< Esaamootkaat 18 >

1 Erah lih dophi, Pool Ethen nawa Korin ni wangta.
Baada ya haya, Paulo akaondoka Athene akaenda Korintho.
2 Erah ni Jehudiite wasiit Akuila ngeh ih chomuita, heh Poontus ni tup arah angta, nengnyi heh minuh Prisilla ah langla, Luuwanglong Kladius ih Room hah nawa Jehudi loong ah dokphan rum kano erah ngangah ih Itali nawa ra nyuutaha. Eno Pool ah erah nyi damdi,
Huko akakutana na Myahudi mmoja jina lake Akila, mwenyeji wa Ponto, ambaye alikuwa amewasili karibuni kutoka Italia pamoja na mkewe Prisila, kwa sababu Klaudio alikuwa ameamuru Wayahudi wote waondoke Rumi. Paulo akaenda kuwaona,
3 ngunbi suh nok roonghoon waktong wangta, tiimnge liidi Pool uh nengnyi likhiikkhiik ih hetui hewok raang ih nok hoon nawa ngun kabiita.
naye kwa kuwa alikuwa mtengeneza mahema kama wao, akakaa na kufanya kazi pamoja nao.
4 Pool Jehudi rangsoomnok ni Naangtongsa rookweh Jehudi nyia Grik damdi roongwaan leh kataat nuune rumta.
Kila Sabato Paulo alikuwa akihojiana nao katika sinagogi, akijitahidi kuwashawishi Wayahudi na Wayunani.
5 Mesidonia nawa Silas nyia Timothi ah thoknyu kano, Pool ih saapoot ah saarookwet Rangte tiit baat suh kota, Jehudi loong suh Jisu juuba Kristo ngeh ih baat rumta.
Sila na Timotheo walipowasili kutoka Makedonia, walimkuta Paulo akiwa amejitolea muda wake wote katika kuhubiri, akiwashuhudia Wayahudi kwamba Yesu ndiye Kristo
6 Mina loong ah ih ethih ethih jeng rum ano Pool suh liirum kano, neng jeng daan lakbi ah heh nyuh dowa botla ah jaabuh ano li rumta, “Sen mat e an bah sen teeteewah suh joong an! Nga mat tah angka, Arah dophi bah ngah Ranglajatte taangko ih kah ang.”
Wayahudi walipompinga Paulo na kukufuru, yeye aliyakungʼuta mavazi yake, akawaambia, “Damu yenu na iwe juu ya vichwa vyenu! Mimi sina hatia, nimetimiza wajibu wangu. Kuanzia sasa nitawaendea watu wa Mataifa.”
7 Erah lih adi neng re dowa doksoon kah ano, Ranglajatte mina Rangte rangsoomte ih hoon arah, heh men Taitias Justus kapoon rumta nok ni tong kata; heh nok ah Jehudi rangsoomnok reeni angta.
Kisha akaondoka mle kwenye sinagogi, akaenda nyumbani kwa mtu mmoja jina lake Tito Yusto, aliyekuwa mcha Mungu. Nyumba yake ilikuwa karibu na sinagogi.
8 Kispus ah Jehudi rangsoomnok ni mihak phokhoh angta, heh teewah nyia heh jaatang loongtang Teesu hanpiite ang rumta; Korin ni uh Rangte jengkhaap ah chaat rum ano hanpiite rapne ih dong ano ju ah tem ih rumta.
Kiongozi wa hilo sinagogi, aliyeitwa Krispo, akamwamini Bwana, yeye pamoja na watu wote wa nyumbani mwake. Nao Wakorintho wengi waliomsikia Paulo pia wakaamini na kubatizwa.
9 Pheesiit Pool suh motmang ni heh Teesu ih baatta, “An nakcho uh, erah nang ebah larit haat thang ih baat ba jangbaat theng,
Usiku mmoja Bwana akamwambia Paulo katika maono, “Usiogope, lakini endelea kusema wala usinyamaze,
10 timnge liidi an damdi ngah eje. O ih uh tajen thet haatru; samnuthung adi nga mih rapne ih je ah.”
kwa maana mimi niko pamoja nawe, wala hakuna mtu atakayeweza kukushambulia ili kukudhuru, kwa kuwa ninao watu wengi katika mji huu ambao ni watu wangu.”
11 Erah raangtaan ih Pool paangsiit paangthom tongthiin ano, mina loong asuh Rangte Jengkhaap ah nyootsoot thiin rumta.
Hivyo Paulo akakaa huko kwa muda wa mwaka mmoja na nusu, akiwafundisha neno la Mungu.
12 Akaia hah ni Gallio ah, Room nawa kobono angta doh, Jehudi loong lomkhoon rum ano, Pool ah joh ih rumta; eno mat hoon thengni siitkaat rumta.
Lakini wakati Galio alipokuwa msaidizi wa mwakilishi wa mtawala huko Akaya, Wayahudi waliungana kumshambulia Paulo, wakamkamata na kumpeleka mahakamani.
13 “Arah mih” rah ih seng “Hootthe ni lajeeka rah Rangte rangsoom thuk suh miloong asuh laatbaat rumha!”
Wakamshtaki wakisema, “Mtu huyu anawashawishi watu wamwabudu Mungu kinyume cha sheria.”
14 Pool ah jeng ih ang ngeh taat thun adi Gallio ih Jehudi loong asuh liita, “Arah matthih changkhah tiit ang dobah, Ngah ih mat ah hoon etheng tang Jehudi noksong loong.”
Paulo alipotaka kujitetea, Galio akawaambia Wayahudi, “Kama ninyi Wayahudi mlikuwa mkilalamika kuhusu makosa makubwa ya uhalifu ingekuwa haki kwangu kuwasikiliza.
