< 2 Kongebok 8 >
1 Elisa sa til den kvinne hvis sønn han hadde gjort levende: Gjør dig rede og dra bort med hele ditt hus og ophold dig på et eller annet fremmed sted! For Herren har kalt på hungersnøden, og den kommer også over landet og skal vare i syv år.
Basi, Elisha alikuwa amemwambia yule mwanamke ambaye alimfufulia mtoto wake. Akamwambia, “Inuka na uenede pamoja na nyumba yako, na uishi popote uwezapo katika nchi nyingine, kwa sababu Yahwe ameiita njaa ambayo itakuja katika hii nchi kwa miaka saba.”
2 Og kvinnen gjorde sig rede og gjorde efter den Guds manns ord; hun drog bort med hele sitt hus og opholdt sig som fremmed i filistrenes land i syv år.
Basi yule mwanamke akainuka na akatii lile neno la mtumishi wa Mungu. Akaenda na nyumba yake na kuishi kwenye nchi ya Wafilisti miaka saba.
3 Men da syv år var gått, vendte kvinnen tilbake fra filistrenes land; og hun gikk avsted for å be kongen om hans hjelp til å få igjen sitt hus og sin jord.
Ikafika kama mwishoni mwa miaka saba yule mwanamke akarudi kutoka kwenye ile nchi ya Wafilisti, na kwenda kwa mfalme kumuomba nyumba yake na kwa ajili ya nchi yake.
4 Kongen holdt da på å tale med Gehasi, den Guds manns dreng, og sa: Fortell mig om alle de store gjerninger Elisa har gjort!
Basi mfalme alikuwa anaongea na Gehazi yule mtumishi wa Mungu, akisema, “Tafadhali niambie yale mambo makubwa ambayo Elisha ameyafanya.”
5 Og just som han fortalte kongen at han hadde gjort den døde levende, kom den kvinne hvis sønn han hadde gjort levende, og bad kongen om hans hjelp til å få sitt hus og sin jord. Da sa Gehasi: Herre konge! Her er kvinnen, og her er hennes sønn som Elisa gjorde levende.
Basi alipokuwa akimwambia yule mfalme jinsi gani Elisha alivyomfufua yule mtoto aliyekufa, huyo mwanamke ambaye mtoto wake aliyekuwa amefufuliwa akaja kumuomba yule mfalme kwa ajili ya nyumba yake na nchi yake. Gehazi akasema, “Bwana wangu, mfalme, huyu ndiye yule mwanamke, na huyu ndiye mtoto wake, ambaye Elisha amemfufua.”
6 Så spurte kongen kvinnen, og hun fortalte ham det; og kongen lot henne få en av hoffolkene med sig og sa: Sørg for at hun får igjen alt det som hører henne til, og alt hvad hennes jord har kastet av sig fra den dag hun forlot landet, og til nu!
Wakati yule mfalme alipomuuliza yule mwanamke kuhusu mtoto wake, alimwelezea yule mfalme. Ndipo mfalme akamwagizia ofisa makini, akisema, “Mrudishie vyote vilivyokuwa vyake na mavuno yake yote ya kwenye mashamba tangu siku alipoondoka hadi sasa.”
7 Elisa kom til Damaskus mens kongen i Syria Benhadad lå syk. Da det blev fortalt kongen at den Guds mann var kommet dit,
Elisha akaja Damaskasi ambako Ben Hadadi yule mfalme wa Shamu alikuwa anaumwa. Yule mfalme aliambiwa, “Yule mtu wa Mungu amekuja hapa.”
8 sa han til Hasael: Ta en gave med dig og gå den Guds mann i møte og spør Herren gjennem ham om jeg skal komme mig av denne sykdom!
Mfalme akamwambia Hazaeli, “Chukua zawadi kwenye mkono wako na uende ukakutane na mtu wa Mungu, na ukazungumze na Yahwe kupitia yeye, ukisema, “Je nitapona huu ugonjwa wangu?”
9 Så drog Hasael ham i møte og tok en gave med sig av det beste som fantes i Damaskus, så meget som firti kameler kunde bære; og han kom og stod frem for ham og sa: Din sønn Benhadad, kongen i Syria, har sendt mig til dig og lar spørre: Skal jeg komme mig av denne sykdom?
