< Salmenes 96 >
1 Syng for Herren en ny sang, syng for Herren, all jorden!
Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
2 Syng for Herren, lov hans navn, forkynn fra dag til dag hans frelse!
Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
3 Fortell blandt hedningene hans ære, blandt alle folkene hans undergjerninger!
Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
4 For stor er Herren og høilovet, forferdelig er han over alle guder.
Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
5 For alle folkenes guder er intet; men Herren har gjort himmelen.
Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
6 Høihet og herlighet er for hans åsyn, styrke og prydelse er i hans helligdom.
Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
7 Gi Herren, I folkeslekter, gi Herren ære og makt!
Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
8 Gi Herren hans navns ære, bær frem gaver og kom til hans forgårder!
Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
9 Tilbed Herren i hellig prydelse, bev for hans åsyn, all jorden!
Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
10 Si blandt hedningene: Herren er blitt konge, og jorderike står fast, det rokkes ikke; han dømmer folkene med rettvishet.
Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
11 Himmelen glede sig, og jorden fryde sig, havet bruse og alt det som fyller det!
Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
12 Marken fryde sig og alt det som er på den! Da jubler alle trær i skogen
mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
13 for Herrens åsyn; for han kommer, han kommer for å dømme jorden; han skal dømme jorderike i rettferdighet og folkene i sin trofasthet.
itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.