< Ugubukulo 19 >
1 Pagamaliki genago nayuwini lwami luvaha lwa msambi uvaha wa vandu kunani kwa Chapanga yijova, “Chapanga alumbiwa! Usangula, na ukulu na makakala ndi vindu vyaku!
Baada ya haya nikasikia sauti kama ya umati mkubwa mbinguni wakipiga kelele wakisema: “Haleluya! Wokovu na utukufu na uweza ni vya Mungu wetu,
2 Uhamula waki ndi wa chakaka na yabwina palongolo ya Chapanga. Umhamwili yula mweimanyikana neju mkemi mweawuyagisi mulima kwa ukemi waki. Chapanga avalipisi gevahengili ndava ya kuvakoma vanalihengu vaki.”
kwa maana hukumu zake ni za kweli na za haki. Amemhukumu yule kahaba mkuu aliyeuharibu ulimwengu kwa uzinzi wake. Mungu amemlipiza kisasi kwa ajili ya damu ya watumishi wake.”
3 Vakajova kavili, “Chapanga alumbiwa! Lyohi la motu weutinyisa muji wenuwo likwela mbaka kunani magono goha gangali mwishu!” (aiōn )
Wakasema tena kwa nguvu: “Haleluya! Moshi wake huyo kahaba unapanda juu milele na milele.” (aiōn )
4 Vagogo vala ishilini na mcheche, na vala viumbi wumi mcheche, vakajigwisa chakukupama pahi, vakamgundamila Chapanga mweatamili panani pachigoda cha unkosi vakajova. “Ena! Chapanga alumbiwa!”
Wale wazee ishirini na wanne pamoja na wale viumbe wanne wenye uhai wakaanguka kifudifudi, wakamwabudu Mungu, aliyekuwa ameketi kwenye kile kiti cha enzi. Wakasema kwa sauti kuu: “Amen, Haleluya!”
5 Kangi, lukahumila lwami muchigoda cha unkosi, “Mumlumbayi Chapanga witu, nyenye mwavatumisi vaki voha, mwavoha mwemukumtopesa, vadebe kwa vavaha.”
Kisha sauti ikatoka katika kile kiti cha enzi, ikisema: “Msifuni Mungu wetu, ninyi watumishi wake wote, ninyi nyote mnaomcha, wadogo kwa wakubwa!”
6 Kangi nayuwini lwami, ngati lwami lwa msambi uvaha wa vandu, ngati lwami lwa manji gamahele pegihelela kwa mbulumo uvaha wa mbamba lukajova, “Chapanga alumbiwa! Muni Bambu witu mweavi na uhotola woha ndi Nkosi!
Kisha nikasikia sauti kama ya umati mkubwa, kama sauti ya maji mengi yaendayo kasi na kama ngurumo kubwa ya radi wakipiga kelele wakisema: “Haleluya! Kwa maana Bwana Mungu wetu Mwenyezi anatawala.
7 Tihekelela na kululuta, timulumba Chapanga cheavi mkulu, muni lukumbi lwa ndowa ya Mwanalimbelele luhikili na mdala kamwali ajitendekili.
Tufurahi, tushangilie na kumpa utukufu! Kwa maana arusi ya Mwana-Kondoo imewadia na bibi arusi wake amejiweka tayari.
8 Kamwali yula ayidakiliwi kujiwalika nyula zezing'asima neju. Nyula yeniyo yeying'asima!” Ndi matendu gabwina ga vandu va Chapanga.
Akapewa kitani safi, nyeupe inayongʼaa, ili avae.” (Hiyo kitani safi inawakilisha matendo ya haki ya watakatifu.)
9 Kangi mtumu wa kunani kwa Chapanga anijovili, “Yandika aga: Vamotisiwayi vala vevagongoliwi pamselubuko wa chakulya cha ndowa ya Mwanalimbelele!” Kangi akanijovela, “Genaga ndi malovi gachakaka ga Chapanga.”
Ndipo malaika akaniambia, “Andika: ‘Wamebarikiwa wale walioalikwa kwenye karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo!’” Naye akaongeza kusema, “Haya ndiyo maneno ya kweli ya Mungu.”
10 Hinu, nene nikagwa chakukupama palongolo ya magendelelu gaki, naganili kumuyupa. Nambu mwene akanijovela, “Ukoto kukita genago! Nene namtumisi muyaku pamonga na valongo vaku vevakuukamulila uchakaka ndi Yesu mweaugubukwili umanyikanayi kwitu. Uchakaka wenuwo wihuma kwa Mpungu Msopi mweakuvatangatila vandu vaujovayi ujumbi wa Chapanga.”
Ndipo nikaanguka kifudifudi miguuni pake ili kumwabudu, lakini yeye akaniambia, “Usifanye hivyo! Mimi pia ni mtumishi mwenzako pamoja na ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu. Mwabudu Mungu! Maana ushuhuda wa Yesu ndio roho ya unabii.”
