< Esaias 16 >

1 Send landsherren de lam han skal ha, fra Sela gjennem ørkenen til Sions datters berg!
Pelekeni wana-kondoo kama ushuru kwa mtawala wa nchi, Kutoka Sela, kupitia jangwani, hadi mlima wa Binti Sayuni.
2 Som flagrende fugler, lik unger som er jaget bort fra redet, skal Moabs døtre være ved Arnons ferjesteder.
Kama ndege wanaopapatika waliofukuzwa kutoka kwenye kiota, ndivyo walivyo wanawake wa Moabu kwenye vivuko vya Arnoni.
3 Gi råd, finn utvei for oss! La din skygge midt på dagen være som natten! Skjul de fordrevne, forråd ikke dem som flykter!
“Tupeni shauri, toeni uamuzi. Wakati wa adhuhuri, fanyeni kivuli chenu kama usiku. Waficheni watoro, msisaliti wakimbizi.
4 La mine fordrevne barn få herberge hos dig! Vær et skjul for Moab mot ødeleggeren! For det er forbi med voldsmannen, ødeleggelsen får ende, undertrykkerne blir borte av landet.
Waacheni watoro wa Moabu wakae pamoja nanyi; kuweni mahali pao pa salama ili kuepuka mharabu.” Mtesi atafikia mwisho na maangamizi yatakoma, aletaye vita atatoweka kutoka nchi.
5 Så skal tronen bli grunnfestet ved miskunnhet, og en konge skal sitte trygt på den i Davids telt, en fyrste som søker rett og fremmer rettferdighet.
Kwa upendo kiti cha enzi kitaimarishwa, kwa uaminifu mtu ataketi juu yake, yeye atokaye nyumba ya Daudi: yeye ambaye katika kuhukumu hutafuta haki, na huhimiza njia ya haki.
6 Vi har hørt om Moabs veldige overmot, om dets stolthet, dets overmot og dets storaktighet, dets tomme skryt.
Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu: kiburi chake cha kujivuna na udanganyifu, kiburi chake na ufidhuli wake, lakini majivuno yake si kitu.
7 Derfor skal Moab klage over Moab, alle skal klage; over Kir-Haresets druekaker skal I sukke i dyp sorg.
Kwa hiyo Wamoabu wanaomboleza, wanaiombolezea Moabu kwa pamoja. Wanaomboleza na kuhuzunika kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi.
8 For Hesbons marker er visnet, og Sibmas vintre, hvis edle ranker slo folkenes herskere til jorden; de nådde like til Jaser og forvillet sig ut i ørkenen; dets kvister bredte sig ut og gikk over havet.
Mashamba ya Heshboni yananyauka, pia na mizabibu ya Sibma. Watawala wa mataifa wamekanyaga mizabibu iliyo mizuri sana, ambayo ilipata kufika Yazeri na kuenea kuelekea jangwani. Machipukizi yake yalienea yakafika hadi baharini.
9 Derfor gråter jeg med Jaser over Sibmas vintre; jeg vanner dig med mine tårer, Hesbon, og dig El'ale! For over din frukthøst og over din kornhøst faller frydeskrik.
Hivyo ninalia kama Yazeri aliavyo, kwa ajili ya mizabibu ya Sibma. Ee Heshboni, ee Eleale, ninakulowesha kwa machozi! Kelele za furaha kwa ajili ya tunda lako lililoiva na kwa ajili ya mavuno zimekomeshwa.
10 Og glede og fryd tas bort fra frukthavene, og i vingårdene lyder ingen frydesang, intet jubelrop; ingen treder vin i persekarene; frydeskriket gjør jeg ende på.
Furaha na shangwe zimeondolewa kutoka mashamba ya matunda; hakuna yeyote aimbaye wala apazaye sauti katika mashamba ya mizabibu; hakuna yeyote akanyagaye zabibu shinikizoni, kwa kuwa nimekomesha makelele.
11 Derfor bruser mitt indre for Moab som en citar, og mitt hjerte for Kir-Heres.
Moyo wangu unaomboleza kwa ajili ya Moabu kama kinubi, nafsi yangu yote kwa ajili ya Kir-Haresethi.
12 Og når Moab har møtt frem på offerhaugen og trettet sig ut der, og det går til sin helligdom for å bede, da utretter det intet.
Wakati Moabu anapojitokeza mahali pake pa juu, anajichosha mwenyewe tu; anapokwenda mahali pake pa kuabudia miungu ili kuomba, haitamfaidi lolote.
13 Dette er det ord som Herren fordum talte mot Moab.
Hili ndilo neno ambalo Bwana ameshasema kuhusu Moabu.
14 Men nu taler Herren og sier: Innen tre år, således som en dagarbeider regner årene, skal Moabs herlighet være aktet ringe tross hele dets store folkemengde, og det som blir levnet, skal være lite og ringe og ikke meget verdt.
Lakini sasa Bwana anasema: “Katika miaka mitatu, kama vile mtumishi aliyefungwa na mkataba angeihesabu, fahari ya Moabu na watu wake wengi watadharauliwa, nao walionusurika watakuwa wachache sana, tena wanyonge.”

< Esaias 16 >