< Jobs 11 >

1 Da tok Sofar fra Na'ama til orde og sa:
Ndipo Sofari Mnaamathi alijibu na kusema,
2 Skulde en ordflom bli uten svar, eller en ordgyter få rett?
“Huo wingi wa maneno haupaswi kujibiwa? Mtu huyu, aliyejaa maneno mengi awe wa kuaminiwa?
3 Skulde dine store ord drive menn til taushet, skulde du spotte uten at nogen skammer dig ut?
Kujivuna kwako kunapaswa kuwafanya wengine wabaki wamenyamaza? Wakati unapoyadhihaki mafundisho yetu, hakuna awaye yote atakayekufanya wewe ujisikie mwenye aibu?
4 Og skal du få si: Ren er min lære, og skyldfri er jeg i dine øine?
Kwa kuwa wewe unasema kwa Mungu, 'Imani yangu ni safi, Mimi sina waa lolote machoni pako.'
5 Men bare Gud vilde tale og oplate sine leber mot dig
Lakini, laiti, Mungu huyo angesema na kufungua midomo yake dhidi yako;
6 og åpenbare dig visdommens hemmeligheter, at det i dem er dobbelt forstand! Da måtte du nok innse at Gud tilgir dig noget av din misgjerning.
hivyo angekuonyesha wewe siri za hekima! Kwa kuwa yeye ni mkuu katika ufahamu. Tena tambua huyo Mungu anataka kutoka kwako kidogo kuliko uovu wako unavyostahili.
7 Mon du kan finne bunn i Guds vesen eller nå frem til den Allmektiges ytterste grense?
Je, wewe unaweza kumfahamu Mungu kwa kumtafuta yeye? Unaweza kumtambua aliye mkuu kwa ukamilifu?
8 Himmelhøi er den, hvad kan du gjøre? Dypere enn dødsriket, hvad vet du? (Sheol h7585)
Upeo uko juu kama mbingu; unaweza kufanya nini wewe? Ni wenye kina kirefu kuliko kuzimu; waweza kufahamu nini wewe? (Sheol h7585)
9 Lengere enn jorden er dens mål og bredere enn havet.
Vipimo vyake ni virefu kuliko nchi, na vipana kuliko bahari.
10 Om han farer frem og setter i fengsel og sammenkaller retten, hvem vil da hindre ham?
kama yeye akipita kati na kumyamazisha mtu yeyote, kama yeye akimwita mtu yeyote hukumuni, tena ni nani anayeweza kumzuia yeye?
11 For han, han kjenner de falske folk og ser uretten, uten at han trenger å gi akt på den,
Kwa maana anawajua watu waongo; wakati anapoona uovu, hawezi yeye kuukumbuka?
12 og selv en uvettig mann får forstand, og et ungt villesel blir født til menneske.
Lakini watu wapumbavu hawana ufahamu; wataupata wakati punda mwitu atakapozaa mtu.
13 Hvis du retter ditt hjerte og utbreder dine hender til ham -
Lakini ikiwa umeuelekeza moyo wako kwa haki na umeunyosha mkono wako karibu na Mungu;
14 er det synd i din hånd, da ha den bort og la ikke urett bo i dine telt -
ikiwa huo uovu ulikuwa katika mikono yako, lakini hivyo tena unauweka mbali nawe, na haukuruhusu kutokuwa mwenye haki kukaa hemani mwako.
15 ja, da skal du, fri for lyte, opløfte ditt åsyn og stå fast og ikke frykte;
Ndipo kwa hakika ungeinua juu uso wako bila ishara ya aibu; Ni dhahiri, ungethibitika na usingeogopa.
16 for du skal glemme din møie, som forbifarne vann skal du komme den i hu.
Wewe ungesahau mateso yako; ungeyakumbuka hayo tu kama maji ambayo yametiririka mbali.
17 Og lysere enn middagen blir da ditt liv; mørket blir for dig som morgenen.
Maisha yako yangekuwa angavu kuliko adhuhuri; japokuwa kulikuwa na giza, litakuwa kama asubuhi.
18 Og du skal være trygg, for da er det håp, og når du har sett dig vel omkring, kan du legge dig trygt til ro.
Ungekuwa salama kwa sababu kuna tumaini; ni dhahiri, wewe utapata usalama juu yako na utachukua pumziko lako katika usalama.
19 Og du skal hvile, og ingen skal skremme dig op, og mange skal søke din yndest.
Pia ungelala chini katika pumziko, na hakuna ambaye angekufanya wewe uogope; hakika wengi wangetafuta upendeleo wako.
20 Men de ugudeliges øine tæres bort; de har ingen tilflukt mere, og deres håp er å utånde sjelen.
Lakini macho ya watu waovu yatashindwa; hawatakuwa na njia ya kukimbia; tumaini lao la pekee litakuwa pumzi yao ya mwisho ya uhai.

< Jobs 11 >