleta yale mavazi yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika patakatifu, yale mavazi matakatifu kwa ajili ya Aruni kuhani na mavazi ya wanawe ya kutumikia wakiwa makuhani.
موافق آنچه خداوند به موسی‌امرفرموده بود، بنی‌اسرائیل همچنین تمام کار راساختند. ۴۲ 42
Kulingana na yote ambayo Yahweh alikuwa amemwamuru Musa, hivyo ndivyo wana wa Israeli walivyoufanya utumishi wote.
و موسی تمام کارها را ملاحظه کرد، و اینک موافق آنچه خداوند امر فرموده بودساخته بودند، همچنین کرده بودند. و موسی ایشان را برکت داد. ۴۳ 43
Naye Musa akaiona ile kazi yote, na, tazama, walikuwa wameifanya kama vile Yahweh alivyokuwa ameamuru. Hivyo ndivyo walivyokuwa wamefanya. Basi Musa akawabariki.

< خروج 39 >