< Esekiel 40 >
1 I det fem og tyvende år efterat vi var bortført, i begynnelsen av året, på den tiende dag i måneden, i det fjortende år efterat staden var inntatt, nettop på den dag kom Herrens hånd over mig, og han førte mig dit.
Katika mwaka wa ishirini na tano wa uhamisho wetu, mwanzoni mwa huo mwaka, siku ya kumi ya mwezi, katika mwaka wa kumi na nne baada ya kuanguka kwa mji, siku hiyo hiyo mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu, naye akanipeleka huko.
2 I syner fra Gud førte han mig til Israels land og satte mig ned på et meget høit fjell, og på det var det likesom en bygget stad i syd.
Nikiwa katika maono ya Mungu alinichukua mpaka nchi ya Israeli, naye akaniweka kwenye mlima mrefu sana, ambako upande wa kusini kulikuwepo baadhi ya majengo ambayo yalionekana kama mji.
3 Og han førte mig dit, og se, der var en mann hvis utseende var som kobber, og han hadde en linsnor og en målestang i hånden, og han stod i porten.
Akanipeleka huko, nami nikamwona mtu ambaye kuonekana kwake kulikuwa kama kuonekana kwa shaba. Alikuwa amesimama kwenye lango akiwa na kamba ya kitani na ufito wa kupimia mkononi mwake.
4 Og mannen talte til mig og sa: Menneskesønn! Se med dine øine og hør med dine ører og akt på alt det jeg vil la dig se! For du er ført hit, forat jeg skal la dig se det. Forkynn Israels hus alt det du ser!
Mtu huyo akaniambia, “Mwanadamu, angalia kwa macho yako na usikie kwa masikio yako nawe uzingatie kitu nitakachokuonyesha, kwa kuwa ndiyo sababu umeletwa hapa. Iambie nyumba ya Israeli kila kitu utakachoona.”
5 Og se, der var en mur utenom huset rundt omkring, og målestangen som mannen hadde i hånden, var seks alen lang, hver alen regnet til en almindelig alen og en håndsbredd, og han målte murens bredde: den var én stang, og dens høide: den var én stang.
Nikaona ukuta uliozunguka eneo lote la Hekalu. Ule ufito wa kupimia uliokuwa mkononi mwa yule mtu ulikuwa na urefu wa dhiraa ndefu sita, yaani, dhiraa ndefu ni sawa na dhiraa na nyanda nne, akapima ule ukuta. Ukuta huo ulikuwa na unene wa dhiraa ndefu sita na kimo cha dhiraa ndefu sita.
6 Så kom han til den port hvis forside vendte mot øst, og han steg op efter dens trin, og han målte portens treskel: den var én stang i bredden - det var den første treskel, og den var én stang i bredden.
Kisha akaenda kwenye lango linaloelekea mashariki. Akapanda ngazi zake akapima kizingiti cha lango, nacho kilikuwa na kina cha huo ufito.
7 Og hver vaktstue var én stang i lengden og én stang i bredden, og mellem vaktstuene var det fem alen, og portens treskel ved portens forhall på den indre side var én stang.
Vyumba vya kupumzikia vya walinzi vilikuwa na urefu wa huo ufito mmoja na upana wa huo ufito, kuta zilizogawa vyumba hivyo vya mapumziko zilikuwa na unene wa dhiraa tano. Nacho kizingiti cha lango lililokuwa karibu na ukumbi unaoelekea hekaluni ulikuwa na kina cha huo ufito.
8 Og han målte portens forhall på den indre side: den var én stang.
Kisha akapima baraza ya njia ya lango,
9 Og han målte portens forhall: den var åtte alen, og dens pilarer: de var to alen, og portens forhall lå på innsiden.
ambayo ilikuwa na kina cha dhiraa nane na miimo yake ilikuwa na unene wa dhiraa mbili. Baraza ya lango ilielekea Hekalu.
10 Og vaktstuene i porten mot øst var tre på hver side; alle tre var like store, og pilarene på begge sider var også like store.
Ndani ya lango la mashariki kulikuwepo vyumba vitatu vya kupumzikia kila upande, vyote vitatu vilikuwa na vipimo vilivyo sawa, nazo nyuso za kuta zilizotenganisha kila upande zilikuwa na vipimo vilivyo sawa.
