< Yohani 19 >

1 Kangi, Pilatu akalagiza vamtola Yesu na kumtova michapilu.
Ndipo Pilato akamtoa Yesu akaamuru apigwe mijeledi.
2 Vala manjolinjoli vakabota njingwa ya minga, vakamuwalika kumutu, vakamuwalika nyula ya chinkosi langi ya zambalau.
Askari wakasokota taji ya miiba, wakamvika Yesu kichwani. Wakamvalisha joho la zambarau.
3 Vakavya kumbwelela palongolo yaki na kujova, “Tikuwoni, Nkosi wa Vayawudi!” Kuni vakumpamanda.
Wakawa wanapanda pale alipo tena na tena, wakisema, “Salamu! Mfalme wa Wayahudi!” Huku wakimpiga makofi usoni.
4 Pilatu akahuma kuvala kavili, akaujovela msambi wula, “Lola, nikumgotola mundu uyu kwinu, muhotola kumanya kuvya nene nichiwene lepi chindu chochoha cheabudili cha kumuhamula.”
Pilato akatoka tena nje akawaambia wale waliokusanyika, “Tazameni, namkabidhi Yesu kwenu kuwajulisha kwamba mimi sikumwona ana hatia.”
5 Hinu, Yesu, akahuma kuvala kuni awalili njingwa ya minga na nyula ya chinkosi. Pilatu akavajovela, “Mlola! Mundu mwene ndi uyu.”
Kwa hiyo Yesu akatoka nje akiwa amevaa ile taji ya miiba na lile vazi la zambarau. Pilato akawaambia, “Tazameni, huyu hapa huyo mtu!”
6 Vakulu va kuteta na valonda pavamuwene vakayangula. “Mvambayi pamsalaba! Mvambayi pamsalaba!” Pilatu akavajovela. “Mwavene mumtola hinu, mukamvamba muni nene nichiweni lepi chindu cheabudili.”
Wale viongozi wa makuhani na maafisa walipomwona, wakapiga kelele wakisema, “Msulubishe! Msulubishe!” Pilato akawaambia, “Mchukueni ninyi mkamsulubishe, mimi sioni hatia juu yake.”
7 Vayawudi vakamyangula, “Tavete tivii nagu Malagizu, na malagizu gitu gijova, yikumgana afwayi, ndava mwene ajidetekisi kuvya Mwana wa Chapanga.”
Wayahudi wakamjibu, “Sisi tunayo sheria na kutokana na sheria hiyo, hana budi kufa kwa sababu yeye alijiita Mwana wa Mungu.”
8 Pilatu peagayuwini malovi ago, akayogopa neju.
Pilato aliposikia haya, akaogopa zaidi.
9 Kangi Pilatu akayingila munyumba ya unkosi, akamkota Yesu, “Veve uhumili koki?” Nambu Yesu amyangwili lepi chindu.
Akaingia tena ndani ya jumba la kifalme, akamuuliza Yesu, “Wewe umetoka wapi?” Lakini Yesu hakumjibu.
10 Pilatu akamjovela, “Wu, wibela kulongela na nene? Wu, umanyi lepi kuvya nene nihotola kukudindulila na nihotola kulagiza uvambiwa pamsalaba?”
Pilato akamwambia, “Wewe unakataa kuongea na mimi? Hujui ya kuwa nina mamlaka ya kukuachia huru au kukusulubisha?”
11 Yesu akamyangula, “Ngauvi lepi na uhotola panani yangu changali kupewa na Chapanga. Ndava yeniyo yula mweaniletili kwaku ambudili neju.”
Ndipo Yesu akamwambia, “Wewe hungekuwa na mamlaka yoyote juu yangu kama hungepewa kutoka juu. Kwa hiyo yeye aliyenitia mikononi mwako ana hatia ya dhambi iliyo kubwa zaidi.”
12 Kutumbula penapo, Pilatu alonda njila ya kumlekekesa Yesu, nambu Vayawudi vakaywanga. “Ngati umlekekisi mundu uyu, veve nkozi lepi wa nkosi wa ku Loma, mundu yoyoha mweajikita kuvya nkosi akumpinga nkosi mkulu wa Loma!”
