< Jeremias 50 >

1 Dette er det ord Herren talte om Babel, om kaldeernes land, ved profeten Jeremias.
Hili ndilo neno alilosema Bwana kupitia nabii Yeremia kuhusu Babeli na nchi ya Wakaldayo:
2 Forkynn det iblandt folkene og kunngjør det og løft op banner, kunngjør det, dølg det ikke, si: Babel er inntatt, Bel er blitt til skamme, Merodak er blitt forferdet, dets gudebilleder er blitt til skamme, dets vederstyggelige avguder er forferdet!
“Tangazeni na mhubiri katikati ya mataifa, twekeni bendera na mkahubiri; msiache kitu chochote, bali semeni, ‘Babeli utatekwa; Beli ataaibishwa, Merodaki atajazwa na hofu kuu. Sanamu zake zitaaibishwa na vinyago vyake vitajazwa hofu kuu.’
3 For et folk drar op imot det fra nord, det gjør dets land til en ørken, og det er ingen som bor i det; både mennesker og dyr er flyktet bort.
Taifa kutoka kaskazini litamshambulia, na kuifanya nchi yake ukiwa. Hakuna hata mmoja atakayeishi ndani yake, watu na wanyama wataikimbia.
4 I de dager og på den tid, sier Herren, skal Israels barn komme, de og Judas barn sammen; de skal gå og gråte, og Herren sin Gud skal de søke.
“Katika siku hizo, wakati huo,” asema Bwana, “watu wa Israeli pamoja na watu wa Yuda wataenda wakilia ili kumtafuta Bwana Mungu wao.
5 Efter Sion skal de spørre, hit er deres åsyn vendt: Kom og gi eder til Herren ved en evig pakt, som ikke glemmes!
Wataiuliza njia iendayo Sayuni na kuelekeza nyuso zao huko. Watakuja na kuambatana na Bwana katika agano la milele ambalo halitasahaulika.
6 Fortapte får var mitt folk, deres hyrder hadde ført dem vill, til fjellene hadde de drevet dem bort; fra fjell til haug gikk de, de glemte sitt hvilested.
“Watu wangu wamekuwa kondoo waliopotea; wachungaji wao wamewapotosha na kuwasababisha kuzurura juu ya milima. Walitangatanga juu ya mlima na kilima, na kusahau mahali pao wenyewe pa kupumzikia.
7 Alle som traff dem, åt dem, og deres fiender sa: Vi skal ikke bøte for det - fordi de hadde syndet mot Herren, rettferdighetens bolig, og mot sine fedres håp, Herren.
Yeyote aliyewakuta aliwala; adui zao walisema, ‘Sisi hatuna hatia, kwa kuwa wao walitenda dhambi dhidi ya Bwana, malisho yao halisi, Bwana, aliye tumaini la baba zao.’
8 Fly ut av Babel og dra bort fra kaldeernes land, og gå som bukker foran hjorden!
“Kimbieni kutoka Babeli; ondokeni katika nchi ya Wakaldayo tena kuweni kama mbuzi wale waongozao kundi.
9 For se, jeg vekker og fører op imot Babel en skare av store folkeslag fra landet i nord, og de skal stille sig op imot det; av dem skal det bli inntatt; deres piler er som en prøvet kjempes, ingen vender tilbake med uforrettet sak.
Kwa maana nitaamsha na kuleta dhidi ya Babeli muungano wa mataifa makubwa kutoka nchi ya kaskazini. Watashika nafasi zao dhidi yake, naye kutokea kaskazini atatekwa. Mishale yao itakuwa kama mishale ya mashujaa walio hodari, ambao hawawezi kurudi mikono mitupu.
10 Og Kaldea skal bli til rov; alle som røver det, skal mettes, sier Herren.
Kwa hiyo Ukaldayo utatekwa nyara; wote wamtekao nyara watapata za kutosha,” asema Bwana.
11 Ja, gled eder bare, ja, juble bare, I som plyndrer min arv! Ja, hopp bare som en treskende kvige og vrinsk som de sterke hester!
“Kwa sababu hushangilia na kufurahi, wewe utekaye urithi wangu, kwa sababu unachezacheza kama mtamba anayepura nafaka, na kulia kama farasi dume,
12 Eders mor blir storlig til skamme, hun som fødte eder, blues; se, hun blir det siste blandt folkene, en ørken, et tørt land og en øde mark.
mama yako ataaibika mno, yeye aliyekuzaa atatahayari. Atakuwa mdogo kuliko mataifa mengine yote, atakuwa nyika, nchi kame na jangwa.