11 Og han målte bredden av portåpningen: den var ti alen, og portens lengde: den var tretten alen.
Kisha akapima upana wa ingilio la lango, ilikuwa dhiraa kumi na urefu wake ulikuwa dhiraa kumi na tatu.
12 Foran vaktstuene var det et rum på én alen, og på den andre side likeledes et rum på én alen, og hver vaktstue var seks alen på den ene og seks alen på den andre side.
Mbele ya kila chumba cha kupumzikia kulikuwepo ukuta uliokuwa na kimo cha dhiraa moja kwenda juu, navyo hivyo vyumba vilikuwa dhiraa sita mraba.
13 Og han målte porten fra den ene vaktstues tak til den andres tak; bredden var fem og tyve alen, dør midt imot dør.
Kisha akapima njia ya lango kuanzia juu ya ukuta wa nyuma wa chumba kimoja cha kupumzikia hadi juu ya ukuta wa nyuma wa chumba upande wa pili; kukawa na nafasi ya dhiraa ishirini na tano kuanzia lango la ukuta mmoja hadi lango la ukuta uliokuwa upande mwingine.
14 Og han gjorde pilarene seksti alen høie, og tett inn til pilarene lå forgården, rundt omkring porten.
Akapima pia ukumbi, urefu wa dhiraa ishirini na lango linalofuatia hiyo nguzo kila upande wa huo ukumbi.
15 Og fra forsiden av inngangsporten til forsiden av den indre ports forhall var det femti alen.
Umbali kuanzia ingilio la njia ya lango hadi mwisho kabisa wa baraza yake ulikuwa dhiraa hamsini.
16 Og det var vinduer med fast gitter på vaktstuene og på deres pilarer innentil mot porten rundt omkring, og likeså på hallene; og således var det vinduer rundt omkring innentil, og på pilarene var det palmer.
Kulikuwa na vidirisha kwenye hivyo vyumba vya walinzi na nguzo za hivyo vyumba zilikuwa kwenye mzunguko wa hilo lango, vivyo hivyo kulikuwa na madirisha yaliyozunguka kuelekeana na ua na juu ya kila nguzo kulikuwa na mapambo ya miti ya mitende.
17 Så førte han mig til den ytre forgård, og se, der var kammere og et stenlagt gulv i forgården rundt omkring; det var tretti kammer på stengulvet.
Kisha akanileta katika ukumbi wa nje. Huko nikaona vyumba vingine pamoja na njia iliyokuwa imejengwa kuzunguka ukumbi wote, kulikuwa na vyumba thelathini vimepangana kando ya hiyo njia.
18 Og stengulvet var ved siden av portene, svarende til portenes lengde; det var det nedre stengulv.
Njia hii iliyojengwa iliambaa na lango, ikiwa na urefu sawa na lango, hii ilikuwa ni njia ya chini.
19 Og han målte bredden fra forsiden av den nedre port til den ytre forside av den indre forgård: den var hundre alen mot øst og mot nord.
Kisha akapima umbali kutoka ndani ya lango la chini mpaka nje ya ukumbi wa ndani, nao ulikuwa dhiraa mia moja upande wa mashariki na dhiraa mia moja upande wa kaskazini.
20 Så målte han lengden og bredden av den port hvis forside vendte mot nord, og som hørte til den ytre forgård.
Kisha akapima urefu na upana wa lango linaloelekea kaskazini, kukabili ukumbi wa nje.
21 Den hadde tre vaktstuer på hver side, og dens pilarer og haller var like store som de i den første port; den var femti alen lang og fem og tyve alen bred.
Vyumba vyake vilikuwa vitatu kila upande, kuta zilizogawanya vyumba na baraza ilikuwa na vipimo sawa na zile kuta za lango la kwanza. Zilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
22 Og vinduene og hallene og palmene var like store som i den port hvis forside vendte mot øst, og på syv trin steg en op i den, og dens haller lå foran dem.
Madirisha yake, baraza yake na nakshi yake ya miti ya mitende vilikuwa na vipimo sawasawa na vile vya lango linaloelekea mashariki. Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo.
