< Luka 6 >

1 Ligono la Kupumulila, Yesu apitayi mumigunda ya nganu. Vawuliwa vaki vakatumbula kudenya njechela za nganu, vakagayogola mumawoko gavi vakalya ngele zaki.
Siku moja ya Sabato, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano, na wanafunzi wake wakaanza kukwanyua masuke ya ngano, wakaondoa punje zake kwa mikono, wakala.
2 Nambu Vafalisayu vangi vakavakota, “Ndava kyani nyenye mukita chindu chechibesiwi Ligono la Kupumulila?”
Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, “Mbona mnafanya jambo ambalo si halali siku ya Sabato?”
3 Yesu akavayangula, “Wu! Mwangasoma cheakitili Daudi na vayaki pevavi na njala?
Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma jinsi alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?
4 Ayingili mu Nyumba ya Chapanga, akatola mabumunda gegavikiwi pandu pa Chapanga, akalya na akavagavila na vayaki. Mabumunda genago gavi ndava ya vamlota va Chapanga ndu, ndi vevalyayi.”
Yeye aliingia ndani ya nyumba ya Mungu, akachukua ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu, akala na kuwapa wenzake. Kisheria, ni makuhani tu peke yao ndio walioruhusiwa kula mikate hiyo.”
5 Kangi akavajovela, “Mwana wa Mundu ndi Bambu wa Ligono la Kupumulila.”
Hivyo akawaambia, “Mwana wa Mtu ni Bwana wa Sabato.”
6 Ligono lingi la Kupumulila, Yesu akahamba munyumba ya kukonganekela Vayawudi kuwula. Kumbi mugati mula avili mundu mmonga mwaapopotwiki chiwoko chaki cha kulyelela.
Siku nyingine ya Sabato, Yesu aliingia katika sunagogi, akafundisha. Mle ndani mlikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.
7 Vawula va malagizu ga Chapanga geampeli Musa na Vafalisayu vamlolokisi takataka Yesu, valola ngati akumlamisa mundu Ligono la Kupumulila muni valonda lilovi la kumtakila.
Walimu wa Sheria na Mafarisayo walitaka kupata kisingizio cha kumshtaki Yesu na hivyo wakawa wanangojea waone kama angemponya mtu siku ya Sabato.
8 Nambu Yesu agamanyili goha gavaholalela na akamjovela mweagogodili chiwoko yula, “Yimuka, uyima palongolo yavi.” Mundu yula akayima akahamba penapo.
Lakini Yesu alijua mawazo yao, akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Inuka, simama katikati.” Yule mtu akaenda akasimama katikati.
9 Yesu akavajovela, “Nikuvakota nyenye, malagizu gitu gijova wuli kuyivala Ligono la Kupumulila? Wu, tihotola kukita lijambu labwina amala tihotola kukita lijambu lihakau? Wu, tihotola kusangula wumi wa mundu amala tihotola kukoma?”
Kisha Yesu akawaambia, “Nawaulizeni, je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuyaangamiza?”
10 Akavalolokesa vandu voha vevavili penapo, akamjovela mwaapopotwiki chiwoko yula, “Golosa chiwoko chaku.” Mundu yula akagolosa, na akalama chiwoko chaki.
Baada ya kuwatazama wote waliokuwa pale, akamwambia yule mtu, “Nyosha mkono wako.” Naye akafanya hivyo, na mkono wake ukawa mzima tena.
11 Nambu vene vakayoma neju, vakajovesana, vamkitila kyani Yesu.
Lakini wao wakakasirika sana, wakajadiliana jinsi ya kumtendea Yesu maovu.
12 Lukumbi luhupu palongolo, Yesu akahamba kuchitumbi kuyupa kwa Chapanga, akatama mihu kilu yoha kumuyupa Chapanga.
Siku moja Yesu alikwenda mlimani kusali, akakesha huko usiku kucha akimwomba Mungu.
