< 2 Timoteo 2 >
1 Bhai ugwe mwanangu, ukole mashili kwa nema jitupegwa nkulundana na a Yeshu Kilishitu.
Basi, wewe mwanangu, uwe hodari katika neema iliyo ndani ya Kristo Yesu.
2 Na majiganyo gumpilikene ngulijiganya pa bhaakong'ondela bhabhagwinji, numbe mmwe mwaajiganyanje bhandunji bhaakulupalika, bhaakombolanga kwaajiganyanga bhananji.
Nayo mambo yale uliyonisikia nikiyasema mbele ya mashahidi wengi, uwakabidhi watu waaminifu watakaoweza kuwafundisha watu wengine vilevile.
3 Gwiilunde mmboteko pamo na nne, malinga nkomana ngondo jwa mmbone jwa a Yeshu Kilishitu.
Vumilia taabu pamoja nasi kama askari mwema wa Kristo Yesu.
4 Linjola pabha nkukomana ngondo akakwiibhuka nkukamula maengo gana, pabha shaapinga ni kwaanonyeya bhakulungwa bha likundi lyakwe.
Hakuna askari yeyote ambaye akiwa vitani hujishughulisha na mambo ya kawaida ya maisha haya kwa sababu nia yake ni kumpendeza yule aliyemwandika awe askari.
5 Nneyo peyo mundu apwatanila upo mwiing'ando, akapegwa upo ya kombola monaga jwangakaguya ikubho ya nng'andogo.
Vivyo hivyo, yeye ashindanaye katika michezo hawezi kupewa tuzo ya ushindi asiposhindana kulingana na kanuni za mashindano.
6 Mundu atumbila kulima, ni apinjikwa abhe jwantai kupata shipeta sha mauno.
Mkulima mwenye bidii ya kazi ndiye anayestahili kuwa wa kwanza kupata fungu la mavuno.
7 Nnganishiye kaje malobhe gungummalanjila gano, pabha Bhakulungwa shibhampe lumanyio lwa kugamanya gowe.
Fikiri sana kuhusu haya nisemayo, kwa maana Bwana atakupa ufahamu katika mambo hayo yote.
8 Mwaakumbushile a Yeshu Kilishitu bhayushiywe bhakaweje, bha shipinga sha a Daudi, malinga shijitaya Ngani ja Mmbone jingulunguya jino.
Mkumbuke Yesu Kristo, aliyefufuliwa kutoka kwa wafu, yeye aliye wa uzao wa Daudi. Hii ndiyo Injili yangu,
9 Kwa lyene ligongolyo ngunapotekwa nitabhwa mbuti nkulebha, ikabheje lilobhe lya a Nnungu likatabhwa.
ambayo kwayo ninateseka hata kufikia hatua ya kufungwa minyororo kama mhalifu. Lakini neno la Mungu halifungwi.
10 Kwa nneyo ngunakwiipililila gowe, kwa ligongo lya bhandunji bhaagwilwenje na a Nnungu, nkupinga na bhalabhonji bhapatanje ntapulo nkulundana na a Yeshu Kilishitu, na ukonjelo gwa pitipiti. (aiōnios )
Kwa hiyo ninavumilia mambo yote kwa ajili ya wateule wa Mungu, kusudi wao nao wapate wokovu ulio katika Kristo Yesu, pamoja na utukufu wa milele. (aiōnios )
11 Na malobhe ga kulupalika gakuti, “Monaga tuwile pamo na bhenebho, nneyo peyo shitulame pamo na bhenebho.
Hili ni neno la kuaminiwa: Kwa maana kama tumekufa pamoja naye, tutaishi pia pamoja naye.
12 Monaga shituipililile, shitutagwale pamo na bhenebho. Na ibhaga shitwaakane bhenebho, na bhalabho shibhatukane uwe.
Kama tukistahimili, pia tutatawala pamoja naye. Kama tukimkana yeye, naye atatukana sisi.
13 Nkali tubhe bhangakulupalilanga, bhenebho ni bhaakulupalikape, pabha ikaakomboleka kwiikana bhayene.”
Kama tusipoamini, yeye hudumu kuwa mwaminifu, kwa maana hawezi kujikana mwenyewe.
14 Bhai, mwaakumbushiyanje bhandu gene malobhego, na mwaaleyanje pa meyo ga a Nnungu, bhanakolanje malobhe ga mitau, pabha gangali mana, ikabhe ganapuganya bhaapilikananga.
Endelea kuwakumbusha mambo haya ukiwaonya mbele za Bwana waache kushindana kwa maneno ambayo hayana faida yoyote bali huwaangamiza tu wale wanaoyasikia.