13 For Herrens vredes skyld skal det aldri bo folk der igjen, det hele skal bli til en ørken; hver den som går forbi Babel, skal forferdes og spotte over alle dets plager.
Kwa sababu ya hasira ya Bwana hatakaliwa na mtu, lakini ataachwa ukiwa kabisa. Wote watakaopita Babeli watatiwa hofu na kudhihaki kwa sababu ya majeraha yake yote.
14 Still eder op mot Babel rundt omkring, alle I som spenner bue! Skyt på det, spar ikke på pilene! For mot Herren har det syndet.
“Shikeni nafasi zenu kuzunguka Babeli, enyi nyote mvutao upinde. Mpigeni! Msibakize mshale wowote, kwa kuwa ametenda dhambi dhidi ya Bwana.
15 Opløft hærskrik mot det rundt omkring! Det har overgitt sig, dets grunnvoller er falt, dets murer er brutt ned; for det er Herrens hevn. Hevn eder på det! Gjør mot det således som det har gjort!
Piga kelele dhidi yake kila upande! Anajisalimisha, minara yake inaanguka, kuta zake zimebomoka. Kwa kuwa hiki ni kisasi cha Bwana, mlipizeni kisasi; mtendeeni kama alivyowatendea wengine.
16 Utrydd av Babel både såmann og den som fører sigden i høstens tid! For det herjende sverd skal de vende sig hver til sitt folk og fly hver til sitt land.
Katilieni mbali mpanzi kutoka Babeli, pamoja na mvunaji na mundu wake akivuna. Kwa sababu ya upanga wa mdhalimu kila mmoja na arejee kwa watu wake mwenyewe, kila mmoja na akimbilie kwenye nchi yake mwenyewe.
17 Et bortdrevet lam er Israel, løver har jaget det bort; først åt Assurs konge det, og nu sist har Babels konge Nebukadnesar knust dets ben.
“Israeli ni kundi lililotawanyika ambalo simba wamelifukuzia mbali. Wa kwanza kumla alikuwa mfalme wa Ashuru, wa mwisho kuponda mifupa yake alikuwa Nebukadneza mfalme wa Babeli.”
18 Derfor sier Herren, hærskarenes Gud, Israels Gud, så: Se, jeg hjemsøker Babels konge og hans land, likesom jeg har hjemsøkt Assurs konge.
Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Nitamwadhibu mfalme wa Babeli na nchi yake kama nilivyomwadhibu mfalme wa Ashuru.
19 Og jeg vil føre Israel tilbake til dets beitemarker, og det skal beite på Karmel og i Basan, og på Efra'ims fjell og i Gilead skal det ete sig mett.
Lakini nitamrudisha Israeli katika malisho yake mwenyewe naye atalisha huko Karmeli na Bashani; njaa yake itashibishwa juu ya vilima vya Efraimu na Gileadi.
20 I de dager og på den tid, sier Herren, skal de søke efter Israels misgjerning, men den skal ikke være til, og efter Judas synder, men de skal ikke finnes; for jeg vil tilgi dem som jeg lar bli igjen.
Katika siku hizo, wakati huo,” asema Bwana, “uchunguzi utafanyika kwa ajili ya kosa la Israeli, lakini halitakuwepo, kwa ajili ya dhambi za Yuda, lakini haitapatikana hata moja, kwa kuwa nitawasamehe mabaki nitakaowaacha.
21 Dra op mot Merata'ims land og mot Pekods innbyggere! Forfølg dem, ødelegg dem og slå dem med bann, sier Herren, og gjør i alle deler som jeg har befalt dig!
“Shambulieni nchi ya Merathaimu na wale waishio huko Pekodi. Wafuatieni, waueni na kuwaangamiza kabisa,” asema Bwana. “Fanyeni kila kitu nilichowaamuru.
22 Det er larm av krig i landet og stor ødeleggelse.
Kelele ya vita iko ndani ya nchi, kelele ya maangamizi makuu!
23 Hvor den er blitt knekket og knust den hammer som slo hele jorden! Hvor Babel er blitt til en forferdelse blandt folkene!
Tazama jinsi nyundo ya dunia yote ilivyovunjika na kuharibika! Tazama jinsi Babeli ilivyokuwa ukiwa miongoni mwa mataifa!