23 Og porten til den indre forgård lå midt imot porten som vendte mot nord og mot øst, og han målte hundre alen fra port til port.
Kulikuwa na lango kwenye ukumbi wa ndani lililoelekea lile lango la kaskazini, kama vile ilivyokuwa ule upande wa mashariki. Akapima kutoka lango moja hadi lile lililo mkabala nalo, lilikuwa dhiraa mia moja.
24 Så førte han mig mot syd, og se, der var en port som vendte mot syd; og han målte dens pilarer og haller: de var like store som de andre.
Ndipo akaniongoza mpaka upande wa kusini, nami nikaona lango linaloelekea kusini. Akaipima miimo yake na baraza yake, navyo vilikuwa na vipimo sawa kama hivyo vingine.
25 Og det var vinduer på den og på dens haller rundt omkring, likesom de andre vinduer; den var femti alen lang og fem og tyve alen bred.
Lango na baraza yake vilikuwa na madirisha membamba pande zote, kama madirisha ya huko kwingine. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
26 Dens trapper hadde syv trin, og dens haller lå foran dem, og på dens pilarer var det palmer, én på hver side.
Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo. Ilikuwa na nakshi za miti ya mitende kwenye kuta zilizogawanya vyumba kila upande.
27 Og der var en port til den indre forgård mot syd, og fra denne port til porten mot syd målte han hundre alen.
Ukumbi wa ndani pia ulikuwa na lango lililoelekea kusini. Naye akapima kutoka lango hili mpaka kwenye lango la nje upande wa kusini; ilikuwa dhiraa mia moja.
28 Så førte han mig til den indre forgård gjennem sydporten, og han målte sydporten: den var like stor som de andre.
Kisha akanileta mpaka ukumbi wa ndani kwa kupitia lango la kusini, naye akapima lango la kusini, ambalo lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine.
29 Og dens vaktstuer og pilarer og haller var like store som de andre, og det var vinduer på den og på dens haller rundt omkring; den var femti alen lang og fem og tyve alen bred.
Vyumba vyake, kuta zilizogawanya vyumba na ukumbi wake zilikuwa na vipimo sawasawa na zile nyingine. Hilo lango na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Navyo vilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
30 Og det var haller rundt omkring, fem og tyve alen lange og fem alen brede.
(Baraza za malango zilizozunguka ukumbi wa ndani zilikuwa na upana wa dhiraa ishirini na tano na kina cha dhiraa tano.)
31 Hallene vendte ut mot den ytre forgård, og det var palmer på pilarene, og trappene hadde åtte trin.
Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
32 Så førte han mig til den indre forgård mot øst, og han målte porten: den var like stor som de andre.
Kisha akanileta mpaka kwenye ukumbi wa ndani ulioko upande wa mashariki, naye akalipima lango hilo, lilikuwa na vipimo vilivyo sawasawa na yale mengine.
33 Og dens vaktstuer og pilarer og haller var like store som de andre; og det var vinduer på den og på dens haller rundt omkring; den var femti alen lang og fem og tyve alen bred.
Vyumba vyake, kuta zake na baraza yake vilikuwa na vipimo vilivyo sawa na vile vingine. Lile lango pamoja na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Urefu wake ulikuwa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
34 Hallene vendte ut mot den ytre forgård, og det var palmer på pilarene på begge sider, og trappene hadde åtte trin.
Baraza yake ilielekea ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote. Kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
35 Så førte han mig til nordporten, og han målte den: den var like stor som de andre;
Kisha akanileta mpaka kwenye lango la kaskazini na kulipima. Lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine,
36 likeså målte han dens vaktstuer, pilarer og haller, og det var vinduer på den rundt omkring; den var femti alen lang og fem og tyve alen bred.
kama vile ilivyokuwa kwa vyumba, kuta zake na baraza yake, tena kulikuwa na madirisha pande zote. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
37 Dens pilarer vendte mot den ytre forgård, og det var palmer på pilarene på begge sider, og trappene hadde åtte trin.
Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
38 Og det var et kammer med dør i pilarene ved portene; der skulde de skylle brennofferet.
Kulikuwa na chumba na mlango karibu na baraza katika kila njia ya ndani ya lango ambamo sadaka za kuteketezwa zilioshwa.
