< Matendu 21 >

1 Patamali kulagana nawu, tayingili muwatu na kuhamba lumonga mbaka Kosi. Chilau yaki tahikili kumuji wa Lode, na patahumili kwenuko tikahamba kumuji wa Patala.
Tulipokwisha kujitenga nao, tukaanza safari kwa njia ya bahari moja kwa moja mpaka Kosi. Siku ya pili yake tukafika Rodo na kutoka huko tukaenda Patara.
2 Kula taukolili watu wewihamba mbaka ku Foinike, ndi tikayingila na kuyendelela lugendu.
Hapo tukapata meli iliyokuwa inavuka kwenda Foinike tukapanda tukasafiri nayo.
3 Ndi patahikili pandu patahotwili kulola Kuplo, tikahamba upandi wa kusini mbaka Silia. Tikahamba kuyima ku Tilo ndi pandu pa watu wula payahulusayi ndwika.
Tulipokiona kisiwa cha Kipro, tukakizunguka tukakiacha upande wetu wa kushoto, tukasafiri mpaka Shamu, tukatia nanga katika bandari ya Tiro ambapo meli yetu ilikuwa ipakue shehena yake.
4 Kwenuko tavakoli vamsadika, tatamili nawu mulukumbi lwa lijuma limonga. Vamsadika venavo vakavya vilongela mukulongoswa na Mpungu Msopi, vakamjovela Pauli akotoka kuhamba ku Yelusalemu.
Baada ya kuwatafuta wanafunzi wa huko, tukakaa nao kwa siku saba. Wale wanafunzi wakiongozwa na Roho wakamwambia Paulo asiende Yerusalemu.
5 Nambu lukumbi lwitu palwamaliki tavoha tawukili. Vawuliwa pamonga na vadala na vana vavi vatihindikili mbaka kuvala ya muji. Patahikili kumbwani tavoha tikafugama na kumuyupa Chapanga.
Lakini muda wetu ulipokwisha, tukaondoka tukaendelea na safari yetu. Wale wanafunzi pamoja na wake zao na watoto wakatusindikiza hadi nje ya mji. Wote tukapiga magoti pale pwani tukaomba.
6 Kangi patamali kulagana nawu, tayingili muwatu na vene vakawuya kunyumba zavi.
Baada ya kuagana, tukapanda melini, nao wakarudi majumbani mwao.
7 Tete tayendalili na lugendu lwitu tahumili ku Tilo na kuhamba Tolemai kwetavajambwisi valongo vitu, tatamili nawu ligono limonga.
Tukaendelea na safari yetu toka Tiro tukafika Tolemai, tukawasalimu ndugu wa huko, tukakaa nao kwa siku moja.
8 Chilau yaki tahumili penapo na kuhamba Kaisalia. Kwenuko tikatama kunyumba ya Filipi mkokosa wa Lilovi la Bwina. Mwene ndi avi mmonga wa vamtangatila saba vevahaguliwi ku Yelusalemu kula.
Siku iliyofuata tukaondoka, tukafika Kaisaria. Huko tukaenda nyumbani kwa mwinjilisti mmoja jina lake Filipo, aliyekuwa mmoja wa wale Saba, tukakaa kwake.
9 Mwenuyu avi na vakamwali mcheche vevavi na chipanji cha kulota malovi ga Chapanga.
Filipo alikuwa na binti wanne mabikira waliokuwa wanatoa unabii.
10 Patatamili kwenuko magono gamahele, mlota mmonga wa Chapanga liina laki Agabo ahikili kuhuma ku Yudea.
Baada ya kukaa kwa siku kadhaa, akateremka nabii mmoja kutoka Uyahudi jina lake Agabo.
11 Ndi atibwelili, akatola mkungi wa Pauli akajikunga mawoko na magendelu, akajova, “Mpungu Msopi ajovili aga, ‘Vayawudi va ku Yelusalemu kula yati vakumkunga mewa mundu mweavi na mkungi uwu na kumgotola kwa vandu vangali Vayawudi.’”
