< Matendu 17 >

1 Mulugendu lwavi vakapitila Amfipoli na Apolonia, vakahika ku Tesalonike kwavili na nyumba ya kukonganekela Vayawudi.
Wakasafiri kupitia Amfipoli na Apolonia wakafika Thesalonike, ambako kulikuwa na sinagogi la Wayahudi.
2 Na ngati chayavili mvelu wa Pauli, akayingila mugati mula na kukotana nawu kugavala mu Mayandiku Gamsopi Magono gadatu ga Kupumulila gegagekilini.
Kama desturi yake, Paulo aliingia ndani ya sinagogi, na kwa muda wa Sabato tatu akawa anahojiana nao kutoka kwenye Maandiko,
3 Avadandaulili na kuvalangisa kuvya yikumgana Kilisitu kung'aiswa na kuyuka. Akavajovela, “Yesu mwenikuvakokosela nyenye ndi Kilisitu.”
akidhihirisha wazi na kuthibitisha kwamba ilikuwa lazima Kristo ateswe na afufuke kutoka kwa wafu. Akasema, “Huyu Yesu ninayewaambia habari zake, ndiye Kristo.”
4 Vangi pagati yavi vakasadika na kuvya pamonga na Pauli na Sila. Mewawa Vagiliki vamahele vevakumsadika Chapanga pamonga na vadala vevitopeswa vakavya pamonga.
Baadhi ya Wayahudi wakasadiki, wakaungana na Paulo na Sila, wakiwepo idadi kubwa ya Wayunani waliomcha Mungu na wanawake wengi mashuhuri.
5 Nambu Vayawudi vakavya na wihu, hati vakavakoka valauni va pabomani na kukita msambi na kuhenga chitututu muji woha. Vakaizangila nyumba ya Yasoni vahuvalilayi vihotola kuvapata Pauli na Sila muni vavaleta pavandu.
Lakini Wayahudi ambao hawakuwa wameamini wakawa na wivu, wakawakodi watu waovu kutoka sokoni, wakakutanisha umati wa watu, wakaanzisha ghasia mjini. Wakaenda mbio nyumbani kwa Yasoni wakiwatafuta Paulo na Sila ili kuwaleta nje penye ule umati wa watu.
6 Ndava vavapatili lepi, ndi vakamukwega Yasoni na vamsadika vangi mbaka pavakulu va muji, vakajova kwa lwami luvaha, “Vandu ava ndi vevikita chitututu pamulima woha na hinu vahikili kwitu.
Lakini walipowakosa wakamburuta Yasoni na ndugu wengine mbele ya maafisa wa mji, wakipiga kelele: “Watu hawa ni wale walioupindua ulimwengu wamekuja huku,
7 Yasoni avagongolili kunyumba yaki. Voha vihenga chimumbele na malagizu ga nkosi wa ku Loma, vijova kuvya avi nkosi yungi liina laki Yesu.”
naye Yasoni amewakaribisha nyumbani mwake. Hawa wote wanaasi amri za Kaisari wakisema yuko mfalme mwingine aitwaye Yesu.”
8 Ndava ya malovi ago vakavamesa ligoga vandu vamahele na vachilongosi va muji.
Waliposikia haya, ule umati wa watu na maafisa wa mji wakaongeza ghasia.
9 Hinu pevamali kumlipisa mashonga Yasoni na vayaki kangi vakavaleka vahamba.
Nao baada ya kuchukua dhamana kwa ajili ya Yasoni na wenzake wakawaacha waende zao.
10 Kanyata kilu yila, vamsadika vala vakavatuma Pauli na Sila vahamba ku Belea. Navene pavahikili kwenuko vakayingila munyumba ya kukonganekela Vayawudi.
Usiku ule ule, wale ndugu walioamini wakawapeleka Paulo na Sila waende zao Beroya. Walipowasili huko wakaenda kwenye sinagogi la Wayahudi.
11 Vayawudi va ku Belea vavi vayuwanaji neju kuliku Vayawudi va ku Tesalonike, valipokili Lilovi la Chapanga na kugalingulila bwina Mayandiku Gamsopi muni vamanya ngati Pauli na Sila ijova malovi ga chakaka.
Hawa Waberoya walikuwa waungwana zaidi kuliko wale wa Thesalonike, kwa kuwa waliupokea ule ujumbe kwa shauku kubwa na kuyachunguza Maandiko kila siku ili kuona kama yale Paulo aliyosema yalikuwa kweli.
