< دوم سموئیل 23 >
و این است سخنان آخر داود: «وحی داود بن یسا. و وحی مردی که بر مقام بلند ممتاز گردید، مسیح خدای یعقوب، و مغنی شیرین اسرائیل. | ۱ 1 |
Haya ni maneno ya mwisho ya Daudi: “Neno la Daudi mwana wa Yese, neno la mtu aliyeinuliwa na Aliye Juu Sana, mtu aliyepakwa mafuta na Mungu wa Yakobo, mwimbaji wa nyimbo wa Israeli:
روح خداوند به وسیله من متکلم شد و کلام او بر زبانم جاری گردید. | ۲ 2 |
“Roho wa Bwana alinena kupitia kwangu, neno lake lilikuwa ulimini mwangu.
خدای اسرائیل متکلم شد و صخره اسرائیل مراگفت: آنکه بر مردمان حکمرانی کند، عادل باشدو با خدا ترسی سلطنت نماید. | ۳ 3 |
Mungu wa Israeli alinena, mwamba wa Israeli akaniambia: ‘Mtu anatawala watu kwa haki, wakati anapotawala akiwa na hofu ya Mungu,
و او خواهد بودمثل روشنایی صبح، وقتی که آفتاب طلوع نماید، یعنی صبح بیابر، هنگامی که علف سبز از زمین میروید، بهسبب درخشندگی بعد از باران. | ۴ 4 |
yeye ni kama mwanga wa asubuhi jua lichomozapo asubuhi isiyo na mawingu, kama mwanga baada ya mvua uchipuzao majani kutoka ardhini.’
یقین خانه من با خدا چنین نیست. لیکن عهدجاودانی با من بسته است، که در همهچیز آراسته و مستحکم است. و تمامی نجات و تمامی مسرت من این است، هرچند آن را نمو نمی دهد. | ۵ 5 |
“Je, si hivyo ilivyo nyumba yangu mbele za Mungu? Je, hajafanya Agano la milele nami, lililopangwa na kuimarishwa kila sehemu? Je, hatanifanya niufurahie wokovu wangu na kunijalia matakwa yangu yote?
لیکن جمیع مردان بلیعال مثل خارهایند که دورانداخته میشوند. چونکه آنها را بهدست نتوان گرفت. | ۶ 6 |
Lakini watu waovu wote watatupwa kando kama miiba, ambayo haikusanywi kwa mkono.
و کسیکه ایشان را لمس نماید، میبایدبا آهن و نی نیزه مسلح شود. و ایشان در مسکن خود با آتش سوخته خواهند شد.» | ۷ 7 |
Yeyote agusaye miiba hutumia chombo cha chuma au mpini wa mkuki, nayo huchomwa pale ilipo.”
و نامهای شجاعانی که داود داشت این است: یوشیب بشبت تحکمونی که سردار شالیشیم بودکه همان عدینو عصنی باشد که بر هشتصد نفرتاخت آورد و ایشان را در یک وقت کشت. | ۸ 8 |
Haya ndiyo majina ya mashujaa wa Daudi: Yosheb-Bashebethi, Mtahkemoni, alikuwa kiongozi wa wale Watatu; yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 800, ambao aliwaua katika pambano moja.
و بعد از او العازار بن دودو ابن اخوخی، یکی از آن سه مرد شجاع که با داود بودند، هنگامی که فلسطینیان را که در آنجا برای جنگ جمع شده، ومردان اسرائیل رفته بودند، به مقاتله طلبیدند. | ۹ 9 |
Wa pili wake alikuwa Eleazari mwana wa Dodai, Mwahohi. Akiwa mmojawapo wa wale mashujaa watatu, alikuwa pamoja na Daudi wakati waliwadhihaki Wafilisti waliokuwa wamekusanyika huko Pas-Damimu kwa ajili ya vita. Kisha watu wa Israeli wakarudi nyuma,
واما او برخاسته، با فلسطینیان جنگ کرد تا دستش خسته شد و دستش به شمشیر چسبید و خداونددر آن روز، ظفر عظیمی داد، و قوم در عقب اوفقط برای غارت کردن برگشتند. | ۱۰ 10 |
lakini yeye alisimama imara akawaua Wafilisti hadi mkono wake ukachoka na ukagandamana na upanga. Bwana akawapa ushindi mkubwa siku ile. Vikosi vikarudi kwa Eleazari, kuteka tu nyara za waliokufa.