39 Og i portens forhall stod det to bord på hver side til å slakte brennofferet og syndofferet og skyldofferet på.
Kwenye baraza ya lile lango kulikuwepo meza mbili kila upande, ambako sadaka za kuteketezwa, sadaka za dhambi na sadaka za hatia zilichinjiwa.
40 Og ved den ytre sidevegg, når en steg op i inngangen til porten mot nord, stod det to bord, og ved deri andre sidevegg på portens forhall stod det også to bord -
Karibu na ukuta wa nje wa baraza ya lile lango karibu na ngazi kwenye ingilio kuelekea kaskazini kulikuwa na meza mbili, nako upande mwingine wa ngazi kulikuwepo na meza mbili.
41 fire bord ved hver sidevegg på porten, tilsammen åtte bord; på dem skulde de slakte.
Kwa hiyo kulikuwa na meza nne upande mmoja wa lango na nyingine nne upande mwingine, zote zilikuwa meza nane, ambapo dhabihu zilichinjiwa.
42 Og det var fire bord til brennofferet; de var av hugne stener, halvannen alen lange og halvannen alen brede og én alen høie; på dem skulde de legge de redskaper som de skulde slakte brennofferet og slaktofferet med.
Pia kulikuwa na meza nne za mawe yaliyochongwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, kila meza ilikuwa na urefu wa dhiraa moja na nusu, upana wake dhiraa moja na nusu na kimo cha dhiraa moja. Juu ya meza hizo viliwekwa vyombo vya kuchinjia sadaka za kuteketezwa na dhabihu nyingine mbalimbali.
43 Og dobbelte knagger, en hånd brede, var festet på huset rundt omkring, og på bordene skulde offerkjøttet legges.
Kulikuwa na kulabu, urefu wake nyanda nne, zilikuwa zimeshikizwa ukutani pande zote. Meza zilikuwa kwa ajili ya nyama za sadaka.
44 Og utenfor den indre port var det kammere for sangerne i den indre forgård, ved siden av nordporten, og deres forside vendte mot syd; og en annen rad kammer lå ved siden av østporten, med forsiden mot nord.
Nje ya lango la ndani, kwenye ukumbi wa ndani, kulikuwa na vyumba viwili, kimoja upande wa lango la kaskazini nacho kilielekea kusini, kingine upande wa lango la kusini nacho kilielekea kaskazini.
45 Og han talte til mig og sa: Denne rad kammer, hvis forside vender mot syd, er for de prester som tar vare på det som er å vareta ved huset;
Akaniambia, “Chumba kinachoelekea upande wa kusini ni kwa ajili ya makuhani ambao wana usimamizi wa hekaluni,
46 men den rad kammer hvis forside vender mot nord, er for de prester som tar vare på det som er å vareta ved alteret; det er Sadoks sønner, de av Levis sønner som treder nær til Herren for å tjene ham.
nacho chumba kinachoelekea upande wa kaskazini ni kwa ajili ya makuhani wenye usimamizi wa madhabahuni. Hawa ni wana wa Sadoki, ambao ndio Walawi pekee wanaoweza kumkaribia Bwana ili kuhudumu mbele zake.”
47 Og han målte forgården: den var hundre alen lang og hundre alen bred i firkant, og alteret stod foran huset.
Ndipo alipopima ukumbi: nao ulikuwa mraba wa dhiraa mia moja urefu na upana. Madhabahu yalikuwa mbele ya Hekalu.
48 Så førte han mig til husets forhall og målte forhallens pilarer: de var fem alen på den ene og fem alen på den andre side, og portens bredde: den var tre alen på hver side.
Akanileta mpaka kwenye baraza ya Hekalu naye akaipima miimo ya hiyo baraza, nayo ilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande. Upana wa ingilio ulikuwa dhiraa kumi na nne na kuta zake zilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande.
49 Forhallen var tyve alen lang og elleve alen bred, og den hadde trin som førte op til den, og ved pilarene stod der søiler, én på hver side.
Baraza ilikuwa na dhiraa ishirini kwenda juu na dhiraa kumi na mbili kuanzia mbele hadi nyuma. Kulikuwa na ngazi kumi za kupandia huko, pia kulikuwa na nguzo kwa kila upande wa miimo.