< Salmenes 120 >
1 En sang ved festreisene. Til Herren ropte jeg i min nød, og han svarte mig.
Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
2 Herre, fri min sjel fra en løgnaktig lebe, fra en falsk tunge!
Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
3 Hvad vil han gi dig, og hvad mere vil han gi dig, du falske tunge?
Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
4 Voldsmannens skarpe piler og glør av gyvelbusken.
Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
5 Ve mig, at jeg lever som fremmed iblandt Mesek, at jeg bor ved Kedars telt!
Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
6 Lenge nok har min sjel bodd hos dem som hater fred.
Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
7 Jeg er bare fred, men når jeg taler, er de ferdige til krig.
Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.