< Matendu 7 >

1 Kangi, Mteta Mkulu akamkota, “Wu, mambu genaga ndi chakaka?”
Ndipo kuhani mkuu akamuuliza Stefano, “Je, mashtaka haya ni ya kweli?”
2 Mwene akayangula, “Valongo vangu na vadadi vangu, muniyuwanila! Chapanga amuhumalili gogo witu Ibulahimu peavili ku Mesopotamia kwakona kuhamila ku Halani.
Stefano akajibu, “Ndugu zangu na baba zangu, nisikilizeni! Mungu wa utukufu alimtokea baba yetu Abrahamu, alipokuwa bado yuko Mesopotamia, kabla hajaishi Harani,
3 Chapanga akamjovela, ‘Wuka pamulima waku, valeka valongo vaku, ndi uhamba pamulima wenikulangisa.’
akamwambia, ‘Ondoka kutoka nchi yako na kutoka kwa jamii yako, uende hadi nchi nitakayokuonyesha.’
4 Hinu, Ibulahimu ahamalili kumulima wa Kalidayo akahamba kutama ku Halani. Dadi waki peamali kufwa, Chapanga akamuwusa kavili ku Halani akabwela kutama pamulima uwu wemwitama hinu.
“Hivyo aliondoka katika nchi ya Wakaldayo akaenda kukaa Harani. Baada ya kifo cha baba yake, Mungu akamtoa huko akamleta katika nchi hii ambayo mnaishi sasa.
5 Chapanga nakumpela hati pandu padebe pamulima pavyaa uhali waki, nambu amlagizi akumpela mulima wenuwu uvyaa waki, na chiveleku chaki. Lukumbi lwenulo avi lepi na mwana.
Mungu hakumpa urithi wowote katika nchi hii, hakumpa hata mahali pa kuweka wayo mmoja. Bali Mungu alimwahidi kuwa yeye na uzao wake baada yake wangeirithi hii nchi, ingawa wakati huo Abrahamu hakuwa na mtoto.
6 Chapanga akamjovela, ‘Viveleku vyaku yati vipelekwa kumulima wa vandu vangi, kwenuko ndi yati vivya vavanda na kuhengewa uhakau mulukumbi lwa miyaka miya mcheche.
Mungu akasema naye hivi: ‘Wazao wako watakuwa wageni kwenye nchi ambayo si yao, nao watafanywa watumwa na kuteswa kwa miaka mia nne.’
7 Nambu nene yati nikuvahamula vandu avo, vevavahengili uvanda. Kangi yati nikuvawusa mumulima wenuwo muni vabwela penapa kunifugamila pandu apa.’
Mungu akasema, ‘Lakini mimi nitaliadhibu taifa watakalolitumikia kama watumwa, na baadaye watatoka katika nchi hiyo na wataniabudu mahali hapa.’
8 Kangi Chapanga akampela lilaganu la jandu, Ibulahimu akamyingisa jandu mwana waki Izaki mu ligono la nane, kuhuma kuvelekewa. Mewawa Izaki akamdumula jandu Yakobo, namwene Yakobo mewawa akavakitila vagogo kumi na vavili.”
Ndipo akampa Abrahamu Agano la tohara. Naye Abrahamu akamzaa Isaki na kumtahiri siku ya nane. Baadaye Isaki akamzaa Yakobo, naye Yakobo akawazaa wale wazee wetu kumi na wawili.
9 “Vagogo vala vavi na wihu kwa Yosefu ndi vakamgulisa kuuvanda ku Misili. Nambu Chapanga avi pamonga nayu,
“Kwa sababu wazee wetu walimwonea wivu Yosefu ndugu yao, walimuuza kama mtumwa huko Misri. Lakini Mungu alikuwa pamoja naye.
10 akamsangula mu mang'ahiso gaki goha, Chapanga akamganisa na luhala palongolo ya Falao, nkosi wa ku Misili, hati Falao akamhagula kuvya chilongosi wa mulima wula na nyumba ya nkosi.
Akamwokoa kutoka mateso yote yaliyompata, tena akampa kibali na hekima aliposimama mbele ya Farao, mfalme wa Misri, ambaye alimweka kuwa mtawala juu ya Misri na juu ya jumba lote la kifalme.
11 Kangi yikahumila njala yikulu, pamulima woha wa ku Misili na ku Kanani, yikaleta ungangu uvaha. Vagogo vitu vahotwili lepi kupata chakulya chochoha.