Tangu wakati huo, Pilato akajitahidi kutafuta njia ya kumfungua Yesu, lakini Wayahudi wakazidi kupiga kelele wakisema, “Ukimwachia huyu mtu, wewe si rafiki wa Kaisari. Mtu yeyote anayedai kuwa mfalme anampinga Kaisari.”
13 Hinu, Pilatu peayuwini malovi ago akamuhumisa Yesu kuvala, akatama pachigoda cha uhamula, pandu pepikemelewa “Luvanja lwelutengenizwi kwa maganga.” Amala kwa Chiebulania Gabata.
Pilato aliposikia maneno haya akamtoa Yesu nje tena akaketi katika kiti chake cha hukumu, mahali palipoitwa Sakafu ya Jiwe, kwa Kiebrania paliitwa Gabatha
14 Yavi lukumbi lwa muhi, ligono la kutendelekela Pasaka. Pilatu akavajovela Vayawudi, “nkosi winu ndi uyu!”
Basi ilikuwa siku ya Maandalio ya Pasaka, yapata kama saa sita hivi. Pilato akawaambia Wayahudi, “Huyu hapa mfalme wenu!”
15 Vene vakaywanga, “Mkomayi! Mkomayi! Mvambayi pamsalaba?” Pilatu akavakota, “Wu, nimvamba pamsalaba nkosi winu?” Vakulu va kuteta vakayangula, “Tete tivii lepi na nkosi yungi nambu nga nkosi wa ku Loma!”
Wao wakapiga kelele, “Mwondoe! Mwondoe! Msulubishe!” Pilato akawauliza, “Je, nimsulubishe mfalme wenu?” Wale viongozi wa makuhani wakamjibu, “Sisi hatuna mfalme mwingine ila Kaisari.”
16 Hinu, Pilatu akamgotola Yesu mumawoko gavi muni vamvambayi pamsalaba. Manjolinjoli, vakamtola Yesu.
Ndipo Pilato akamkabidhi Yesu kwao ili wamsulubishe. Kwa hiyo askari wakamchukua Yesu.
17 Yesu akahuma kuni agegili msalaba waki, mbaka pandu pepikemelewa “Libangu la Mutu.” Kwa Chiebulania pikemelewa Goligota.
Yesu, akiwa ameubeba msalaba wake, akatoka kuelekea mahali palipoitwa Fuvu la Kichwa (kwa Kiebrania ni Golgotha).
18 Penapo ndi pavamvambili pamsalaba, na pamonga nayu vavavambili pamisalaba yavi vandu vangi vavili mmonga upandi wa kulyela na yungi upandi wa kumangeya, Yesu ndi pagati yavi.
Hapo ndipo walipomsulubisha. Pamoja naye walisulubisha watu wengine wawili, mmoja kila upande wake, naye Yesu katikati.
19 Pilatu akayandika likokoso pachibau akakivika panani ya msalaba, akayandika, “Yesu Mnazaleti Nkosi wa Vayawudi.”
Pilato akaamuru tangazo liandikwe na liwekwe juu kwenye msalaba wa Yesu, likasema: “Yesu wa Nazareti, Mfalme wa Wayahudi.”
20 Hinu, Vayawudi vamahele vasomili likokoso ilo, muni pandu peavambiwi Yesu pamsalaba pavi papipi na muji. Kangi likokoso lenilo layandikwi kwa Chiebulania na Chilatini na Chigiliki.
Kwa kuwa mahali hapo Yesu aliposulubiwa palikuwa karibu na mjini, Wayahudi wengi walisoma maandishi haya yaliyokuwa yameandikwa kwa lugha za Kiebrania, Kiyunani na Kilatini.
21 Hinu, Vakulu va kuteta vakamjovela Pilatu, “Kotoka kuyandika. ‘Nkosi wa Vayawudi,’ Nambu mundu uyu ajovili kuvya, ‘Nene ndi Nkosi wa Vayawudi.’”
Viongozi wa makuhani wa Wayahudi wakapinga, wakamwambia Pilato, “Usiandike ‘Mfalme wa Wayahudi,’ bali andika kwamba mtu huyu alisema yeye ni mfalme wa Wayahudi.”
