< 3 Mosebok 7 >

1 Og dette er loven om skyldofferet: Det er høihellig.
Hii ndiyo sheria ya sadaka ya hatia. Kwa sababu hiyo ni sadaka takatifu sana.
2 På det sted hvor brennofferet slaktes, skal skyldofferet slaktes, og dets blod skal sprenges rundt om på alteret.
Ni lazima waichinje sadaka ya hatia mahali panapostali kuchinjwa, na ni lazima watainyunyiza damu yake pande zote za madhabahu.
3 Og alt fettet skal ofres, både halen og fettet som dekker innvollene,
Mafuta yote yaliyomo ndani yake yataondolewa: mafuta ya mkiani, mafuta yaliyo sehamu za ndani,
4 og begge nyrene med det fett som er på dem, ved lendene, og den store leverlapp; den skal tas ut sammen med nyrene.
zile figo mbili pamoja na mafuta yaliyo juu yake, yaliyo karibu na kiuno, na yanayofunika ini—nyama hii yote lazima iondolewe pamoja na hizo figo.
5 Og presten skal brenne det på alteret som ildoffer til Herren; det er et skyldoffer.
Kuhani ataviteketeza vipande hivi juu ya madhabahu viwe dhabihu iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto. Hii ni sadaka ya hatia
6 Alt mannkjønn blandt prestene kan ete det; på et hellig sted skal det etes; det er høihellig.
Kila mwanaume miongoni mwa familia ya kuhani anaweza kula sehemu ya sadaka hii. Lakini ni lazima iliwe ndani ya mahali patakatifu kwa sababu ni takatifu sana.
7 Med skyldofferet skal det være likesom med syndofferet; det gjelder én lov for begge; den prest som gjør soning med det, ham skal det tilhøre.
Nayo sadaka ya dhambi ni kama ilivyo sadaka ya hatia. Ni sheria ileile hutumika kwa zote mbili. Zote ni mali ya kuhani azitumiaye kufanya upatanisho.
8 Når en prest ofrer brennoffer for nogen, så skal huden av det brennoffer han har ofret, tilhøre den samme prest.
Kuhani atoaye sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya mtu yeyote anaweza kuchuku ngozi ya sadaka hiyo kwa ajili yake mwenyewe.
9 Og ethvert matoffer som bakes i ovn, eller som stekes i panne eller på helle, skal tilhøre den prest som ofrer det.
Kila sadaka ya nafaka inayookwa mekoni, na kila sadaka kama hiyo ipikwayo kaangoni au kwenye sufuria itakuwa ya kuhani aitoaye.
10 Og ethvert matoffer som er blandet med olje, eller som er tørt, skal høre alle Arons sønner til, den ene som den andre.
Kila sadaka ya nafaka, ama iwe unga mkavu au uliochanganywa na mafuta ya zeitu itakuwa ya ukoo wa Aroni kwa usawa.
11 Og dette er loven om takkofferet som ofres til Herren:
Hii ndiyo sheria ya dhabihu ya sadaka za amani, ambazo watu watazitoa kwa Yahweh.
12 Dersom nogen ofrer det til lovprisning, så skal han foruten slaktofferet som bæres frem til lovprisning, ofre usyrede kaker med olje i og usyrede brødleiver smurt med olje, og fint mel knadd til kaker med olje i.
Iwapo mtu yeyote anaitoa ili kuonyesha shukrani kwa Yahweh, basi ataitoa pamoja na dhabih uya mikate iliyotengenezwa bila hamira, bali kwa mafuta ya zeituni yaliyochanganywa na unga lakini bila hamira, na maandazi yaliyotengenezwa bila hamira, bali yaliyopakwa mafuta juu yake, na mikate miembamba iliyofanywa kwa unga laini uliochanganywa na mafuta.
13 Dette er den offergave han skal bære frem foruten det slaktoffer som bæres frem til takk og lovprisning, og dessuten syrede kaker.
Kwa kusudi la kutoa shukrani, pia anapaswa kutoa pamoja na sadaka yake ya amani, vipande vya mikate iliyotiwa hamira.
14 Av dette offer skal han bære frem én kake av hvert slag som gave til Herren; det skal tilhøre presten som sprenger takkofferets blod på alteret.
