< دانیال 4 >

از نبوکدنصر پادشاه، به تمامی قومها و امت‌ها و زبانها که بر تمامی زمین ساکنندسلامتی شما افزون باد! ۱ 1
Mfalme Nebukadneza, Kwa kabila za watu, mataifa na watu wa kila lugha, wanaoishi katika ulimwengu wote: Mafanikio yawe kwenu sana!
من مصلحت دانستم که آیات و عجایبی را که خدای تعالی به من نموده است بیان نمایم. ۲ 2
Ni furaha yangu kuwaambia kuhusu ishara za miujiza na maajabu ambayo Mungu Aliye Juu Sana amenifanyia.
آیات او چه قدر بزرگ وعجایب او چه قدر عظیم است. ملکوت اوملکوت جاودانی است و سلطنت او تا ابدالاباد. ۳ 3
Ishara zake ni kuu aje, na maajabu yake yana nguvu aje! Ufalme wake ni ufalme wa milele; enzi yake hudumu kutoka kizazi hadi kizazi.
من که نبوکدنصر هستم در خانه خود مطمئن ودر قصر خویش خرم می‌بودم. ۴ 4
Mimi, Nebukadneza, nilikuwa nyumbani katika jumba langu la kifalme, nikiwa ninaishi kwa raha na hali ya kufanikiwa.
خوابی دیدم که مرا ترسانید و فکرهایم در بسترم و رویاهای سرم مرا مضطرب ساخت. ۵ 5
Niliota ndoto iliyoniogopesha. Nilipokuwa nimelala kitandani mwangu, njozi na maono yaliyopita mawazoni mwangu vilinitisha.
پس فرمانی از من صادرگردید که جمیع حکیمان بابل را به حضورم بیاورند تا تعبیر خواب را برای من بیان نمایند. ۶ 6
Hivyo nikaagiza kwamba watu wote wenye hekima wa Babeli waletwe mbele yangu kunifasiria ndoto yangu.
آنگاه مجوسیان و جادوگران و کلدانیان ومنجمان حاضر شدند و من خواب را برای ایشان بازگفتم لیکن تعبیرش را برای من بیان نتوانستندنمود. ۷ 7
Walipokuja waganga, wasihiri, wanajimu na waaguzi, niliwaambia ndoto yangu, lakini hawakuweza kunifasiria.
بالاخره دانیال که موافق اسم خدای من به بلطشصر مسمی است و روح خدایان قدوس دراو می‌باشد، درآمد و خواب را به او باز‌گفتم. ۸ 8
Mwishoni, Danieli alikuja mbele yangu nikamweleza hiyo ndoto. (Danieli anaitwa Belteshaza, kwa jina la mungu wangu, nayo roho ya miungu mitakatifu inakaa ndani yake.)
که «ای بلطشصر، رئیس مجوسیان، چون می‌دانم که روح خدایان قدوس در تو می‌باشد و هیچ سری برای تو مشکل نیست، پس خوابی که دیده‌ام وتعبیرش را به من بگو. ۹ 9
Nilisema, “Belteshaza, mkuu wa waganga, ninajua kuwa roho ya miungu mitakatifu iko ndani yako, wala hakuna siri iliyo ngumu kwako. Hii ndiyo ndoto yangu, nifasirie.
رویاهای سرم در بسترم این بود که نظرکردم و اینک درختی در وسط زمین که ارتفاعش عظیم بود. ۱۰ 10
Haya ndiyo maono niliyoona nilipokuwa nimelala kitandani mwangu: Nilitazama, na mbele yangu ulisimama mti katikati ya nchi. Ulikuwa mrefu sana.
این درخت بزرگ و قوی گردید وبلندیش تا به آسمان رسید و منظرش تا اقصای تمامی زمین بود. ۱۱ 11
Mti ule ulikua, ukawa mkubwa na wenye nguvu, nayo ncha yake ikagusa anga; ulionekana mpaka miisho ya dunia.
برگهایش جمیل و میوه‌اش بسیار و آذوقه برای همه در آن بود. حیوانات صحرا در زیر آن سایه گرفتند و مرغان هوا برشاخه هایش ماوا گزیدند و تمامی بشر از آن پرورش یافتند. ۱۲ 12
Majani yake yalikuwa ya kupendeza, matunda yake yalikuwa mengi, na juu yake kulikuwa na chakula kwa ajili ya wote. Chini ya kivuli chake wanyama wa kondeni walipata hifadhi, na ndege wa angani waliishi katika matawi yake. Kila kiumbe kililishwa kutokana na mti huo.
