< Salamo 68 >

1 Hiongake t’i Andrianañahare, le hiparaitake o rafelahi’eo; vaho hibioñe aolo’e eo o malaiñe Azeo.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo. Mungu na ainuke, watesi wake watawanyike, adui zake na wakimbie mbele zake.
2 Hambañe ami’ty fampisaohañe hatoeñe, isaoho añe ka; manahake ty fitranaha’ o karafo tantele aolo’ afoo, ty hikoromaha’ o tsivokatseo añatrefan’Añahare.
Kama vile moshi upeperushwavyo na upepo, vivyo hivyo uwapeperushe mbali, kama vile nta iyeyukavyo kwenye moto, vivyo hivyo waovu na waangamie mbele za Mungu.
3 Ho ehake o vañoñeo, hirebeke añ’atrefan’Añahare eo, hiriñariña an-kobaiñe.
Bali wenye haki na wafurahi, washangilie mbele za Mungu, wafurahi na kushangilia.
4 Misaboa aman’ Añahare, bangò i tahina’ey; onjono i Mpiningitse miranga i montombeiy, Ià ty tahina’e; vaho mitreñà añatrefa’e eo.
Mwimbieni Mungu, liimbieni sifa jina lake, mtukuzeni yeye aendeshwaye juu ya mawingu: jina lake ni Bwana, furahini mbele zake.
5 Raem-bode-rae naho mpañomey to amo vantotseo t’i Andrianañahare an-kivoho’e miavake ao.
Baba wa yatima, mtetezi wa wajane, ni Mungu katika makao yake matakatifu.
6 Ampimoneñan’ Añahare añ’akiba ao ty jorý; akare’e mb’an-kavokarañe o rinohio; fe mitobok’ an-tane kirikintàñe ao o mpitrabikeo.
Mungu huwaweka wapweke katika jamaa, huwaongoza wafungwa wakiimba, bali waasi huishi katika nchi kame.
7 O Andrianañahare, ie niaoloa’o ondati’oo, ie nihofiha’o firanga i fatram-beiy, Selà
Ee Mungu, ulipowatangulia watu wako, ulipopita nyikani,
8 niezeñezeñe i taney, nihotrake i likerañey aolo’ i Andrianamboatse, Nihondrahondra ty Sinay añatrefa’ i Abo Tia, Andrianañahare’ Israele eo.
dunia ilitikisika, mbingu zikanyesha mvua, mbele za Mungu, Yule wa Sinai, mbele za Mungu, Mungu wa Israeli.
9 Nanondraha’o oran-joba, ry Andrianañahare; niventè’o i lova’o navozoy,
Ee Mungu, ulinyesha mvua nyingi na kuiburudisha ardhi iliyokuwa imechoka.
10 Nitobok’ ao i mpirai-lia’oy, nifahana’o ami’ty havokara’o o rarakeo, ry Andrianamboatse.
Ee Mungu, watu wako waliishi huko, nawe kwa wingi wa utajiri wako uliwapa maskini mahitaji yao.
11 Nitaroñe t’i Talè; mitozantoza o rakemba mitalily i entañeio.
Bwana alitangaza neno, waliolitangaza neno hilo walikuwa kundi kubwa:
12 Nitriban-day mb’eo o mpanjakan- dahindefoñeo! Nivoratsake; le ho zarae’ i tambatse an-kiboho’e ao o kinopakeo,
“Wafalme na majeshi walikimbia upesi, watu waliobaki kambini waligawana nyara.
13 ie mandre am-bàlan’añondry ao, le manahake ty elan-deho misarom-bola-foty; mimilemiletse volamena o volo’eo.
Hata ulalapo katikati ya mioto ya kambini, mabawa ya njiwa wangu yamefunikwa kwa fedha, manyoya yake kwa dhahabu ingʼaayo.”
14 Ie nampivarakai’ i El-Sadai i mpanjaka rey, le niavy an-Tsalmone ty oram-panala.
Wakati Mwenyezi alipowatawanya wafalme katika nchi, ilikuwa kama theluji iliyoanguka juu ya Salmoni.
15 Vohin’ Añahare ty vohy Basane; vohitse lako-lengo’e ty haboa’ i Basane;
Milima ya Bashani ni milima iliyotukuka, milima ya Bashani ina vilele vilivyochongoka.
16 Inoñe ty ikiraña’ areo ry haboañe maro-lengo’eo, i vohitse nirien’Añahare himoneña’ey? Eka himoneñe ao nainai’e t’Iehovà.
Enyi milima yenye vilele vilivyochongoka, kwa nini mnakazia macho kwa wivu, katika mlima Mungu anaochagua kutawala, ambako Bwana mwenyewe ataishi milele?
17 Añ’ale’ale o sareten’ Añahareo, arivo-añ’arivo’e; ama’e ao an-kamasiña’e t’i Talè manahake e Sinay añe.
Magari ya Mungu ni makumi ya maelfu, na maelfu ya maelfu; Bwana amekuja kutoka Sinai hadi katika patakatifu pake.
18 Nionjoñe añ’abo eñe irehe, nikozozote’o an-drohy o fandrohizañeo, nandrambe ravoravo am’ondatio, vaho amo mpiolao, himoneña’ Ià, Andrianañahare.
