< دانیال 8 >
در سال سوم سلطنت بلشصر پادشاه، رویایی بر من دانیال ظاهر شد بعد از آنکه اول به من ظاهر شده بود. | ۱ 1 |
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Mfalme Belshaza, mimi Danieli, nilipata maono, baada ya maono ambayo yalikuwa yamenitokea mbeleni.
و در رویا نظر کردم ومی دیدم که من در دارالسلطنه شوشن که درولایت عیلام میباشد بودم و در عالم رویا دیدم که نزد نهر اولای میباشم. | ۲ 2 |
Katika maono yangu, nilijiona nikiwa ndani ya ngome ya Shushani katika jimbo la Elamu. Katika maono nilikuwa kando ya Mto Ulai.
پس چشمان خود رابرافراشته، دیدم که ناگاه قوچی نزد نهر ایستاده بود که دو شاخ داشت و شاخهایش بلند بود ویکی از دیگری بلندتر و بلندترین آنها آخربرآمد. | ۳ 3 |
Nikatazama juu, na hapo mbele yangu kulikuwa na kondoo dume mwenye pembe mbili, akiwa amesimama kando ya mto, nazo pembe zake zilikuwa ndefu. Pembe moja ilikuwa ndefu kuliko hiyo nyingine, lakini iliendelea kukua baadaye.
و قوچ را دیدم که به سمت مغرب وشمال و جنوب شاخ میزد و هیچ وحشی با اومقاومت نتوانست کرد و کسی نبود که از دستش رهایی دهد و برحسب رای خود عمل نموده، بزرگ میشد. | ۴ 4 |
Nikamtazama yule kondoo dume alivyokuwa akishambulia kuelekea magharibi, kaskazini na kusini. Hakuna mnyama yeyote aliyeweza kusimama dhidi yake, wala hakuna aliyeweza kuokoa kutoka nguvu zake. Alifanya kama atakavyo, naye akawa mkuu.
و حینی که متفکر میبودم اینک بز نری ازطرف مغرب بر روی تمامی زمین میآمد و زمین را لمس نمی کرد و در میان چشمان بز نر شاخی معتبر بود. | ۵ 5 |
Nilipokuwa ninatafakari hili, ghafula beberu mwenye pembe moja kubwa sana katikati ya macho yake alikuja kutoka magharibi, akiruka kasi juu ya dunia yote bila kugusa ardhi.
و به سوی آن قوچ صاحب دو شاخ که آن را نزد نهر ایستاده دیدم آمد و بشدت قوت خویش نزد او دوید. | ۶ 6 |
Alikuja akimwelekea yule kondoo dume mwenye pembe mbili niliyemwona akisimama kando ya mto, akamshambulia kwa hasira nyingi.
و او را دیدم که چون نزدقوچ رسید با او بشدت غضبناک شده، قوچ را زد وهر دو شاخ او را شکست و قوچ را یارای مقاومت با وی نبود پس وی را به زمین انداخته، پایمال کردو کسی نبود که قوچ را از دستش رهایی دهد. | ۷ 7 |
Nikamwona akimshambulia yule kondoo dume kwa hasira nyingi, akimpiga yule kondoo dume na kuvunja pembe zake mbili. Yule kondoo dume hakuwa na nguvu za kumzuia yule beberu, hivyo akamwangusha yule kondoo dume chini na kumkanyaga, wala hakuna aliyeweza kumwokoa yule kondoo dume kutoka nguvu za huyo beberu.
وبز نر بینهایت بزرگ شد و چون قوی گشت آن شاخ بزرگ شکسته شد و در جایش چهار شاخ معتبر بسوی بادهای اربعه آسمان برآمد. | ۸ 8 |
Yule beberu akawa mkubwa sana, lakini katika kilele cha nguvu zake ile pembe yake ndefu ilivunjika, na mahali pake pakaota pembe nne kubwa kuelekea pande nne za dunia.