در رویاهای سرم در بسترم نظر کردم و اینک پاسبانی و مقدسی از آسمان نازل شد، ۱۳ 13
“Katika maono niliyoyaona nikiwa nimelala kitandani mwangu, nilitazama, na mbele yangu alikuwepo mlinzi, aliye mtakatifu, akishuka kutoka mbinguni.
که به آواز بلند ندا درداد و چنین گفت: درخت را ببرید و شاخه هایش را قطع نمایید و برگهایش را بیفشانید و میوه هایش راپراکنده سازید تا حیوانات از زیرش و مرغان ازشاخه هایش آواره گردند. ۱۴ 14
Akaita kwa sauti kubwa: ‘Kateni mti huu, myafyeke matawi yake; yaondoeni majani yake na kuyatawanya matunda yake. Wanyama na wakimbie kutoka chini yake na ndege waondoke kutoka matawi yake.
لیکن کنده ریشه هایش را با بند آهن و برنج در زمین در میان سبزه های صحرا واگذارید و از شبنم آسمان ترشود و نصیب او از علف زمین با حیوانات باشد. ۱۵ 15
Lakini acheni kisiki chake na mizizi, kikiwa kimefungwa kwa chuma na shaba, kibaki ardhini, kwenye majani ya kondeni. “‘Mwacheni aloweshwe na umande wa mbinguni, naye aachwe aishi pamoja na wanyama miongoni mwa mimea ya dunia.
دل او از انسانیت تبدیل شود و دل حیوان را به او بدهند و هفت زمان براو بگذرد. ۱۶ 16
Akili yake na ibadilishwe kutoka ile ya mwanadamu na apewe akili ya mnyama, mpaka nyakati saba zipite juu yake.
این امر ازفرمان پاسبانان شده و این حکم از کلام مقدسین گردیده است تا زندگان بدانند که حضرت متعال بر ممالک آدمیان حکمرانی می‌کند و آن را بهرکه می‌خواهد می‌دهد و پست‌ترین مردمان را بر آن نصب می‌نماید. ۱۷ 17
“‘Uamuzi huu umetangazwa na walinzi, hukumu imetangazwa na watakatifu, ili walio hai wajue kuwa Aliye Juu Sana ndiye anayetawala juu ya falme zote za wanadamu, naye humpa yeyote amtakaye na kumtawaza juu yake hata yeye aliye mnyonge sana miongoni mwa wanadamu.’
این خواب را من که نبوکدنصرپادشاه هستم دیدم و تو‌ای بلطشصر تعبیرش رابیان کن زیرا که تمامی حکیمان مملکتم نتوانستندمرا از تعبیرش اطلاع دهند، اما تو می‌توانی چونکه روح خدایان قدوس در تو می‌باشد.» ۱۸ 18
“Hii ndiyo ndoto niliyoipata mimi, Mfalme Nebukadneza. Sasa Belteshaza, niambie maana yake, kwa maana hakuna hata mmoja wa wenye hekima katika ufalme wangu anayeweza kunifasiria. Bali wewe waweza, kwa sababu roho ya miungu mitakatifu imo ndani yako.”
آنگاه دانیال که به بلطشصر مسمی می‌باشد، ساعتی متحیر ماند و فکرهایش او رامضطرب ساخت. پس پادشاه متکلم شده، گفت: «ای بلطشصر خواب و تعبیرش تو را مضطرب نسازد.» بلطشصر در جواب گفت: «ای آقای من! خواب از برای دشمنانت و تعبیرش از برای خصمانت باشد. ۱۹ 19
Ndipo Danieli (aliyeitwa pia Belteshaza) alipofadhaika sana kwa muda, nayo mawazo yake yakamtia hofu. Basi mfalme akasema, “Belteshaza, usiruhusu ndoto wala maana yake kukutia hofu.” Belteshaza akamjibu, “Bwana wangu, laiti ndoto hii ingehusu adui zako, na maana yake iwahusu watesi wako!
درختی که دیدی که بزرگ وقوی گردید و ارتفاعش تا به آسمان رسید ومنظرش به تمامی زمین ۲۰ 20
Mti uliouona, uliokua ukawa mkubwa na wenye nguvu, nayo ncha yake ikagusa anga na kuonekana duniani kote,
و برگهایش جمیل و میوه‌اش بسیار و آذوقه برای همه در آن بود وحیوانات صحرا زیرش ساکن بودند و مرغان هوادر شاخه هایش ماوا گزیدند، ۲۱ 21
ukiwa na majani ya kupendeza na matunda mengi, ukitoa chakula kwa wote, na ukiwapa hifadhi wanyama wa kondeni na kuwa mahali pa viota katika matawi yake kwa ajili ya ndege wa angani.