Ulipopanda juu, uliteka mateka, ukapokea vipawa kutoka kwa wanadamu, hata kutoka kwa wale walioasi, ili wewe, Ee Bwana Mungu, upate kuishi huko.
19 Andriañeñe t’i Talè mpivave o kilankan-tikañeo boak’andro, i Andrianañaharem- pandrombahantikañey. Selà
Sifa apewe Bwana, Mungu Mwokozi wetu, ambaye siku kwa siku hutuchukulia mizigo yetu.
20 Andrianañaharem-pañaha an-tika t’i Andrianamboatse; Toe a Iehovà Talè ty famotsorañe an-kavilasy.
Mungu wetu ni Mungu aokoaye, Bwana Mwenyezi hutuokoa na kifo.
21 Le hanorotoro ty loha’ o rafelahi’eo t’i Andrianañahare, ty kovo-doha minankanankañe amo hakeo’eo.
Hakika Mungu ataponda vichwa vya adui zake, vichwa vya hao waendao katika njia za dhambi.
22 Hoe t’i Talè: Hampoliko o e Basaneo, hahereko boak’ an-keraheran-driak’ ao,
Bwana alisema, “Nitawarudisha kutoka Bashani; nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari,
23 Ho demohem-pandia’o an-dio o rafelahi’oo, hanañ’anjara an-dion-drafilahy ka o lelan’ amboa’oo.
ili uweze kuchovya miguu yako katika damu ya adui zako, huku ndimi za mbwa wako zikiwa na fungu lake.”
24 Fa niisa’ iareo o fañaveloa’oo ry Andrianañahare, ty fionjonan’ Añahareko, toe i Mpanjakakoy, mb’amy miavakey ao.
Ee Mungu, maandamano yako yameonekana, maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu, yakielekea patakatifu pake.
25 Miaolo o mpisaboo, manonjohy o mpititikeo; añivo’e ao o somondrara mampikantsankantsàñe o kantsàñeo:
Mbele wako waimbaji, baada yao wapiga vinanda, pamoja nao wako wanawali wakipiga matari.
26 Andriaño am-pivory ao t’i Andrianañahare, i Iehovà boak’am-pigoa­ngoaña’ Israele.
Msifuni Mungu katika kusanyiko kubwa, msifuni Bwana katika kusanyiko la Israeli.
27 Ingo t’i Beniamine tsitso’e, miaolo iareo, o roandria’ Iehodào am-pirimboña’eo, o roandria’ i Zeboloneo, o roandria’ i Naftalio.
Liko kabila dogo la Benyamini likiwaongoza, wakifuatwa na kundi kubwa la watawala wa Yuda, hatimaye watawala wa Zabuloni na Naftali.
28 Fa linilin’ Añahare’o ty haozara’o; mihaozara! Ry Andrianañahare, nañenefa’o ho anay izay,
Ee Mungu, amuru uwezo wako, Ee Mungu tuonyeshe nguvu zako, kama ulivyofanya hapo awali.
29 ty kiboho’o e Ierosalaime añe, ty ibanabanà’ o mpanjakao ama’oy.
Kwa sababu ya Hekalu lako Yerusalemu wafalme watakuletea zawadi.
30 Endaho o biby hako am-bindao, o añombelahy maroo rekets’ o dronga’ ondatioo, songa mandialia tseram-bolafoty; navarakai’e ondaty tea alio.
Mkemee mnyama aliyeko kwenye manyasi, kundi la mafahali katikati ya ndama za mataifa. Na walete minara ya madini ya fedha wakinyenyekea. Tawanya mataifa yapendayo vita.
31 Hiavotse e Mitsraime ao o sorotà’eo, halisa hañity fitàñe aman’Añahare t’i Kose.
Wajumbe watakuja kutoka Misri, Kushi atajisalimisha kwa Mungu.
32 Misaboa aman’Andrianañahare, ry fifehea’ ty tane toio; rengeo an-tsabo t’i Talè; Selà
Mwimbieni Mungu, enyi falme za dunia, mwimbieni Bwana sifa,
33 I miningitse andindì’ o likerañe haehaeo, Inay, ampionjone’e i fiarañanaña’ey, i fiarañanañañe ra’elahiy.
mwimbieni sifa yeye apandaye mbingu za kale zilizo juu, yeye angurumaye kwa sauti kuu.
34 Iantofo te an’Andrianañahare ty haozarañe ambone’ Israele eo ty ahe’e an-dikerañe ao ty hafatrara’e.
Tangazeni uwezo wa Mungu, ambaye fahari yake iko juu ya Israeli, ambaye uwezo wake uko katika anga.
35 Mampañeven-drehe, ry Andrianañahare, an-toe’o miavake ao; I Andrianañahare’ Israele, ro mpanolotse haozarañe naho hafatrarañe am’ondati’eo. Andriañeñe t’i Andrianañahare!
Ee Mungu, wewe unatisha katika mahali patakatifu pako, Mungu wa Israeli huwapa watu wake uwezo na nguvu. Mungu Asifiwe!

< Salamo 68 >