< Salmenes 108 >

1 En sang, en salme av David. Mitt hjerte er rolig, Gud! Jeg vil synge og lovprise, ja, det skal min ære.
Wimbo. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
2 Våkn op, harpe og citar! Jeg vil vekke morgenrøden.
Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
3 Jeg vil prise dig blandt folkene, Herre, og lovsynge dig blandt folkeslagene.
Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
4 For stor over himmelen er din miskunnhet, og inntil skyene din trofasthet.
Kwa maana upendo wako ni mkuu, ni juu kuliko mbingu; uaminifu wako unazifikia anga.
5 Vis dig høi over himmelen, Gud, og din ære over all jorden!
Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
6 Forat de du elsker, må bli frelst, så hjelp med din høire hånd og bønnhør oss!
Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
7 Gud har talt i sin hellighet. Jeg vil fryde mig; jeg vil utskifte Sikem og opmåle Sukkots dal.
Mungu amenena kutoka patakatifu pake: “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi na kulipima Bonde la Sukothi.
8 Mig hører Gilead til, mig hører Manasse til, og Efra'im er vern for mitt hode, Juda er min herskerstav.
Gileadi ni yangu, Manase ni yangu, Efraimu ni kofia yangu ya chuma, nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
9 Moab er mitt vaskefat, på Edom kaster jeg min sko, over Filisterland jubler jeg.
Moabu ni sinia langu la kunawia, juu ya Edomu natupa kiatu changu; nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
10 Hvem vil føre mig til den faste by? Hvem leder mig inn til Edom?
Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
11 Mon ikke du, Gud, som forkastet oss og ikke drog ut med våre hærer, Gud?
Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, na hutoki tena na majeshi yetu?
12 Gi oss hjelp mot fienden, for menneskehjelp er tomhet!
Tuletee msaada dhidi ya adui, kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
13 Ved Gud skal vi gjøre storverk, og han skal trede ned våre fiender.
Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, naye atawaponda adui zetu.

< Salmenes 108 >