Basi Hazaeli akaenda kuonana naye na kuchukua zawadi zake za kila kitu kizuri cha Damskasi, akabeba ngamia arobaini. Hivyo Hazaeli akaja na kusimama mbele ya Elisha na kusema, “Mtoto wako Ben Hadadi mfalme wa Shamu amenituma kwako, kusema, “Je nitapona huu ugonjwa?”
10 Elisa svarte: Gå du bare og si til ham: Du skal leve. Men Herren har latt mig se at han skal dø.
Elisha akamwambia, “Nenda, kwa Ben Hadadi, 'Utapona hakika,' lakini Yahwe amenionyesha kwamba atakufa hahkika.”
11 Og den Guds mann holdt sine øine festet på ham overmåte lenge og begynte å gråte.
Basi Elisha akamtumbulia macho Hazaeli hadi alipojisikia aibu, na yule mtu wa Mungu akalia machozi.
12 Da sa Hasael: Hvorfor gråter min herre? Han svarte: Fordi jeg vet at du skal gjøre Israels barn meget ondt; deres festninger skal du sette ild på, deres unge menn skal du drepe med sverdet, deres små barn skal du knuse, og deres fruktsommelige kvinner skal du opskjære.
Hazaeli akauliza, kwa nini unalia, bwana wangu?” Akajibu, “Kwa sababu najua uovu ambao utakaoufanya kwa watu wa Israeli. Utazichoma moto ngome zao kwa moto, na utawaua vijana wao kwa upanga, kuwaseta vipande vipande watoto wao wachanga, na kuwapasua mimba zao wanawake wenye mimba.”
13 Hasael sa: Hvad er din tjener, den hund, at han skulde gjøre så store ting? Elisa svarte: Herren har latt mig se dig som konge over Syria.
Hazaeli akajibu, Ni nani mtumwa wako, ambaye atafanya jambo hili kubwa? Yeye ni mbwa tu.” Elisha akajibu, “Yahwe amenionyesha kwamba utakuwa mfalme juu ya Shamu.”
14 Så forlot han Elisa og kom til sin herre; han spurte ham: Hvad sa Elisa til dig? Han svarte: Han sa til mig at du skal leve.
Ndipo Hazaeli akamwacha Elisha na kuja kwa bwana wake, ambaye alimwambia, “Je Elisha alikwambiaje?” Akajibu, “Ameniambia kwamba utapona bila shaka.”
15 Men dagen efter tok han et teppe og dyppet det i vann og bredte det over hans ansikt, og han døde; og Hasael blev konge i hans sted.
Basi siku ya pili yake Hazaeli akachukua blangeti na kulichovya kwenye maji, na kulitandaza kwenye uso wa Ben Hadadi hivyo akafa. Basi Hazaeli akawa mfalme katika sehemu sehemu yake.
16 I Israels konge Jorams, Akabs sønns femte år, mens Josafat ennu var konge i Juda, blev Joram, Josafats sønn, konge i Juda.
Katika mwaka wa kumi na tano wa Yoramu mwana wa Ahabu, mfalme wa Israeli, Yehoramu akaanza kutawala. Alikuwa mwana wa Yehoshafati mfalme wa Yuda. Alianza wakati Yehoshafati alikuwa mfalme wa Yuda.
17 Han var to og tretti år gammel da han blev konge, og regjerte åtte år i Jerusalem.
Yoramu alikuwa na umri wa miaka thelathini na mbili alipoanza kutawala, na alitawala kwa mda wa miaka minane katika Yerusalemu.
18 Han vandret på Israels kongers vei, likesom Akabs hus hadde gjort, for han hadde en datter av Akab til hustru, og han gjorde hvad ondt var i Herrens øine.
Yoramu akatembea kwenye njia ya huyo mfalme wa Israeli, kama walivyokuwa wakifanya kwenye nyumba ya Ahabu; kwa kuwa alikuwa na binti wa Ahabu kama mke wake, na alifanya uovu usoni kwa Yahwe.
19 Men Herren vilde ikke ødelegge Juda for sin tjener Davids skyld, fordi han hadde lovt ham at han vilde la en lampe brenne for ham og hans sønner gjennem alle tider.
