< 2 Samuel 22 >

1 David kvad denne sang for Herren den dag da Herren hadde utfridd ham av alle hans fienders hånd og av Sauls hånd.
Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
2 Og han sa: Herren er min klippe og min festning og min redder,
Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
3 min klippefaste Gud, som jeg setter min lit til, mitt skjold og min frelses horn, min borg og min tilflukt, min frelser; fra vold frelser du mig.
Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
4 Jeg påkaller den Høilovede, Herren, og blir frelst fra mine fiender.
Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
5 Dødens bølger omspente mig, fordervelsens strømmer forferdet mig.
“Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
6 Dødsrikets rep omgav mig, dødens snarer overfalt mig. (Sheol h7585)
Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
7 I min trengsel påkalte jeg Herren, og jeg ropte til min Gud; han hørte fra sitt tempel min røst, og mitt skrik kom for hans ører.
Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
8 Da rystet og bevet jorden, himmelens grunnvoller skalv, og de rystet; for hans vrede var optendt.
“Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
9 Det steg røk op av hans nese, og fortærende ild fra hans munn; glør brente ut av ham.
Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
10 Og han bøide himmelen og steg ned, og det var mørke under hans føtter.
Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
11 Og han fór på kjeruber og fløi, og han lot sig se på vindens vinger.
Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
12 Og han gjorde mørke til skjul rundt omkring sig, vannmasser, tykke skyer.
Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
13 Frem av glansen foran ham brente gloende kull.
Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
14 Herren tordnet fra himmelen, den Høieste lot sin røst høre.
Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
15 Og han utsendte piler og spredte dem omkring - lyn og forvirret dem.
Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
16 Da kom havets strømmer til syne; jordens grunnvoller blev avdekket ved Herrens trusel, for hans neses åndepust.
Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
17 Han rakte sin hånd ut fra det høie, han grep mig; han drog mig op av store vann.
“Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
18 Han fridde mig ut fra min sterke fiende, fra mine avindsmenn; for de var mig for mektige.
Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
19 De overfalt mig på min motgangs dag; men Herren blev min støtte.
Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
20 Og han førte mig ut i fritt rum; han frelste mig, for han hadde behag i mig.
Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
21 Herren gjengjeldte mig efter min rettferdighet, han betalte mig efter mine henders renhet.
“Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
22 For jeg tok vare på Herrens veier og vek ikke i ondskap fra min Gud;
Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
23 for alle hans lover hadde jeg for øie, og fra hans bud vek jeg ikke,
Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
24 og jeg var ulastelig for ham og voktet mig vel for min synd.
Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
25 Og Herren gjengjeldte mig efter min rettferdighet, efter min renhet for hans øine.
Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
26 Mot den fromme viser du dig from, mot den rettvise stridsmann viser du dig rettvis,
“Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
27 mot den rene viser du dig ren, mot den forvendte viser du dig vrang.
kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
28 Elendige folk frelser du, men dine øine er mot de overmodige; dem fornedrer du.
Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
29 For du er mitt lys, Herre, og Herren opklarer mitt mørke.
Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
30 For ved dig stormer jeg løs på fiendeskarer, ved min Gud springer jeg over murer.
Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
31 Gud, hans vei er fullkommen; Herrens ord er rent, han er et skjold for alle dem som setter sin lit til ham.
“Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
32 For hvem er Gud foruten Herren, og hvem er en klippe foruten vår Gud?
Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
33 Gud, han er mitt sterke vern og leder den ulastelige på hans vei.
Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
34 Han gir ham føtter likesom hindene og stiller mig på mine høider.
Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
35 Han oplærer mine hender til krig, så mine armer spenner kobberbuen.
Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
36 Og du gir mig din frelse til skjold, og din mildhet gjør mig stor.
Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
37 Du gjør rummet vidt for mine skritt under mig, og mine ankler vakler ikke.
Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
38 Jeg vil forfølge mine fiender og ødelegge dem, og jeg vender ikke tilbake før jeg har gjort ende på dem.
“Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
39 Jeg gjør ende på dem og knuser dem, så de ikke kan reise sig; de faller under mine føtter.
Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
40 Og du omgjorder mig med kraft til krig, du bøier mine motstandere under mig.
Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
41 Og mine fiender lar du vende mig ryggen, mine avindsmenn utrydder jeg.
Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
42 De ser sig om, men der er ingen frelser - efter Herren, men han svarer dem ikke.
Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
43 Og jeg knuser dem som jordens støv; jeg sønderknuser dem, tramper dem ned som søle på gatene.
Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
44 Og du redder mig fra mitt folks kamper, du bevarer mig til å være hode for hedninger; folkeferd som jeg ikke kjenner, tjener mig.
“Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
45 Fremmede kryper for mig; bare de hører om mig, blir de mig lydige.
nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
46 Fremmede visner bort og går bevende ut av sine borger.
Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
47 Herren lever, og priset er min klippe, og ophøiet er min frelses klippefaste Gud,
“Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
48 den Gud som gir mig hevn og legger folkeferd under mig,
Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
49 og som fører mig ut fra mine fiender; over mine motstandere ophøier du mig, fra voldsmannen redder du mig.
aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
50 Derfor vil jeg prise dig, Herre, blandt hedningene og lovsynge ditt navn.
Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
51 Han gjør frelsen stor for sin konge, og han gjør miskunnhet mot sin salvede, mot David og mot hans ætt til evig tid.
Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”

< 2 Samuel 22 >