< Salomos Ordsprog 26 >

1 Som sne om sommeren og som regn i høsttiden, slik høver ære for en dåre.
Kama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno, ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu.
2 Som spurven i fart, som svalen i flukt, slik er det med en uforskyldt forbannelse - den rammer ikke.
Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi, ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.
3 Svepe for hesten, tømme for asenet, og kjepp for dårers rygg!
Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!
4 Svar ikke dåren efter hans dårskap, forat du ikke selv skal bli ham lik!
Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.
5 Svar dåren efter hans dårskap, forat han ikke skal bli vis i egne øine!
Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.
6 Den som sender bud med en dåre, han hugger føttene av sig, han må tåle slem medfart.
Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara, ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.
7 Visne henger benene på den lamme og likeså ordsprog i munnen på dårer.
Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.
8 Lik den som legger sten i slyngen, er den som gir en dåre ære.
Kama kufunga jiwe kwenye kombeo, ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.
9 Som en torn i en drukken manns hånd, slik er et ordsprog i dårers munn.
Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.
10 En mester får alt i stand, men den som leier en dåre, er lik den som leier en som går forbi.
Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo, ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.
11 Lik hunden som vender tilbake til sitt eget spy, er en dåre som kommer igjen med sin dårskap.
Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake, ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.
12 Ser du en mann som er vis i egne øine - det er mere håp for dåren enn for ham.
Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
13 Den late sier: Det er en løve på veien, en løve i gatene.
Mvivu husema, “Yuko simba barabarani, simba mkali anazunguka mitaa!”
14 Døren dreier sig på sitt hengsel, og den late snur sig på sitt leie.
Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake, ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.
15 Den late stikker sin hånd fatet; han gider ikke føre den tilbake til sin munn.
Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake.
16 Den late er visere i egne øine enn syv som svarer med forstand.
Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.
17 Lik den som tar fatt i øret på en hund som løper forbi, er den som lar sig egge til vrede over en trette som ikke kommer ham ved.
Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio, ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.
18 Lik en gal mann som kaster ut brandpiler og skyter og dreper,
Kama mtu mwendawazimu atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,
19 er en mann som har sveket sin venn og så sier: Jeg spøker jo bare!
ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”
20 Når det er forbi med veden, slukner ilden, og når det ingen øretuter er, stilles trette.
Bila kuni moto huzimika; pasipo uchongezi ugomvi humalizika.
21 Som kull blir til glør, og som ved nærer ild, slik voldes kiv av en trettekjær mann.
Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.
22 En øretuters ord er som velsmakende retter, og de trenger ned i hjertets indre.
Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
23 Lik et lerkar som er overdratt med bly-glette, er brennende leber sammen med et ondt hjerte.
Kama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya.
24 Med sine leber skaper den hatefulle sig til, men i sitt indre gjemmer han svik.
Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake, lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.
25 Når han gjør sin røst blid, så tro ham ikke! For der er syv vederstyggeligheter i hans hjerte.
Ingawa maneno yake huvutia, usimwamini, kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake.
26 Den hatefulle skjuler sig i svik, men hans ondskap blir åpenbar i forsamlingen.
Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu, lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko.
27 Den som graver en grav, skal falle i den, og den som velter en sten op, på ham skal den rulle tilbake.
Kama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake, kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia.
28 En løgnaktig tunge hater dem som den har knust, og en falsk munn volder fall.
Ulimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza, nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.

< Salomos Ordsprog 26 >