< Yohani 21 >

1 Pagamaliki genago, Yesu akavahumila kavili vawuliwa vaki pamuhana ya nyanja Tibelia. Avahumili naha,
Baada ya haya Yesu akawatokea tena wanafunzi wake kando ya Bahari ya Tiberia. Yeye alijionyesha kwao hivi:
2 Simoni Petili, Tomasi mweikemewa Mapaha, na Natanyeli mkolonjinji wa Kana ya ku Galilaya, vana vavili va Zebedayo na vawuliwa vaki vangi vavili, vakavya voha pamonga.
Simoni Petro, Tomaso aitwaye Didimasi, yaani Pacha, Nathanaeli wa Kana ya Galilaya, wana wa Zebedayo na wanafunzi wengine wawili walikuwa pamoja.
3 Simoni Petili akavajovela, “Nihamba kulova somba.” Vene vakamjovela, “Tete tilongosana na veve.” Vakahamba, vakakwela muwatu, nambu kilu yila nakupata chindu.
Simoni Petro akawaambia wenzake, “Mimi naenda kuvua samaki.” Nao wakamwambia, “Tutakwenda pamoja nawe.” Wakatoka, wakaingia ndani ya mashua, lakini usiku ule hawakupata chochote.
4 Hamba kucha, Yesu ayimili kumwambu ya nyanja, nambu vawuliwa vamanyili lepi kuvya avi Yesu.
Mara baada ya kupambazuka, Yesu akasimama ufuoni, lakini wanafunzi hawakumtambua kwamba alikuwa Yesu.
5 Yesu akavakota, “Vankozi, mupatili lepi somba?” Vakamyangula, “Lepi! Kawaka.”
Yesu akawaambia, “Wanangu, je, mna samaki wowote?” Wakamjibu, “La.”
6 Yesu akavajovela, “Muhelesa ngwanda upandi wa kulyela wa watu na nyenye yati mwipata somba.” Ndi vakazihelesa ngwanda, nambu hinu nakuhotola kuhuta kavili ndava ya somba zamahele.
Akawaambia, “Shusheni nyavu upande wa kuume wa mashua yenu nanyi mtapata samaki.” Wakashusha nyavu na tazama wakapata samaki wengi mno hata wakashindwa kuvutia zile nyavu zilizojaa samaki ndani ya mashua.
7 Kangi muwuliwa yula, Yesu mweamganili neju, akamjovela Petili, “Ndi Bambu!” Simoni Petili peayuwini kuvya ndi Bambu, akajikunga nyula yaki ya kuvala muni ahulili, akajitaga mumanji.
Yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akamwambia Petro, “Huyu ni Bwana!” Simoni Petro aliposikia haya, akajifunga nguo yake kwa kuwa alikuwa uchi, naye akajitosa baharini.
8 Nambu vawuliwa vangi vala vabwelili kumbwani na watu kuni vihuta ngwanda zezimemili somba, vavi lepi kutali na pandumba, ndi vavi utali wa mita miya yimonga kuhuma mu mkingisa.
Wale wanafunzi wengine wakaja kwa ile mashua huku wakikokota ule wavu uliyojaa samaki, maana hawakuwa mbali na nchi kavu, ilikuwa yapata dhiraa 200
9 Pavahikili pandumba wauwene motu wa makalakala, wiyaka, na panani yaki pavikiwi somba na libumunda.
Walipofika ufuoni, wakaona moto wa makaa na samaki wakiokwa juu yake na mikate.
10 Yesu akavajovela, “Mgava somba zingi mleta penapa zemlovili.”
Yesu akawaambia, “Leteni baadhi ya hao samaki mliovua sasa hivi.”
11 Simoni Petili akayingila muwatu, akahuta mbaka kundumba ngwanda yila yeyimemili somba zivaha miya yimonga na makumi mhanu na zidatu. Pamonga wamemili somba zamahele, nambu ngwanda yadawiki lepi.
Simoni Petro akapanda kwenye mashua na kuukokota ule wavu pwani. Ulikuwa umejaa samaki wakubwa 153. Ingawa samaki walikuwa wengi kiasi hicho, ule wavu haukuchanika.
12 Yesu akavajovela “Mbwela mlawuka.” Kawaka hati mmonga wavi. Mwealingili kumkota. “Veve ndi wayani,” Vammanyili kuvya Bambu.
Yesu akawaambia, “Njooni mpate kifungua kinywa.” Hakuna hata mmoja wa wanafunzi aliyethubutu kumuuliza, “Wewe ni nani?” Kwa sababu walijua ya kuwa ni Bwana.
13 Yesu akabwela, akatola, libumunda akavapela, akakita mewawa na somba zila.
Yesu akaja, akachukua ule mkate, akawapa na vivyo hivyo akawagawia pia wale samaki.
14 Yeniyi yavi mala ya datu Yesu kuvahumila vawuliwa vaki peamali kuyuka.
Hii ilikuwa mara ya tatu Yesu kuwatokea wanafunzi wake baada yake kufufuliwa kutoka kwa wafu.