22 Pilatu akayangula, “Geniyandiki gala nimali, kuyandika!”
Pilato akawajibu, “Nilichokwisha kuandika, nimeandika!”
23 Manjolinjoli pevamali kumvamba Yesu pamsalaba, vakazitola nyula zaki, vakavika malundu mcheche, kila mmonga na lilundu laki. Mewawa vakatola na lijoho laki la unkosi, lijoho ilo labotiwi kwa chipandi chimonga ndu, changali kutotewa.
Askari walipokwisha kumsulubisha Yesu, walichukua nguo zake wakazigawa mafungu manne, kila askari fungu lake. Ila walikubaliana wasilichane lile vazi lake kwa maana lilikuwa halina mshono bali limefumwa tangu juu hadi chini.
24 Manjolinjoli vala, vakajovesana. “Tikotoka kuyipapula, muni titova kula yati livya la yani.” Lijambu lenili lahengiki muni Mayandiku Gamsopi gegijova, “Vagavini nyula zangu, Na nyula yangu vakayitovela kula.” Ndi, chevahengili vala manjolinjoli.
Wakaambiana, “Tusilichane ila tulipigie kura ili kuamua ni nani atalichukua.” Hili lilitukia ili Maandiko yapate kutimizwa yale yaliyosema, “Wanagawana nguo zangu, na vazi langu wanalipigia kura.” Hayo ndiyo waliyoyafanya wale askari.
25 Papipi na msalaba wa Yesu vayimili nyina waki Yesu, na mlumbu wa nyina waki na Maliya mdala wa Kileopa, na Maliya Magidala.
Wakati huo huo karibu na msalaba wa Yesu walikuwa wamesimama mama yake, na dada wa mamaye, na Maria mke wa Klopa, na Maria Magdalene.
26 Yesu peamuwene nyina waki, na papipi yaki ayimili muwuliwa yula mweamganili, akamjovela nyina waki. “Mau, Lola, mwenuyo ndi mwana waku.”
Yesu alipomwona mama yake mahali pale pamoja na yule mwanafunzi aliyempenda wamesimama karibu, akamwambia mama yake, “Mwanamke, huyo hapo ndiye mwanao,”
27 Kangi akamjovela muwuliwa yula. “Lola, mwenuyo ndi nyina waku.” Na kutumbula lukumbi lula muwuliwa yula akamtola atama kunyumba yaki.
kisha akamwambia yule mwanafunzi, “Nawe huyo hapo ndiye mama yako.” Tangu wakati huo yule mwanafunzi akamchukua mama yake Yesu nyumbani kwake.
28 Yesu amanyili kuvya goha gamali kutimila, muni Mayandiku Gamsopi gatimilayi, akajova, “Niyuana njota.”
Baada ya haya, Yesu hali akijua kuwa mambo yote yamemalizika, alisema ili kutimiza Maandiko, “Naona kiu.”
29 Penapo pavi na nkele weumemili divayi yivavanu. Hinu vakajwiga litonji mudivayi yivavanu vakavika mulungoda lwa mkongo weukemiwa hisopo, vakamvikila pamlomo.
Hapo palikuwa na bakuli lililojaa siki. Kwa hiyo wakachovya sifongo kwenye hiyo siki, wakaiweka kwenye ufito wa mti wa hisopo, wakampelekea mdomoni.
30 Yesu peamali kupewa divayi yivavanu yila, akajova, “Goha gatimili!” Kangi akagundama mutu, akafwa.
Baada ya kuionja hiyo siki, Yesu akasema, “Imekwisha.” Akainamisha kichwa chake, akaitoa roho yake.
31 Yavi ijumaa, ligono la kutendelekeha. Ndava muni, higa yikoto kutama pamsalaba Ligono la Kupumulila, muni ligono ilo lavi likulu kwa Vayawudi. Hinu vachilongosi va Vayawudi vakamuyupa Pilatu, magendelu ga vala vevavambiwi pamsalaba gadenyewayi na higa zavi ziwusiwayi.
Kwa kuwa ilikuwa siku ya Maandalio ya Pasaka, Wayahudi hawakutaka miili ibaki msalabani siku ya Sabato, hasa kwa kuwa hiyo Sabato ingekuwa Sikukuu. Wakamwomba Pilato aamuru miguu ya wale waliosulubiwa ivunjwe ili wafe haraka miili iondolewe kwenye misalaba.