و ازیکی از آنها یک شاخ کوچک برآمد و به سمت جنوب و مشرق و فخر زمینها بسیار بزرگ شد. | ۹ 9 |
Kutoka mojawapo ya zile pembe nne palitokea pembe ndogo ukaongezeka nguvu kuelekea kusini, na kuelekea mashariki, na kuelekea Nchi ya Kupendeza.
و به ضد لشکر آسمانها قوی شده، بعضی ازلشکر و ستارگان را به زمین انداخته، پایمال نمود. | ۱۰ 10 |
Pembe hiyo ikaendelea kukua hadi kufikia jeshi la mbinguni, nayo ikalitupa baadhi ya jeshi la vitu vya angani hapa chini duniani, na kulikanyaga.
و به ضد سردار لشکر بزرگ شد و قربانی دایمی از او گرفته شد و مکان مقدس او منهدم گردید. | ۱۱ 11 |
Pembe hiyo ikajikweza ili iwe kama Mkuu wa hilo jeshi; ikamwondolea dhabihu ya kila siku, napo mahali pake patakatifu pakashushwa chini.
و لشکری به ضد قربانی دایمی، بهسبب عصیان (قوم به وی ) داده شد و آن (لشکر)راستی را به زمین انداختند و او (موافق رای خود) عمل نموده، کامیاب گردید. | ۱۲ 12 |
Kwa sababu ya uasi, jeshi la watakatifu na dhabihu za kila siku vikatiwa mikononi mwake. Ikafanikiwa katika kila kitu ilichofanya, nayo kweli ikatupwa chini.
و مقدسی را شنیدم که سخن میگفت و مقدس دیگری از آن یک که سخن میگفت، پرسید که رویا درباره قربانی دایمی و معصیت مهلک که قدس و لشکررا به پایمال شدن تسلیم میکند تا بکی خواهدبود. | ۱۳ 13 |
Kisha nikamsikia mtakatifu mmoja akizungumza na mtakatifu mwingine, akamwambia, “Je, itachukua muda gani maono haya yatimie: maono kuhusu dhabihu ya kila siku, uasi unaosababisha ukiwa, kutwaliwa kwa mahali patakatifu, na jeshi litakalokanyagwa chini ya nyayo?”
و او به من گفت: «تا دو هزار و سیصد شام وصبح، آنگاه مقدس تطهیر خواهد شد.» | ۱۴ 14 |
Akaniambia, “Itachukua siku 2,300. Ndipo mahali patakatifu patawekwa wakfu tena.”
و چون من دانیال رویا را دیدم و معنی آن راطلبیدم، ناگاه شبیه مردی نزد من بایستاد. | ۱۵ 15 |
Mimi Danieli nilipokuwa ninaangalia maono na kujaribu kuelewa, mbele yangu alisimama mmoja aliyefanana na mwanadamu.
وآواز آدمی را از میان (نهر) اولای شنیدم که نداکرده، میگفت: «ای جبرائیل این مرد را از معنیاینرویا مطلع ساز.» | ۱۶ 16 |
Kisha nikasikia sauti ya mwanadamu kutoka Mto Ulai ikiita, “Gabrieli, mwambie mtu huyu maana ya maono haya.”
پس او نزد جایی که ایستاده بودم آمد و چون آمد من ترسان شده، به روی خود درافتادم و او مرا گفت: «ای پسر انسان بدانکه اینرویا برای زمان آخر میباشد.» | ۱۷ 17 |
Alipokuwa akikaribia pale nilipokuwa nimesimama, niliogopa, nikaanguka kifudifudi. Akaniambia, “Mwana wa mwanadamu, fahamu kuwa maono haya yanahusu siku za mwisho.”
و حینی که او با من سخن میگفت، من برروی خود بر زمین در خواب سنگین میبودم و اومرا لمس نموده، در جایی که بودم برپا داشت. | ۱۸ 18 |
Alipokuwa akinena nami, nilikuwa katika usingizi mzito, huku nimelala kifudifudi. Ndipo aliponigusa na kunisimamisha wima.