24 Jeg stilte snare for dig, og du blev fanget, Babel, uten at du visste av det; du blev funnet og grepet; for mot Herren hadde du gitt dig i strid.
Nimetega mtego kwa ajili yako, ee Babeli, nawe ukakamatwa kabla haujafahamu; ulipatikana na ukakamatwa kwa sababu ulimpinga Bwana.
25 Herren har åpnet sitt rustkammer og tatt frem sin vredes våben; for Herren, Israels Gud, hærskarenes Gud, har et arbeid fore i kaldeernes land.
Bwana amefungua ghala lake la silaha na kuzitoa silaha za ghadhabu yake, kwa kuwa Bwana Mwenyezi Mwenye Nguvu Zote anayo kazi ya kufanya katika nchi ya Wakaldayo.
26 Kom imot det fra alle kanter! Åpne dets forrådshus, dyng op som korndynger det som finnes der, og slå det med bann! La det ikke ha noget igjen!
Njooni dhidi yake kutoka mbali. Zifungueni ghala zake za nafaka; mlundikeni kama lundo la nafaka. Mwangamizeni kabisa na msimwachie mabaki yoyote.
27 Drep alle dets okser, la dem stige ned for å slaktes! Ve over dem! For deres dag er kommet, deres hjemsøkelses tid.
Waueni mafahali wake wachanga wote; waacheni washuke machinjoni! Ole wao! Kwa kuwa siku yao imewadia, wakati wao wa kuadhibiwa.
28 Hør! De er flyktet og undkommet fra Babels land for å kunngjøre i Sion Herrens, vår Guds hevn, hevnen for hans tempel!
Wasikilizeni watoro na wakimbizi kutoka Babeli wakitangaza katika Sayuni jinsi Bwana, Mungu wetu alivyolipiza kisasi, kisasi kwa ajili ya Hekalu lake.
29 Kall skytterne sammen mot Babel, alle dem som spenner bue! Slå leir mot det rundt omkring, la ingen slippe unda! Betal det efter dets gjerninger, gjør mot det i alle deler som det har gjort! For mot Herren har det ophøiet sig, mot Israels Hellige.
“Waiteni wapiga mishale dhidi ya Babeli, wote wale wavutao upinde. Pigeni kambi kumzunguka kabisa, asitoroke mtu yeyote. Mlipizeni kwa matendo yake; mtendeeni kama alivyotenda. Kwa kuwa alimdharau Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
30 Derfor skal dets unge menn falle på dets gater, og alle dets krigsmenn skal tilintetgjøres på den dag, sier Herren.
Kwa hiyo, vijana wake wanaume wataanguka barabarani; askari wake wote watanyamazishwa siku ile,” asema Bwana.
31 Se, jeg kommer over dig, Sadon, sier Herren, Israels Gud, hærskarenes Gud; for din dag er kommet, den tid da jeg hjemsøker dig.
“Tazama, niko kinyume nawe, ewe mwenye majivuno,” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, “kwa kuwa siku yako imewadia, yaani, wakati wako wa kuadhibiwa.
32 Og Sadon skal snuble og falle uten å ha nogen som reiser det op, og jeg vil sette ild på dets byer, og den skal fortære alt rundt omkring det.
Mwenye majivuno atajikwaa na kuanguka, wala hakuna yeyote atakayemuinua; nitawasha moto katika miji yake, utakaowateketeza wote wanaomzunguka.”
33 Så sier Herren, hærskarenes Gud: Undertrykt er både Israels barn og Judas barn, og alle de som har ført dem i fangenskap, holder dem fast; de nekter å la dem fare.
Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Watu wa Israeli wameonewa, nao watu wa Yuda pia. Wote waliowateka wamewashikilia sana, wanakataa kuwaachia waende.
34 Deres gjenløser er sterk, Herren, hærskarenes Gud, er hans navn; han skal visselig føre deres sak og la jorden få ro, men volde Babels innbyggere uro.
Lakini Mkombozi wao ana nguvu; Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake. Atatetea kwa nguvu shauri lao ili alete raha katika nchi yao, lakini ataleta msukosuko kwa wale waishio Babeli.
35 Sverd over kaldeerne, sier Herren, over Babels innbyggere, over dets høvdinger og over dets vismenn!
“Upanga dhidi ya Wakaldayo!” asema Bwana, “dhidi ya wale waishio Babeli na dhidi ya maafisa wake na watu wenye busara!
