< 1 Vatesolonike 1 >
1 Nene Pauli na Siliwano na Timoti, tikuvayandikila msambi wa vandu vevakumsadika Kilisitu va ku Tesalonike. Ndi vandu voha vevakumuyupa Chapanga Dadi, na va BAMBU Yesu Kilisitu. Tikuvaganila ubwina wa Chapanga na uteke.
Paulo, Silvano na Timotheo: Kwa kanisa la Wathesalonike, ninyi mlio ndani ya Mungu Baba yetu na ndani ya Bwana Yesu Kristo: Neema iwe kwenu na amani.
2 Tikumsengusa Chapanga magono goha ndava yinu mwavoha na kuvakumbuka magono goha mukuyupa kwitu Chapanga.
Siku zote tunamshukuru Mungu kwa ajili yenu ninyi nyote, tukiwataja kwenye maombi yetu daima.
3 Muni, palongolo ya Chapanga Dadi witu, tikumbuka ndi chemwilasa sadika yinu kwa matendu, na uganu winu cheukuvakita muhenga lihengu neju, na chila sadika yitu kwa BAMBU Yesu Kilisitu yanganyugusika.
Tunaikumbuka daima kazi yenu ya imani mbele za Mungu aliye Baba yetu, taabu yenu katika upendo na saburi yenu ya tumaini katika Bwana wetu Yesu Kristo.
4 Valongo timanyili kuvya Chapanga avaganili na avahagwili muvya vandu vaki,
Ndugu zetu mpendwao na Mungu, kwa kuwa tunajua kwamba Mungu amewachagua,
5 muni lukumbi lwetavakokosili Lilovi la Bwina gavili lepi malovi gene, ndi kwa makakala na kwa Mpungu Msopi, na chakaka kuvya ujumbi wenuwo wavili wachakaka. Mmanyili chatatamili pamonga na nyenye, tatamili kwa kuvatangatila nyenye.
kwa sababu ujumbe wetu wa Injili haukuja kwenu kwa maneno matupu bali pia ulidhihirishwa katika nguvu na katika Roho Mtakatifu, tena ukiwa na uthibitisho kamili, kama vile ninyi wenyewe mnavyojua jinsi tulivyoenenda katikati yenu kwa ajili yenu.
6 Nyenye mwalandili luhumu lwitu, mwamyigili BAMBU. Pamonga na mwaviniswi neju, mwapokili ujumbi wenuwo kwa luheku wewihuma kwa Mpungu Msopi.
Nanyi mkawa wafuasi wetu na wa Bwana, ingawa mlipata mateso mengi, mlilipokea lile Neno kwa furaha katika Roho Mtakatifu.
7 Hinu nyenye ndi luhumu lwabwina neju kwa vandu voha vevakumsadika va Makedonia na Akaya.
Hivyo ninyi mkawa kielelezo kwa waumini wote katika Makedonia na Akaya.
8 Muni, ndava ya ukangamala winu ujumbi wa BAMBU uyuwaniki lepi ku Makedonia na ku Akaya kwene, ndi sadika ya Chapanga yidandasiki kwoha. Kangi niganili lepi kujova neju,
Kwa maana kutoka kwenu neno la Bwana limesikika, si katika Makedonia na Akaya tu, bali pia imani yenu katika Mungu imejulikana kila mahali kiasi kwamba hatuna haja ya kusema lolote kwa habari yake.
9 Vandu venavo vevitama patali na nyenye vilongela kuvala lugendu lwitu kwinu na chemwatipokili, ndi chemwalekili chimong'omong'o, na kumhengela Chapanga mweavimumi na wa chakaka,
Kwa maana watu wa maeneo hayo wenyewe wanaeleza jinsi mlivyotupokea na jinsi mlivyomgeukia Mungu mkaacha sanamu, ili kumtumikia Mungu aliye hai na wa kweli
10 Hinu mkumlindila Mwana waki ahelela kuhuma kunani kwa Chapanga, ndi Yesu, na mwene ndi Chapanga amyukisi kuhuma mu lifwa na mweakutisangula kuhuma muligoga la Chapanga lelibwela.
na ili kumngojea Mwanawe kutoka mbinguni, ambaye Mungu alimfufua kutoka kwa wafu: yaani, Yesu, yeye aliyetuokoa kutoka ghadhabu inayokuja.