و بعد از او شمه بن آجی هراری بود وفلسطینیان، لشکری فراهم آوردند، در جایی که قطعه زمینی پر از عدس بود، و قوم از حضورفلسطینیان فرار میکردند. | ۱۱ 11 |
Aliyefuata alikuwa Shama mwana wa Agee, Mharari. Wafilisti walipokusanyika pamoja mahali palipokuwa shamba lililojaa dengu, vikosi vya Israeli viliwakimbia.
آنگاه او در میان آن قطعه زمین ایستاد و آن را نگاه داشته، فلسطینیان را شکست داد و خداوند ظفر عظیمی داد. | ۱۲ 12 |
Lakini Shama akasimama imara katikati ya lile shamba. Akalitetea na kuwaua Wafilisti, naye Bwana akawapa ushindi mkubwa.
و سه نفر از آن سی سردار فرود شده، نزدداود در وقت حصاد به مغاره عدلام آمدند، ولشکر فلسطینیان در وادی رفائیم اردو زده بودند. | ۱۳ 13 |
Wakati wa mavuno, viongozi watatu kati ya viongozi thelathini walishuka, wakamwendea Daudi katika pango la Adulamu, wakati kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la Warefai.
و داود در آن وقت در ملاذ خویش بود و قراول فلسطینیان در بیت لحم. | ۱۴ 14 |
Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome, na kambi ya Wafilisti ilikuwa huko Bethlehemu.
و داود خواهش نموده، گفت: «کاش کسی مرا از چاهی که نزددروازه بیت لحم است آب بنوشاند.» | ۱۵ 15 |
Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu!”
پس آن سه مرد شجاع، لشکر فلسطینیان را از میان شکافته، آب را از چاهی که نزد دروازه بیت لحم است کشیده، برداشتند و آن را نزد داود آوردند، اما نخواست که آن را بنوشد و آن را به جهت خداوند ریخت. | ۱۶ 16 |
Basi mashujaa hao watatu wakapenya katikati ya Wafilisti, wakaenda kuchota maji kutoka kwa kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu, wakamletea Daudi. Lakini Daudi akakataa kuyanywa. Badala yake, aliyamimina mbele za Bwana.
و گفت: «ای خداوند حاشا ازمن که این کار را بکنم، مگر این خون آن کسان نیست که به خطر جان خود رفتند؟» از این جهت نخواست که بنوشد. کاری که این سه مرد کردند، این است. | ۱۷ 17 |
Akasema, “Iwe mbali nami, Ee Bwana, kufanya kitu hiki. Je, hii si damu ya watu ambao walikwenda kwa kuhatarisha maisha yao?” Naye Daudi hakuyanywa. Haya yalifanywa na hao mashujaa watatu.
و ابیشای، برادر یوآب بن صرویه، سردارسه نفر بود و نیزه خود را بر سیصد نفر حرکت داده، ایشان را کشت و در میان آن سه نفر اسم یافت. | ۱۸ 18 |
Abishai ndugu yake Yoabu mwana wa Seruya ndiye alikuwa kiongozi wa hao Watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300 ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao Watatu.
آیا از آن سه نفر مکرم تر نبود؟ پس سردار ایشان شد لیکن به سه نفر اول نرسید. | ۱۹ 19 |
Je, hakupata heshima kubwa zaidi kuliko hao Watatu? Alikuwa jemadari wao, ingawa hakuhesabiwa miongoni mwao.
و بنایاهو ابن یهویاداع، پسر مردی شجاع قبصئیلی، که کارهای عظیم کرده بود، دو پسراریئیل موآبی را کشت و در روز برف به حفرهای فرود شده، شیری را بکشت. | ۲۰ 20 |
Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabseeli ambaye alifanya mambo makubwa ya ujasiri. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka shimoni kulipokuwa na theluji na kumuua simba.