12 Vandu vamahele pagati yavi vasadiki, vavi na vadala va Chigiliki vevitopeswa mewa na vagosi.
Wayahudi wengi wakaamini pamoja na wanawake na wanaume wa Kiyunani wa tabaka la juu.
13 Nambu Vayawudi wa ku Tesalonike pevamanyili kuvya Pauli akokosayi Lilovi la Chapanga Belea, vakahamba kwenuko na kutumbula chitututu na kuvakokeha vandu vamahele.
Lakini wale Wayahudi wa Thesalonike waliposikia kuwa Paulo anahubiri neno la Mungu huko Beroya, wakaenda huko ili kuwashawishi watu na kuwachochea.
14 Vamsadika vala vakamhindikila kanyata Pauli ahamba kumbwani, nambu Sila na Timoti vasigalili balapala.
Mara hiyo, wale ndugu wakamsafirisha Paulo hadi pwani, lakini Sila na Timotheo wakabaki Beroya.
15 Vandu vala vakamhindikila Pauli mbaka Atene. Kangi vakawuya na kuni valagaziwi na Pauli kuvya, Sila na Timoti vamlanda kanyata.
Wale waliomsindikiza Paulo wakaenda naye mpaka Athene, kisha wakarudi Beroya wakiwa na maagizo kutoka kwa Paulo kuhusu Sila na Timotheo kwamba wamfuate upesi iwezekanavyo.
16 Pauli peavalindilayi Sila na Timoti ku Atene kula, akaviniswa neju mumtima waki ndava auwene muji wula umemili vimong'omong'o vya uchapanga.
Paulo alipokuwa akiwasubiri huko Athene, alisumbuka sana moyoni mwake kuona vile mji huo ulivyojaa sanamu.
17 Ajovisini na Vayawudi na vandu vangi vevakumsadika Chapanga, munyumba ya kukonganekela Vayawudi, ndi kila ligono ajovesana na vandu vevahumila pandu pakugulisila vindu.
Hivyo akahojiana kwenye sinagogi na Wayahudi pamoja na Wayunani waliomcha Mungu, na pia sokoni kila siku na watu aliopatana nao huko.
18 Vandu vevalanda mawuliwu ga Epikulo na Stoiki vakotini nayu. Ndi vangi vakajova, “Igana kujova kyani muyimu uyu?” Hinu vangi vakajova, “Ikokosela vachapanga vachiyehe.” Ndava Pauli avakokosela malovi ga kumvala Yesu na kuyuka,
Kisha baadhi ya Waepikureo na Wastoiko wenye falsafa wakakutana naye. Baadhi yao wakasema, “Je, huyu mpayukaji anajaribu kusema nini?” Wengine wakasema, “Inaonekana anasema habari za miungu ya kigeni.” Walisema haya kwa sababu Paulo alikuwa anahubiri habari njema kuhusu Yesu na ufufuo wa wafu.
19 Kangi vakamgongolela Pauli na ahamba palongolo ya libanji lelikemelewa Aleopago, vakajova, “Tigana utimanyisa mawuliwu aga gamupya geukugajova.
Hivyo wakamchukua na kumleta kwenye mkutano wa Areopago, walikomwambia, “Je, tunaweza kujua mafundisho haya mapya unayofundisha ni nini?
20 Ndava muni ukutijovela mambu ga chiyehe mumakutu gitu. Tigana kumanya maana ya mambu ago.”
Wewe unaleta mambo mapya masikioni mwetu, hivyo tungetaka kujua maana yake ni nini.”
21 Vandu va ku Atene pamonga na vayehe va kwenuko lukumbi lwavi lwoha vadandaulilana na kuyuwanila mambu gamupya.
(Waathene na wageni wote walioishi humo hawakutumia muda wao kufanya chochote kingine isipokuwa kueleza au kusikia mambo mapya).
22 Pauli akayima pa libanji la Aleopago, akajova, “Vandu va ku Atene! Nikuvalola nyenye kuvya vandu mwemukumuyupa Chapanga.
Ndipo Paulo akasimama katikati ya Areopago akasema, “Enyi watu wa Athene! Ninaona kwamba katika kila jambo ninyi ni watu wa dini sana.
23 Ndava panapitayi kuni na kula na kulola mambu ga kuyupa kwinu, nayiwene lusanja lwa luteta lweluyandikwi, ‘Kwa Chapanga Angamanyikana.’ Hinu nene nikuvakokosela malovi gaki mwenuyo mwemukumuyupa changali kumanya.