15 Pevamali kulya, Yesu akamkota Simoni Petili, “Simoni mwana wa Yohani! Wu, ukunigana nene kuliku ava?” Mwene akayangula, “Ena, Bambu, umanyili kuvya nene nikukugana.” Yesu akamjovela, “Dima vana mambelele vangu.”
Walipokwisha kula, Yesu akamuuliza Simoni Petro, “Je, Simoni mwana wa Yohana, unanipenda kweli kuliko hawa?” Yeye akamjibu, “Ndiyo Bwana, wewe unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha wana-kondoo wangu.”
16 Kavili akamjovela, “Simoni mwana wa Yohani! Wu, ukunigana?” Petili akamyangula, “Ena, Bambu, umanyili kuvya nikukugana.” Yesu akamjovela “Dima mambelele gangu.”
Yesu akamwambia tena, “Simoni, mwana wa Yohana, wanipenda?” Petro akamjibu, “Ndiyo Bwana, wewe unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Chunga kondoo zangu.”
17 Yesu akamkota mala ya datu, “Simoni mwana wa Yohani! Wu, ukunigana?” Penapo Petili akavya ngolongondi ndava amkotili mala ya datu. “Ukunigana?” Akamjovela, “Bambu, wamwene umanyili kila chindu, umanyili kuvya nene nikukugana.” Yesu akamjovela, “Dima mambelele gangu!
Kwa mara ya tatu Yesu akamuuliza Petro, “Simoni mwana wa Yohana, unanipenda?” Petro akahuzunika sana kwa kuwa Yesu alimuuliza mara ya tatu, “Unanipenda?” Akamjibu, “Bwana, wewe unajua yote, unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha kondoo wangu.
18 Chakaka nikukujovela, pawavi msongolo wayovalili kujitendelekeha wamwene na kuhamba kwewigana. Nambu pawivya mgogolo wiyinula mawoko gaku, mundu yungi ndi yati akukunga na kuhamba kwe wangagana kuhamba.”
Amin, amin nakuambia, ulipokuwa kijana ulivaa na kwenda unakotaka, lakini utakapokuwa mzee utanyoosha mikono yako na mtu mwingine atakuvika na kukupeleka usipotaka kwenda.”
19 Yesu ajovili genago, kulangisa namuna Petili cheifwa na kumpela ukulu Chapanga. Kangi akamjovela Petili, “Nilanda.”
Yesu alisema haya ili kuashiria ni kifo cha aina gani Petro atakachomtukuza nacho Mungu. Kisha Yesu akamwambia Petro, “Nifuate!”
20 Petili akang'anamuka, amuwene muwuliwa yula mweaganiwi na Yesu, akumlanda mweneuyo ndi yula mweatamili papipi neju na Yesu lukumbi pevalyayi na kumkota, “Bambu ndi yani mweakukung'anamukila?”
Petro akageuka, akamwona yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akiwafuata. (Huyu ndiye yule mwanafunzi aliyeegama kifuani mwa Yesu walipokula naye chakula cha mwisho na kuuliza, “Bwana, ni nani atakayekusaliti?”)
21 Hinu, Petili peamuwene mwenuyo, akamkota Yesu, “Bambu, mundu uyu chikumuhumila kyani?”
Petro alipomwona huyo mwanafunzi, akamuuliza Yesu, “Bwana na huyu je?”
22 Yesu akayangula, “Ngati nigana asigalila mbaka penibwela, chikuvala kyani? Veve unilanda nene.”
Yesu akamjibu, “Ikiwa nataka aishi mpaka nitakaporudi, inakuhusu nini? Wewe inakupasa unifuate!”
23 Malovi ago, gadandasiki pagati ya valongo vevakumsadika Kilisitu kuvya muwuliwa mwenuyo yati ifwa lepi. Nambu Yesu amjovili lepi muwuliwa yula ifwa lepi, nambu ajovili, “Ngati nigana asigalila mbaka panibwela yikukuvala kyani?”
Kwa sababu ya maneno haya ya Yesu, uvumi ukaenea miongoni mwa ndugu kwamba huyu mwanafunzi hangekufa. Lakini Yesu hakusema kuwa hangekufa. Yeye alisema tu kwamba, “Ikiwa nataka aishi mpaka nitakaporudi, inakuhusu nini?”
24 Mwenuyu ndi muwuliwa, mwealoli mambu ago na kugayandika. Tete timanyili ajovili chakaka.
Huyu ndiye yule mwanafunzi anayeshuhudia mambo haya na ndiye ambaye ameandika habari hizi. Nasi tunajua ya kuwa ushuhuda wake ni kweli.
25 Gavi mambu gangi gamahele geagahengili Yesu. Ngati goha ngagiyandikwayi, niholela hati mulima woha nakuvya pandu pa kuvika hitabu yeyiyandikwi. Ena.
Lakini kuna mambo mengine mengi ambayo Yesu alifanya. Kama yote yangeliandikwa, nadhani hata ulimwengu wote usingekuwa na nafasi ya kutosha kuweka vitabu vyote ambavyo vingeandikwa. Amen.

< Yohani 21 >