13 Chilau yaki lukela, akavakemela vawuliwa vaki, ndi akavahagula vandu kumi na vavili ndi akavakemela vamitumi.
Kesho yake aliwaita wanafunzi wake, na miongoni mwao akachagua kumi na wawili ambao aliwaita mitume:
14 Simoni mewa mwapewili liina lingi na Yesu la Petili, na mbena waki Andelea mlongo waki na Yakobo na Yohani na Filipi na Batolomei,
Simoni (ambaye Yesu alimpa jina Petro) na Andrea ndugu yake, Yakobo na Yohane, Filipo na Bartholomayo,
15 Na Matei na Tomasi na Yakobo mwana wa Alufayo na Simoni mweakemeliwi Zelote, ndava avili mundu wa kukengelela mulima waki,
Mathayo na Thoma, Yakobo wa Alfayo na Simoni (aliyeitwa Zelote),
16 Na Yuda mwana wa Yakobo na Yuda Isikalioti mweabweli kumung'anamukila Yesu.
Yuda wa Yakobo na Yuda Iskarioti ambaye baadaye alikuwa msaliti.
17 Yesu paahelili kuchitumbi pamonga nawu, akayima pamtambu, penapo pavi na vawuliwa vaki na msambi wa vandu vamahele vakuhuma ku Yudea yoha, na ku Yelusalemu na pamulima wa kumbwani ya ku Tilo na ku Sidoni.
Baada ya kushuka mlimani pamoja na mitume, Yesu alisimama mahali palipokuwa tambarare. Hapo palikuwa na kundi kubwa la wanafunzi wake na umati wa watu waliotoka pande zote za Yudea na Yerusalemu na pwani ya Tiro na Sidoni. Wote walifika kumsikiliza Yesu na kuponywa magonjwa yao.
18 Vandu voha vabweli kumyuwanila Yesu na vevavi na utamu vagana valamisiwayi. Mewa ayihakalili mizuka kuhuma kwa vandu venavo.
Aliwaponya pia wote waliokuwa wanasumbuliwa na pepo wachafu.
19 Ndi kila mundu alingayi kumpamisa, muni makakala gamuhumayi mwene na kuvalamisa vandu voha.
Watu wote walitaka kumgusa, kwa maana nguvu ilikuwa inatoka ndani yake na kuwaponya wote.
20 Yesu akavalola vawuliwa vaki akavajovela, Mhekayi nyenye mwavangangu, muni Unkosi wa Chapanga ndi winu!
Yesu akawageukia wanafunzi wake, akasema: “Heri ninyi mlio maskini, maana Ufalme wa Mungu ni wenu.
21 Mhekayi nyenye mwemuvi na njala hinu, muni yati mwiyukuta! Mhekayi nyenye mwemvemba hinu, muni yati muheka kwa luheku!
Heri ninyi mnaosikia njaa sasa, maana baadaye mtashiba. Heri ninyi mnaolia sasa, maana baadaye mtacheka kwa furaha.
22 Mhekayi, nyenye, ngati vandu vavagani lepi, amala kuvabagula, amala kuvaliga na kugahakasa mahina ginu ndava ya Mwana wa Mundu!
“Heri yenu ninyi iwapo watu watawachukia, watawatenga, watawatukana na kuwaharibieni jina kwa ajili ya Mwana wa Mtu!
23 Lukumbi genago pegihumila, mhekayi na kukina, muni njombi yinu yivaha kunani kwa Chapanga. Ndava muni vagogo vavi vavakitili vamlota va Chapanga mewawa.
Wakati hayo yatakapotokea, furahini na kucheza, maana hakika tuzo lenu ni kubwa mbinguni. Kwa maana wazee wao waliwatendea manabii vivyo hivyo.
24 “Nambu mwalachikolela nyenye mwemuvi na vindu vyamahele hinu, ndava mmali kupoleswa mitima, yati mpoleswa lepi kavili mitima yinu.
Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, maana mmekwisha pata faraja yenu.
25 Mwalachikolela nyenye mwemwiyukuta hinu, muni njala yati yikuvavina! Mwalachikolela nyenye mwemuheka hinu, mwalavemba na kuvya milyangu.”
Ole wenu ninyi mnaoshiba sasa, maana baadaye mtasikia njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka kwa furaha sasa, maana baadaye mtaomboleza na kulia.
26 “Mwalachikolela nyenye ngati vandu voha vakuvalumbalila, muni vagogo vavi vavalumbalili vamlota va Chapanga vaudese mewawa.”
Ole wenu ninyi iwapo watu wote wanawasifu, maana wazee wao waliwafanyia manabii wa uongo vivyo hivyo.
