< Jobs 31 >

1 Med augo hev eg gjort ei pakt; eg skal’kje skygna etter møy.
Nimefanya patano na macho yangu; ni kwa namna gani tena napaswa kumtazama mwanamwali kwa tamaa?
2 Kva gav meg elles Gud der uppe? Kva arv gav Allvald frå det høge?
Ni sehemu gani kutoka kwa Mungu juu, na urithi gani kutoka kwake mwenye nguvu aliye juu?
3 Kjem ikkje udådsmann i naud? Og illgjersmenn i ulukka?
Nilikuwa nafikiri kwamba majanga ni kwa watu wasio na haki, na misiba ni kwa ajili ya watu watendao mabaya.
4 Ser ikkje han på mine vegar? Tel ikkje han kvart stig eg gjeng?
Je Mungu hazioni njia zangu na kuzihesabu hatua zangu zote?
5 Dersom eg fram med fals hev fare, og foten sprunge etter svik
Kama nimetembea katika udanganyifu, kama mguu wangu umeharakisha katika uongo,
6 - Gud vege meg på rettferds vegt, so han kann sjå eg skuldlaus er! -
na nipimwe katika vipimo vilivyo sawa ili kwamba Mungu aujue uadilifu wangu.
7 Veik mine stig frå vegen av, hev hjarta etter augo gjenge, var det ein flekk på mine hender,
Kama hatua zangu zimegeuka kutoka katika njia sahihi, kama moyo wangu umetembea kwa kufuata macho yangu, na kama doa lolote la uchafu limeng'ang'ania katika mikono yangu,
8 so gjev ein annan et mitt såd, og riv mi planting upp med rot!
na kisha mimi nipande na mtu mwingine na ale; mavuno na yang'olewe katika shamba langu.
9 Let eg min hug av kvinna dåra, sneik eg til grannens dør meg fram,
Na kama moyo wangu umevutiwa na mwanamke mwingine, ikiwa nimelala na mke wa jirani yangu katika hali ya kusubiria katika mlango wake,
10 so lat mitt viv åt andre mala, og andre yver ho seg bøygje!
na ndipo mke wangu na asage nafaka kwa mwanaume mwingine, na wanaume wengine na walale naye.
11 For dette er ei skjemdarferd, eit brot som dom og straff fortener,
Na kwa hilo litakuwa ni kosa kubwa; kwa kweli, utakuwa ni uovu wa kuadhibiwa na waamuzi.
12 ein eld som eta vil til avgrunns og øydeleggja all mi eiga.
Kwa kuwa ni moto ambao unateketeza kila kitu kwa uharibifu, na kwamba utaunguza mavuno yangu yote.
13 Vanvyrd’ eg retten åt min træl og trælkvinna i trætta med deim?
Ikiwa nilikataa ombi la haki kutoka kwa watumishi wangu wa kiume na wa kike wakati walipohojiana nami,
14 - Kva gjord’ eg då, når Gud reis upp? Kva svara eg, når han meg klaga?
kisha nini basi ningefanya wakati Mungu anapoinuka ili kunishitaki mimi? Atakapokuja kunihukumu, nitamjibuje?
15 Dei er som meg i morsliv skapte; ein forma oss i moderfang -
Je yeye aliyenifanya mimi tumboni hakuwafanya wao pia? Je yeye si yeye yule aliyetuumba sisi wote katika tumbo?
16 Um eg sagde nei når arming bad, og let enkja gråtande gå burt,
kama nimewanyima watu masikini matakwa yao, au kama nimesababisha macho ya wajane yafifie kwa kulia,
17 hev eg mitt brød åleine ete, so farlaus inkje fekk ein bit,
au ikiwa kama nimekula kipande changu na sijawaruhusu wale wasio na baba kukila pia -
18 - nei, far for han eg var frå yngdi, frå morsliv var eg hennar førar -
kwasababu tangu ujana wangu yatima walikua pamoja nami kama kuwa na baba, nami nimemwongoza mama yake, mjane, tangu katika tumbo la mama yangu mwenyewe.
19 Såg eg ein stakar utan klæde, ein fatig utan yverplagg,
ikiwa nimemwona yeyote akiangamia kwa kwa kukosa mavazi, au kama nimemwona mtu mhitaji akiwa hana nguo;
20 og so hans lender ei meg signa, og ei mi saueull han vermde,
ikiwa moyo wake haujanibariki kwasababu amekuwa hajatiwa joto na sufu ya kondoo zangu,
21 hev eg mot farlaus handi lyft, av di eg medhald fekk i retten:
ikiwa nimeinua juu mkono wangu kinyume na watu wasio na baba kwa kuwa niliona msaada wangu katika lango la mji, na kisha kuleta mashitaka dhidi yangu.