15 Ntumbile kwiilanguya kwa a Nnungu kuti mmaakulupalika, ntumishi jwangali oni, nnilunguya kwa aki ntenga gwa kweli gwa a Nnungu.
Jitahidi kujionyesha kwa Mungu kuwa umekubaliwa naye, mtendakazi asiye na sababu ya kuona aibu, ukilitumia kwa usahihi neno la kweli.
16 Mwiembuye na nkungulu gwangali mana na gwa shingumba, pabha ganakwaashoyanga bhandunji nngulupai niileka kwaajogopa a Nnungu.
Jiepushe na maneno mabaya, yasiyo na maana, yasiyo ya utauwa, kwa maana hayo huzidi kuwatosa watu katika kukosa heshima kwa Mungu.
17 Majiganyo gabhonji ganajambushiya malinga libhanga shilijenela nshiilu, munkumbi gwabhonji bhapalinji a Imenayo na a Piletushi.
Mafundisho yao yataenea kama kidonda kisichopona. Miongoni mwao wamo Himenayo na Fileto
18 Bhanganyabho bhapuganikenje niileka ya kweli, bhalinkutinji kuyuywa kwa bhandunji kupitile, nipuganya ngulupai ya bhandu bhabhagwinji.
ambao wameiacha kweli, wakisema kwamba ufufuo wa wafu umekwisha kuwako, nao huharibu imani ya baadhi ya watu.
19 Ikabheje a Nnungu bhabhishile ishi ya nyumba, ishimilishwe kwa olela ukoto, na gene malobhe gano, gashijandikwa pantundu yene ishii, “Bhakulungwa bhaamanyi bhandunji bhabho,” na kabhili, “Kila ashema lina lya Bhakulungwa, aleshe ilebho.”
Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, ukiwa na muhuri wenye maandishi haya: “Bwana anawajua walio wake”; tena, “Kila alitajaye jina la Bwana, na auache uovu.”
20 Nnyumba jikulungwa ikaapagwa indu ya shaabhu na ela pe, ikabhe na indu ya mikongo na ya lilongo, ina ya tendela maengo gamashoko ina ya maengo gamakulungwa.
Katika nyumba kubwa si kwamba kuna vyombo vya dhahabu na fedha tu, bali pia vimo vyombo vya miti na vya udongo; vingine kwa matumizi maalum, na vingine kwa matumizi ya kawaida.
21 Bhai mundu aikonjeleyaga niileka ilebho, shaabhe mundu jwa maengo gamakulungwa, sha ukonjelo shibhishilwe na bhayene nyumba, shaapwae kwa kila liengo lya mmbone.
Basi ikiwa mtu amejitakasa na kujitenga na hayo niliyoyataja, atakuwa chombo maalum, kilichotengwa na ambacho kinamfaa mwenye nyumba, kimeandaliwa tayari kwa kila kazi njema.
22 Mwiembuye na ilokoli ya ushanda, nkagulile uguja na ngulupai na kupingana na ulele, pamo na bhene bhakwaajuganga Bhakulungwa kwa ntima gwa mmbone.
Zikimbie tamaa mbaya za ujana, ufuate haki, imani, upendo na amani pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi.
23 Mwiembuye na mitau ja shingumba na jangali mana, pabha mmumanyi kuti yeneyo inakumbuya mipwai.
Jiepushe na mabishano ya kipumbavu na yasiyo na maana, kwa kuwa wajua ya kwamba hayo huzaa magomvi.
24 Numbe ntumishi jwa Bhakulungwa akapinjikwa kubha jwa mipwai, ikabhe jwa kwiitimalika kubhandu bhowe, akombola kujiganya na kwiipililila.
Tena haimpasi mtumishi wa Bwana kuwa mgomvi, bali inampasa awe mwema kwa kila mtu, awezaye kufundisha, tena mvumilivu.
25 Anapinjikwa kwaaleyanga kwa kwiitimalika bhakuntaukanga, pana a Nnungu shibhaajalianje kwiipeta nikagula ya kweli.
Inampasa kuwaonya kwa upole wale wanaopingana naye, kwa matumaini kwamba Mungu atawajalia kutubu na kuijua kweli,
26 Nkupinga lunda lwabhonji lwaabhujilanje kabhili nikolobhoka nniyau lika Lishetani, lyabhatanjiyenje nkupinga bhatendanje yapinga jwenejo.
ili fahamu zao ziwarudie tena, nao waponyoke katika mtego wa ibilisi ambaye amewateka wapate kufanya mapenzi yake.