< Romerne 1 >

1 Paulus, Jesu Kristi tjener, kalt til apostel, utkåret til å forkynne Guds evangelium,
Paulo, mtumishi wa Kristo Yesu, aliyeitwa kuwa mtume na kutengwa kwa ajili ya Injili ya Mungu,
2 som han forut lovte ved sine profeter i hellige skrifter,
Injili ambayo Mungu alitangulia kuiahidi kwa vinywa vya manabii wake katika Maandiko Matakatifu,
3 om hans Sønn, som efter kjødet er kommet av Davids ætt,
yaani, Injili inayomhusu Mwanawe, yeye ambaye kwa uzao wa mwili alikuwa mzao wa Daudi,
4 som efter hellighets ånd er godtgjort å være Guds veldige Sønn ved opstandelsen fra de døde, Jesus Kristus, vår Herre,
na ambaye kwa uwezo wa Roho wa utakatifu alidhihirishwa kuwa Mwana wa Mungu kwa ufufuo wake kutoka kwa wafu, yaani, Yesu Kristo, Bwana wetu.
5 ved hvem vi fikk nåde og apostelembede for å virke troens lydighet blandt alle hedningefolkene til hans navns ære,
Kwa kupitia kwake na kwa ajili ya Jina lake, tumepokea neema na utume ili kuwaita watu miongoni mwa watu wa mataifa yote, waje kwenye utii utokanao na imani.
6 blandt hvilke også I er kalt til Jesus Kristus
Ninyi nyote pia mko miongoni mwa watu walioitwa ili mpate kuwa mali ya Yesu Kristo.
7 - til alle Guds elskede, kalte, hellige som er i Rom: Nåde være med eder og fred fra Gud vår Fader og den Herre Jesus Kristus!
Kwa wote walioko Rumi wapendwao na Mungu na kuitwa kuwa watakatifu: Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi.
8 Først takker jeg min Gud ved Jesus Kristus for eder alle, fordi eders tro er navnkundig i hele verden.
Kwanza kabisa, namshukuru Mungu wangu kwa njia ya Yesu Kristo kwa ajili yenu nyote, kwa sababu imani yenu inatangazwa duniani kote.
9 For Gud, som jeg tjener i min ånd i hans Sønns evangelium, er mitt vidne hvor uavlatelig jeg kommer eder i hu,
Kwa maana Mungu ninayemtumikia kwa moyo wangu wote katika kuhubiri Injili ya Mwanawe, ni shahidi wangu jinsi ninavyowakumbuka
10 idet jeg alltid i mine bønner beder om at jeg dog endelig engang ved Guds vilje må få lykke til å komme til eder.
katika maombi yangu siku zote, nami ninaomba kwamba hatimaye sasa kwa mapenzi ya Mungu, njia ipate kufunguliwa kwa ajili yangu ili nije kwenu.
11 For jeg lenges efter å se eder, så jeg kunde la eder få del med mig i nogen åndelig nådegave, forat I kunde styrkes,
Ninatamani sana kuwaona ili nipate kuweka juu yenu karama za rohoni ili mwe imara,
12 det vil si at jeg hos eder kunde vederkveges sammen med eder ved den felles tro, eders og min.
au zaidi, ninyi pamoja nami tuweze kutiana moyo katika imani sisi kwa sisi.
13 Og jeg vil ikke, brødre, at I skal være uvitende om at jeg ofte har satt mig fore å komme til eder - men jeg er blitt hindret inntil nu - forat jeg kunde ha nogen frukt også blandt eder likesom blandt de andre hedningefolk.
Ndugu zangu, napenda mfahamu kwamba mara nyingi nimekusudia kuja kwenu (ingawa mpaka sasa nimezuiliwa), ili nipate kuvuna mavuno miongoni mwenu kama nilivyovuna miongoni mwa wengine ambao ni watu wa Mataifa wasiomjua Mungu.
14 Jeg står i gjeld både til grekere og til barbarer, både til vise og uvise;
Mimi ni mdeni kwa Wayunani na kwa wasio Wayunani, kwa wenye hekima na kwa wasio na hekima.
15 således er jeg for min del villig til å forkynne evangeliet også for eder i Rom.
Ndiyo sababu ninatamani sana kuihubiri Injili kwenu pia ninyi mlioko Rumi.
16 For jeg skammer mig ikke ved evangeliet; for det er en Guds kraft til frelse for hver den som tror, både for jøde først og så for greker;
Mimi siionei haya Injili ya Kristo kwa maana ni uweza wa Mungu uletao wokovu kwa kila aaminiye, kwanza kwa Myahudi na kwa Myunani pia.
17 for i det åpenbares Guds rettferdighet av tro til tro, som skrevet er: Den rettferdige, ved tro skal han leve.
Kwa maana katika Injili haki itokayo kwa Mungu imedhihirishwa, haki ile iliyo kwa njia ya imani hadi imani. Kama ilivyoandikwa: “Mwenye haki ataishi kwa imani.”