“Basi kukawa na njaa katika nchi yote ya Misri na Kanaani, ikasababisha dhiki kubwa, nao baba zetu wakawa hawana chakula.
12 Hinu, Yakobo peayuwini kuvya ku Misili kula kuvi na mabenu, akavatuma vana vaki, ndi vagogo vitu vahamba kwenuko yavi mala ya kutumbula.
Lakini Yakobo aliposikia kwamba kuna nafaka huko Misri, aliwatuma baba zetu, wakaenda huko kwa mara yao ya kwanza.
13 Mulugendu lwavi lwa pili, Yosefu akajimanyisa kwa valongo vaki, ndi Falao akavamanya valongo va Yosefu.
Walipokwenda mara ya pili, Yosefu alijitambulisha kwa ndugu zake, nao ndugu zake Yosefu wakajulishwa kwa Farao.
14 Yosefu atumili ujumbi kwa dadi waki na valongo vaki, vandu sabini na mhanu, vabwela ku Misili.
Ndipo Yosefu akawatuma kumleta Yakobo baba yake pamoja na jamaa yake yote, jumla yao walikuwa watu sabini na watano.
15 Hinu, Yakobo ahambili ku Misili, kwenuko mwene pamonga na vagogo vitu vafwili.
Hivyo Yakobo akaenda Misri ambako yeye na baba zetu walifia.
16 Higa zavi zaletiwi mbaka ku Shekemu, zikazikiwa mu litinda la mbugu leagulili Ibulahimu kuhuma kwa vana va Hamoli kwa mashonga nunuyu.”
Miili yao ilirudishwa Shekemu na kuzikwa katika kaburi ambalo Abrahamu alinunua kutoka kwa wana wa Hamori kwa kiasi fulani cha fedha.
17 “Lukumbi palwahikili Chapanga atimilisa lilaganu leajovili akumpela Ibulahimu, ku Misili kula vandu vayonjokisi na kuvya vamahele neju.
“Lakini wakati ulipokuwa unakaribia wa kutimizwa kwa ile ahadi ambayo Mungu alikuwa amempa Abrahamu, watu wetu walizidi kuongezeka sana huko Misri.
18 Pamwishu, nkosi mmonga mweanga mmanya Yosefu, akatumbula kulongosa kula ku Misili.
Ndipo mfalme mwingine ambaye hakujua lolote kuhusu Yosefu akatawala Misri.
19 Mwenuyu avakitili uhakau vandu vitu na vagogo vitu changali kugana vene vavavika kuvala vana vavi vadebe muni vafwayi.
Huyu mfalme akawatendea watu wetu hila na kuwatesa baba zetu kwa kuwalazimisha wawatupe watoto wao wachanga ili wafe.
20 Musa avelekiwi lukumbi lwenulo, avili mwana mbwina neju palongolo ya Chapanga. Aleliwi panyumba mulukumbi lwa miyehi yidatu,
“Wakati huo Mose alizaliwa, naye hakuwa mtoto wa kawaida. Akalelewa nyumbani kwa baba yake kwa muda wa miezi mitatu.
21 na peaumiswi kuvala, ndi msikana wa Falao akamtola na kumlela ngati mwana waki mwene.
Waliposhindwa kumficha zaidi, wakamweka nje mtoni na binti Farao akamchukua akamtunza kama mtoto wake mwenyewe.
22 Musa awuliwi mambu goha galuhala ga Vamisili akavya mkekesi kwa malovi na matendu.”
Mose akafundishwa hekima yote ya Wamisri, akawa mtu hodari kwa maneno na matendo.
23 “Hinu Musa peahikisi miyaka alobaini ndi akahamba kuvagendela kuvalola va Isilaeli vayaki.
“Mose alipokuwa na umri wa miaka arobaini aliamua kuwatembelea ndugu zake Waisraeli.
24 Kwenuko amuwene mmonga wa valongo vaki ihengewa uhakau, ndi akahamba kumkengelela, ndi akamkoma Mmisili yula.
Aliona mmoja wao akidhulumiwa na Mmisri, akamtetea yule aliyeonewa, akampiga yule Mmisri akamuua kulipiza kisasi.
25 Aholalili manya Vaisilaeli vayaki yati vimanya kuvya Chapanga ngaamtumili mwene kuvagombola, nambu vene nakugamanya ago.
Mose alidhani kuwa ndugu zake wangetambua kwamba Mungu anamtumia ili kuwaokoa, lakini wao hawakuelewa.