22 Let herdi mi or led då losna, og armen brotna frå sitt bein!
Ndipo bega langu na lianguake kutoka katika sehemu yake, na mkono wangu uvunjike katika kiungo chake.
23 For eg var ovleg rædd Guds straff, eg magtlaus stod framfor hans velde.
Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu; kwasababu ya mawazo ya ukuu wake, nisingeweza kufanya mambo hayo.
24 Um eg mi lit til gullet sette, og voni til det fine gull,
Kama ningeifanya dhahabu kuwa tumaini langu, na kama ningesema kwa dhahabu safi, 'wewe unanifanya kuwa na tumaini';
25 Gledde eg meg ved auka rikdom, og alt eg vann meg med mi hand,
na kama nimefurahi kwasababu ya utajiri wangu ulikuwa mkubwa, kwa kuwa mkono wangu umepata mali nyingi, na kisha kuleta mashitaka dhidi yangu!
26 såg eg på ljoset når det stråla, på månen der han skreid i glans,
Ikiwa nimeliona jua lilipowaka, au mwezi ukitembea katika mng'ao wake,
27 vart hjarta mitt i løyndom dåra, so kyss på hand til deim eg sende,
na kama moyo wangu umevutwa kwa siri, ili kwamba mdomo wangu umeubusu mkono wangu katika ibada yao -
28 so var det og straffande brot, då neitta eg min Gud der uppe.
hili nalo pia lingekuwa ni ubaya wa kuadhibiwa na waamuzi, kwa kuwa ningekuwa nimemkana Mungu aliyejuu.
29 Hev eg meg gledt ved uvens uferd, og jubla når han kom i skade,
Ikiwa nimefurahia uharibifu wa yeyote ambaye ananichukia mimi, au kuwapa hongera wakati majanga yanapowapata, ndipo ulete mashitaka dhidi yangu!
30 - men eg let ikkje munnen synda og banna honom ifrå livet -
Kwa kweli sijauruhusu hata mdomo wangu kutenda dhambi kwa kuuomba uhai wake kwa laana.
31 hev ei mitt husfolk stendigt sagt: «Kven gjekk vel svolten frå hans bord?»
Ikiwa watu wa hema yangu hawajasema,' Nani aweza kumpata mtu ambaye hayashibishwa na chakula cha Ayubu?
32 - Eg let’kje framand natta ute; for ferdamann eg opna døri -
(hata mgeni hajawahi kukaa katika pembe ya mji, kwa kuwa siku zote nimefungua milango yangu kwa ajili ya wasafiri), na kama haiko hivyo, ndipo mlete mashitaka kinyume nami!
33 hev eg som Adam dult mi synd, og løynt mi misgjerd i min barm,
Ikiwa, kama binadamu nimezificha dhambi zangu kwa kuficha hatia ndani ya kanzu yangu -
34 di eg var rædd den store hop og ottast spott frå ættefrendar, so stilt eg heldt meg innum dører?
kwa kuwa niliogopa kusanyiko kubwa, kwasababu ya matwezo ya familia yaliniogopesha, hivyo basi nilinyamaza kimya na sikuweza kwenda nje, basi nileteni mashitaka dhidi yangu!
35 Å, vilde nokon høyra på meg! Sjå her er underskrifti mi, lat berre Allvald svara meg! Fekk eg den skrift min motpart skreiv,
Ee, kama nilikuwa na mtu wa kunisikiliza! Ona, hii ni saini yangu; na Mwenye nguvu na anijibu! Ikiwa nilikuwa na shitaka rasmi ambalo adui yangu ameliandika!
36 den skulde eg på oksli bera og binda på meg som ein krans
Hakika ningelibeba hadharani juu ya bega langu; ningeliweka juu kama taji.
37 eg melde honom kvart mitt stig, og som ein hovding møta honom.
Ningemweleza hesabu ya hatua zangu; na kama mwana wa mfalme mwenye kujiamini ningepanda kwenda kwake.
38 Dersom min åker klagar meg, og um plogforerne lyt gråta,
Kama nchi yangu ingelia dhidi yangu, na matuta yake yaomboleza pamoja,
39 åt eg hans grøda ubetalt, tok livet eg av eigarmannen:
ikiwa nimekula mavuno yake bila kulipia au kama nimesababisha wamiliki wake kupoteza maisha yao,
40 Lat då for kveite klunger gro, og ugras der eg sådde bygg!» Her endar Jobs tale.
ndipo miiba na iote badala ya ngano na magugu badala ya shayiri.” Maneno ya Ayubu yamemalizika.

< Jobs 31 >