18 For Guds vrede åpenbares fra himmelen over all ugudelighet og urettferdighet hos mennesker som holder sannheten nede i urettferdighet;
Ghadhabu ya Mungu imedhihirishwa kutoka mbinguni dhidi ya uasi wote na uovu wa wanadamu ambao huipinga kweli kwa uovu wao,
19 for det som en kan vite om Gud, ligger åpent for dem, for Gud har åpenbaret dem det.
kwa maana yote yanayoweza kujulikana kumhusu Mungu ni dhahiri kwao, kwa sababu Mungu mwenyewe ameyadhihirisha kwao.
20 For hans usynlige vesen, både hans evige kraft og hans guddommelighet, er synlig fra verdens skapelse av, idet det kjennes av hans gjerninger, forat de skal være uten undskyldning, (aïdios g126)
Kwa maana tangu kuumbwa kwa ulimwengu, asili ya Mungu asiyeonekana kwa macho, yaani, uweza wake wa milele na asili yake ya Uungu, imeonekana waziwazi, ikitambuliwa kutokana na yale aliyoyafanya ili wanadamu wasiwe na udhuru. (aïdios g126)
21 fordi de, enda de kjente Gud, dog ikke æret eller takket ham som Gud, men blev dårlige i sine tanker, og deres uforstandige hjerte blev formørket.
Kwa maana ingawa walimjua Mungu, hawakumtukuza yeye kama ndiye Mungu wala hawakumshukuru, bali fikira zao zimekuwa batili na mioyo yao ya ujinga ikatiwa giza.
22 Mens de gjorde sig til av å være vise, blev de dårer,
Ingawa walijidai kuwa wenye hekima, wakawa wajinga
23 og byttet den uforgjengelige Guds herlighet bort mot et billede, en avbildning av et forgjengelig menneske og av fugler og av firføtte dyr og av krypdyr.
na kubadili utukufu wa Mungu aishiye milele kwa sanamu zilizofanywa zifanane na mwanadamu ambaye hufa, na mfano wa ndege, wanyama na viumbe vitambaavyo.
24 Derfor overgav også Gud dem i deres hjerters lyster til urenhet, til å vanære sine legemer sig imellem,
Kwa hiyo, Mungu akawaacha wazifuate tamaa mbaya za mioyo yao katika uasherati, hata wakavunjiana heshima miili yao wao kwa wao.
25 de som byttet Guds sannhet bort mot løgn og æret og dyrket skapningen fremfor skaperen, han som er velsignet i evighet. Amen. (aiōn g165)
Kwa sababu waliibadili kweli ya Mungu kuwa uongo, wakaabudu na kutumikia kiumbe badala ya Muumba, ahimidiwaye milele! Amen. (aiōn g165)
26 Derfor overgav Gud dem til skammelige lyster; for både deres kvinner forvendte den naturlige bruk til den unaturlige,
Kwa sababu hii, Mungu aliwaacha wavunjiane heshima kwa kufuata tamaa zao za aibu. Hata wanawake wao wakabadili matumizi ya asili ya miili yao wakaitumia isivyokusudiwa.
27 og på samme vis forlot også mennene den naturlige bruk av kvinnen og brente i sin lyst efter hverandre, så at menn drev skjenselsverk med menn, og fikk på sig selv det vvederlag for sin forvillelse som rett var.
Vivyo hivyo wanaume pia wakiacha matumizi ya asili ya wanawake wakawakiana tamaa wao kwa wao. Wanaume wakafanyiana matendo ya aibu na wanaume wengine nao wakapata katika maisha yao adhabu iliyowastahili kwa ajili ya upotovu wao.
28 Og likesom de ikke brydde sig om å eie Gud i kunnskap, så overgav Gud dem til et sinn som intet duer, så de gjorde det usømmelige:
Nao kwa kuwa hawakuona umuhimu wa kudumisha ufahamu wa Mungu, yeye akawaachilia wafuate akili za upotovu, watende mambo yale yasiyostahili kutendwa.
29 fulle av all urettferdighet, vanart, havesyke, ondskap; fulle av avind, mord, trette, svik, list;
Wakiwa wamejawa na udhalimu wa kila namna, uasherati, uovu, tamaa mbaya na hila. Wamejawa na husuda, uuaji, ugomvi, udanganyifu, hadaa na nia mbaya. Wao pia ni wasengenyaji,
30 øretutere, baktalere, gudsforhatte, voldsmenn, overmodige, storskrytere, opfinnsomme til ondt; ulydige mot foreldre,
wasingiziaji, wanaomchukia Mungu, wajeuri, wenye kiburi na majivuno, wenye hila, wasiotii wazazi wao,
31 uforstandige, upålitelige, ukjærlige, ubarmhjertige;
wajinga, wasioamini, wasio na huruma na wakatili.
32 slike som godt kjenner Guds dom at de som gjør sådant, fortjener døden, og dog ikke bare gjør det, men endog holder med dem som gjør det.
Ingawa wanafahamu sheria ya haki ya Mungu kwamba watu wanaofanya mambo kama hayo wanastahili mauti, si kwamba wanaendelea kutenda hayo tu, bali pia wanakubaliana na wale wanaoyatenda.

< Romerne 1 >