< Matei 25 >

1 Kangi lukumbi lwenulo, Unkosi wa kunani kwa Chapanga uwanangana na vakamwali kumi vevagegili hahi zavi, vevahambili kumlindila mkolo ndowa.
“Wakati huo, Ufalme wa Mbinguni utakuwa kama wanawali kumi waliochukua taa zao na kwenda kumlaki bwana arusi.
2 Mhanu pagati yavi vavi vayimu na mhanu vangi vavi na luhala.
Watano wao walikuwa wapumbavu na watano walikuwa wenye busara.
3 Vala vayimu vagegii hahi zavi, nambu vagegili lepi mahuta gangi gachibana.
Wale wapumbavu walichukua taa zao lakini hawakuchukua mafuta ya akiba,
4 Nambu vevavi na luhala vala vagegili mahuta muchupa na mu hahi zavi.
lakini wale wenye busara walichukua taa zao na mafuta ya akiba kwenye vyombo.
5 Ndava muni mkolo ndowa acheliwi kubwela, ndi vasikana vala vatumbwili kutitila na vakagona.
Bwana arusi alipokawia kuja wale wanawali wote wakasinzia na kulala.
6 “Pagati ya kilu lwami luvaha lwayuwaniki, ‘Yumuka, mkolo ndowa ibwela mhamba mukampokela!’
“Usiku wa manane pakawa na kelele: ‘Tazameni, huyu hapa bwana arusi! Tokeni nje mkamlaki!’
7 Kangi vakamwali vala voha vakayumuka, na kutendelekela hahi zavi.
“Ndipo wale wanawali wote wakaamka na kuzitengeneza taa zao.
8 Vayimu vala vakavajovela vayavi vevavi na luhala, mutitangatila mahuta ginu padebe, ndava muni hahi zitu zijimika.
Wale wapumbavu wakawaambia wale wenye busara, ‘Tupatieni mafuta yenu kidogo; taa zetu zinazimika.’
9 Nambu vevavi na luhala vala vakavayangula, lepi, ‘Gikola lepi, nyenye na tete.’ ‘Mbanga mhamba kuliduka mukajigulila mwavene.’
“Lakini wale wenye busara wakawajibu, ‘Sivyo, hayatutoshi sisi na ninyi pia. Afadhali mwende kwa wauzao mkajinunulie mafuta yenu.’
10 Hinu, vakamwali vayimu vala, pevahambili kugula mahuta, mkolo ndowa ndi abwelili, vevajitendelekili vala vayingili munyumba ya ndowa pamonga nayu, kangi mlyangu wadindiwi.”
“Nao walipokuwa wakienda kununua mafuta, bwana arusi akafika. Wale wanawali waliokuwa tayari wakaingia ndani pamoja naye kwenye karamu ya arusi na mlango ukafungwa.
11 Mwanakandahi vakawuya vakamwali vangi vala, vakakemela “Mkulu, ‘Mkulu, tidindulila!’
“Baadaye wale wanawali wengine nao wakaja, wakaita, ‘Bwana! Bwana! Tufungulie mlango!’
12 Nambu mkulu yula akavayangula, ‘Nikuvajovela chakaka, nakuvamanya nyenye.’”
“Lakini yeye bwana arusi akawajibu, ‘Amin, amin nawaambia, siwajui ninyi!’
13 Kangi Yesu akavajovela, “Mujiyangalila! Ndava mwimanya lepi ligono amala lisaa yeibwela Mwana wa Mundu.”
“Kwa hiyo kesheni, kwa sababu hamjui siku wala saa.
14 “Kangi Unkosi wa kunani kwa Chapanga uwanangana ngati mundu mmonga mweaganili kuhamba lugendu lwa kutali, avakemili vatumisi vaki na kuvagotolela vindu vyaki.
“Tena, Ufalme wa Mbinguni ni kama mtu aliyetaka kusafiri, naye akawaita watumishi wake na kuweka mali yake kwenye uangalizi wao.
