< Jeremias 36 >
1 I Judas konge Jojakims, Josias' sønns fjerde år kom dette ord til Jeremias fra Herren:
Katika mwaka wa nne wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, neno hili lilimjia nabii Yeremia kutoka kwa Bwana, kusema:
2 Ta dig en bokrull og skriv i den alle de ord jeg har talt til dig om Israel og Juda og alle hedningefolkene fra den dag da jeg først talte til dig, fra Josias' dager og like til denne dag!
“Chukua kitabu uandike ndani yake maneno yote niliyonena nawe kuhusu Israeli, Yuda na mataifa mengine yote, tangu nilipoanza kunena nawe wakati wa utawala wa Yosia hadi sasa.
3 Kanskje Judas hus vil merke sig all den ulykke jeg tenker å gjøre dem, så de kan vende om, hver fra sin onde vei, og jeg kan forlate dem deres misgjerning og deres synd.
Labda watu wa Yuda watakaposikia juu ya kila maafa ninayokusudia kuwapiga nayo, kila mmoja wao atageuka kutoka njia zake mbaya, kisha nitasamehe uovu wao na dhambi yao.”
4 Da kalte Jeremias til sig Baruk, Nerijas sønn, og Baruk skrev efter Jeremias' munn alle de ord som Herren hadde talt til ham, i en bokrull.
Hivyo Yeremia akamwita Baruku mwana wa Neria, naye Yeremia alipokuwa akiyakariri maneno yote aliyoyasema Bwana, Baruku akayaandika katika kitabu.
5 Og Jeremias talte til Baruk og sa: Jeg er forhindret, jeg kan ikke komme til Herrens hus.
Kisha Yeremia akamwambia Baruku, “Nimezuiliwa, mimi siwezi kuingia katika Hekalu la Bwana.
6 Men gå du dit og les av rullen som du har skrevet efter min munn, Herrens ord op for folket i Herrens hus på en fastedag! Også for hele Juda, som kommer fra sine byer, skal du lese den.
Basi wewe nenda katika nyumba ya Bwana siku ya kufunga, uwasomee watu maneno ya Bwana kutoka kitabu hiki yale uliyoyaandika kutoka kinywani mwangu. Wasomee watu wote wa Yuda waliofika kutoka miji yao.
7 Kanskje de vil legge sin ydmyke bønn frem for Herrens åsyn og vende om, hver fra sin onde vei; for stor er den vrede og harme som Herren har uttalt over dette folk.
Labda wataomba na kusihi mbele za Bwana na kila mmoja akageuka kutoka njia zake mbaya, kwa sababu hasira na ghadhabu zilizotamkwa dhidi ya watu hawa na Bwana ni kubwa.”
8 Og Baruk, Nerijas sønn, gjorde alt som profeten Jeremias hadde pålagt ham, og leste Herrens ord op av boken i Herrens hus.
Baruku mwana wa Neria akafanya kila kitu nabii Yeremia alichomwambia kufanya. Alisoma maneno ya Bwana katika Hekalu la Bwana kutoka kile kitabu.
9 For i Judas konge Jojakims, Josias' sønns femte år, i den niende måned, blev det ropt ut at alt folket i Jerusalem og alt folket som var kommet fra Judas byer til Jerusalem, skulde faste for Herrens åsyn.
Katika mwezi wa tisa, mnamo mwaka wa tano wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, wakati wa kufunga mbele za Bwana, ilitangazwa kwa watu wote walioko Yerusalemu, na wale wote waliokuwa wamekuja kutoka miji ya Yuda.
10 Da leste Baruk op av boken Jeremias' ord i Herrens hus, i statsskriveren Gemarjas, Safans sønns kammer i den øvre forgård, ved inngangen til den nye port i Herrens hus, mens alt folket hørte på.
Kutoka chumba cha Gemaria mwana wa Shafani mwandishi, kilichokuwa katika ua wa juu kwenye ingilio la Lango Jipya la Hekalu, Baruku akawasomea watu wote waliokuwa katika Hekalu la Bwana maneno ya Yeremia kutoka kwenye kile kitabu.