Alipotufikia akachukua mshipi wa Paulo akajifunga, akautumia kufunga mikono na miguu yake mwenyewe akasema, “Roho Mtakatifu anasema: ‘Hivi ndivyo Wayahudi wa Yerusalemu watakavyomfunga mwenye mshipi huu na kumkabidhi kwa watu wa Mataifa.’”
12 Patayuwini genago, tete pamonga na vandu vangi vevavi penapo, tamuyupili Pauli akotoka kuhamba ku Yelusalemu.
Tuliposikia maneno haya sisi na ndugu wengine tukamsihi Paulo asiende Yerusalemu.
13 Nambu Pauli avayangwili, “Ndava kyani mwivemba? Na kunidenya mtima? Nijitendelekili, lepi ndava ya kukungiwa ndu ku Yelusalemu, nambu hati mewawa kufwa ndava ya liina la Bambu Yesu.”
Lakini Paulo akajibu, “Kwa nini mnalia na kunivunja moyo? Mimi niko tayari si kufungwa tu, bali hata kufa huko Yerusalemu kwa ajili ya jina la Bwana Yesu.”
14 Peabeli getamjovili tagunii tikajova, “Maganu ga Bambu gahengekayi!”
Alipokuwa hashawishiki, tukaacha kumsihi, tukasema, “Mapenzi ya Bwana na yatendeke.”
15 Patamali kutama mulukumbi, ndi takungili ndwika yitu, tayendalili na lugendu kuhamba ku Yelusalemu.
Baada ya haya, tukajiandaa, tukaondoka kwenda Yerusalemu.
16 Vamsadika nunuyu va ku Kaisalia valongosini na tete, vatipeliki kunyumba ya mundu mmonga liina laki Mnasoni, ndi mwetahambayi kutama kwa lukumbi. Mwenuyo avi mkolonjinji wa muji wa Kuplo, msadika wa kadeni.
Baadhi ya wanafunzi kutoka Kaisaria wakafuatana nasi na kutupeleka nyumbani kwa Mnasoni, ambaye tungekaa kwake. Yeye alikuwa mtu wa Kipro, mmoja wa wanafunzi wa zamani.
17 Hinu patahikili ku Yelusalemu, vamsadika vayitu vatipokili kwa luheku.
Tulipofika Yerusalemu ndugu wakatukaribisha kwa furaha.
18 Chilau yaki Pauli pamonga na tete tahambili kumjambusa Yakobo na vagogo voha va msambi wa vandu vevakumsadika Kilisitu.
Kesho yake Paulo pamoja na wengine wetu tulikwenda kumwona Yakobo, na wazee wote walikuwepo.
19 Patamali kuvajambusa, Pauli avajovili mambu goha Chapanga geagahengili kwa vandu vangalikuvya Vayawudi munjila ya lihengu laki.
Baada ya kuwasalimu, Paulo akatoa taarifa kamili ya mambo yote ambayo Mungu alikuwa amefanya miongoni mwa watu wa Mataifa kupitia huduma yake.
20 Ndi pavagayuwini ago, vakamulumba Chapanga. Kangi vakamjovela Pauli, “Mlongo, uhotola kulola kuvya vavi maelufu ga Vayawudi vevavi vamsadika hinu na voha vilanda cha kukangamala malagizu ga Bambu geampeli Musa.
Baada ya kusikia mambo haya wakamwadhimisha Mungu. Ndipo wakamwambia Paulo, “Ndugu, unaona kulivyo na maelfu ya Wayahudi walioamini, nao wote wana juhudi kwa ajili ya sheria.
21 Vayuwini mambu gaku gewiwula Vayawudi vevitama pagati ya vandu vangalikuvya Vayawudi, kuvya vakotoka kulanda malagizu ga Bambu geampeli Musa, vakotoka kuvadumula jandu vana vavi kavili vakotoka kulanda mivelu ya Vayawudi.
Lakini wameambiwa habari zako kwamba unafundisha Wayahudi wote waishio miongoni mwa watu wa Mataifa kumkataa Mose, na kwamba unawaambia wasiwatahiri watoto wao wala kufuata desturi zetu.
22 Hinu tikita wuli? Chakaka yati viyuwana kuvya ubwelili.
Sasa tufanyeje? Bila shaka watasikia kwamba umekuja Yerusalemu.