Walakini, kwa sababu ya mtumishi wake Daudi, Yahwe hakutaka kuiharibu Yuda, tangu alipomwambia kwamba atampatia wazao.
20 I hans dager falt Edom fra Juda og tok sig en konge.
Katika siku za Yoramu, Edomu akaasi kutoka chini ya mkono wa Yuda, na wakamfanya mfalme juu yao wenyewe.
21 Da drog Joram over til Sa'ir med alle sine stridsvogner; han brøt op om natten og slo edomittene, som hadde omringet ham, og høvedsmennene over deres vogner; men folket flyktet til sine hjem.
Basi Yehoramu akaenda na maamri jeshi na magari ya farasi yote. Ilitokea kwamba akaamka usiku na kushambulia na kuwazunguka Waedomu, waliokuwa wamemzunguka na wale maamri jeshi wa magari ya farasi. Ndipo wanajeshi wa Yehoramu wakakimbilia wajumbani kwao.
22 Således falt Edom fra Juda og har vært skilt fra dem til den dag idag; på samme tid falt også Libna fra.
Hivyo Edomu aliasi dhidi ya utawala wa Yuda katika siku hizi. Libna pia aliasi katika kipindi hicho hicho.
23 Hvad som ellers er å fortelle om Joram og om alt det han gjorde, er opskrevet i Judas kongers krønike.
Kwa mambo mengine yamhusuyo Yehoramu, yote aliyoyafanya, je hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya mfalme wa Yuda?
24 Og Joram la sig til hvile hos sine fedre og blev begravet hos sine fedre i Davids stad; og hans sønn Akasja blev konge i hans sted.
Yehoramu akafa na kuzikwa pamoja na baba zake, na akalala pamoja na baba zake katika mji wa Daudi. Ndipo Ahazi mtoto wake akawa mfalme katika sehemu yake.
25 I Israels konge Jorams, Akabs sønns tolvte år, blev Akasja, Jorams sønn, konge i Juda.
Katika mwaka wa kumi na mbili wa Yohoramu mwana wa Ahabu, mfalme wa Israeli, Ahazi mwana wa Yehoramu, mfalme wa Yuda, alianza kutawala.
26 Akasja var to og tyve år gammel da han blev konge, og regjerte ett år i Jerusalem; hans mor hette Atalja og var en datter av Israels konge Omri.
Ahazi alikuwa ana umri wa miaka ishirini na mbili wakati alipoanza kutawala; alitawala kwa mda wa mwaka mmoja katika Yerusalemu. Mama yake alikuwa anaitwa Athalia; alikuwa mtoto wa Omri, mfalme wa Israeli.
27 Han vandret på samme vei som Akabs hus og gjorde hvad ondt var i Herrens øine, likesom Akabs hus; for han var en slektning av Akabs hus.
Ahazia alitembelea katika nyumba ya Ahabu; alifanya yale yaliyo maovu katika uso wa Yahwe, kama nyumba ya Ahabu ilivyokuwa ikifanya, kwa kuwa Ahazia alikuwa mkwe kwenye nyumba ya Aabu.
28 Sammen med Joram, Akabs sønn, drog han ut i krig mot Hasael, kongen i Syria, og stred mot ham ved Ramot i Gilead. Men syrerne såret Joram.
Ahazia akaenda pamoja na Yoramu mwana wa Ahabu, kupigana dhidi ya Hazaeli, mfalme wa Shamu, katika Ramath Geleadi. Washami wakamjeruhi Yoramu.
29 Da vendte kong Joram tilbake for å la sig læge i Jisre'el for de sår syrerne hadde slått ham ved Rama da han stred mot Syrias konge Hasael; og Judas konge Akasja, Jorams sønn, drog ned til Jisre'el for å se til Joram, Akabs sønn, fordi han var syk.
Mfalme Yoramu akarudi ili auguzwe huko Yezreeli kwenye yale majeraha ambayo Washami walimpatia huko Rama. Wakati alipopigana dhidi ya Hazaeli mfalme wa Shamu. Hivyo Ahazi mwana wa Yehoramu, mfalme Yuda, akashuka kwa Yezreeli kumuona Yoramu mwana wa Ahabu, kwa sababu Yoramu alikuwa amejeruhiwa.