Ni lazima atatoa moja kila aina ya sadaka hizi kama sadaka iliyoletwa kwa Yahweh. Nayo itakuwa ya makuhani wanaonyunyizia damu ya sadaka ya amani kwenye madhabahu.
15 Kjøttet av et takkoffer som bæres frem til lovprisning, skal etes på den dag det ofres; intet av det skal bli liggende til om morgenen.
Mtu anayeleta sadaka ya amani kwa kusudi la kutoa shukrani ni lazima ataila nyama ya sadaka yake siku ya kutoa dhabihu. Hatakiwi kusaza chochote kilicho cha sadaka hiyo hata asubuhi ya pili.
16 Dersom nogens slaktoffer er et lovet offer eller et frivillig offer, skal det etes på den dag det ofres; men det som levnes, kan etes den næste dag.
Lakini iwapo dhabihu ya matoleo yake kusudi lake ni nadhiri, au kwa kusudi la sadaka ya hiari, nyama yake italiwa siku iyo hiyo aitoapo dhabihu yake, lakini chochote kinachosalia cha sadaka hiyo kinaweza kuliwa siku inayofuata.
17 Men hvad som enda blir tilovers av slaktofferets kjøtt, skal på den tredje dag brennes op med ild.
Hata hivyo, nyama yoyote ya dhabihu inayobaki siku ya tatu ni lazima ichomwe moto.
18 Om nogen på den tredje dag eter av takkofferets kjøtt, da har Herren ikke velbehag i offeret; det skal ikke regnes den som ofret det, til gode, det skal være en vederstyggelighet, og den som eter av det, gjør en misgjerning som han kommer til å bøte for.
Iwapo kipande chochote cha nyama hiyo ya dhabihu kinachobaki kinaliwa katika siku ya tatu, hakitakubalika, wala hakitatolewa kwa aliyeitoa. Kitakuwa ni kitu cha kuchukiza, na mtu akilaye atabeba hatia ya dhambi mwenyewe yake.
19 Kjøtt som kommer nær noget urent, skal ikke etes, det skal brennes op med ild; ellers kan alle som er rene, ete av kjøttet.
Nyama yoyote inayogusa kitu kilicho najisi haitaliwa. Ni lazima ichomwe moto. Na kwa ajili ya nyama inayobaki, yeyote aliye safi anaweza kuila.
20 Men den som eter kjøtt av Herrens takkoffer mens det er noget urent på ham, han skal utryddes av sitt folk.
Hata hivyo, mtu najisi anayekula nyama kutoka kwenye dhabihu ya matoleo ya amani ambayo ni ya Yahweh yapasa mtu huyu akatiliwe mbali kutoka kwa watu wake.
21 Og når nogen rører ved noget urent, enten det er et menneskes urenhet eller et urent dyr eller noget annet urent og vederstyggelig, og så eter av kjøttet av Herrens takkoffer, da skal han utryddes av sitt folk.
Iwapo mtu yeyote anagusa kitu chochote kilichonajisi—iwe ni unajisi wa binadamu, au wa mnyama aliyenajisi, au wa kitu fulani kilichonajisi na chenye kuchukiza, na kisha akala baadhi ya nyama ya dhabihu ya sadaka ya amani iliyotolewa kwa Yahweh, lazima mtu huyo akatiliwe mbali kutoka kwa watu wake.
22 Og Herren talte til Moses og sa:
Kisha Yahweh akazungumza na Musa, akisema,
23 Tal til Israels barn og si: I skal ikke ete fett av okse eller får eller gjet.
“Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, 'hamruhusiwi kula mafuta ya fahali au kondoo au mbuzi.
24 Fettet av et selvdødt dyr eller av et sønderrevet dyr kan brukes til alle slags arbeid; men ete det må I ikke;
Mafuta ya mnyama yoyote afaye peke yake bila ya kuwa dhabihu, au mafuta ya mnyama yeyote aliyeraruliwa na wanyama pori, yanaweza kutumika kwa makusudi mengine, lakini hakika hamtayala.
25 for hver den som eter fettet av noget dyr som det ofres ildoffer av til Herren, han skal utryddes av sitt folk.
