< Salmenes 48 >
1 En sang, en salme; av Korahs barn. Stor er Herren og høilovet i vår Guds stad, på hans hellige berg.
Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
2 Fagert hever det sig, en glede for all jorden er Sions berg, det ytterste Norden, den store konges stad.
Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
3 Gud er i dens borger, han er blitt kjent som et fast vern.
Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
4 For se, kongene samlet sig, de drog frem tilsammen.
Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
5 De så, da blev de forferdet; de blev slått med redsel, flyktet i hast.
walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
6 Beven grep dem der, angst som hos en fødende kvinne.
Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
7 Ved østenvind knuste du Tarsis-skib.
Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
8 Likesom vi hadde hørt, så har vi nu sett det i Herrens, hærskarenes Guds stad, i vår Guds stad; Gud gjør den fast til evig tid. (Sela)
Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
9 Vi grunder, Gud, på din miskunnhet midt i ditt tempel.
Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
10 Som ditt navn, Gud, så er din pris inntil jordens ender; din høire hånd er full av rettferdighet.
Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
11 Sions berg gleder sig, Judas døtre fryder sig for dine dommers skyld.
Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
12 Gå omkring Sion og vandre rundt om det, tell dets tårn!
Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
13 Gi akt på dets voller, vandre gjennem dets borger, forat I kan fortelle derom til den kommende slekt.
yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
14 For denne Gud er vår Gud evindelig og alltid; han skal føre oss ut over døden.
Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.