< Sakarias 12 >
1 Dette utsagn er Herrens ord om Israel. Så sier Herren, som utspente himmelen og grunnfestet jorden og dannet menneskets ånd i hans indre:
Hili ni tamko la neno la Yahwe kwa Israeli - Bwana asema, azitandaye mbingu na kuweka msingi wa dunia, aiumbaye roho ya mtu ndani yake,
2 Se, jeg gjør Jerusalem til en tumleskål for alle folkene rundt omkring; også over Juda skal det gå ut når Jerusalem blir kringsatt.
“Tazama, nitaifanya Yerusalemu kuwa kikombe kiwafadhaishacho watu wote wamzungukao. Itakuwa hivyo hivyo pia kwa Yuda wakati wa kuhusuriwa kwa Yerusalemu.
3 Og det skal skje på den dag at jeg vil gjøre Jerusalem til en sten å løfte på for alle folkene; alle som løfter på den, skal såre sig selv. Ja, alle jordens hedningefolk skal samle sig mot det.
Katika siku hiyo, nitaifanya Yerusalemu kuwa jiwe zito kwa watu wa jamaa zote. Kila atakayejaribu kuliinua jiwe hilo atajihumiza sana, na mataifa yote ya dunia yatakusanyika kinyume cha mji huo.
4 På den dag, sier Herren, vil jeg slå hver hest med skyhet og dens rytter med vanvidd; men over Judas hus vil jeg oplate mine øine, og alle folkenes hester vil jeg slå med blindhet.
Katika siku hiyo asema Yahwe - nitampiga kila farasi kwa ushangao na kila mpanda farasi kwa wendawazimu. Nitaiangalia nyumba ya Yuda kwa upendeleo na nami nitawapiga kwa upofu farasi wa majeshi.
5 Og Judas stammehøvdinger skal si i sitt hjerte: Vår styrke er Jerusalems innbyggere ved Herren, hærskarenes Gud, deres Gud.
Ndipo watawala wa Yuda watakapojisemea mioyoni mwao, 'Wakaao Yerusalemu ndio nguvu yetu kwa sababu ya Yahwe wa majeshi, Mungu wao.'
6 På den dag vil jeg gjøre Judas stammehøvdinger lik et fyrfat mellem vedtrær og et ildbluss blandt kornbånd, og de skal fortære alle folkene rundt omkring, til høire og til venstre; og Jerusalem-folket skal fremdeles bli på sitt sted, i Jerusalem.
Katika siku hiyo nitawafanya watawala wa Yuda kuwa kama mitungi ya moto katika miti na kama miali ya moto kati ya nafaka isimamayo, kwani utateketeza watu wote walio karibu upande wao wa kulia na kushoto. Yerusalemu atakaa mahali pake tena.
7 Og Herren skal frelse Judas telter først, forat ikke Davids hus og Jerusalems innbyggere skal ha større herlighet enn Juda.
Yahwe ataziokoa hema za Yuda kwanza, ili kwamba utukufu ya nyumba ya Daudi na utukufu wa wale waishio Yerusalemu hautazidi sehemu iliyosalia ya Yuda.
8 På den dag skal Herren verne Jerusalems innbyggere, og den iblandt dem som snubler, skal på den dag være som David, og Davids hus skal være som Gud, som Herrens engel foran dem.
Katika siku hiyo Yahwe atakuwa mtetezi wa wakao Yerusalemu, na siku hiyo waliodhaifu miongoni mwao watakuwa kama Daudi, wakati nyumba ya Daudi watakuwa kama Mungu, kama malaika wa Yahwe mbele yao.
9 Og på den dag vil jeg søke å ødelegge alle de hedningefolk som drar mot Jerusalem.
“Itakuwa kwamba katika siku hiyo nitaanza kuyaharibu mataifa yote yajayo kinyume cha Yerusalemu.
10 Men over Davids hus og over Jerusalems innbyggere vil jeg utgyde nådens og bønnens ånd, og de skal skue op til mig som de har gjennemstunget; og de skal sørge over ham som en sørger over sin enbårne sønn, og klage sårt over ham som en klager over sin førstefødte.
Lakini nitamwaga roho ya huruma na kuiombea nyumba ya Daudi na wakao Yerusalemu, hivyo wataniangalia mimi, waliomchoma kwa mkuki. Wataniombolezea, kama amwombolezeaye mwana wa pekee; watamwombolezea kwa uchungu sana kama aombolezaye kifo cha mzaliwa wa kwanza.
11 På den dag skal sorgen bli stor i Jerusalem, som sorgen over ulykken i Hadadrimmon i Megiddons dal.
Katika siku hiyo maombolezo huko Yerusalemu yatakuwa kama maombolezo ya Hadadi Rimoni katika tambarare za Megido.
12 Og landet skal sørge, hver slekt for sig, Davids huses slekt for sig og deres kvinner for sig, Natans huses slekt for sig og deres kvinner for sig,
Nchi itaomboleza, kila ukoo peke yao. Ukoo wa nyumba ya Daudi utakuwa peke yake na wake zao watakuwa peke yao mbali na wanaume. Ukoo wa nyumba ya Nathani utakuwa peke yao na wake zao watakuwa peke yao mbali na waume.
13 Levis huses slekt for sig og deres kvinner for sig, sime'ittenes slekt for sig og deres kvinner for sig,
Ukoo wa nyumba ya Lawi utakuwa peke yao na wake zao watakuwa peke yao mbali na waume. Ukoo wa Washimei utakuwa peke yao na wake zao watakuwa peke yao mbali na waume.
14 og likeså alle de andre slekter, hver slekt for sig og deres kvinner for sig.
Kila ukoo uliosalia - kila mmoja utakuwa peke yake na wake watakuwa pekee mbali na waume.