27 “Nambu nikuvajovela nyenye mwemukuniyuwanila, muvagana vandu vevavi makoko vinu, muvakitila gabwina vandu vangavagana nyenye.
“Lakini nawaambieni ninyi mnaonisikiliza: wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale wanaowachukieni.
28 Muvamotisa vala vevalapikisa likoto, muvawombelayi vala vevakuvakitila gahakau.
Watakieni baraka wale wanaowalaani, na waombeeni wale wanaowatendea vibaya.
29 Ngati mundu yoyoha yula akutovili mulitama, veve mung'anamusila na lingi. Ngati mundu akunyagili likoti laku, mewa veve mulekelayi na nyula.
Mtu akikupiga shavu moja mgeuzie na la pili. Mtu akikunyang'anya koti lako mwachie pia shati lako.
30 Mundu yoyoha yula mweakukuyupa chindu veve mpelayi, ngati mudu akunyagi vindu vyaku, veve kotoka kumjovela akuwuyisila.
Yeyote anayekuomba mpe, na mtu akikunyang'anya mali yako usimtake akurudishie.
31 Ngati chemwigana vandu vangi vavakitilayi, na nyenye muvakitila vene mewawa.”
Watendeeni wengine kama mnavyotaka wawatendee ninyi.
32 “Ngati mukuvagana nga vandu vevakuvagana nyenye mwavene, mwipata njombi yoki? Kawaka! Muni na vevakumbudila Chapanga na vene viganana mewa.
“Na ikiwa mnawapenda tu wale wanaowapenda ninyi, je, mtapata tuzo gani? Hakuna! Kwa maana hata wenye dhambi huwapenda wale wanaowapenda wao.
33 Na, ngati mukuvakitila gakumganisa Chapanga nga vala vevakuvawuyisila, nyenye mwipata njombi yoki? Muni hati vandu vevakumbudila Chapanga, vikita mewawa,
Tena, kama mkiwatendea mema wale tu wanaowatendeeni mema, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi hufanya vivyo hivyo!
34 na ngati mukuvayaika vandu vemuvahuvalila vavawuyisilayi ndu, mwipata njombi kiki? Muni na vandu vevakumbudila Chapanga vakuvayayika mewawa vayavi, ndava vawuyisiwayi.
Na kama mnawakopesha wale tu mnaotumaini watawalipeni, je, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi wenzao ili warudishiwe kima kilekile!
35 Nambu nyenye muvaganayi makoko vinu, mvakitila gabwina, na pemukuvayaika mkotoka kugana kuwuyisiwa kavili. Ndi penapo njombi yinu yati yivya yivaha na nyenye yati mwivya vana va Chapanga Mkulu. Muni mwene akuvagana vandu vangamsengusa na vahakau.
Ila nyinyi wapendeni adui zenu, na kuwatendea mema; kopesheni bila kutazamia malipo, na tuzo lenu litakuwa kubwa, nanyi mtakuwa watoto wa Mungu aliye juu. Kwa maana yeye ni mwema kwa wale wasio na shukrani na walio wabaya.
36 Muvya na lipyana ngati Dadi winu cheavi na lipyana.”
Muwe na huruma kama Baba yenu alivyo na huruma.
37 “Mkotoka kuvahamula vangi, na Chapanga yati akuvahamula lepi, mkotoka kuvalaumu vayinu na nyenye yati mwilaumiwa lepi, muvalekelekesa vayinu na Chapanga yati avalekelekesa nyenye.
“Msiwahukumu wengine, nanyi hamtahukumiwa; msiwalaumu wengine, nanyi hamtalaumiwa; wasameheni wengine, nanyi mtasamehewa.
38 Muvapela vangi gevigana, na Chapanga yati avapela nyenye, ndi mupokela mulihaku linu. Ndava muni chipimu chichocho chemvahengela vangi na nyenye yati mpokela kuhuma kwa Chapanga, chipimu cha bwina cha kumema na kuhindiliwa na kunyuguswa mbaka kuyitika.”
Wapeni wengine wanavyohitaji, nanyi mtapewa. Naam, mtapokea mikononi mwenu kipimo kilichojaa, kikashindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika. Kwa maana kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho ambacho Mungu atatumia kwenu.”
39 Yesu akavajovela luhumu ulu, “Wu, ngalola, ihotola kumlongosa ngalola muyaki? Lepi! Voha yati vidumbukila muligodi.
Akawaambia mfano huu: “Je, kipofu anaweza kumwongoza kipofu mwenzake? La! Wote wataanguka shimoni.