11 Da Mikaja, sønn av Gemarja, sønn av Safan, hørte alle Herrens ord bli lest op av boken,
Basi Mikaya mwana wa Gemaria, mwana wa Shafani, aliposikia maneno yote ya Bwana kutoka kwenye kile kitabu,
12 gikk han ned til kongens hus, til statsskriverens kammer, og der fant han alle høvdingene sittende: statsskriveren Elisama og Delaja, Sjemajas sønn, og Elnatan, Akbors sønn, og Gemarja, Safans sønn, og Sedekias, Hananjas sønn, og alle de andre høvdinger.
alishuka hadi kwenye chumba cha mwandishi kwenye jumba la kifalme, mahali walipokuwa wameketi maafisa wote: yaani Elishama mwandishi, Delaya mwana wa Shemaya, Elnathani mwana wa Akbori, Gemaria mwana wa Shafani, Sedekia mwana wa Hanania, na maafisa wengine wote.
13 Og Mikaja fortalte dem om alle de ord han hadde hørt da Baruk leste op av boken for folket.
Baada ya Mikaya kuwaambia kila kitu ambacho alikuwa amesikia Baruku akiwasomea watu kutoka kwenye kile kitabu,
14 Da sendte alle høvdingene Jehudi, sønn av Netanja, sønn av Selemja, sønn av Kusi, til Baruk og sa: Ta med dig rullen som du leste op av for folket, og kom hit! Og Baruk, Nerijas sønn, tok rullen med sig og kom til dem.
maafisa wote wakamtuma Yehudi mwana wa Nethania, mwana wa Shelemia, mwana wa Kushi, kumwambia Baruku, “Leta hicho kitabu ambacho umewasomea watu, nawe mwenyewe uje.” Ndipo Baruku mwana wa Neria akawaendea akiwa na hicho kitabu mkononi mwake.
15 De sa til ham: Sett dig ned og les den for oss! Og Baruk leste den for dem.
Wakamwambia, “Tafadhali, keti na utusomee hicho kitabu.” Ndipo Baruku akawasomea kile kitabu.
16 Og da de hørte alle ordene, vendte de sig forferdet til hverandre, og de sa til Baruk: Vi må melde kongen alt dette.
Walipoyasikia maneno hayo yote, wakatazamana wao kwa wao kwa woga na kumwambia Baruku, “Lazima tutoe taarifa ya maneno haya yote kwa mfalme.”
17 Så spurte de Baruk: Fortell oss hvorledes du skrev alle disse ord efter hans munn!
Kisha wakamuuliza Baruku, “Tuambie, uliandikaje haya yote? Je, yalitoka kinywani mwa Yeremia?”
18 Baruk svarte: Med sin munn foresa han mig alle disse ord, og jeg skrev dem i boken med blekk.
Baruku akajibu, “Ndiyo, maneno haya yote yalitoka kinywani mwa Yeremia, nami nikayaandika kwa wino katika hiki kitabu.”
19 Da sa høvdingene til Baruk: Gå og skjul dig, du og Jeremias, og la ingen vite hvor I er!
Ndipo wale maafisa wakamwambia Baruku, “Wewe na Yeremia nendeni mkajifiche. Mtu yeyote asijue mahali mlipo.”
20 Så gikk de inn til kongen i forgården, men rullen la de ned i statsskriveren Elisamas kammer; og de fortalte alt dette til kongen.
Baada ya kuhifadhi kile kitabu ndani ya chumba cha Elishama mwandishi, wakamwendea mfalme katika ua wa nje na kumwarifu kila kitu.
21 Da sendte kongen Jehudi avsted for å hente rullen, og han hentet den fra statsskriveren Elisamas kammer, og Jehudi leste den op for kongen og alle høvdingene som stod hos kongen.
Mfalme akamtuma Yehudi akachukue kile kitabu. Yehudi akakileta hicho kitabu kutoka kwenye chumba cha Elishama mwandishi, na akakisoma mbele ya mfalme na maafisa wakiwa wamesimama kando ya mfalme.
22 Kongen satt i vinterhuset, for det var den niende måned, og det brente ild i et fyrfat foran ham,
Ulikuwa mwezi wa tisa, na mfalme alikuwa ameketi chumba cha wakati wa baridi akiota moto.
23 og da Jehudi hadde lest op tre eller fire blad, skar kongen rullen i stykker med en pennekniv og kastet den på ilden i fyrfatet, inntil hele rullen var fortært av ilden der i fyrfatet.