23 Hinu kitayi ngati chetikujovela, penapa tivii na vagosi mcheche vevaviki chilapu kwa Chapanga.
Kwa hiyo fanya lile tunalokuambia. Tunao watu wanne hapa ambao wameweka nadhiri.
24 Uwungana nawu mukuyupa kunyambiswa, ulipa mashonga gegiganikwa, kangi vaketewayi mayunju gavi. Ndi vandu voha yati vimanya kuvya mambu gala gevayuwini kukuvala veve gangali mana, ndi wamwene wakona witama na kulanda malagizu ga Malagizu ga Musa.
Jiunge na watu hawa, mfanye utaratibu wa ibada ya kujitakasa pamoja nao, na ulipe gharama ili wanyoe nywele zao. Kwa njia hii kila mtu atafahamu ya kuwa mambo waliyosikia si ya kweli na kwamba wewe unaishika sheria.
25 Nambu kuvavala vandu vangalikuvya Vayawudi vevasadiki, tivapelekili balua yetiyandiki mambu getihamwili, vakotoka kulya chindu chochoha chechiwusiwi luteta vachapanga va udese, vakotoka kunywa ngasi, na vakotoka kulya nyama ya hinyama yidodanu, vayepa ukemi.”
Lakini kuhusu wale watu wa Mataifa walioamini, tumewaandikia uamuzi wetu: kwamba wajitenge na vyakula vilivyotolewa sadaka kwa sanamu, na damu, au kula nyama ya mnyama aliyenyongwa, na wajiepushe na uasherati.”
26 Hinu chilau yaki Pauli akavatola vandu vala muni ajinyambisa nawu pamonga, kangi akayingila Munyumba ya Chapanga, na kujova ligono la mwishu la kunyambiswa na luteta lweluwusiwa ndava ya kila mmonga.
Ndipo kesho yake Paulo akawachukua wale watu na akajitakasa pamoja nao. Akaingia ndani ya hekalu ili atoe taarifa ya tarehe ambayo siku zao za utakaso zingemalizika na sadaka ingetolewa kwa ajili ya kila mmoja wao.
27 Hinu magono gala saba pagihegelela kumalika, Vayawudi vevahumili wa Asia vamuwene Pauli Munyumba ya Chapanga. Ndi vakavakohokea ligoga msambi woha wa vandu, ndi vakamkamula.
Zile siku saba zilipokaribia kumalizika, baadhi ya Wayahudi kutoka sehemu za Asia waliokuwa wamemwona Paulo ndani ya Hekalu, wakachochea umati wote wa watu, nao wakamkamata.
28 Vakaywanga, “Vagosi va Isilaeli, mutitangatila! Mundu mwenuyu ndi mweakuvawula vandu kila pandu mambu gegibelana na vandu va Isilaeli, gegibesa malagizu ga Chapanga geampeli Musa na pandu apa Pamsopi. Hati hinu avayingisi vandu vangali Vayawudi Munyumba ya Chapanga na kupahakasa pandu pamsopi.”
Wakapiga kelele wakisema, “Waisraeli wenzetu, tusaidieni! Huyu ndiye yule mtu anayefundisha kila mtu na kila mahali, kinyume na watu wetu, sheria zetu na hata Hekalu hili. Zaidi ya hayo amewaleta Wayunani ndani ya Hekalu na kupanajisi mahali hapa patakatifu.”
29 Vajovili genago ndava vamuwene Tofimo mkolonjinji wa ku Efeso, alongosini na Pauli kumujini, vakaholalela manya Pauli amuyingisi Munyumba ya Chapanga.
(Walikuwa wamemwona Trofimo, mwenyeji wa Efeso, akiwa mjini pamoja na Paulo wakadhani kuwa Paulo alikuwa amemwingiza Hekaluni.)
30 Chitututu chadandasiki muji woha, vandu vakonganiki kuhuma pandi zoha, vakamukamula Pauli, vakamuhuta na kumuhumisa kuvala ya Nyumba ya Chapanga, na bahapo milyangu hikadindwa.
Mji wote ukataharuki, watu wakaja wakikimbia kutoka pande zote wakamkamata Paulo, wakamburuta kutoka Hekaluni. Milango ya Hekalu ikafungwa.