و مرد خوش اندام مصریای را کشت و آن مصری در دست خود نیزهای داشت اما نزد وی با چوب دستی رفت و نیزه را از دست مصری ربود و وی را با نیزه خودش کشت. | ۲۱ 21 |
Pia alimuua Mmisri mrefu mkubwa. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki mkononi mwake, Benaya alimwendea akiwa na rungu. Alipokonya mkuki kutoka mkononi mwa Mmisri na kumuua kwa mkuki wake mwenyewe.
و بنایاهو ابن یهویاداع این کارها را کرد و در میان آن سه مرد شجاع اسم یافت. | ۲۲ 22 |
Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada; naye pia alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu.
و از آن سی نفر مکرمتر شد لیکن به آن سه نفر اول نرسید و داود او را بر اهل مشورت خود گماشت. | ۲۳ 23 |
Yeye aliheshimiwa zaidi ya wale Thelathini, lakini hakujumuishwa miongoni mwa wale Watatu. Daudi akamweka kuwa kiongozi wa walinzi wake.
و عسائیل برادر یوآب یکی از آن سی نفربود و الحانان بن دودوی بیت لحمی، | ۲۴ 24 |
Miongoni mwa wale Thelathini walikuwepo: Asaheli ndugu wa Yoabu; Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu;
و شمه حرودی و الیقای حرودی، | ۲۵ 25 |
Shama, Mharodi; Elika, Mharodi;
و حالص فلطی و عیرا ابن عقیش تقوعی، | ۲۶ 26 |
Helesi, Mpalti; Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa;
و ابیعزر عناتوتی ومبونای حوشاتی، | ۲۷ 27 |
Abiezeri kutoka Anathothi; Mebunai, Mhushathi;
و صلمون اخوخی و مهرای نطوفاتی، | ۲۸ 28 |
Salmoni, Mwahohi; Maharai, Mnetofathi;
و حالب بن بعنه نطوفاتی و اتای بن ریبای از جبعه بنی بنیامین، | ۲۹ 29 |
Heledi mwana wa Baana, Mnetofathi; Itai mwana wa Ribai kutoka Gibea ya Benyamini;
و بنایای فرعاتونی و هدای از وادیهای جاعش، | ۳۰ 30 |
Benaya Mpirathoni; Hidai kutoka mabonde ya Gaashi;
و ابوعلبون عرباتی و عزموت برحومی، | ۳۱ 31 |
Abi-Alboni, Mwaribathi; Azmawethi, Mbarhumi;
و الیحبای شعلبونی و از بنی یاشن یوناتان، | ۳۲ 32 |
Eliaba, Mshaalboni; wana wa Yasheni; Yonathani
و شمه حراری و اخیام بن شارر اراری، | ۳۳ 33 |
mwana wa Shama, Mharari; Ahiamu mwana wa Sharari, Mharari;
و الیفلط بن احسبای ابن معکاتی و الیعام بن اخیتوفل جیلونی، | ۳۴ 34 |
Elifeleti mwana wa Ahasbai, Mmaakathi; Eliamu mwana wa Ahithofeli, Mgiloni;
وحصرای کرملی و فعرای اربی، | ۳۵ 35 |
Hezro, Mkarmeli; Paarai, Mwarbi;
و یجال بن ناتان از صوبه و بانی جادی، | ۳۶ 36 |
Igali mwana wa Nathani kutoka Soba; Bani, Mgadi;
و صالق عمونی ونحرای بئیروتی که سلاحداران یوآب بن صرویه بودند، | ۳۷ 37 |
Seleki, Mwamoni; Naharai, Mbeerothi, aliyekuwa mbeba silaha za Yoabu mwana wa Seruya;
و عیرای یتری و جارب یتری، | ۳۸ 38 |
Ira, Mwithiri; Garebu, Mwithiri;
واوریای حتی، که جمیع اینها سی و هفت نفربودند. | ۳۹ 39 |
na Uria, Mhiti. Jumla yao wote walikuwa watu thelathini na saba.