< Matei 15 >
1 Vafalisayu vangi na vawula va malagizu vakahika kuhuma ku Yelusalemu, vakamhambila Yesu vakamkota,
Ndipo baadhi ya Mafarisayo na walimu wa sheria wakamjia Yesu kutoka Yerusalemu na kumuuliza,
2 “Ndava kyani vawuliwa vaku vitopesa lepi mawuliwu ga vagogo vitu? Visamba lepi chabwina mawoko kwakona kulya chakulya!”
“Mbona wanafunzi wako wanakiuka mapokeo ya wazee? Kwa maana wao hawanawi mikono yao kabla ya kula!”
3 Yesu akayangula, “Ndava kyani nyenye mwidenya mihilu ya Chapanga, ndava ya kulanda mawuliwu ginu?”
Yesu akawajibu, “Mbona ninyi mnavunja amri ya Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu?
4 Chapanga amali kujova, uvatopesa dadi waku na nyina waku, na mweampela likoto dadi waki amala nyina waki yikumgana akomiwa.
Kwa maana Mungu alisema, ‘Waheshimu baba yako na mama yako,’ na, ‘Yeyote amtukanaye baba yake au mama yake, na auawe.’
5 Nambu nyenye mwijova, mundu mweakumjovela dadi waki amala nyina waki kuvya, chochoha chenihotola kukutangatila, nimuwusili Chapanga,
Lakini ninyi mwafundisha kwamba mtu akimwambia baba yake au mama yake, ‘Kile ambacho ningeweza kukusaidia kimewekwa wakfu kwa Mungu,’
6 iganikiwa lepi kumtangatila dadi waki amala nyina waki. Chenichi ndi chemdenya amuli ya Chapanga kwa kugalanda mawuliwu ginu!
basi hana tena sababu ya kumheshimu baba yake nacho. Basi kwa ajili ya mafundisho yenu mnavunja amri ya Mungu.
7 “Nyenye mwemkujikita kuvya vandu vabwina! Isaya alotili chakaka, ndava yinu, peajovili malovi aga!
Ninyi wanafiki! Isaya alikuwa sawa alipotabiri juu yenu kwamba:
8 ‘Chapanga ijova, vandu ava vakunitopesa kwa malovi ndu, nambu mitima yavi yivii kutali na nene.
“‘Watu hawa huniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami.
9 Kunigundamila kwavi ndi waka, ndava mambu geviwula ndi malagizu ga vandu ndu.’”
Huniabudu bure; nayo mafundisho yao ni maagizo ya wanadamu tu.’”
10 Kangi Yesu aukemili msambi wa vandu akaujovela, “Myuwanila na kumanya malovi genikuvajovela!
Yesu akaita ule umati wa watu, akawaambia, “Sikilizeni na mwelewe:
11 Chindu chechikumyingisa mundu uhakasa palongolo ya Chapanga lepi chechiyingila mumlomo, nambu ndi chila chechikumuhuma mundu mumlomo.”
kinachomfanya mtu kuwa najisi mbele za Mungu si kile kiingiacho kinywani mwake, bali ni kile kitokacho kinywani mwake.”
12 Kangi vawuliwa vaki vakamhambila, vakamjovela, “Wu, umanyili kuvya Vafalisayu vayomili pevayuwini malovi gaku?”
Kisha wanafunzi wake wakamjia na kumuuliza, “Je, unajua kwamba Mafarisayo walichukizwa sana waliposikia yale uliyosema?”
13 Nambu mwene akavayangula, “Mbeyu yeyoha angamija Dadi wangu mweavi kunani, yati yitupuliwa.
Akawajibu, “Kila pando ambalo Baba yangu wa mbinguni hakulipanda, litangʼolewa.
14 Mvaleka vene! Vene ndi vangalola, vachilongosi wa vangalola, na ngalola akamlongosa ngalola muyaki, voha vavili yati vidumbukila muligodi.”
Waacheni; wao ni viongozi vipofu, wanaoongoza vipofu. Kama kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, wote wawili watatumbukia shimoni.”
15 Petili akajova, “Utidandaulila luhumu wenuwo.”
Petro akasema, “Tueleze maana ya huu mfano.”
16 Yesu akajova, “Hati nyenye mwakona mwangagamanya ago?
Yesu akawauliza, “Je, bado ninyi hamfahamu?
17 Wu, mwihotola lepi kumanya chechiyingila mumlomo chihamba mulileme na chiumiswa kuvala kundindima?
Je, hamwelewi kwamba chochote kiingiacho kinywani huenda tumboni, na hatimaye hutolewa nje kikiwa uchafu?
18 Nambu mambu gegihumila mumlomo gihuma mumtima, genago ndi gegakumkita mundu akotoka kuyidakiliwa palongolo ya Chapanga.
Lakini kitokacho kinywani hutoka moyoni, na hiki ndicho kimtiacho mtu unajisi.
19 Ndi mumtima gihuma maholo na ukomaji na ugoni na ukemi na kuyiva na malovi ga udese na maligu.
Kwa maana ndani ya moyo hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushahidi wa uongo na masingizio.
20 Genago ndi gegakumkita mundu kuvya mhakasa palongolo ya Chapanga. Nambu kulya chakulya changasamba nakumuyingisa mundu uhakasa.”
Haya ndiyo yamtiayo mtu unajisi; lakini kula bila kunawa mikono hakumtii mtu unajisi.”
21 Yesu awukili pandu penapo akahamba kutama kumuji wa Tilo na Sidoni.
Yesu aliondoka mahali pale, akaenda sehemu za Tiro na Sidoni.