32 Manjolinjoli vakahamba, vakayidenya magendelu ga mundu wa upandi wa kumangeya na yula wa upandi wa kulyela vevavambiwi pamisalaba pamonga na Yesu vala.
Kwa hiyo askari wakaenda wakavunja miguu ya mtu wa kwanza aliyesulubiwa pamoja na Yesu na yule mwingine pia.
33 Nambu pavamhikili Yesu vamkoli amali kufwa, ndi vamdenyili lepi magendelu.
Lakini walipomkaribia Yesu, wakaona ya kuwa amekwisha kufa, hivyo hawakuvunja miguu yake.
34 Nambu mmonga wavi amuhomili Yesu muluvafu na mgoha, bahapo yikahuma ngasi na manji.
Badala yake mmoja wa wale askari akamchoma mkuki ubavuni na mara pakatoka damu na maji.
35 Mwene yula mwealoli lijambu lenilo, alijovili muni na nyenye musadika. Na aga geajovili ndi uchakaka, kavili mwene imanya kuvya ijova chakaka.
Mtu aliyeona mambo hayo ndiye alitoa ushuhuda, nao ushuhuda wake ni kweli. Anajua kuwa anasema kweli, naye anashuhudia ili pia nanyi mpate kuamini.
36 Lijambu lenili lahengiki muni Mayandiku Gamsopi gatimila. “Kawaka hati lijege laki limonga lelidenyewa.”
Kwa maana mambo haya yalitukia ili Maandiko yapate kutimia, yale yasemayo, “Hakuna hata mfupa wake mmoja utakaovunjwa.”
37 Mewawa Mayandiku Gamsopi gijova. “Vakumlola yula mwevamuhomili.”
Tena Andiko lingine lasema, “Watamtazama yeye waliyemchoma.”
38 Pagamaliki genago, Yosefu mkolonjinji wa Alimatei, akamuyupa Pilatu kuyihulusa higa ya Yesu kuhuma pamsalaba. Yosefu avi mulanda waki Yesu, nambu chamfiyu, muni ayogwipi vachilongosi wa Vayawudi. Ndi Pilatu akamyidakila, Yosefu ahambili kuyiwusa higa ya Yesu.
Baada ya mambo haya, Yosefu wa Arimathaya, aliyekuwa mfuasi wa Yesu, ingawa kwa siri kwa sababu ya kuwaogopa Wayahudi, alimwomba Pilato ruhusa ili kuuchukua mwili wa Yesu. Pilato alimruhusu, hivyo akaja, akauchukua.
39 Yosefu alongosini na Nikodemu, mweamuhambili Yesu kimihi, akabwela agegili mahuta gegikemelewa manemane gegahangisini na ubani vibaba selasini.
Naye Nikodemo, yule ambaye kwanza alimwendea Yesu usiku, akaja, akaleta mchanganyiko wa manemane na manukato, yenye uzito wa zaidi ya kilo thelathini
40 Hinu voha vavili vakayitola higa ya Yesu, na kuyitindisila nyula ya msopi pamonga na mahuta ago ngati cheyavili mivelu ya Vayawudi pakuvika higa mulitinda.
Wakauchukua mwili wa Yesu, wakaufunga katika sanda ya kitani safi pamoja na yale manukato, kama ilivyokuwa desturi ya Wayahudi.
41 Pandu pala pevamvambili Yesu pamsalaba, pavi na lidimba palidimba lenilo pavi na litinda la mupya lelavi lakona kumvika mundu yoyoha mugati yaki.
Basi palikuwa na bustani karibu na mahali pale aliposulubiwa, na pale ndani ya ile bustani palikuwa na kaburi jipya, ambalo halikuwa limezikiwa mtu bado.
42 Ndava ya mahengu ga Vayawudi ga kutendelekeha Ligono la Kupumulila, ndava litinda lenilo lavi papipi vakamuvika Yesu mwenumo.
Kwa hiyo, kwa kuwa ilikuwa siku ya Wayahudi ya Maandalio, nalo kaburi hilo lilikuwa karibu, wakamzika Yesu humo.

< Yohani 19 >