< Matei 4 >
1 Kangi Mpungu Msopi wamlongwisi Yesu mbaka kulugangatu muni alingiwa na Setani.
Kisha Yesu akaongozwa na Roho Mtakatifu kwenda nyikani ili akajaribiwe na ibilisi.
2 Ajihinisi chakulya lukumbi lwa magono alobaini kilu na muhi pamwishu njala yamvinili.
Baada ya kufunga siku arobaini usiku na mchana, hatimaye akaona njaa.
3 Hinu Setani akabwela na kumjovela, “Ngati veve wa Mwana wa Chapanga amula aga maganga gavyai libumunda.”
Mjaribu akamjia na kumwambia, “Ikiwa wewe ndiye Mwana wa Mungu, amuru mawe haya yawe mikate.”
4 Nambu Yesu akayangula, “Yiyandikwi mu Mayandiku Gamsopi, ‘Mundu itama lepi ndava ya libumunda lene, nambu kwa kulanda kila lilovi leijova Chapanga.’”
Lakini Yesu akajibu, “Imeandikwa: ‘Mtu haishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.’”
5 Kangi Setani akamtola Yesu mbaka Yelusalemu weuvi muji wa msopi, akamkita ayima panani pa chituvilu cha Nyumba ya Chapanga,
Ndipo ibilisi akamchukua Yesu mpaka mji mtakatifu na kumweka juu ya mnara mrefu wa Hekalu,
6 akamjovela, “Ngati veve mwana wa Chapanga ujitagayi pahi, ndava vayandiki, ‘Chapanga akuvalagazila vamitumu va kunani kwa Chapanga ndava yaku, Yati vakukuyanga mu mawoko gavi, ukotoka kujikuvala chigendelu chaku paliganga.’”
akamwambia, “Kama wewe ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini. Kwa kuwa imeandikwa: “‘Atakuagizia malaika zake, nao watakuchukua mikononi mwao ili usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.’”
7 Yesu akamyangula, mewawa “Mayandiku Gamsopi gijova, ‘Kotoka kumlinga Bambu Chapanga waku.’”
Yesu akamjibu, “Pia imeandikwa: ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’”
8 Kangi Setani akamtola na kuhamba nayu panani pachitumbi chitali, na kumlangisa unkosi woha wa pamulima na ukulu waki,
Kwa mara nyingine, ibilisi akamchukua Yesu mpaka kwenye kilele cha mlima mrefu na kumwonyesha falme zote za dunia na fahari zake,
9 akamjovela, “Goha aga yati nikupela, ngati ukunigundamila na kunifugamila.”
kisha akamwambia, “Nitakupa hivi vyote kama ukinisujudia na kuniabudu.”
10 Penapo, Yesu akayangula, “Wuka Setani! Vayandiki, mu Mayandiku Gamsopi yati ‘Umgundamila Bambu Chapanga waku, na kumhengela mwene ndu!’”
Yesu akamwambia, “Ondoka mbele yangu, Shetani! Kwa maana imeandikwa, ‘Mwabudu Bwana Mungu wako, na umtumikie yeye peke yake.’”
11 Hinu Setani, akamleka Yesu na vamitumu va kunani kwa Chapanga vakabwela vakamhengela.
Ndipo ibilisi akamwacha, nao malaika wakaja na kumhudumia.
12 Yesu peayuwini kuvya Yohani vamkungili muchifungu akahamba ku Galilaya.
Yesu aliposikia kwamba Yohana Mbatizaji alikuwa ametiwa gerezani, alirudi Galilaya.
13 Akawuka ku Nazaleti akahamba ku Kapelanaumu, muji wa kumwambu ya nyanja Galilaya mumilima ya Zebuloni na Nafutali, akatama kwenuko.