15 Akavapela kila mundu ngati cheavi na uhotola waki, mmonga mahaku mhanu ga mashonga na yungi mahaku gavili ga mashonga na yungi talanta yimonga ya mashonga akahamba.
Mmoja akampa talantatano, mwingine talanta mbili, na mwingine talanta moja. Kila mmoja alipewa kwa kadiri ya uwezo wake. Kisha yeye akasafiri.
16 Yula mweagotoliwi talanta mhanu za mashonga, bahapo akazihengela lihengu na, kuziyonjokesa mahaku gangi mhanu.
Yule aliyepewa talanta tano akaenda mara moja akafanya nazo biashara akapata talanta nyingine tano zaidi.
17 Mewawa yungi mweagotoliwi mahaku gavili ga mashonga, akayonjokesa mahaku gangi gavili.
Yule aliyepewa talanta mbili akafanya vivyo hivyo, akapata nyingine mbili zaidi.
18 Nambu mtumisi mweagotoliwi talanta yimonga ya lishonga akahamba kugimila pahi, kuyifiya mashonga ga mkulu waki.”
Lakini yule mtumishi aliyekuwa amepokea talanta moja, alikwenda akachimba shimo ardhini na kuificha ile fedha ya bwana wake.
19 “Pagamaliki magono gamahele, mkulu yula awuyili na kutumbula kuvalanga vindu mashonga gaki pamonga nawu.
“Baada ya muda mrefu, yule bwana wa wale watumishi akarudi na kufanya hesabu nao.
20 Yula mtumisi mweagotoliwi mahaku mhanu ga mashonga abwelili kuni agegili mahaku ga mashonga gangi mhanu, ndi akamjovela, ‘Mkulu, wanipeli talanta mashonga mhanu, hinu niyonjokisi talanta zingi mhanu zeniyonjokisi.’
Yule mtumishi aliyepokea talanta tano akaja, akaleta nyingine tano zaidi. Akasema, ‘Bwana uliweka kwenye uangalizi wangu talanta tano. Tazama, nimepata faida ya talanta tano zaidi.’
21 Mkulu waki, akamjovela ‘Uhengili chabwina, mtumisi msadikika na mbwina.’ Usadikiwi mu mambu gadebe yati nikugotolela mambu gavaha. Bwelayi uhekayi pamonga na mkulu waku!”
“Bwana wake akamwambia, ‘Umefanya vizuri sana, mtumishi mwema na mwaminifu! Umekuwa mwaminifu kwa vitu vichache; nami nitakuweka kuwa msimamizi wa vitu vingi. Njoo ushiriki katika furaha ya bwana wako!’
22 “Kangi mtumisi yungi mweagotoliwi mahaku gavili ga mashonga, abwelili, na kujova, ‘Mkulu wanigotolili mahaku gavili ga mashonga, lola aga apa mahaku gangi gavili geayonjokisi.’
“Yule mwenye talanta mbili naye akaja. Akasema, ‘Bwana, uliweka kwenye uangalizi wangu talanta mbili. Tazama nimepata hapa talanta mbili zaidi.’
23 ‘Mkulu waki akamjovela, chabwina, veve mtumisi msadikika na mbwina!’ ‘Ukitili chabwina mu mambu gadebe, yati nikugotolela mambu gavaha, bwelayi uhekayi pamonga na nene.’”
“Bwana wake akajibu, ‘Umefanya vizuri sana, mtumishi mwema na mwaminifu. Umekuwa mwaminifu kwa vitu vichache; nami nitakuweka kuwa msimamizi wa vitu vingi. Njoo ushiriki katika furaha ya bwana wako!’
24 “Nambu yula mweagotoliwi talanta yimonga ya lishonga, abwelili akajova, ‘Mkulu nikumanyili veve wa mundu munonopo wibena pewangalima, na kutola pewangadandasa mbeyu.
