< Jobs 3 >
1 Då let Job upp munnen og banna fødedagen sin.
Baada ya hayo, Ayubu akafunua kinywa chake na kuilani siku aliyozaliwa.
2 Job tok til ords og sagde:
Akasema,
3 «Burt med den dag då eg vart fødd, den natt som sa: «Ein svein er avla!»
“Na ipotelee mbali siku niliyozaliwa mimi, usiku uliosema, 'Mimba ya mtoto wa kiume imetungwa.'
4 Må denne dag til myrker verta - burtgløymd av Gud i høge himmel - og inkje ljos på honom skina!
Siku hiyo na iwe giza; Mungu toka juu asiifikilie, wala mwanga usiiangazie.
5 Lat svarte myrkret honom eiga og skyer seg kring honom samla! Dagmyrkjingar skal honom skræma
Ishikwe na giza na giza la mauti liwe lake. Wingu na likae juu yake; kila kitu kiifanyacho siku kuwa giza kweli na kiitishe.
6 og myrkret gløypa denne natt! Burt med den natt frå årsens dagar, ho kome ei i månads tal!
Usiku huo, na ukamatwe na giza tororo. Usihesabiwe miongoni mwa siku za mwaka; na usiwekwe katika hesabu ya miezi.
7 Ja, aud og tom skal natti verta og ingen fagnad i ho klinga;
Tazama, usiku huo na uwe tasa; na sauti ya shangwe isiwe ndani yake.
8 Dagbannarar skal henne banna, dei som kann mana upp Livjatan,
Na wailani siku hiyo, hao wafahamuo namna ya kumuamsha lewiathani.
9 Og morgonstjernor skal’kje skina; fåfengt ho venta skal på ljoset - augbrunerne av morgonroden -
Nyota za mapambazuko yake zitiwe giza. Siku hiyo iutafute mwanga, lakini isiupate; wala makope ya mapambazuko isiyaone,
10 av di ho ei livsdøri stengde på mor mi, so eg slapp for kval.
kwasababu haikuifunga milango ya tumbo la mama yangu, na kwasababu haikunifichia taabu machoni pangu.
11 Kvi døydd’ eg ei i moders liv? Ell’ slokna då eg rett var fødd?
Kwanini si-kufa wakati lipotokeza katika tumbo la uzazi? Kwanini sikuitoa roho yangu hapo mama aliponizaa?
12 Kvi fanst det kne som mot meg tok; og brjost eg kunde suga ved?
kwanini magoti yake yalinipokea? Kwanini maziwa yake yanipokee hata ninyonye?
13 So låg eg still og kvilde no, eg sov og hadde ro og fred
Kwa sasa ningelikuwa nimelala chini kimya kimya. Ningelala usingizi na kupata pumziko
14 hjå kongar og hjå fyrstar, som til gravstad pyramider bygde,
pamoja na wafalme na washauri wa dunia, ambao walijijengea makaburi ambayo sasa ni magofu.
15 hjå hovdingar som åtte gull og fyllte sine hus med sylv;
Au Ningelikuwa nimelala pamoja na wakuu wenye dhahabu, waliozijaza nyumba zao fedha.
16 ell’ ufødd var eg ikkje til, lik born som aldri ljoset såg.
Au pengine ningekuwa sijazaliwa, kama watoto wachanga wasio uona mwanga kabisa.
17 Der rasar ei dei vonde meir; der kviler dei som trøytte er;
Huko waovu huacha kusumbua; huko waliochoka hupumzika.
18 og fangarne er trygge der; dei høyrer ingen drivar meir.
Huko wafungwa kwa pamoja hupata amani; hawaisikii sauti ya msimamizi wa watumwa.
19 Der stor og liten like er, og trælen fri for herren sin.
Wote wadogo na watu maarufu wako huko; mtumishi yuko huru kwa bwana wake huko.
20 Kvi gjev han ljos til den som lid, og liv til deim som gremmer seg,
Kwa nini yeye aliye mashakani kupewa mwanga? Kwa nini hao wenye uchungu moyoni kupewa uhai,
21 som fåfengt stundar etter dauden, og søkjer han som løynde skatt,
ambao hutamani mauti lakini hawapati; ambao huyachimbulia mauti zaidi ya kutafuta hazina iliyofichika?
22 som gled seg, ja, som jublar høgt, og fegnast når dei finn ei grav -
Kwa nini kupewa mwanga ambao hushangilia mno na kufurahi walionapo kaburi?
23 til mannen som ei finn sin veg, som Gud set fast og stengjer inne?
Kwanini kupewa mwanga mtu ambaye njia zake zimefichika, mtu ambaye Mungu amemzungushia uwa?
24 Min sukk hev vorte daglegt brød, og klaga mi som vatnet strøymar.
Kwa kuwa kushusha kwangu pumzi kwatokea badala ya kula; kuugua kwangu kumemiminika kama maji.
25 Meg råkar det eg ottast fyre; det som eg ræddast, hender meg.
Maana jambo lile niliogopalo limenipata; nalo linitialo hofu limenijilia.
26 Snaudt fær eg fred, snaudt fær eg ro, snaudt lindring - so kjem uro att.»
Mimi sioni raha, sipati utulivu, na sipati pumziko; badala yake huja taabu.”