40 Muwuliwa mkulu lepi kuliku muwula waki, nambu akawuliwayi na kumanya ndi iwanangana na muwula waki.
Mwanafunzi hamshindi mwalimu wake, lakini kila mwanafunzi akisha hitimu huwa kama mwalimu wake.
41 Ndava kyani ulola lungoda lweluvi mulihu la mlongo waku, nambu wamwene uvi na lumbagalu mulihu laku?
Unawezaje kukiona kibanzi kilicho katika jicho la mwenzio, usione boriti iliyo katika jicho lako mwenyewe?
42 Uhotola wuli kumjovela mlongo waku, ‘Chondi nikuwusayi lungoda mulihu laku,’ Kuni nakuluwona lumbagalu mulihu laku wamwene? Mweukujikita mbwina veve! Wusa hoti lumbagalu mulihu laku ndi yati ulola bwina kuwusa kabasi mulihu la mlongo waku.”
Au, unawezaje kumwambia mwenzako, Ndugu, ngoja nikuondoe kibanzi katika jicho lako, na huku huioni boriti iliyoko katika jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe! Toa kwanza boriti iliyoko jichoni mwako, na hivyo utaona sawasawa kiasi cha kuweza kuondoa kibanzi kilicho katika jicho la ndugu yako.
43 “Mewawa mkongo wabwina upambika lepi matunda gahakau na wala mkongo uhakau upambika lepi matunda gabwina.
“Mti mwema hauzai matunda mabaya, wala mti mbaya hauzai matunda mazuri.
44 Mkongo wowoha wula umanyikana ndava ya matunda gaki. Muni vandu viyava lepi matunda ga tini mumkongo wa michongoma na wala viyava lepi zabibu mumbigili.
Watu huutambua mti kutokana na matunda yake. Ni wazi kwamba watu hawachumi tini katika michongoma, wala hawachumi zabibu katika mbigili.
45 Mundu mbwina iwusa vindu vyabwina kuhuma muvindu yveavikili muchibana cha mtima waki na mundu mhakau iwusa vindu vihakau kuhuma muchibana cha mtima waki. Ndava muni mundu ilongela gegamemili mumtima waki.”
Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka katika hazina bora iliyo moyoni mwake; na mtu mbaya hutoa yaliyo mabaya katika hazina mbaya iliyo moyoni mwake, kwa maana mtu huongea kutokana na yale yaliyojaa moyoni mwake.
46 “Ndava kyani mukunikemela ‘Bambu, Bambu,’ Kuni mwihenga lepi chenikuvajovela?
“Mbona mwaniita Bwana, Bwana, na huku hamtimizi yale ninayosema?
47 Nikuvapela luhumu lwa mundu yula mweibwela kwa nene, akugayuwana malovi gangu na kuhenga chenijova.
Nitawapeni mfano unaofaa kuonyesha alivyo yeyote yule anayekuja kwangu, akasikia maneno yangu na kuyatimiza:
48 Mwenuyo iwanangana ngati mundu mweijenga nyumba, mwe agimili mkingisa neju mbaka akaukolela litalau, akatumbula kujenga penapo. Peyaumili mfuleni kumema manji gana makakala na kuyitova nyumba yila, nambu nyumba yila yanyugusiki lepi, ndava yajengiwi chakukangamala.
Huyo anafanana na mtu ajengaye nyumba, ambaye amechimba chini na kuweka msingi wake juu ya mwamba; kukatokea mafuriko ya mto, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, lakini haukuweza kuitikisa, kwa sababu ilikuwa imejengwa imara.
49 Nambu mundu yula mweiyuwana malovi gangu na ihenga lepi chindu chochoha, mwenuyo iwanangana na mundu mweajengili nyumba panani ya ludaka changali kugima mkingisa neju. Peyahumili mifuleni kumema manji gana makakala, gakayitova nyumba yila, yikagwa na kudenyekana nyiminyimi!”
Lakini yeyote anayesikia maneno yangu lakini asifanye chochote, huyo anafanana na mtu aliyejenga nyumba juu ya udongo, bila msingi. Mafuriko ya mto yakatokea, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, ikaanguka na kuharibika kabisa!”

< Luka 6 >