Kwa kuwa nilipokuwa nikitembea mjini na kuangalia kwa bidii vitu vyenu vya kuabudiwa, niliona huko madhabahu moja iliyoandikwa: Kwa Mungu Asiyejulikana. Basi sasa kile ambacho mmekuwa mkikiabudu kama kisichojulikana, ndicho ninachowahubiria.
24 Chapanga mweawumbili mulima pamonga vindu vyoha yvevivi mugati yaki, ndi Bambu wa kunani na pamulima, mwene nakutama Nyumba za Chapanga zezijengiwi na mawoko ga vandu.
“Mungu aliyeumba dunia na vyote vilivyomo ndani yake, yeye ndiye Bwana wa mbingu na nchi, hakai katika mahekalu yaliyojengwa kwa mikono ya wanadamu.
25 Mwene igana lepi kuhengewa na vandu, ngati kuvya igana utangatila wowoha wula, ndava muni mwene ndi mweakuvapela vandu wumi, mweakuvahotosa kukeka na kuvapela kila chindu.
Wala hatumikiwi na mikono ya wanadamu kana kwamba anahitaji chochote, kwa sababu yeye mwenyewe ndiye awapaye watu wote uhai na pumzi na vitu vyote.
26 Kuhuma kwa mundu mmonga, mwene awumbili vandu va milima yoha muni vatama pamulima woha, avapangili lusenje na mibaka ya pandu pakutama.
Kutoka kwa mtu mmoja, yeye aliumba mataifa yote ya wanadamu ili waikalie dunia yote, naye akaweka nyakati za kuishi.
27 Chapanga aganili vandu vamulanda na hati cha kupapasa, vahotola kumhikila. Nambu mwene avi lepi patali na kila mmonga witu.
Mungu alifanya hivyo ili wanadamu wamtafute na huenda wakamfikia ingawa kwa kupapasapapasa ijapokuwa kwa kweli hakai mbali na kila mmoja wetu.
28 Ngati cheajovili mundu mmonga kuvya, ‘mugati mwaki tete titama na kugenda na tivili!’ Ngati vayimbaji vangi chavijova, ‘Tete ndi vana vaki.’
‘Kwa kuwa katika yeye tunaishi, tunatembea na kuwa na uzima wetu.’ Kama baadhi ya watunga mashairi wenu walivyosema, ‘Sisi ni watoto wake.’
29 Muni tete tavana vaki Chapanga, nakuganikiwa kumhololela mwene kuvya avi ngati zahabu amala mashonga amala liganga lelihongoliwi kwa luhala na vandu.
“Kwa kuwa sisi ni watoto wa Mungu, haitupasi kudhani kuwa uungu ni kama sanamu ya dhahabu au ya fedha au ya jiwe, mfano uliotengenezwa kwa ubunifu na ustadi wa mwanadamu.
30 Chapanga akitili ngati ilola lepi lusenje lula vandu pavahimwiki. Nambu hinu, ihamula vandu voha kila pandu vamuwuyila mwene.
Zamani wakati wa ujinga, Mungu alijifanya kama haoni, lakini sasa anawaamuru watu wote kila mahali watubu.
31 Ndava amali kuhagula ligono leihamula mulima pangali kumganisila yoyoha munjila ya mundu mmonga mweamhagwili. Chapanga avalangisi voha lijambu lenilo kwa kumyukisa mundu mwenuyo kwevafwili.”
Kwa kuwa ameweka siku ambayo atauhukumu ulimwengu kwa haki akimtumia mtu aliyemchagua. Amewahakikishia watu wote mambo haya kwa kumfufua Kristo kutoka kwa wafu.”
32 Pavamuyuwini Pauli ijova lijambu la kuyuka kuhuma kwa vafwili, vangi vakamuheka nambu vangi vakajova, “Tigana kuyuwana kavili lijambu lenili.”
Waliposikia habari za ufufuo wa wafu, baadhi yao wakadhihaki, lakini wengine wakasema, “Tunataka kukusikia tena ukizungumza juu ya jambo hili.”
33 Na Pauli akavaleka akahuma mu libanji.
Kwa hiyo Paulo akaondoka katikati yao.
34 Nambu vandu nunuyu vakawungana nayu, vakavya vamsadika. Pagati yavi avi Dionisi wa ku Aleopago na mdala mmonga liina laki Damali, pamonga na vandu vangi.
Lakini baadhi yao wakaungana naye wakaamini. Kati yao alikuwepo Dionisio, Mwareopago na mwanamke mmoja aliyeitwa Damari na wengine wengi.

< Matendu 17 >