15 Enoothong, sen loong ah jengkhaap thoidi nyia sen Hootthe tungdi ba daanmui lan, erah tiit abah sensen ih hoonjih. Arah likhiik ah ngah ih tapaat korumra!”
Lakini kwa kuwa linahusu maneno, majina na sheria yenu, amueni ninyi wenyewe. Mimi sitakuwa mwamuzi wa mambo haya.”
16 Eno matpaat theng nawa phanhaat rumta.
Akawafukuza kutoka mahakamani.
17 Erah lih adi Jehudi rangsoomnok dowa mihak phokhoh, Sosthens ah joh rum ano mat hoon theng nokka adi nobuh rumta. Enoothong tiim ih rum abah uh Gallio ah tasoot saamta.
Ndipo wote wakamkamata Sosthene kiongozi wa sinagogi, wakampiga mbele ya mahakama, lakini Galio hakujali kitendo chao hata kidogo.
18 Hanpiite loong damdi Pool Korin hani rekamdook tongthiinta, eno Prisilla nyia Akuila damdi Siria ni juulam ih daan soon wangta. Seneria ni maang daansoon kaadi, heh ih thoomhoon thoidi heh khoh ah suihaat eta.
Baada ya kukaa Korintho kwa muda, Paulo akaagana na wale ndugu walioamini, akasafiri kwa njia ya bahari kwenda Shamu akiwa amefuatana na Prisila na Akila. Walipofika Kenkrea, Paulo alinyoa nywele zake kwa kuwa alikuwa ameweka nadhiri.
19 Ephesas ni thokrum ano, Pool ih Prisilla nyi Akuila ah thiinhaat ih nyuuta. Pool Jehudi rangsoomnok ni kah ano, Jehudi loong damdi roongwaan kata.
Walipofika Efeso, Paulo aliwaacha Prisila na Akila huko, lakini yeye akaingia kwenye sinagogi akawa anajadiliana na Wayahudi.
20 Miloong ah ih rekam tongthiin taatbaat rumta, eno Pool tanookta.
Walipomwomba akae nao kwa muda mrefu zaidi hakukubali.
21 Erah nang ebah Pool ih kaat elang ngeh ih baatthiin rum ano amah jeng thiinta, “Rangte tenthun mongtham ang abah sen jiinnah we ngaakwang ehang.” Erah baat rum ano Ephesas nawa juulam ih daansoon kata.
Lakini alipokuwa akiondoka, akaahidi, “Nitarudi kama Mungu akipenda.” Kisha akasafiri kwa njia ya bahari kutoka Efeso.
22 Pool Kaisiria ni thok ano, Jerusalem chaas ni kata, eno jengseera ano, Entiok ni wangta.
Alitia nanga Kaisaria, akaenda Yerusalemu na kulisalimu kanisa, kisha akaenda Antiokia.
23 Erah ni chomroe tongthiin ano, Galitia nyia Phrigia hah lam ih wang ano chaankot jengkhaap ah hanpiite loong asuh jeng koh thiinta.
Baada ya kukaa huko kwa muda, akaondoka na kwenda sehemu moja hadi nyingine huko Galatia na Frigia, akiwaimarisha wanafunzi wote.
24 Erah tokdi Korin Jehudi mih wasiit, heh men ah Apollos, erah warah Alejandria ni tup dowa, eno Ephesas ni ra taha. Heh tiitwah loong angta eno Rangte Jengkhaap uh jat eta.
Basi akaja Efeso Myahudi mmoja, jina lake Apolo, mwenyeji wa Iskanderia. Yeye alikuwa na elimu kubwa, pia alikuwa hodari katika Maandiko.
25 Teesu lampo ni khoom suh heh renbaat choi nyia nyootsoot choi angta, erah thoidi Jisu thoilam ah naririh ih nyootsootta. Erabah uh, heh ih Joon Juutem luulu ba jatta.
Alikuwa amefundishwa katika njia ya Bwana, naye alikuwa na bidii katika roho, akafundisha kwa usahihi juu ya Yesu, ingawa alijua tu ubatizo wa Yohana.
26 Heh Jehudi rangsoomnok ni lacho laphaan ih phang jengkongta. Prisilla nyia Akuilla ih heh jeng ah chaat nyu ano, nengnyi damdi nok ni siitwan nyuuta, eno Rangte lampo ah rapniine ih hukbaat nyuuta.
Apolo alianza kunena kwa ujasiri mkubwa katika sinagogi. Lakini Prisila na Akila walipomsikia, walimchukua kando na kumweleza njia ya Mungu kwa ufasaha zaidi.
27 Erah lih adi Apollos Akaia ni kaat chungta, erah raangtaan ih Ephesas dowa hanpiite loong ah ih Akaia nok hah suh rapniine ih sokboi an ngeh ih le ah raangmaat ih rumta. Apollos thokkhoom ano, Rangte minchan di kristaan loong ah raangtaan ih neng moot chosok suh rapne ese angta.
Naye Apolo alipotaka kwenda Akaya, ndugu wa Efeso walimtia moyo, wakawaandikia wanafunzi huko ili wamkaribishe. Alipofika huko, aliwasaidia sana wale ambao, kwa neema ya Mungu, walikuwa wameamini.
28 Tiimnge liidi, Apollos ah Jehudi loong damdi rapne daanmui ano Rangteele nawa ih Jisu ah Kristo ngeh ih jatthuk rumta.
Kwa uwezo mkubwa aliwakanusha hadharani Wayahudi waliokuwa wakipinga, akionyesha kwa njia ya Maandiko kwamba Yesu ndiye Kristo.

< Esaamootkaat 18 >