26 Chilalu yaki Musa avawene Vaisilaeli vavili vitovana, akalinga kuvatepulanisa akavajovela, ‘Nyenye mwavalongo ndava kyani hinu, mukomana mwavene?’
Siku iliyofuata Mose aliwakuta Waisraeli wawili wakigombana, akajaribu kuwapatanisha kwa kuwaambia, ‘Enyi watu, ninyi ni ndugu, mbona mnataka kudhulumiana?’
27 Nambu yungi mweamtovayi yula muyaki akamkang'a Musa pamuhana akajova, ‘Yani mweakuvikili veve kuvya chilongosi na mhamula pagati yitu?
“Lakini yule mtu aliyekuwa akimdhulumu mwenzake akamsukuma Mose kando, akamuuliza, ‘Ni nani aliyekufanya mtawala na mwamuzi juu yetu?
28 Wu, ugana kunikoma ngati chewamkomili Mmisili golo?’
Je, unataka kuniua kama ulivyomuua yule Mmisri jana?’
29 Musa peagayuwini malovi ago, akatila na kuhamba kutama kumulima wa Midiani kwenuko akavya myehe ndi akavya na vana vasongolo vavili.”
Mose aliposikia maneno haya, alikimbilia huko Midiani alikokaa kama mgeni, naye akapata watoto wawili wa kiume.
30 “Peyahikili miyaka alobaini, mtumu wa kunani kwa Chapanga akamhumila Musa padahi pepiyaka motu kulugangatu papipi na Chitumbi cha Sinai.
“Basi baada ya miaka arobaini kupita, malaika wa Mungu akamtokea Mose jangwani karibu na Mlima Sinai katika kichaka kilichokuwa kinawaka moto.
31 Musa akakangasa kulola lijambu lenilo hati akahegelela papipi muni alingulila, ndi akayuwana lwami lwa Bambu.
Alipoona mambo haya, alishangaa yale maono. Aliposogea ili aangalie kwa karibu, akaisikia sauti ya Bwana, ikisema:
32 ‘Nene ndi Chapanga wa vagogo vaku, Chapanga wa Ibulahimu wa Izaki na Yakobo.’ Musa akavagaya kwa wogohi ndi nakuhotola kulolokesa neju.
‘Mimi ndimi Mungu wa baba zako, Mungu wa Abrahamu, Isaki na Yakobo.’ Mose alitetemeka kwa hofu na hakuthubutu kutazama.
33 Bambu akamjovela, ‘Hula champali zaku muni peuyima apa ndi pandu pamsopi.
“Ndipo Bwana akamwambia, ‘Vua viatu vyako kwa maana mahali unaposimama ni patakatifu.
34 Nigawene mahakau gevihengiwa vandu vangu ku Misili kula. Niyuwini lwami lwa mang'ahiso gavi, ndi nene nibweli kuvagombola. Hinu bwela, yati nikukutuma ku Misili.’”
Hakika nimeona mateso ya watu wangu huko Misri. Nimesikia kilio chao cha uchungu, nami nimeshuka ili niwaokoe. Basi sasa njoo, nami nitakutuma Misri.’
35 “Musa mwenuyu ndi yula mweabeleliwi na vandu va Isilaeli pavamjovili, ‘Yani mweakuvikili kuvya chilongosi na mhamula pagati yitu?’ Chapanga amtumili Musa kuvya chilongosi na mgombozi, kwa njila ya mtumu wa kunani kwa Chapanga mweamhumalili padahi pepiyaka motu.
“Huyu ndiye Mose yule waliyemkataa wakisema, ‘Ni nani aliyekufanya mtawala na mwamuzi juu yetu?’ Alikuwa ametumwa na Mungu mwenyewe kuwa mtawala na mkombozi wao, kwa njia ya yule malaika aliyemtokea katika kile kichaka.
36 Ndi mweavalongwisi vandu vala vawuka ku Misili kwa kuhenga ulangisu wa gachinamtiti na makangaso pamulima wa Misili na Kunyanja ya Shamu na kulugangatu, mulukumbi lwa miyaka alobaini.
Aliwaongoza wana wa Israeli kutoka Misri, baada ya kufanya ishara na maajabu mengi huko Misri, katika Bahari ya Shamu, na katika jangwa kwa muda wa miaka arobaini.
37 Musa ndi mweavajovili vandu va Isilaeli, ‘Chapanga yati akuvahagulila mlota waki ngati nene pagati ya valongo vinu mwavene.’