Akaondoka Nazareti akaenda kuishi Kapernaumu, mji ulioko karibu na bahari, katika mipaka ya nchi ya Zabuloni na Naftali,
14 Ndi gatimili gala geajovili Isaya, mweavi mlota wa Chapanga,
ili kutimiza unabii wa nabii Isaya, kama alivyosema:
15 “Mulima wa Zebuloni na mulima wa Nafutali, njila ya kuhamba kunyanja mwambu ya mumfuleni Yoludani, Galilaya muji wa vandu vangali Vayawudi!
“Nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, kwenye njia ya kuelekea baharini, ngʼambo ya Yordani, Galilaya ya watu wa Mataifa:
16 Vandu vevatami kuchitita. Vauweni lumuli luvaha. Vene vitama mumuji wa chitita na chimuwili cha lifwa, lumuli luvalangasili.”
watu wale waliokaa gizani wameona nuru kuu; nao wale walioishi katika nchi ya uvuli wa mauti, nuru imewazukia.”
17 Kuhumila lukumbi lwenulo Yesu atumbwili kukokosa, “Mumuwuyila Chapanga, muni Unkosi wa kunani kwa Chapanga uvi papipi!”
Tangu wakati huo, Yesu alianza kuhubiri akisema: “Tubuni, kwa maana Ufalme wa Mbinguni umekaribia.”
18 Yesu peagendayi mumhana wa nyanja Galilaya, avaweni valongo vavili vevilova somba Simoni, mweikemiwa Petili na Andelea mlongo waki, valova somba na ngwanda munyanja ndava vavi valova.
Yesu alipokuwa anatembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona ndugu wawili, Simoni aitwaye Petro, na Andrea ndugu yake. Walikuwa wakizitupa nyavu zao baharini kwa kuwa wao walikuwa wavuvi.
19 Yesu akavajovela, ngati chamwilova somba, “Munilandayi, nene yati nikuvakita nyenye kuvya vakuvaleta vandu kwa Bambu.”
Yesu akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”
20 Bahapo vazilekili ngwanda zavi, vakamlanda.
Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
21 Peahegalili kulongolo, avaweni valongo vangi vavili, Yakobo na Yohani, vana va Zebedayo. Vene vavi mugati ya watu pamonga na dadi wavi Zebedayo, vatengenezayi ngwanda za kulovela somba. Yesu akavakemela,
Alipoendelea mbele kutoka pale, akawaona ndugu wengine wawili, Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, wakiwa wamekaa kwenye mashua pamoja na baba yao Zebedayo, wakizitengeneza nyavu zao. Yesu akawaita.
22 navene kanyata vakauleka watu pamonga na dadi wavi, vakamlanda Yesu.
Nao mara wakaiacha mashua yao, pamoja na baba yao, wakamfuata.
23 Yesu ahambili kila pandu ku Galilaya, iwula munyumba za kukonganekela Vayawudi na kuvakokosela Lilovi la Bwina la Unkosi wa Chapanga. Akavalamisa matamu ndalindali gevavi nagu vandu.
Yesu akapita katika Galilaya yote, akifundisha katika masinagogi yao, akihubiri habari njema za Ufalme, na akiponya kila ugonjwa na kila aina ya maradhi miongoni mwa watu.
24 Malovi gaki gadandasiki pandi zoha za ku Silia. Vandu voha vevavi na matamu na mang'ahiso, mewa vevatalaliwi na mizuka na vevihinduka na vevagogodili higa vavapeliki kwaki na mwene akavalamisa.
Kwa hiyo sifa zake zikaenea sehemu zote za Shamu, nao watu wakamletea wote waliokuwa na magonjwa mbalimbali na maumivu, waliopagawa na pepo wachafu, wenye kifafa na waliopooza, naye akawaponya.
25 Msambi wa vandu kuhuma ku Galilaya na Dekapoli ndi miji kumi, mewa Yelusalemu na Yudea na kumwambu ya mfuleni Yoludani vakamlanda.
Makutano makubwa ya watu yakawa yanamjia kutoka Galilaya, Dekapoli, Yerusalemu, Uyahudi na kutoka ngʼambo ya Mto Yordani.