و گفت: «اینک من تو را از آنچه در آخر غضب واقع خواهد شد اطلاع میدهم زیرا که انتها درزمان معین واقع خواهد شد. | ۱۹ 19 |
Akaniambia, “Nitakuambia yale yatakayotokea baadaye wakati wa ghadhabu, kwa sababu maono haya yanahusu wakati wa mwisho ulioamriwa.
اما آن قوچ صاحب دو شاخ که آن را دیدی پادشاهان مادیان و فارسیان میباشد. | ۲۰ 20 |
Kondoo dume mwenye pembe mbili ambaye ulimwona anawakilisha wafalme wa Umedi na Uajemi.
و آن بز نر ستبر پادشاه یونان میباشد و آن شاخ بزرگی که در میان دوچشمش بود پادشاه اول است. | ۲۱ 21 |
Yule beberu mwenye nywele nyingi ni mfalme wa Uyunani, nayo ile pembe ndefu katikati ya macho yake ni mfalme wa kwanza.
و اما آن شکسته شدن و چهار در جایش برآمدن، چهارسلطنت از قوم او اما نه از قوت او برپا خواهندشد. | ۲۲ 22 |
Zile pembe nne zilizoota badala ya ile pembe iliyovunjika zinawakilisha falme nne ambazo zitatokea kutoka taifa lake, lakini hakuna hata mmoja utakaokuwa na nguvu kama ule uliovunjika.
و در آخر سلطنت ایشان چون گناه عاصیان به اتمام رسیده باشد، آنگاه پادشاهی سخت روی و در مکرها ماهر، خواهد برخاست. | ۲۳ 23 |
“Katika sehemu ya mwisho ya utawala wao, wakati waasi watakapokuwa waovu kabisa, atainuka mfalme mwenye uso mkali, aliye stadi wa hila.
و قوت او عظیم خواهد شد، لیکن نه از توانایی خودش. و خرابیهای عجیب خواهد نمود وکامیاب شده، (موافق رای خود) عمل خواهدنمود و عظما و قوم مقدسان را هلاک خواهدنمود. | ۲۴ 24 |
Atakuwa na nguvu nyingi, lakini si kwa uwezo wake mwenyewe. Atasababisha uharibifu wa kutisha, na atafanikiwa kwa chochote anachofanya. Atawaangamiza watu maarufu na watu watakatifu.
و از مهارت او مکر در دستش پیش خواهد رفت و در دل خود مغرور شده، بسیاری را بغته هلاک خواهد ساخت و با امیر امیران مقاومت خواهد نمود، اما بدون دست، شکسته خواهد شد. | ۲۵ 25 |
Atasababisha udanganyifu ustawi, naye atajihesabu mwenyewe kuwa bora. Wakati wajisikiapo kuwa wako salama, atawaangamiza wengi, na kushindana na Mkuu wa wakuu. Lakini ataangamizwa, isipokuwa si kwa uwezo wa mwanadamu.
پس رویایی که درباره شام و صبح گفته شد یقین است اما تو رویا را بر هم نه زیرا که بعد از ایام بسیار واقع خواهد شد.» | ۲۶ 26 |
“Maono kuhusu jioni na asubuhi ambayo umepewa ni kweli, lakini yatie muhuri maono haya, kwa maana yanahusu wakati mrefu ujao.”
آنگاه من دانیال تا اندک زمانی ضعیف وبیمار شدم. پس برخاسته، بهکارهای پادشاه مشغول گردیدم، اما درباره رویا متحیر ماندم واحدی معنی آن را نفهمید. | ۲۷ 27 |
Mimi Danieli nilikuwa nimechoka sana, na nikalala nikiwa mgonjwa kwa siku kadhaa. Ndipo nikaamka, nikaenda kwenye shughuli za mfalme. Nilifadhaishwa na maono hayo, nami sikuweza kuyaelewa.