“Huyu ndiye yule Mose aliyewaambia Waisraeli, ‘Mungu atawainulia nabii kama mimi kutoka miongoni mwa ndugu zenu wenyewe.’
38 Mwene ndi mweavili kulugangatu kula, pevakonganiki vandu va Isilaeli. Musa avili ngati mjumbi pagati ya vagogo vitu, na mtumu wa kunani kwa Chapanga, lukumbi pealongili nayu kuchitumbi cha Sinai ndi mweagotoliwi malovi ga wumi atijovela tete.”
Huyu ndiye yule Mose aliyekuwa katika kusanyiko huko jangwani, ambaye malaika alisema naye pamoja na baba zetu kwenye Mlima Sinai, naye akapokea maneno yaliyo hai ili atupatie.
39 “Nambu vagogo vitu ndi vabelili kumyidakila, ndi vakamkang'a pamuhana kuni mumitima yavi vakanogela kuwuya ku Misili.
“Lakini baba zetu walikataa kumtii Mose, badala yake wakamkataa na kuielekeza mioyo yao Misri tena.
40 Vakamjovela mlongo wa Musa Aloni, ‘Utikitila vachapanga yeyikutulongosa munjila, muni nakumanya chechimkolili Musa mweatilongwisi kuhuma ku Misili!’
Wakamwambia Aroni, ‘Tufanyie miungu watakaotuongoza, kwa maana mtu huyu Mose aliyetutoa nchi ya Misri, hatujui yaliyompata.’
41 Penapo ndi pavajikitili chimong'omong'o cha mpapakasi wa ng'ombi, vakayitetela na vakakita mselebuko ndava ya lihengu la mawoko gavi vene.
Huu ni ule wakati walitengeneza sanamu katika umbo la ndama, wakailetea sadaka kufanya maadhimisho kwa ajili ya kile kitu walichokitengeneza kwa mikono yao wenyewe.
42 Nambu Chapanga akawuka pagati yavi na kuvaleka vazifugundamila ndondo za kunani, ngati cheyiyandikwi muhitabu ya vamlota va Chapanga. ‘Nyenye vandu va Isilaeli! Lepi nene mwemwanihinjili hinyama ndava ya luteta, Mumiyaka alobaini kulugangatu kula!
Ndipo Mungu akageuka, akawaacha waabudu jeshi lote la mbinguni, kama ilivyoandikwa katika Kitabu cha Manabii: “‘Je, mliniletea dhabihu na sadaka kwa miaka arobaini kule jangwani, ee nyumba ya Israeli?
43 Nyenye mwagegili chindanda cha chapanga Moloki, na vindu vyemwajikitili kwa luhumu lwa ndondo ya chapanga winu Lefani. Vindu vyemwajikitili ndi vyemwavifugamili. Ndava ya yeniyo yati nikuvapeleka uvanda kutali na Babeli.’
La, ninyi mliinua madhabahu ya Moleki, na nyota ya mungu wenu Refani, vinyago mlivyotengeneza ili kuviabudu. Kwa hiyo nitawapeleka mbali’ kuliko Babeli.
44 Kulugangatu kula vagogo vitu vavi na lindanda la kulangisa, lakitiwi ngati Chapanga cheamlagazili Musa ahengayi, ulangisu wulawula ngati weauwene.
“Baba zetu walikuwa na lile Hema la Ushuhuda huko jangwani. Lilikuwa limetengenezwa kama Mungu alivyokuwa amemwelekeza Mose, kulingana na kielelezo alichoona.
45 Kangi Vagogo vitu vahalilini lindanda vene kwa vene mbaka lukumbi lwa Yoshua, pevatolili mulima wula kuhuma kwa milima, Chapanga mweavingili palongolo yavi. Penapo ndi latamili mbaka lusenje lwa Daudi.
Baba zetu wakiisha kulipokea hema kwa kupokezana wakiongozwa na Yoshua katika milki ya nchi kutoka kwa yale mataifa ambayo Mungu aliyafukuza mbele yao, nalo likadumu katika nchi mpaka wakati wa Daudi,
46 Daudi apewili uganu na Chapanga, akamuyupa ayidakila amujengela pandu pa kutama, mwene mweavi Chapanga wa Yakobo.
ambaye alipata kibali kwa Mungu, naye akaomba kwamba ampatie Mungu wa Yakobo maskani.
47 Nambu Solomoni ndi mweamjengili Chapanga nyumba.”
Lakini alikuwa Solomoni ndiye alimjengea Mungu nyumba.