22 Mau mmonga Mkanani wa mulima wenuwo ambwelili na kuywanga neju, “Bambu Mwana wa Daudi, unihengela lipyana! Msikana wangu ing'ahiswa na mzuka.”
Mwanamke mmoja Mkanaani aliyeishi sehemu jirani na hizo akaja kwake akilia, akasema, “Nihurumie, Ee Bwana, Mwana wa Daudi! Binti yangu amepagawa na pepo mchafu, na anateseka sana.”
23 Nambu Yesu ayangwili lepi, hinu vawuliwa vaki vakamhambila, vakamjovela, “Mjovela awuka lola akutilanda kuni iywanga.”
Lakini Yesu hakumjibu neno. Hivyo wanafunzi wake wakamwendea na kumsihi sana, wakisema, “Mwambie aende zake, kwa maana anaendelea kutupigia kelele.”
24 Yesu akayangula, “Nitumwili ndu kwa mulima wa Isilaeli, vevavi ngati limbelele leliyagili.”
Yesu akajibu, “Nimetumwa tu kwa ajili ya kondoo wa Israeli waliopotea.”
25 Nambu mau yula akabwela akamfugamila, akajova “Bambu, unitangatila.”
Lakini yule mwanamke akaja, akapiga magoti mbele ya Yesu, akasema, “Bwana, nisaidie!”
26 Yesu akamyangula “Chabwina lepi kutola chakulya cha vana na kutagila mabwa.”
Yesu akajibu, “Si haki kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.”
27 Hinu mau yula akayangula, “Chakaka, Bambu, nambu hati mabwa gilya masigalilu gegigwa pahi pameza ya bambu wavi.”
Yule mwanamke akajibu, “Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yanayoanguka kutoka kwenye meza za bwana zao.”
28 Penapo ndi Yesu akayangula, “Mau veve, sadika yaku yivaha! Uhengewa ngati chaugana.” Msikana waki akalama lukumbi lulalula.
Ndipo Yesu akamwambia, “Mwanamke, imani yako ni kubwa! Iwe kwako kama unavyotaka.” Naye binti yake akapona tangu saa ile.
29 Yesu akawuka penapo akahamba mumhana wa nyanja Galilaya, akakwela pachitumbi, akatama pahi.
Yesu akaondoka na kwenda kando ya Bahari ya Galilaya. Kisha akapanda mlimani, akaketi huko.
30 Msambi wa vandu vambwelili vamletili vevagogodili higa na vangalola na vangajova pamonga na vangi vamahele vevagogodili magendelu vana matamu, vakavavika palongolo ya magendelu gaki, mwene akavalamisa
Umati mkubwa wa watu ukamjia, wakiwaleta vilema, vipofu, viwete, bubu na wengine wengi, wakawaweka miguuni pake; naye akawaponya.
31 Msambi wa vandu ukakangasa neju pavaweni vangajova vijova, vevagogodili higa vilama vevagogodili magendelu vigenda na vangalola vilola, vandu vakamulumba Chapanga wa Isilaeli.
Hao watu wakashangaa walipoona bubu wakisema, vilema wakipona, viwete wakitembea na vipofu wakiona, wakamtukuza Mungu wa Israeli.
32 Yesu avakemili vawuliwa vaki na kuvajovela, “Nikuvahengela lipyana vandu ava ndava vatamii pamonga na nene magono gadatu, nivii lepi na chindu chakulya. Nangagana vawuka na njala, muni vakotoka kuinduka munjila.”
Kisha Yesu akawaita wanafunzi wake, akawaambia, “Ninauhurumia huu umati wa watu, kwa sababu sasa wamekuwa pamoja nami kwa muda wa siku tatu, na hawana chakula chochote. Nami sipendi kuwaaga wakiwa na njaa, wasije wakazimia njiani.”
33 Vawuliwa vaki vakamjovela, “Penapa palukongolo tipata koki chakulya cha kuyukuta msambi woha wa vandu?”
Wanafunzi wake wakasema, “Tutapata wapi mikate ya kutosha kuwalisha umati huu wa watu mkubwa namna hii, nasi tuko nyikani?”
34 Yesu akavakota, “Mabumunda gavi galinga?” Vakamyangula “Saba na tusomba tudebe.”
Yesu akawauliza, “Mnayo mikate mingapi?” Wakamjibu, “Tunayo mikate saba na visamaki vichache.”
35 Yesu akalagiza vandu vatama pahi.
Yesu akawaambia ule umati wa watu waketi chini.
36 Akatola mabumunda gala saba na tusomba tudebe tula, akalolokesa kunani kwa Chapanga, akamsengusa Chapanga, akavimetula, akavapela vawuliwa vaki, navene vakavagavila vandu.
Kisha akachukua ile mikate saba na wale samaki, naye akiisha kumshukuru Mungu, akavimega na kuwapa wanafunzi wake, nao wakawapa ule umati wa watu.
37 Voha vakalya na kuyukuta. Kangi vakayola masigalilu ga hipandi na kumemesa madengu saba.
Wote wakala na kushiba. Baadaye wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu saba.
38 Vandu vevalili vavi vagosi elufu mcheche changavalanga vadala na vana.
Idadi ya watu walikuwa wanaume 4,000, bila kuhesabu wanawake na watoto.
39 Ndi Yesu akavalaga vandu vala, akayingila muwatu, akahamba kumuji wa Magadani.
Baada ya kuaga ule umati wa watu, Yesu aliingia katika mashua, akaenda sehemu za Magadani.