< Salomos Ordsprog 25 >

1 Også dette er Salomos ordsprog, som Judas konge Esekias' menn har samlet:
Hizi ni mithali zaidi za Solomoni, zilizonakiliwa na watu wa Hezekia mfalme wa Yuda:
2 Det er Guds ære å skjule en sak, men kongers ære å granske en sak.
Ni Utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali ni utukufu wa wafalme kuchunguza jambo.
3 Himmelens høide, jordens dybde og kongers hjerter er uransakelige.
Kama mbingu zilivyo juu na nchi ilivyo chini, ndivyo ambavyo mioyo ya wafalme haichunguziki.
4 Skill slagget fra sølvet, så får gullsmeden et kar ut av det.
Ondoa takataka kwenye madini ya fedha, nako ndani yake kutatokea chombo cha mfua fedha.
5 Før den ugudelige bort fra kongens åsyn, så blir hans trone trygget ved rettferdighet.
Ondoa waovu mbele ya mfalme, nacho kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa njia ya haki.
6 Bryst dig ikke for kongens åsyn og still dig ikke på de stores plass!
Usijikweze mwenyewe mbele ya mfalme, wala usidai nafasi miongoni mwa watu wakuu;
7 For det er bedre de sier til dig: Kom her op, enn at du blir flyttet ned for en stormann, som du hadde sett.
ni afadhali yeye akuambie, “Njoo huku juu,” kuliko yeye kukuaibisha mbele ya mkuu. Kile ulichokiona kwa macho yako
8 Gi dig ikke for hastig i strid med nogen, forat det ikke skal sies: Hvad vil du gjøre til slutt når motparten vinner saken til din skam?
usiharakishe kukipeleka mahakamani, maana utafanya nini mwishoni kama jirani yako atakuaibisha?
9 Før din sak mot din motpart, men åpenbar ikke annen manns hemmelighet,
Kama ukifanya shauri na jirani yako, usisaliti siri ya mtu mwingine,
10 forat ikke den som hører det, skal skjelle dig ut, og ditt dårlige rykte vare ved!
ama yeye aisikiaye aweza kukuaibisha na kamwe sifa yako mbaya haitaondoka.
11 Som epler av gull i skåler av sølv er et ord talt i rette tid.
Neno lisemwalo kwa wakati ufaao ni kama matunda ya mtofaa ya dhahabu yaliyowekwa kwenye vijalizo vya fedha.
12 Som en ring av gull, som et smykke av fint gull er en vismann som taler refsende ord for et hørende øre.
Kama vile kipuli cha dhahabu au pambo la dhahabu safi, ndivyo lilivyo karipio la mtu mwenye hekima kwa sikio lisikilizalo.
13 Som kjølende sne i høstens tid er et pålitelig sendebud for den som sender ham; han vederkveger sin herres sjel.
Kama vile ubaridi wa theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wale wamtumao, huburudisha roho za bwana zake.
14 Som skyer og vind uten regn er den mann som skryter av at han vil gi, men ikke holder ord.
Kama vile mawingu na upepo pasipo mvua ndivyo alivyo mtu ajisifuye kwa zawadi ambazo hatoi.
15 Ved saktmodighet blir en fyrste overtalt, og en mild tunge knuser ben.
Kwa njia ya uvumilivu mtawala aweza kushawishiwa, nao ulimi laini waweza kuvunja mfupa.
16 Har du funnet honning, så et av den det du trenger, forat du ikke skal bli lei av den og spy den ut!
Ukipata asali, kula kiasi tu cha kukutosha, ukila zaidi, utatapika.
17 Sett sjelden din fot i din venns hus, forat han ikke skal bli lei av dig og hate dig!
Ingiza mguu wako nyumbani kwa jirani yako mara chache, ukizidisha, atakukinai na atakuchukia.
18 Som en hammer, et sverd, en hvass pil er en mann som fører falskt vidnesbyrd mot sin næste.
Kama vile rungu au upanga au mshale mkali ndivyo alivyo mtu atoaye ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake.
19 Som en skjør tann og en vaklende fot er tillit til den troløse på nødens dag.
Kama vile jino bovu au mguu uliolemaa, ndivyo ilivyo kumtegemea mtu asiye mwaminifu wakati wa shida.
20 Lik den som legger av sine klær på en vinterdag, lik eddik på pottaske er den som synger viser for et sorgfullt hjerte.
Kama vile avuaye mavazi siku ya baridi, au kama siki iliyomwagwa juu ya magadi, ndivyo alivyo yeye amuimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito.
21 Hungrer din fiende, så gi ham brød å ete, og tørster han, så gi ham vann å drikke!
Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale; kama ana kiu, mpe maji anywe.
22 For da sanker du gloende kull på hans hode, og Herren skal gjengjelde dig det.
Kwa kufanya hivyo, unaweka makaa ya moto yanayowaka kichwani pake, naye Bwana atakupa thawabu.
23 Nordenvind føder regn, og en tunge som hvisker i lønndom, volder sure miner.
Kama vile upepo wa kaskazini uletavyo mvua, ndivyo ulimi usingiziao uletavyo uso wa hasira.
24 Bedre å bo i et hjørne på taket enn med trettekjær kvinne i felles hus.
Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
25 Som friskt vann for den trette er en god tidende fra et fjernt land.
Kama vile maji baridi kwa nafsi iliyochoka ndivyo zilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
26 Som en grumset kilde og en utskjemt brønn er en rettferdig som gir efter for en ugudelig.
Kama vile chemchemi iliyotibuliwa matope au kisima kilichotiwa taka ndivyo alivyo mtu mwenye haki akishiriki na waovu.
27 Å ete for meget honning er ikke godt, og grubleres ære er tung.
Si vyema kula asali nyingi sana, wala si heshima kujitafutia heshima yako mwenyewe.
28 Som en by hvis murer er brutt ned og borte, er en mann som ikke kan styre sitt sinn.
Kama vile mji ambao kuta zake zimebomoka ndivyo alivyo mtu ambaye hawezi kujitawala mwenyewe.

< Salomos Ordsprog 25 >