48 “Nambu Chapanga Mkulu, itama lepi munyumba zezijengiwi na vandu ngati cheajovili mlota wa Chapanga,
“Hata hivyo, Yeye Aliye Juu Sana hakai kwenye nyumba zilizojengwa kwa mikono ya wanadamu. Kama nabii alivyosema:
49 ‘Bambu ijova, kunani ndi chigoda changu cha unkosi, na mulima ndi chigoda cha kuvikila magendelu gangu. Nyumba ya namuna yoki yemukunijengela nene? Ndi pandu poki penipumulila?
“‘Mbingu ni kiti changu cha enzi, nayo dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu. Mtanijengea nyumba ya namna gani? asema Bwana. Au mahali pangu pa kupumzikia patakuwa wapi?
50 Namwene ndi mwenihengili vindu vyoha?’”
Je, mkono wangu haukufanya vitu hivi vyote?’
51 “Nyenye vandu mwemwinonopa, mitima na makutu ginu ndi ngati vandu va milima yangamulanda Chapanga. Nyenye ngati vagogo vinu. Magono goha mukumbela Mpungu Msopi.
“Enyi watu wenye shingo ngumu, msiotahiriwa mioyo wala masikio, daima hamwachi kumpinga Roho Mtakatifu, kama walivyofanya baba zenu.
52 Vagogo vinu vamng'aisi mlota wa Chapanga yeyoha yula, vevavakomili avo, Chapanga avatumili kukokosa kubwela kwa yula mweikita geigana Chapanga. Nambu nyenye mwamgewukili na kumkoma.
Je, kuna nabii gani ambaye baba zenu hawakumtesa? Waliwaua wale waliotabiri habari za kuja kwake yule Mwenye Haki. Nanyi sasa mmekuwa wasaliti wake na wauaji.
53 Nyenye mwapokili malagizu gala gegaletiwi na mtumu wa kunani kwa Chapanga, nambu mwayidakili lepi.”
Ninyi ndio mlipokea sheria zilizoletwa kwenu na malaika, lakini hamkuzitii.”
54 Vala vagogo va libanji pavamuyuwanili Stefani, vakaviniswa mitima, ndi vakajiluma minu cha ligoga.
Waliposikia haya wakaghadhibika, wakamsagia meno.
55 Nambu Stefani kuni amemiswi Mpungu Msopi, akalolokesa kunani kwa Chapanga, auwene ukulu wa Chapanga na Yesu ayimili muchiwoko cha kulyela cha Chapanga.
Lakini yeye Stefano, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alikaza macho mbinguni, akaona utukufu wa Mungu, na Yesu akiwa amesimama mkono wa kuume wa Mungu.
56 Stefani akajova, “Mlola! Niwona kunani kwa Chapanga kudindwiki na Mwana wa Mundu ayimili pachiwoko cha kulyela cha Chapanga!”
Akasema, “Tazameni! Naona mbingu zimefunguka, na Mwana wa Adamu amesimama upande wa kuume wa Mungu.”
57 Vakulu va libanji, vakaywanga na vakagubika makutu gavi kwa mawoko. Kangi vakamuhumbila voha kwa pamonga.
Lakini wao wakapiga kelele kwa sauti kubwa, wakaziba masikio yao, wakamrukia kwa nia moja.
58 Vakamkwekwesa kuvala ya muji, na kutumbula kumtova na maganga, vevavawene vakagavika makoti gavi paulonda wa msongolo mmonga liina laki Sauli.
Wakamtupa nje ya mji, wakampiga kwa mawe. Nao mashahidi wakaweka mavazi yao miguuni mwa kijana mmoja ambaye jina lake aliitwa Sauli.
59 Pevayendalili kumtova na maganga Stefani kuni mwene iyupa kwa Chapanga, “Bambu Yesu upokela mpungu wangu!”
Walipokuwa wakimpiga mawe, Stefano aliomba, “Bwana Yesu, pokea roho yangu.”
60 Akafugama, akavemba kwa lwami luvaha, “Bambu, ukotoka kuvavalangila chevakubudila Chapanga!” Peamalili kujova ago, akafwa. Sauli ayidakili chitendu cha ukomaji wenuwo.
Kisha akapiga magoti, akalia kwa sauti kubwa akasema, “Bwana usiwahesabie dhambi hii.” Baada ya kusema hayo, akalala.

< Matendu 7 >