“Kisha yule mtumishi aliyepokea talanta moja akaja, akasema, ‘Bwana, nilijua kwamba wewe ni mtu mgumu, unayevuna mahali usipopanda na kukusanya mahali usipotawanya mbegu.
25 Ndi nayogwipi, nagimili pandima na kufiya lishonga laku. Hinu ndi utola yaku.’”
Kwa hiyo niliogopa, nikaenda, nikaificha talanta yako ardhini. Tazama, hii hapa ile iliyo mali yako.’
26 “‘Mkulu waki akamyangula veve mtumisi mhakau na mkata! Wimanya kuvya nene nibena panangagaba, na kuyola pala panangadandasa?’
“Bwana wake akajibu, ‘Wewe mtumishi mwovu na mvivu! Ulijua kwamba ninavuna mahali nisipopanda na kukusanya mahali nisipotawanya mbegu.
27 Ndi yakuganili uvika mashonga gangu kwa vandu vevibadilisha na kuwusa mashonga, ndi nene nganitoli chiyonjokesu na mashonga gangu!
Vyema basi, ingekupasa kuweka fedha yangu kwa watoa riba, ili nirudipo, nichukue ile iliyo yangu na faida yake.
28 Hinu mumnyaga mashonga genago, na mumpelayi yula mweavi na talanta kumi za mashonga.
“‘Basi mnyangʼanyeni hiyo talanta, mkampe yule mwenye talanta kumi.
29 Ndava, mundu yeyoha mweavi na chindu yati ipewa na kuyonjokesewa. Nambu yula angali chindu, hati chidebe cheavili nachu yati inyagiwa.
Kwa maana kila mtu aliye na kitu atapewa zaidi, naye atakuwa navyo tele. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyangʼanywa.
30 Na mtumisi yula angali chiyonjokesu, mtaga kuvala kuchitita kwenuko ndi yati kuvya na luvembu na kuyaga minu.”
Nanyi mtupeni huyo mtumishi asiyefaa nje, kwenye giza, mahali ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.’
31 “Lukumbi Mwana wa Mundu peibwela muukulu waki pamonga na vamitumu vaki va kunani kwa Chapanga, penapo yati itama panani ya chigoda cha unkosi chechivii na ukulu.
“Mwana wa Adamu atakapokuja katika utukufu wake na malaika wote watakatifu pamoja naye, ndipo atakapoketi juu ya kiti cha enzi cha utukufu wake.
32 Vandu va milima yoha yati vikonganeka pamonga palongolo yaki. Mwene ndi akuvapangula vandu ngati mdimaji cheipangula mambelele na mene.
Mataifa yote watakusanyika mbele zake, naye atawatenga kama mchungaji anavyotenga kondoo na mbuzi.
33 Mwene yati ivika mambelele ndi vandu vabwina palongolo ya Chapanga muchiwoko chaki cha kulyela na mene ndi vandu vahakau muchiwoko chaki cha kumangeya.”
Atawaweka kondoo upande wake wa kuume, na mbuzi upande wake wa kushoto.
34 Kangi Nkosi akuvajovela vala vevavi upandi waki wa kulyela, mbwela, nyenye mwemumotisiwi na Dadi wangu! Mupokela unkosi wemuvikiwi kutumbula kuwumbwa kwa mulima.
“Ndipo Mfalme atawaambia wale walioko upande wake wa kuume, ‘Njooni, ninyi mliobarikiwa na Baba yangu; urithini Ufalme ulioandaliwa kwa ajili yenu tangu kuumbwa kwa ulimwengu.
35 Muni penavi na njala mwanipeli chakulya, navi na njota mwanipeli manji, avi myehe mwanipokili panyumba yinu,
Kwa maana nilikuwa na njaa mkanipa chakula, nilikuwa na kiu mkaninywesha, nilikuwa mgeni mkanikaribisha,
36 navi nangayatila mwaniwaliki, navi mtamu mwabweli kunilola, navi muchifungu mwanigendelili kunilola.
nilikuwa uchi mkanivika, nilikuwa mgonjwa mkanitunza, nami nilikuwa kifungoni mkaja kunitembelea.’