‌ای پادشاه آن درخت تو هستی زیرا که تو بزرگ و قوی گردیده‌ای و عظمت تو چنان افزوده شده است که به آسمان رسیده و سلطنت تو تا به اقصای زمین. ۲۲ 22
Ee mfalme, wewe ndiwe ule mti! Umekuwa mkubwa na mwenye nguvu, nao ukuu wako umekua mpaka kufika juu angani, nayo mamlaka yako yameenea mpaka miisho ya dunia.
و چونکه پادشاه پاسبانی و مقدسی را دید که ازآسمان نزول نموده، گفت: درخت را ببرید و آن راتلف سازید، لیکن کنده ریشه هایش را با بند آهن و برنج در زمین در میان سبزه های صحراواگذارید و از شبنم آسمان تر شود و نصیبش باحیوانات صحرا باشد تا هفت زمان بر آن بگذرد، ۲۳ 23
“Ee mfalme, wewe ulimwona mlinzi, aliye mtakatifu, akishuka kutoka mbinguni na kusema, ‘Ukateni mti na kuuangamiza, lakini kiacheni kisiki kikiwa kimefungwa kwa chuma na kwa shaba, kwenye majani ya kondeni, wakati mizizi yake inabaki ardhini. Mwacheni aloweshwe na umande wa mbinguni, mwacheni aishi kama wanyama pori mpaka nyakati saba zipite juu yake.’
‌ای پادشاه تعبیر این است و فرمان حضرت متعال که بر آقایم پادشاه وارد شده است همین است، ۲۴ 24
“Ee mfalme, hii ndiyo tafsiri, na hii ni amri ya Aliye Juu Sana aliyoitoa dhidi ya bwana wangu mfalme:
که تو را از میان مردمان خواهند راند ومسکن تو با حیوانات صحرا خواهد بود و تو رامثل گاوان علف خواهند خورانید و تو را از شبنم آسمان تر خواهند ساخت و هفت زمان بر توخواهد گذشت تا بدانی که حضرت متعال برممالک آدمیان حکمرانی می‌کند و آن را بهر‌که می‌خواهد عطا می‌فرماید. ۲۵ 25
Wewe utafukuzwa mbali na wanadamu, nawe utaishi pamoja na wanyama pori; utakula manyasi kama ngʼombe, na kuloana kwa umande wa mbinguni. Nyakati saba zitapita juu yako, mpaka utakapokubali kuwa Yeye Aliye Juu Sana ndiye anayetawala juu ya falme za wanadamu, naye humtawaza yeyote amtakaye.
و چون گفتند که کنده ریشه های درخت را واگذارید، پس سلطنت تو برایت برقرار خواهد ماند بعد از آنکه دانسته باشی که آسمانها حکمرانی می‌کنند. ۲۶ 26
Amri ya kuacha kisiki pamoja na mizizi yake inamaanisha kwamba ufalme wako utarejezwa kwako utakapokubali kwamba Mbingu ndizo zitawalazo.
لهذا‌ای پادشاه نصیحت من تو را پسند آید و گناهان خودرا به عدالت و خطایای خویش را به احسان نمودن بر فقیران فدیه بده که شاید باعث طول اطمینان تو باشد.» ۲۷ 27
Kwa hiyo, ee mfalme, uwe radhi kupokea shauri langu: Acha dhambi zako kwa kutenda yaliyo haki, ukaache uovu wako, na uwe na huruma kwa walioonewa. Hivyo itawezekana baada ya hayo, mafanikio yako yakaendelea.”
این همه بر نبوکدنصرپادشاه واقع شد. ۲۸ 28
Haya yote yalimpata Mfalme Nebukadneza.
بعد از انقضای دوازده ماه او بالای قصرخسروی در بابل می‌خرامید. ۲۹ 29
Miezi kumi na miwili baadaye, mfalme alipokuwa akitembea juu ya paa la jumba la kifalme la Babeli,
و پادشاه متکلم شده، گفت: «آیا این بابل عظیم نیست که من آن را برای خانه سلطنت به توانایی قوت و حشمت جلال خود بنا نموده‌ام؟» ۳۰ 30
alisema, “Je, huu si Babeli mji mkuu nilioujenga kama makao ya kifalme, kwa uwezo wangu mkubwa, na kwa ajili ya utukufu wa enzi yangu?”