31 Pavalingili kumkoma Pauli, malovi gala gakamhikila mkulu wa msambi wa ku Loma kuvya Yelusalemu yoha yimemili chitututu.
Walipokuwa wakitaka kumuua, habari zikamfikia jemadari wa jeshi la askari wa Kirumi kwamba mji wa Yerusalemu wote ulikuwa katika machafuko.
32 Bahapo mkulu wa msambi akavatola manjolinjoli na vachilongosi wavi, vakavajumbila kuhamba. Vayawudi pavamuwene mkulu wa msambi pamonga na manjolinjoli vakaleka kumtova Pauli.
Mara yule jemadari akachukua maafisa wengine wa jeshi pamoja na askari wakakimbilia kwenye ile ghasia, wale watu waliokuwa wakifanya ghasia walipomwona yule jemadari na askari wakija, wakaacha kumpiga Paulo.
33 Mkulu wa msambi yula akamhegelela Pauli, akamkamula na kulagiza akungiwayi minyololo yivili. Kangi akakota, “Mwenuyu ndi yani? Abudili kyani?”
Yule jemadari akaja, akamkamata Paulo akaamuru afungwe kwa minyororo miwili. Akauliza yeye ni nani, na alikuwa amefanya nini.
34 Vangi mu msambi wula vakavya mukuywanga vangi aga na vangi gala. Ndava ya chitututu, mkulu wa msambi wa manjolinjoli amanyili lepi uchakaka wa mhalu waki. Ndi akahamula vandu vaki vampeleka mugati ya ngomi ya manjolinjoli.
Baadhi ya watu katika ule umati wakapiga kelele, hawa wakisema hili na wengine lile. Yule jemadari alipoona kuwa hawezi kupata hakika ya habari kwa sababu ya zile kelele, akaamuru Paulo apelekwe katika ngome ya jeshi.
35 Pauli pahaikili pangazi, yavaganili manjolinjoli kumgega ndava ya chitututu cha vandu.
Paulo alipofika penye ngazi, ilibidi askari wambebe juu juu kwa sababu fujo za ule umati wa watu zilikuwa kubwa.
36 Ndava muni msambi wa vandu uvaha vamlandili kuni viywanga, “Mkomayi!”
Umati wa watu ulikuwa ukifuata ukiendelea kupiga kelele ukisema, “Mwondoe huyu!”
37 Pavamuyingisa mungomi, Pauli akamuyupa mkulu wa msambi wa manjolinjoli yula, “Nihotola kukujovela chindu?” Mkulu wa msambi wa manjolinjoli akamkota, “Wu, umanya kujova Chigiliki?
Mara tu Paulo alipokaribia kuingizwa kwenye ngome ya jeshi, akamwambia yule jemadari, “Je, naweza kukuambia jambo moja?” Yule jemadari akamjibu, “Je, unajua Kiyunani?
38 Wu, veve ndi Mmisili yula magono gegapitili atumbwili chitututu na kuvalongosa vakomaji elufu mcheche kuhamba kulugangatu?”
Je, wewe si yule Mmisri ambaye siku hizi za karibuni alianzisha uasi akaongoza kundi la magaidi 4,000 wenye silaha jangwani?”
39 Pauli akayangula, “Nene na Myawudi, mkolonjinji wa ku Taso muji wa Kilikia, muji weutopeswa. Chondi niyidakila nilongela na vandu.”
Paulo akajibu, “Mimi ni Myahudi, mzaliwa wa Tarso, huko Kilikia, raiya wa mji maarufu. Tafadhali niruhusu nizungumze na hawa watu.”
40 Mkulu wa msambi wa manjolinjoli yula akamyidakila. Ndi Pauli akayima panani ya ngazi akavapungila vandu chiwoko, muni vaguna, akatumbula kulongela nawu muluga ya Chiebulania.
Akiisha kupata ruhusa ya yule jemadari, Paulo akasimama penye ngazi akawapungia watu mkono ili wanyamaze. Wote waliponyamaza kimya, Paulo akazungumza nao kwa lugha ya Kiebrania, akasema:

< Matendu 21 >