Yeyote atakayekula mafuta ya mnyama ambayo watu wanaweza kuyatoa kuwa dhabihu ya iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto, mtu huyo lazima atakatiliwa mbali kutoka kwa watu wake.
26 Og blod skal I ikke ete, hverken av fugl eller fe, hvor I så bor.
Hamtakula damu yoyote katika mojawapo ya nyumba zenu, ama iwe kutoka kwa ndege au mnyama.
27 Enhver som nogensinne eter blod, han skal utryddes av sitt folk.
Yeyote alaye damu yoyote, mtu huyo lazima akatiliwe mbali kutoka kwa watu wake.'”
28 Og Herren talte til Moses og sa:
Kwa hiyo Yahweh akazungumza na Musa na akasema,
29 Tal til Israels barn og si: Den som ofrer sitt takke-slaktoffer til Herren, han skal bære frem for Herren sin offergave av sitt takke-slaktoffer.
“Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, 'Yeye atoaye dhabidhu ya sadaka ya amani kwa Yahweh lazima alete sehemu ya dhabihu yake kwa Yahweh.
30 Med egne hender skal han bære frem Herrens ildoffer; både fettet og brystet skal han bære frem, og brystet skal svinges for Herrens åsyn.
Mikono yake mwenyewe lazima iilete hiyo sadaka ifanywayo kwa Yahweh kwa moto. Naye atayaleta hayo mafuta pamoja na kidari, ili kwamba kidari kiweze kutikiswa kuwa sadaka ya kutikiswa mbele za Yahweh.
31 Og presten skal brenne fettet på alteret; men brystet skal høre Aron og hans sønner til.
Kuhani atayachoma mafuta hayo juu ya madhabahu, lakini kile kidari kitakuwa mali ya Aroni na uzao wake.
32 Og det høire lår skal I gi presten som gave av eders takkoffer.
Ni lazima utatoa paja la kulia kwa kuhani kama sadaka iliyotokana na dhabihu ya sadaka yako ya amani.
33 Den av Arons sønner som ofrer takkoffer-blodet og fettet, han skal ha det høire lår som sin del;
Yule kuhani, mmoja wa wazao wa Aroni, atoaye damu na mafuta ya sadaka ya amani—ni lazima atapata paja la kulia kama mgao wake wa sadaka.
34 for svinge-brystet og løfte-låret har jeg tatt fra Israels barn av deres takke-slaktoffer og gitt til Aron, presten, og til hans sønner som en evig rettighet de kan kreve av Israels barn.
Kwa kuwa nimetwaa kidari, na paja la sadaka ya kutikiswa kutoka kwa watu wa Israeli uwe mchango wao, na amepewa Aroni kuhani na wanawe kuwa mgao wao wa kawaida.
35 Dette er Arons del og hans sønners del av Herrens ildoffer, som gis dem på den dag de føres frem for å tjene Herren som prester,
Huu ndiyo mgao wa Aroni na uzao wake utokanao na matoleo yaliyofanywa kwa Yahweh kwa moto, siku ile Musa alipowaweka wakfu ili kumtumikia Yahweh katika kazi ya kuhani.
36 den del som Herren befalte skulde gis dem av Israels barn på den dag de salves, en evig rettighet, fra slekt til slekt.
Huu ndio mgao ambao Yahweh aliamru waweze kupewa kutoka kwa watu wa Israeli, katika siku hiyo aliyowatia mafuta ya upako wawe makuhani. Nao utakuwa mgao wao wa kila siku katika vizazi vyote.
37 Dette er loven om brennofferet, om matofferet og om syndofferet og om skyldofferet og om innvielsesofferet og om takkofferet,
Hii ndiyo sheria ya sadaka ya kuteketezwa, ya sadaka ya nafaka, ya sadaka ya dhambi, ya sadaka ya hatia, ya sadaka ya kuweka wakfu, na ya dhabihu, ya sadaka za amani,
38 den som Herren gav Moses på Sinai berg den dag han bød Israels barn å ofre Herren sine offer i Sinai ørken.
ni sheria ambazo Yahweh alizitoa kwa Musa kwenye Mlima Sinai siku aliyowaamru watu wa Israeli kutoa dhabihu zao kwa Yahweh katika jangwa la Sinai.'”

< 3 Mosebok 7 >