< Jobs 26 >

1 Da tok Job til orde og sa:
Kisha Ayubu akajibu:
2 Hvor du har hjulpet den avmektige, støttet den kraftløse arm!
“Tazama jinsi ulivyomsaidia mtu asiye na uwezo! Jinsi ulivyouokoa mkono ulio dhaifu!
3 Hvor du har gitt den uvise råd, og hvilket overmål av visdom du har lagt for dagen!
Ni shauri gani ulilompa yeye asiye na hekima? Nayo ni busara gani kubwa uliyoonyesha!
4 Hvem har du fremført dine ord for, og hvis ånd har talt gjennem dig?
Ni nani aliyekusaidia kutamka maneno hayo? Nayo ni roho ya nani iliyosema kutoka kinywani mwako?
5 Dødsrikets skygger skjelver, vannenes dyp og de som bor i dem.
“Wafu wako katika maumivu makuu, wale walio chini ya maji na wale waishio ndani yake.
6 Dødsriket ligger åpent for ham og avgrunnen uten dekke. (Sheol h7585)
Mauti iko wazi mbele za Mungu; Uharibifu haukufunikwa. (Sheol h7585)
7 Han breder Norden ut over det øde rum, han henger jorden på intet.
Hutandaza anga la kaskazini mahali patupu; naye huiningʼiniza dunia mahali pasipo na kitu.
8 Han binder vannene sammen i sine skyer, og skyene brister ikke under dem.
Huyafungia maji kwenye mawingu yake, hata hivyo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.
9 Han lukker for sin trone, breder sine skyer over den.
Huufunika uso wa mwezi mpevu, akitandaza mawingu juu yake.
10 En grense har han dradd i en ring over vannene, der hvor lyset grenser til mørket.
Amechora mstari wa upeo juu ya uso wa maji, ameweka mpaka wa nuru na giza.
11 Himmelens støtter skjelver, og de forferdes for hans trusel.
Nguzo za mbingu nazo zatetemeka, zinatishika anapozikemea.
12 Ved sin kraft oprører han havet, og ved sin forstand knuser han Rahab.
Kwa nguvu zake aliisukasuka bahari; kwa hekima yake alimkata Rahabu vipande vipande.
13 Ved hans ånde blir himmelen klar; hans hånd gjennemborer den lettfarende drage.
Aliisafisha anga kwa pumzi yake; kwa mkono wake alimchoma joka aendaye mbio.
14 Se, dette er bare utkantene av hans verk; hvor svak er lyden av det ord vi hører! Men hans veldes torden - hvem forstår den?
Haya ni mambo madogo tu katika matendo yake; tazama jinsi ulivyo mdogo mnongʼono tunaousikia kumhusu! Ni nani basi awezaye kuelewa ngurumo za nguvu zake?”

< Jobs 26 >