37 “Penapo vandu vabwina palongolo ya Chapanga yati vakamyangula ‘Bambu, takuwene ndali njala yikuvina petakupeli chakulya, amala uvi na njota tete takupeli manji?
“Ndipo wale wenye haki watakapomjibu, ‘Bwana, ni lini tulikuona ukiwa na njaa tukakulisha, au ukiwa na kiu tukakunywesha?
38 Ndali takuwene wa myehe ndi tete takupokili, amala wavi changayatila takuwaliki?
Lini tulikuona ukiwa mgeni tukakukaribisha, au ukiwa uchi tukakuvika?
39 Ndali patakuwene una utamu amala muchifungu tabweli kukulola?’
Tena ni lini tulikuona ukiwa mgonjwa tukakutunza, au ukiwa kifungoni tukakutembelea?’
40 Nkosi yati akuvayangula, ‘Nikuvajovela chakaka, chindu chochoha chamumhengili mmonga wa valongo vangu vadebe ava, mwanihengili nene.’”
“Naye Mfalme atawajibu, ‘Amin nawaambia, kwa jinsi mlivyomtendea mmojawapo wa hawa ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi.’
41 “Kangi yati akuvajovela vala va upandi wa kumangeya, ‘Muwuka, palongolo yangu nyenye mwempewili likoto mhamba kumotu wangajimika wa magono goha gangali mwishu weutendelekiwi kwa Setani na vamitumu vaki. (aiōnios g166)
“Kisha atawaambia wale walio upande wake wa kushoto, ‘Ondokeni kwangu, ninyi mliolaaniwa, nendeni kwenye moto wa milele ulioandaliwa kwa ajili ya ibilisi na malaika zake. (aiōnios g166)
42 Ndava njala peyanivili nyenye mwanipeli lepi chakulya, penavi na njota nyenye mwanipeli lepi manji.
Kwa maana nilikuwa na njaa hamkunipa chakula, nilikuwa na kiu hamkuninywesha,
43 Penavi myehe nyenye mwenipokili lepi, penavi changayatila nyenye mwaniwaliki lepi, penavi mtamu na penavi muchifungu nyenye mwabweli lepi kunilola.’”
nilikuwa mgeni nanyi hamkunikaribisha, nilikuwa uchi hamkunivika, nilikuwa mgonjwa hamkunitunza, na nilikuwa gerezani nanyi hamkuja kunitembelea.’
44 “Penapo yati viyangula, ‘Bambu, ndali petakuwene njala yikuvina, amala uvi na njota amala myehe amala changayatila nyula amala mtamu amala muchifungu tete takuhengili lepi?’
“Ndipo wao pia watajibu, ‘Bwana ni lini tulikuona ukiwa na njaa au kiu, au ukiwa mgeni au uchi, au ukiwa mgonjwa na kifungoni na hatukukuhudumia?’
45 Bambu yati iyangula, ‘Nikuvajovela chakaka, chindu chochoha chamwabeli kumuhengela, mmonga wa vadebe ava, ndi mwabeli kunihengela nene.’
“Naye atawajibu, ‘Amin nawaambia, kwa jinsi ambavyo hamkumtendea mmojawapo wa hawa ndugu zangu walio wadogo, hamkunitendea mimi.’
46 Hinu, venava yati vihamba kumbunu wa magono goha, nambu vala vandu vabwina palongolo ya Chapanga yati vihamba kuwumi wa magono goha gangali mwishu.” (aiōnios g166)
“Ndipo hawa watakapoingia kwenye adhabu ya milele, lakini wale wenye haki wataingia katika uzima wa milele.” (aiōnios g166)

< Matei 25 >