Hata ikawa kila wakati Yehudi alipomaliza kusoma kurasa tatu au nne za hicho kitabu, mfalme alizikata kwa kisu cha mwandishi na kuzitupia motoni, hadi kitabu chote kikateketea.
24 Og de forferdedes ikke og sønderrev ikke sine klær, hverken kongen eller nogen av hans tjenere som hørte alle disse ord,
Mfalme na watumishi wake wote waliosikia yote yaliyosomwa hawakuonyesha hofu yoyote, wala hawakuyararua mavazi yao.
25 og skjønt Elnatan og Delaja og Gemarja inntrengende bad kongen at han ikke skulde brenne rullen, hørte han ikke på dem.
Hata ingawa Elnathani, Delaya na Gemaria walimsihi mfalme asikichome kile kitabu, yeye hakuwasikiliza.
26 Så bød kongen Jerahme'el, kongesønnen, og Seraja, Asriels sønn, og Selemja, Abde'els sønn, å gripe skriveren Baruk og profeten Jeremias; men Herren skjulte dem.
Badala yake, mfalme akamwamuru Yerameeli, mwana wa mfalme, Seraya mwana wa Azrieli, na Shelemia mwana wa Abdeeli kuwakamata mwandishi Baruku na nabii Yeremia. Lakini Bwana alikuwa amewaficha.
27 Da kom Herrens ord til Jeremias, efterat kongen hadde brent op rullen med de ord Baruk hadde skrevet efter Jeremias' munn:
Baada ya mfalme kuchoma kile kitabu kilichokuwa na yale maneno Baruku aliyokuwa ameyaandika kutoka kinywani mwa Yeremia, neno la Bwana lilimjia Yeremia likisema:
28 Ta dig en annen rull og skriv i den alle de forrige ord, de som stod i den forrige rull, som Judas konge Jojakim brente op!
“Chukua kitabu kingine na uandike juu yake maneno yote yaliyokuwa katika kile kitabu cha kwanza, ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda amekiteketeza kwa moto.
29 Og om Judas konge Jojakim skal du si: Så sier Herren: Du brente denne rull og sa: Hvorfor skrev du i den således: Babels konge skal komme og ødelegge dette land og utrydde mennesker og dyr av det?
Mwambie pia Yehoyakimu mfalme wa Yuda, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ulikiteketeza kile kitabu ukasema, “Kwa nini uliandika kwenye kitabu kwamba kwa hakika mfalme wa Babeli angekuja na kuangamiza nchi hii, na kuwakatilia mbali watu na wanyama kutoka humo?”
30 Derfor sier Herren så om Judas konge Jojakim: Han skal ikke ha nogen ætling som skal sitte på Davids trone, og hans døde kropp skal ligge slengt bort, utsatt for heten om dagen og for kulden om natten.
Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana kuhusu Yehoyakimu mfalme wa Yuda: Hatakuwa na mtu yeyote atakayekalia kiti cha enzi cha Daudi; maiti yake itatupwa nje kwenye joto wakati wa mchana na kupigwa na baridi wakati wa usiku.
31 Og jeg vil hjemsøke ham og hans ætt og hans tjenere for deres misgjerning, og jeg vil la komme over dem og over Jerusalems innbyggere og over Judas menn all den ulykke jeg har forkynt dem uten at de vilde høre.
Nitamwadhibu yeye, watoto wake na watumishi wake kwa ajili ya uovu wao. Nitaleta juu yao na wote waishio Yerusalemu na watu wa Yuda kila maafa niliyoyasema dhidi yao, kwa sababu hawajasikiliza.’”
32 Da tok Jeremias en annen rull og gav den til skriveren Baruk, Nerijas sønn, og han skrev i den efter Jeremias' munn alle ordene i den bok som Judas konge Jojakim hadde brent i ilden, og det blev til dem ennu lagt mange lignende ord.
Kisha Yeremia akachukua kitabu kingine na kumpa mwandishi Baruku mwana wa Neria, naye kama Yeremia alivyosema, Baruku akaandika juu yake maneno yote ya kile kitabu ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda alikuwa amekichoma moto, na maneno mengine mengi yaliyofanana na hayo yaliyoongezewa humo.