این سخن هنوز برزبان پادشاه بود که آوازی از آسمان نازل شده، گفت: «ای پادشاه نبوکدنصر به تو گفته می‌شود که سلطنت از تو گذشته است. ۳۱ 31
Maneno hayo yalikuwa bado katika midomo yake wakati sauti ilipokuja kutoka mbinguni, ikisema, “Mfalme Nebukadneza, hiki ndicho kilichoamriwa kwa ajili yako: Mamlaka yako ya ufalme yameondolewa kutoka kwako.
و تو را از میان مردم خواهند راند و مسکن تو با حیوانات صحراخواهد بود و تو را مثل گاوان علف خواهندخورانید و هفت زمان بر تو خواهد گذشت تابدانی که حضرت متعال بر ممالک آدمیان حکمرانی می‌کند و آن را بهر‌که می‌خواهدمی دهد.» ۳۲ 32
Utafukuzwa mbali na wanadamu, ukaishi pamoja na wanyama pori, na utakula manyasi kama ngʼombe. Nyakati saba zitapita juu yako, mpaka utakapokubali kuwa Yeye Aliye Juu Sana ndiye anayetawala juu ya falme za wanadamu, naye humtawaza yeyote amtakaye.”
در همان ساعت این امر بر نبوکدنصر واقع شد و از میان مردمان رانده شده، مثل گاوان علف می‌خورد و بدنش از شبنم آسمان تر می‌شد تامویهایش مثل پرهای عقاب بلند شد وناخنهایش مثل چنگالهای مرغان گردید. ۳۳ 33
Papo hapo yale yaliyokuwa yamesemwa kuhusu Nebukadneza yakatimia. Alifukuzwa mbali na wanadamu, akala majani kama ngʼombe. Mwili wake uliloweshwa kwa umande wa mbinguni mpaka nywele zake zikakua kama manyoya ya tai na kucha zake kama makucha ya ndege.
و بعد از انقضای آن ایام من که نبوکدنصرهستم، چشمان خود را بسوی آسمان برافراشتم و عقل من به من برگشت و حضرت متعال رامتبارک خواندم و حی سرمدی را تسبیح و حمدگفتم زیرا که سلطنت او سلطنت جاودانی وملکوت او تا ابدالاباد است. ۳۴ 34
Mwisho wa huo wakati, mimi Nebukadneza, niliinua macho yangu kuelekea mbinguni, nazo fahamu zangu zikanirudia. Ndipo nikamsifu Yeye Aliye Juu Sana, nikamheshimu na kumhimidi yeye aishiye milele. Utawala wake ni utawala wa milele; ufalme wake hudumu kutoka kizazi na kizazi.
و جمیع ساکنان جهان هیچ شمرده می‌شوند و با جنود آسمان وسکنه جهان بر وفق اراده خود عمل می‌نماید وکسی نیست که دست او را باز‌دارد یا او را بگویدکه چه می‌کنی. ۳۵ 35
Mataifa yote ya dunia yanahesabiwa kuwa si kitu. Hufanya kama atakavyo kwa majeshi ya mbinguni, na kwa mataifa ya dunia. Hakuna anayeweza kuuzuia mkono wake au kumwambia, “Umefanya nini wewe?”
در همان زمان عقل من به من برگشت و به جهت جلال سلطنت من حشمت وزینتم به من باز داده شد و مشیرانم و امرایم مراطلبیدند و بر سلطنت خود استوار گردیدم وعظمت عظیمی بر من افزوده شد. ۳۶ 36
Wakati huo huo fahamu zangu ziliponirudia, nikarudishiwa heshima yangu na fahari yangu kwa ajili ya utukufu wa ufalme wangu. Washauri wangu na wakuu wangu walikuja kunitafuta, nami nikarudishwa kwenye kiti changu cha ufalme hata nikawa mkuu kuliko mwanzoni.
الان من که نبوکدنصر هستم پادشاه آسمانها را تسبیح وتکبیر و حمد می‌گویم که تمام کارهای او حق و طریق های وی عدل است و کسانی که با تکبر راه می‌روند، او قادر است که ایشان را پست نماید. ۳۷ 37
Basi mimi, Nebukadneza, humhimidi, na humtukuza na kumsifu Mfalme wa mbinguni, kwa sababu kila kitu afanyacho ni haki, na njia zake zote ni adili. Nao waendao kwa kiburi anaweza kuwashusha.

< دانیال 4 >