< Maluko 13 >

1 Yesu peahumayi mu Nyumba ya Chapanga, mmonga wa vawuliwa vaki amjovili, “Muwula, lola maganga na majengu aga chegavili gabwina na kukangasa!”
Yesu alipokuwa akitoka Hekaluni, mmojawapo wa wanafunzi wake akamwambia, “Mwalimu! Tazama jinsi mawe haya yalivyo makubwa, na majengo haya yalivyo mazuri!”
2 Yesu akamyangula, “Wu, ukugalola majengu aga zivaha? Kawaka liganga hati limonga lelisigalila panani ya liganga lingi, kila liganga yati ligwisiwa.”
Ndipo Yesu akajibu akasema, “Je, unayaona majengo haya yalivyo makubwa? Hakuna hata jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, bali yote yatabomolewa.”
3 Yesu paatamili panani ya chitumbi cha Mizeituni kulolokesa Nyumba ya Chapanga, Petili na Yakobo na Yohani na Andelea vakamkota pevavi ngavene,
Yesu alipokuwa ameketi kwenye Mlima wa Mizeituni mkabala na Hekalu, Petro, Yakobo, Yohana na Andrea wakamuuliza faraghani,
4 “Tijovela mambu genago yati gihumila ndali? Na ulangisu woki weulangisa kuvya mambu aga gavi papipi kuhumila?”
“Tafadhali tuambie, mambo haya yatatukia lini? Nayo dalili ya kuwa hayo yote yanakaribia kutimia itakuwa gani?”
5 Yesu akatumbula kuvajovela, “Mujiyangalilayi mundu akotoka kuvakonga.”
Yesu akawaambia: “Jihadharini mtu yeyote asiwadanganye.
6 Muni vamahele yati vibwela na kulihengela liina langu, kila mundu yati ijova kuvya mwene ndi Kilisitu! Vene yati vakuvakonga vandu vamahele.
Wengi watakuja kwa Jina langu wakidai, ‘Mimi ndiye,’ nao watawadanganya wengi.
7 Pemyuwana gegivala ngondo na vandu vilongelela mambu ga ngondo mkotoka kuvagaya. Yikugagana mambu genaga kuhumila, nambu mwishu wene wakona.
Msikiapo habari za vita na uvumi wa vita, msiwe na hofu. Mambo haya hayana budi kutukia, lakini ule mwisho bado.
8 Vandu va mulima umonga yati utovana na vandu va mulima wungi, unkosi umonga yati utovana na unkosi wungi, yati kwiva na mindendemo ya ndima pamonga na njala. Mambu ago ndi ngati utumbula wa lipyanda la kuveleka mwana.
Taifa litainuka dhidi ya taifa na ufalme dhidi ya ufalme. Kutakuwa na mitetemeko sehemu mbalimbali na njaa. Haya yatakuwa ndio mwanzo wa utungu.
9 Nambu nyenye mjiyangalila. Muni yati vakuvatakila mumabanji ga mihalu, na kutovewa munyumba za kukonganekela Vayawudi. Mewawa yati vakuvapeleka palongolo ya vachilongosi na vankosi ndava ya nene, muni mujova ndava yangu.
“Lakini ninyi jihadharini. Kwa maana watawapeleka katika mabaraza yao na kupigwa mijeledi katika masinagogi. Mtashtakiwa mbele ya watawala na wafalme kwa ajili yangu, ili kuwa ushuhuda kwao.
10 Nambu yiganikiwa hoti lilovi la Bwina likokosewayi kwa vandu voha kwakona mwishu wangahika.
Nayo habari njema lazima ihubiriwe kwanza kwa mataifa yote kabla ule mwisho haujawadia.
11 Na pamwikamuliwa na kupelekwa mumabanji ga mihalu, mkoto kuhololela chakujova. Lukumbi lwenulo. Nambu mjova chechoha chemwipewa kujova, muni yati gihuma kwa Mpungu Msopi.
Mtakapokamatwa na kushtakiwa, msisumbuke awali kuhusu mtakalosema. Semeni tu lolote mtakalopewa wakati huo, kwa kuwa si ninyi mtakaokuwa mkinena, bali ni Roho Mtakatifu.
12 Mlongo yati akumng'anamukila mhaja waki akomiwa na dadi yati akumng'anamukila mwana waki, na vana yati vakuvang'anamukila dadi na nyina vavi vakomewayi.
“Ndugu atamsaliti ndugu yake ili auawe, naye baba atamsaliti mtoto wake. Watoto nao wataasi dhidi ya wazazi wao na kusababisha wauawe.
13 Vandu voha yati vakuvagana lepi ndava ya liina langu. Nambu mweisindimala mbaka mwishu ndi Chapanga akumsangula kuhuma uhamula wa magono goha gangali mwishu.
Watu wote watawachukia kwa ajili ya Jina langu. Lakini yule atakayevumilia hadi mwisho ataokolewa.
14 “Pemwilola ‘Yomeso lihakau lelilangisa uhalabisu’ Liyimili pandu pangaganikiwa kuvya.” Mweisoma malovi aga amanyalila. Hinu vevavili ku Yudea na vajumbalila kuchitumbi.
“Mtakapoona ‘chukizo la uharibifu’ limesimama mahali pasipolipasa (asomaye na afahamu), basi wale walioko Uyahudi wakimbilie milimani.
15 Mundu mweavili kuvala ya nyumba yaku akotoka kuyingila mugati kutola chindu, nambu atilayi!
Yeyote aliye juu ya dari ya nyumba asishuke au kuingia ndani ili kuchukua chochote.
16 Mewawa mundu mweavili kumgunda akotoka kuwuya kunyumba yaki kutola nyula yaki.
Aliye shambani asirudi nyumbani kuchukua vazi lake.