36 Sverd over snakkerne! De skal stå der som dårer. Sverd over dets kjemper! De skal bli forferdet.
Upanga dhidi ya manabii wake wa uongo! Watakuwa wapumbavu. Upanga dhidi ya mashujaa wake! Watajazwa na hofu kuu
37 Sverd over dets hester og over dets vogner og over alle de fremmede krigsfolk blandt dem! De skal bli til kvinner. Sverd over dets skatter! De skal bli røvet.
Upanga dhidi ya farasi na magari yake ya vita pamoja na askari wake wote wa kigeni katika safu zake! Wao watakuwa kama wanawake. Upanga dhidi ya hazina zake! Hizo zitatekwa nyara.
38 Tørke over dets vann! De skal tørkes ut. For det er et land med avgudsbilleder, og med sine gruelige avguder ter de sig som rasende.
Ukame juu ya maji yake! Nayo yatakauka. Kwa kuwa ni nchi ya sanamu, wao wanaenda wazimu kwa ajili ya sanamu.
39 Derfor skal ørkenens dyr bo der sammen med ville hunder, og strutser skal bo i det; og det skal aldri mere reise sig igjen, og slekt efter slekt skal ingen bo der.
“Kwa hiyo, viumbe vya jangwani na fisi wataishi humo, nao bundi watakaa humo. Kamwe haitakaliwa tena wala watu hawataishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.
40 Som da Gud la Sodoma og Gomorra og dets nabobyer i grus, sier Herren, skal ingen mann bo der, og intet menneskebarn opholde sig der.
Kama vile Mungu alivyoangamiza Sodoma na Gomora pamoja na miji iliyokuwa jirani nayo,” asema Bwana, “vivyo hivyo hakuna mtu yeyote atakayeishi humo. Naam, hakuna mtu yeyote atakayekaa humo.
41 Se, et folk kommer fra nord, et stort folk, og mange konger skal stå frem fra jordens ytterste ende.
“Tazama! Jeshi linakuja kutoka kaskazini; taifa kubwa na wafalme wengi wanaamshwa kutoka miisho ya dunia.
42 Bue og spyd holder de i hånden, de er grusomme og skåner ingen; deres røst bruser som havet, og på hester kommer de ridende, rustet som en krigsmann, mot dig, Babels datter!
Wamejifunga pinde na mikuki; ni wakatili na wasio na huruma. Wanatoa sauti kama bahari inayonguruma wanapoendesha farasi zao; wanakuja kama watu waliojipanga tayari kwa vita ili kukushambulia, ee Binti Babeli.
43 Babels konge har hørt ryktet om dem, og hans hender er blitt kraftløse; angst har grepet ham, smerter som den fødende kvinnes.
Mfalme wa Babeli amesikia habari kuwahusu, nayo mikono yake imelegea. Uchungu umemshika, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
44 Se, han stiger op som en løve fra Jordans prakt til de alltid grønne enger; for i et øieblikk vil jeg jage dem bort derfra, og den som er utvalgt, ham vil jeg sette over det; for hvem er som jeg, og hvem vil stevne mig, og hvem er den hyrde som kan bli stående for mitt åsyn?
Kama simba anayepanda kutoka vichaka vya Yordani kuja kwenye nchi ya malisho mengi, ndivyo nitamfukuza Babeli kutoka nchi yake ghafula. Ni nani aliye mteule, nitakayemweka kwa ajili ya jambo hili? Ni nani aliye kama mimi, na ni nani awezaye kunipinga? Tena ni mchungaji yupi awezaye kusimama kinyume nami?”
45 Hør derfor det råd som Herren har lagt mot Babel, og de tanker som han har tenkt mot kaldeernes land: Visselig, de skal bli slept bort de små lam; visselig, deres beitemark skal forferdes over dem.
Kwa hiyo, sikia kile Bwana alichokipanga dhidi ya Babeli, kile alichokusudia dhidi ya nchi ya Wakaldayo: Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali. Yeye ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao.
46 Ved det rop: Babel er inntatt, bever jorden, og det høres skrik blandt folkene.
Kwa sauti ya kutekwa kwa Babeli, dunia itatetemeka; kilio chake kitasikika pote miongoni mwa mataifa.

< Jeremias 50 >