< Jobs 31 >
1 Med augo hev eg gjort ei pakt; eg skal’kje skygna etter møy.
“Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.
2 Kva gav meg elles Gud der uppe? Kva arv gav Allvald frå det høge?
Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu, urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?
3 Kjem ikkje udådsmann i naud? Og illgjersmenn i ulukka?
Je, si uharibifu kwa watu waovu, maangamizi kwa wale watendao mabaya?
4 Ser ikkje han på mine vegar? Tel ikkje han kvart stig eg gjeng?
Je, yeye hazioni njia zangu na kuihesabu kila hatua yangu?
5 Dersom eg fram med fals hev fare, og foten sprunge etter svik
“Kama nimeishi katika uongo au mguu wangu umekimbilia udanganyifu,
6 - Gud vege meg på rettferds vegt, so han kann sjå eg skuldlaus er! -
Mungu na anipime katika mizani za uaminifu, naye atajua kwamba sina hatia:
7 Veik mine stig frå vegen av, hev hjarta etter augo gjenge, var det ein flekk på mine hender,
kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia, kama moyo wangu umeongozwa na macho yangu, au kama mikono yangu imetiwa unajisi,
8 so gjev ein annan et mitt såd, og riv mi planting upp med rot!
basi wengine na wale nilichokipanda, nayo yale yote niliyootesha na yangʼolewe.
9 Let eg min hug av kvinna dåra, sneik eg til grannens dør meg fram,
“Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke, au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,
10 so lat mitt viv åt andre mala, og andre yver ho seg bøygje!
basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine, nao wanaume wengine walale naye.
11 For dette er ei skjemdarferd, eit brot som dom og straff fortener,
Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu, naam, dhambi ya kuhukumiwa.
12 ein eld som eta vil til avgrunns og øydeleggja all mi eiga.
Ni moto uwakao kwa Uharibifu; ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.
13 Vanvyrd’ eg retten åt min træl og trælkvinna i trætta med deim?
“Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu, walipokuwa na manungʼuniko dhidi yangu,
14 - Kva gjord’ eg då, når Gud reis upp? Kva svara eg, når han meg klaga?
nitafanya nini Mungu atakaponikabili? Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?
15 Dei er som meg i morsliv skapte; ein forma oss i moderfang -
Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu, si ndiye aliwaumba? Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote ndani ya mama zetu?
16 Um eg sagde nei når arming bad, og let enkja gråtande gå burt,
“Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,
17 hev eg mitt brød åleine ete, so farlaus inkje fekk ein bit,
kama nimekula chakula changu mwenyewe, bila kuwashirikisha yatima;
18 - nei, far for han eg var frå yngdi, frå morsliv var eg hennar førar -
lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya, nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:
19 Såg eg ein stakar utan klæde, ein fatig utan yverplagg,
kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo, au mtu mhitaji asiye na mavazi
20 og so hans lender ei meg signa, og ei mi saueull han vermde,
ambaye wala moyo wake haukunibariki kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,
21 hev eg mot farlaus handi lyft, av di eg medhald fekk i retten:
na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima, nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,
22 Let herdi mi or led då losna, og armen brotna frå sitt bein!
basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu, nao na uvunjike kutoka kiungio chake.
23 For eg var ovleg rædd Guds straff, eg magtlaus stod framfor hans velde.
Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu, nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.
24 Um eg mi lit til gullet sette, og voni til det fine gull,
“Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu, au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’
25 Gledde eg meg ved auka rikdom, og alt eg vann meg med mi hand,
kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu, ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,
26 såg eg på ljoset når det stråla, på månen der han skreid i glans,
kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake au mwezi ukienda kwa fahari yake,
27 vart hjarta mitt i løyndom dåra, so kyss på hand til deim eg sende,
hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri, au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,
28 so var det og straffande brot, då neitta eg min Gud der uppe.
basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa, kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.
29 Hev eg meg gledt ved uvens uferd, og jubla når han kom i skade,
“Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu, au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,
30 - men eg let ikkje munnen synda og banna honom ifrå livet -
lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;
31 hev ei mitt husfolk stendigt sagt: «Kven gjekk vel svolten frå hans bord?»
kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema, ‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’
32 - Eg let’kje framand natta ute; for ferdamann eg opna døri -
Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani, kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;
33 hev eg som Adam dult mi synd, og løynt mi misgjerd i min barm,
kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo, kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,
34 di eg var rædd den store hop og ottast spott frå ættefrendar, so stilt eg heldt meg innum dører?
kwa sababu ya kuogopa umati wa watu, na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa, nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:
35 Å, vilde nokon høyra på meg! Sjå her er underskrifti mi, lat berre Allvald svara meg! Fekk eg den skrift min motpart skreiv,
(“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia! Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu: Mwenyezi na anijibu; mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.
36 den skulde eg på oksli bera og binda på meg som ein krans
Hakika ningeyavaa begani mwangu, ningeyavaa kama taji.
37 eg melde honom kvart mitt stig, og som ein hovding møta honom.
Ningempa hesabu ya kila hatua yangu, ningemwendea kama mwana wa mfalme.)
38 Dersom min åker klagar meg, og um plogforerne lyt gråta,
“Kama nchi yangu inalia dhidi yangu, na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,
39 åt eg hans grøda ubetalt, tok livet eg av eigarmannen:
kama nimekula mazao yake bila malipo, au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,
40 Lat då for kveite klunger gro, og ugras der eg sådde bygg!» Her endar Jobs tale.
basi miiba na iote badala ya ngano, na magugu badala ya shayiri.” Mwisho wa maneno ya Ayubu.