17 Niviniswa mtima ndava ya vanandumbu na vevinyong'esa magono ago, ndava yati kwivya na mang'ahiso neju.
Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo!
18 Nambu mumuyupayi Chapanga mambu ago gakotoka kuhumila lukumbi lwa mbepu.
Ombeni mambo haya yasitokee wakati wa baridi.
19 Muni magono ago yati kwiva na mang'ahiso gakulu, gangahumila kuhuma Chapanga kuwumba mulima mbaka lelu, katu yati gihumila lepi kavili.
Kwa maana siku hizo zitakuwa za dhiki kuu ambayo haijapata kuwako tangu mwanzo, hapo Mungu alipoumba ulimwengu, mpaka leo, na wala haitakuwako tena kamwe.
20 Ngati Bambu ngagapunguziwi lepi magono kawaka hati mundu mmonga wa kusanguliwa. Nambu ndava ya vahaguliwa vaki, Bambu agapungwizi magono ago.
Kama Bwana asingelifupisha siku hizo, kamwe asingeliokoka mtu yeyote. Lakini kwa ajili ya wateule, wale aliowachagua, amezifupisha siku hizo.
21 Kangi, mundu akavajovela, lolayi, Kilisitu avili apa! Amala, avili pala, mkotoka kusadika.
Wakati huo mtu yeyote akiwaambia, ‘Tazama, Kristohuyu hapa!’ au, ‘Tazama, yuko kule,’ msisadiki.
22 Muni yati vihumalila vakina Kilisitu vaudese na vamlota va udese, yati vikita ulangisu na chinamtiti, ngati yihotoleka ndava ya kuvabudisa hati vahaguliwa va Chapanga.
Kwa maana watatokea makristo wa uongo na manabii wa uongo, nao watafanya ishara na maajabu ili kuwapotosha, ikiwezekana, hata wale wateule.
23 Nambu nyenye mujiyangalila. Nene nivajovili mambu genaga kwakona gangahumila.
Hivyo jihadharini. Nimekwisha kuwaambia mambo haya yote mapema kabla hayajatukia.
24 “Nambu pegimalika magono ago ga mang'ahiso, lilanga yati lisopewa chitita na mwehi yati ulangasa lepi.
“Lakini katika siku hizo, baada ya hiyo dhiki, “‘jua litatiwa giza nao mwezi hautatoa nuru yake;
25 Ndondo yati zigwa kuhuma kunani, na vindu vyoha vya kumahundi yati vinyuguswa.
nazo nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu za anga zitatikisika.’
26 Penapo yati vakumlola Mwana wa Mundu, ibwela mulihundi kwa makakala gamahele na ukulu.
“Ndipo watu wote watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni kwa nguvu nyingi na utukufu.
27 Ndi yati akuvatuma vamitumu va kunani kwa Chapanga vavalunda vandu vevahaguliwi na Chapanga, kuhuma pandi mcheche za mulima, na hati kuhuma pandu pa kutali ya mulima woha.”
Naye atawatuma malaika wake wawakusanye wateule wake kutoka pande zote nne za dunia, kutoka miisho ya dunia hadi miisho ya mbingu.
28 “Mujiwula kuhuma mumkongo wa mtini. Pemwilola mahamba gimela, nyenye mwimanya kuvya lusenje lwa fula luhegalili.
“Basi jifunzeni somo hili kutokana na mtini: Matawi yake yanapoanza kuchipua na kutoa majani, mnatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
29 Mewawa na nyenye pemwilola mambu genago gihengeka, mmanya kuvya Mwana wa Mundu avi papipi neju kuhika.
Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba wakati u karibu, hata malangoni.
30 Chakaka nikuvajovela, chiveleku ichi chipita lepi kwakona mambu aga kuhumila.
Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.
31 Hati ngati kunani kwa Chapanga na pamulima yati ziwuka, nambu malovi gangu yati gihumila ngati chenajovili.”
Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
32 “Nambu, avi lepi mundu mweimanya ligono la mwishu yati libwela ndali, hati vamitumu va kunani kwa Chapanga, hati Mwana wa Chapanga. Dadi Chapanga ndu mweamanyili.
“Kwa habari ya siku ile na saa hakuna yeyote ajuaye, hata malaika walio mbinguni wala Mwana, ila Baba peke yake.
33 Mujiyangalila na mujitendekela, muni mumanyili lepi ligono amala lukumbi peluhumila.
Jihadharini! Kesheni! Kwa maana hamjui wakati ule utakapowadia.
34 Yati yivya ngati mundu mweahambi lugendu na kuvalekela vahengaji utalalila, kila mundu na lihengu laki, akumjovela mlonda wa mlyangu avyai mihu.
Ni kama mtu anayesafiri. Anaiacha nyumba yake na kuwaachia watumishi wake kuiangalia, kila mtu na kazi yake, kisha akamwamuru yule bawabu aliye mlangoni akeshe.
35 Mujitendelekela, ndava muni mmanyi lepi mkolo nyumba iwuya ndali. Pangi yivya kimihi, pagati ya kilu, hambakucha amala lukela.
“Basi kesheni kwa sababu hamjui ni lini mwenye nyumba atakaporudi: iwapo ni jioni, au ni usiku wa manane, au alfajiri awikapo jogoo, au mapambazuko.
36 Mujitendelekela, muni ngati abwelili cha kukenyemusa, akotoka kuvakolela mgonili.
Kama akija ghafula, asije akawakuta mmelala.
37 Genikuvajovela nyenye, nikuvajovela mwavoha. Muvya mihu!”
Lile ninalowaambia ninyi, nawaambia watu wote: ‘Kesheni!’”

< Maluko 13 >