11 Kangi nawene kunani kwa Chapanga kudinduka na kwenuko nayiwene falasi ya msopi. Mweatamili panani ya falasi mwenuyo akemiwi msadikika na wa chakaka. Kangi ihamula vandu na munjila ya bwina na kutovana ngondo yambwina palongolo ya Bambu.
Kisha nikaona mbingu imefunguka na hapo mbele yangu akiwepo farasi mweupe, ambaye yeye aliyempanda aliitwa Mwaminifu na Kweli. Yeye huhukumu kwa haki na kufanya vita.
12 Mihu gaki gavi ngati mwali wa motu, na panani ya mutu awalili njingwa zamahele. Avi na liina leliyandikwi, kawaka mundu yoyoha mwealimanyili nambu ngamwene.
Macho yake ni kama miali ya moto na juu ya kichwa chake kuna taji nyingi. Ana jina lililoandikwa ambalo hakuna mtu yeyote anayelijua isipokuwa yeye mwenyewe.
13 Awalili nyula yeyijwigiwi mu ngasi. Na liina laki mwenuyo ndi, “Lilovi la Chapanga.”
Amevaa joho lililochoviwa katika damu, na Jina lake ni “Neno la Mungu.”
14 Manjolinjoli ga kunani kwa Chapanga vamlandili kuni gatamili panani ya falasi wamsopi na gawalili nyula zezing'asima neju.
Majeshi ya mbinguni walikuwa wakimfuata, wakiwa wamepanda farasi weupe, hali wamevaa mavazi ya kitani safi, nyeupe na nzuri.
15 Mumlomo waki upanga ukali wihuma wa kuvahotola milima. Mwene yati ilongosa vandu kwa ndonga ya lyuma. Na kuvaminya ngati mundu mweimanya divayi muchiliva cha kuminyila divayi ya ligoga likulu la Chapanga mweavi na makakala.
Kinywani mwake hutoka upanga mkali ambao kwa huo atayaangusha mataifa. “Atayatawala kwa fimbo yake ya utawala ya chuma.” Hulikanyaga shinikizo la mvinyo wa ghadhabu ya Mungu Mwenyezi.
16 Panani ya nyula yaki, na panani ya liwondo laki, ayandikwi liina, “Nkosi wa vankosi na Bambu wa vabambu.”
Kwenye joho lake na paja lake pameandikwa jina hili: Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana.
17 Kangi, namuwene mtumu wa kunani kwa Chapanga mmonga ayimili palilanga. Akavajovela kwa lwami luvaha videge vyoha vevimbululuka kunani, “Mubwela, mukonganeku pamonga pachakulya chikulu cha Chapanga!
Nami nikamwona malaika amesimama ndani kwenye jua, akaita ndege wote warukao angani kwa sauti kuu, “Njooni, kusanyikeni kwa ajili ya karamu kubwa ya Mungu,
18 Mbwela mlyayi higa ya vankosi, na nyama ya vakulu va manjolinjoli, na nyama ya vandu vakekesi, na nyama ya falasi na vevitama panani ya falasi wavi, na nyama ya vandu voha vevalekekiswi na vavanda, vadebe na vavaha.”
ili mpate kula nyama ya wafalme na ya majemadari, ya mashujaa, ya farasi na ya wapanda farasi, nyama ya wanadamu, wote walio huru na watumwa, wadogo na wakubwa.”
19 Kangi nachiwene chila chinyama pamonga na vankosi va mulima na manjolinjoli wavi vakokini pamonga muni vatovana na yula mweatamili panani ya falasi wa msopi na pamonga na msambi waki.
Kisha nikamwona yule mnyama na wafalme wa dunia pamoja na majeshi yao wakiwa wamekusanyika pamoja ili kufanya vita dhidi ya yule aliyempanda farasi pamoja na jeshi lake.
20 Nambu chinyama chila chakamuliwi kwa makakala pamonga na yula mlota wa Chapanga wa udese mweikita ganchinamtiti palongolo yaki. Kwa gachinamtiti yeniyo avayagisi vala vevavi na ulangisu wa chinyama chila na vevagundamili chimong'omong'o chila. Chinyama chenicho pamonga na mlota wa udese vakatagwa kuni vavili mumi munyanja ya motu weumemili maganga ga baluti gegiyaka motu. (Limnē Pyr )
Lakini yule mnyama akakamatwa pamoja na huyo nabii wa uongo ambaye alikuwa amefanya ishara kwa niaba ya huyo mnyama, ambaye kwa ishara hizi aliwadanganya wale waliopokea chapa ya huyo mnyama na kuiabudu sanamu yake. Hawa wawili wakatupwa wakiwa hai ndani ya ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti. (Limnē Pyr )
21 Na vala vevasigalili vakomiwi kwa upanga wewahumili mumlomo wa yula mweakweli panani ya yula falasi wamsopi. Na videge vyoha vakayukutiswa kwa kulya nyama za vala vevakomiwi.
Wale waliosalia waliuawa kwa upanga uliotoka kinywani mwa yule aliyekuwa amempanda farasi nao ndege wote wakajishibisha kwa nyama yao.